Je, Sera ya Elimu Bure haina tija kama hali za wananchi zisipoboreshwa?

Sauti za Wananchi

Senior Member
Sep 2, 2014
113
138
Taasisi ya TWAWEZA ambayo hufanya tafiti kwa kukusanya maoni ya wananchi leo inazindua awamu ya tano ya Tathmini ya Uwezo ya kupima watoto wa miaka 7 hadi 16 ili kubaini uwezo wao katika kusoma na kufanya hesabu.

Ripoti yaonesha, ufaulu wa wanafunzi hutegemea hali ya kijamii na kiuchumi ya kaya anayotoka. Ripoti pia yaonesha kuna tofauti kubwa katika viwango ufaulu kimkoa, Rukwa imeshika mkia katika majaribio ya Kiingereza na Hesabu huku Dar es Salaam na Arusha zikifanya vizuri sana.

Je hii inaashiria nini katika jamii yetu? Je sera ya Elimu Bure haina tija kama hali za Wananchi zisipoboreshwa?

Tunakaribisha maoni yako.

Screenshot from 2016-08-31 16:23:18.png


Screenshot from 2016-08-31 16:21:26.png


Baadhi ya Matokeo mengine ya Ripoti hiyo ni kama yafuatayo:-

1. Watoto ambao waliacha shule, 62% ni wavulana na 38% ni wasichana.

Screenshot from 2016-08-31 16:07:12.png


2. Kiwango cha elimu ya mama kina uhusiano na uwezo wa watoto kujifunza.

Screenshot from 2016-08-31 16:10:57.png


3. Lengo la 6 kimataifa la kutoa Elimu Bora kwa Wote halijafikiwa

Screenshot from 2016-08-31 16:28:54.png


4. 31% ya walimu hakuwepo shule siku ya tathmini ya Uwezo, kiwango cha juu cha utoro kilikuwa Singida (58%) na cha chini Ruvuma (17%)


5. Wanafunzi walikuwa na majibu tofauti walipoulizwa kuhusu uwepo wa walimu darasani

Screenshot from 2016-08-31 16:38:27.png


6. Uwiano wa wanafunzi kwa mwalimu umeongezeka mara mbili zaidi ya ule wa mwaka 2013

Screenshot from 2016-08-31 16:44:56.png


7. Kuna upungufu mkubwa wa matundu ya vyoo kwenye shule

Screenshot from 2016-08-31 16:51:16.png


8. Kumeendelea kutokuwa na uwiano sawa kwenye mikoa katika idadi ya walimu, vifaa na rasilimali za shule.


Screenshot from 2016-08-31 16:56:29.png
 
Watu walishindwa kupeleka watoto shule kwa sababu hawana uwezo then serikali imeamua kulipia ili wasome.
Bado kuna ugumu wa swali hili maana suluhisho la kudumu ilikuwa ni kuwafanya wazazi masikini wawe na kipato cha kuaminika ili waweze kusomesha watoto wao wenewe!
 
Kwanza hakuna elimu bure,elimu bure ilikuwepo kipindi cha Nyerere ambapo mzazi kazi yake Ilikuwa ni kununua uniform na kumpeleka mtoto shule,madaftari,penseli n.k,mwanafunzi alikuwa ana gawia bure hukohuko shuleni na msosi juu.

Elimu ya sasa ni ya bure kwa kusamehewa elfu ishirini na fedha za mulinzi lakini kwa upande mwingine gharama ambazo wazazi wanagharamia ni kubwa zaidi kuliko hata gharama zilizosamehewa.
 
Bado tupo busy na kukusanya madawati ili wapate pakukaa,ili hali akuna majengo ya kutosha na matundu ya choo
 
Una hoja ila umeshindwa kuiwakilisha!Tatizo lilikuwa elimu ya kulipia na maisha magumu!Kitendo cha kulipia elimu kilikuwa kinaongeza ukali/ugumu wa maisha!Kuna wanafunzi walikuwa wakikosa fursa za kukaa darasani kwa kuwa tu hawajato amichango fulani hovyo kutohudhuria masomo kwa ukamilifu. sasa hiyo hali imefutwa na watoto wana fursa sawa, kwa hiyo ripoti hiyo inafaa sana kuwa baseline survey na baada ya miaka mitano ya elimu bure utafiti mwingine ufanyike kuona kama bado sababu hizo zingali na mashiko katika elimu na kwa kiwango gani
 
Tukundane, Nilipoanza kusoma comment yako nilifikiri umewaza kiuchumi kuwa hakuna cha bure ila hata gharama ambazo zinalipwa na serikali ni kwamba watu wngine wamezilipia kupitia kodi zao hata kipindi cha Nyerere hivihivo ni ama kodi za ndani au kodi za wananchi wa mataifa rafiki. Maana cha bure kilichobaki kwa sasa ni Oxygen tu hatulipii labda uwe mgonjwa huwezi pumua una pata ya msaada au uko kwenye ndege usawa ambao hupati oxygen asili. Bahati mbaya sana niliposoma hadi mwisho nikagundua huna msukumo wa kiuchumi bali mahaba ya kisiasa hapo ndo credit yangu kwako nimeifuta huna maana.
 
Bado tupo busy na kukusanya madawati ili wapate pakukaa,ili hali akuna majengo ya kutosha na matundu ya choo
Kwahiyo unashauri nguvu iliyotumika kwenye madawati itumike kwenye madarasa na vyoo? Maana imefanya vizuri tukapata madawati kwa asilimia 110
 
Una hoja ila umeshindwa kuiwakilisha!Tatizo lilikuwa elimu ya kulipia na maisha magumu!Kitendo cha kulipia elimu kilikuwa kinaongeza ukali/ugumu wa maisha!Kuna wanafunzi walikuwa wakikosa fursa za kukaa darasani kwa kuwa tu hawajato amichango fulani hovyo kutohudhuria masomo kwa ukamilifu. sasa hiyo hali imefutwa na watoto wana fursa sawa, kwa hiyo ripoti hiyo inafaa sana kuwa baseline survey na baada ya miaka mitano ya elimu bure utafiti mwingine ufanyike kuona kama bado sababu hizo zingali na mashiko katika elimu na kwa kiwango gani
Sidhani kama ameshindwa kuwakilisha hoja yake. Labda tu hajaiwakilisha vile wewe ulitaka. Ugumu wa maisha na kulipia pesa ya shule ni vitu tofauti. Role zake kwenye kujifunza ni tofauti.
 
Ni wakati wa kujikita katika kutambua kwa nini wanafunzi wanaacha shule; Baadhi ya sababu hizi pia zifuatiliwe:-Njaa, adhabu kali kutoka kwa walimu, ufuatiliaji mdogo kutoka kwa walimu.

Kupunguza utoro wa walimu shuleni: Ukaguzi wa shule urudi kama zamani, siku hizi ukaguzi ni kama haupo kabisa, ninachojua wakaguzi huwa wanatishia kuwa watakuja shuleni lakini hawafiki. Na ilitakiwa kama ni ukaguzi uwe ni wa kushtukiza.

Tanzania katika suala la Elimu tunahitaji transformation na sio kuendelea na mfumo tulionao sasa.
Bila Elimu bora maendeleo ya nchi yetu tutayasikia tuu kwa wengine.
 
Tatizo la utoro linasababishwa na sababu nyingi ikiwemo ufuatiliaji mdogo wa wazazi na walezi, mahusiano hafifu kati ya wazazi na walimu , ukali na adhabu za walimu na kutokuwajibika ipasavyo kwa walimu pamoja na Jamii kutokuwajibika ktk masuala ya elimu . Watoto pia wanahusika kutokana na psychological effects zinazo patikana ktk mitaa,wazazi na Side effects za utandawazi. RAI kwa mzazi inabidituongeze usimamizi wetu kwa watoto pia tuongeze ukaribu na mahusiano Bora na Walimu.
 
toa mifano mwa maeneo ambapo wazazi wanachangia.
Kwanza hakuna elimu bure,elimu bure ilikuwepo kipindi cha Nyerere ambapo mzazi kazi yake Ilikuwa ni kununua uniform na kumpeleka mtoto shule,madaftari,penseli n.k,mwanafunzi alikuwa ana gawia bure hukohuko shuleni na msosi juu.

Elimu ya sasa ni ya bure kwa kusamehewa elfu ishirini na fedha za mulinzi lakini kwa upande mwingine gharama ambazo wazazi wanagharamia ni kubwa zaidi kuliko hata gharama zilizosamehewa.
 
Kwanza hakuna elimu bure,elimu bure ilikuwepo kipindi cha Nyerere ambapo mzazi kazi yake Ilikuwa ni kununua uniform na kumpeleka mtoto shule,madaftari,penseli n.k,mwanafunzi alikuwa ana gawia bure hukohuko shuleni na msosi juu.

Elimu ya sasa ni ya bure kwa kusamehewa elfu ishirini na fedha za mulinzi lakini kwa upande mwingine gharama ambazo wazazi wanagharamia ni kubwa zaidi kuliko hata gharama zilizosamehewa.
Nmependa saini yako mkuu, umetishaa sanaa
 
Hii ratio ya 126:1 mkoan Mara na 83:1 avarage ya taifa Zima wengi waliitarajia baada ya watoto weng kupelekwa shule kwa kua elimu ni bure kabla ya madawati wangeanza na vyoo thn walimu na vitabu mwalimu mmoja hawez fundsha watoto 83 hapo watamaliza wengi lasaba bila kujua kusoma na kuandika pia Tabora dah inaumiza yaan watoto 26 kitabu kimoja. Mimi naona bora watoto wakae chini ila wawe na waalimu na vitabu vya kutosha kuliko kukalia midawati halafu vitabu inakua kama Tabora 26:1 ukijumlisha na mwalimu mmoja watoto 83 nadhan unaelewa output yake hapo
 
Jambo hili lilitaka maandalizi ya kutosha. Sasa maadamu maandaliz hayakufanyika basi twende nalo mdogo-mdogo kama ifuatavyo;
1. Walimu wapelekwe short-courses/refresher course kwa ajili ya kuwakumbusha mabadiliko ya mitaala.
2. Kipaumbele kiwe miundombinu zaidi ya Madawati (sasa tujenge madarasa, ofisi za walimu, nyumba za walimu
3. Maslahi mapana ya walimu (Mishahara minono, posho za uhamisho, likizo & malimbikizo)
4. WAZAZI WACHANGIE (Hakunaga ELIMU BURE kwa nchi isiyo na mizizi imara ya kukusanya kodi)
 
Jambo hili lilitaka maandalizi ya kutosha. Sasa maadamu maandaliz hayakufanyika basi twende nalo mdogo-mdogo kama ifuatavyo;
1. Walimu wapelekwe short-courses/refresher course kwa ajili ya kuwakumbusha mabadiliko ya mitaala.
2. Kipaumbele kiwe miundombinu zaidi ya Madawati (sasa tujenge madarasa, ofisi za walimu, nyumba za walimu
3. Maslahi mapana ya walimu (Mishahara minono, posho za uhamisho, likizo & malimbikizo)
4. WAZAZI WACHANGIE (Hakunaga ELIMU BURE kwa nchi isiyo na mizizi imara ya kukusanya kodi)
Lakini nchi yetu inakusanya kodi za kutosha siku hizi...Tunavuka hadi malengo.
Hilo la wazazi kuchangia mimi siliafiki kwani tumeona ongezeko kubwa la wanafunzi pale elimu ilipotangazwa kuwa bure. Unataka hawa waliofaidika na hili waende wapi?
 
Ni wakati wa kujikita katika kutambua kwa nini wanafunzi wanaacha shule; Baadhi ya sababu hizi pia zifuatiliwe:-Njaa, adhabu kali kutoka kwa walimu, ufuatiliaji mdogo kutoka kwa walimu.

Kupunguza utoro wa walimu shuleni: Ukaguzi wa shule urudi kama zamani, siku hizi ukaguzi ni kama haupo kabisa, ninachojua wakaguzi huwa wanatishia kuwa watakuja shuleni lakini hawafiki. Na ilitakiwa kama ni ukaguzi uwe ni wa kushtukiza.

Tanzania katika suala la Elimu tunahitaji transformation na sio kuendelea na mfumo tulionao sasa.
Bila Elimu bora maendeleo ya nchi yetu tutayasikia tuu kwa wengine.
Tatizo hawa wakaguzi wenyewe ni walimu haohao....Wanatunziana tu siri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom