Moisemusajiografii
JF-Expert Member
- Nov 3, 2013
- 33,884
- 54,119
Hebu tazama vizuri!Sasa ndio naamini kweli Faru John amekufa! Hata picha ya mwanae wameona wasiiiweke! R.I.P
Hebu tazama vizuri!Sasa ndio naamini kweli Faru John amekufa! Hata picha ya mwanae wameona wasiiiweke! R.I.P
Huwa haandiki mwenyewehata Mimi nimeusubiri sana ujumbe wake, pengine yupo busy anaandika hutuba ya keaho
Alieandaa hii picha amemkejeli Rais pakubwa sana...
Sisi ni wafugaji bhanamhh Wanyama wengi kwenye picha moja
Amekosekana faru john
Wewe humuoni juu kidogo ya simba??Si inatakiwa BIG FIVE wawepo? Mbona faru hayupo hapo?? Au ndio faru John alikuwa
Sasa hizo ndio hotuba za kulilia kweli?Umesahau "mniombeee"
Mkuu swali lako ni zuri sana.Mkuu hivi unataka usikie nini kutoka kwa Mh?
Mkuu nmecheka sana, unajua ukiwauliza thematically walioyengeneza hii kadi wanataka kufikisha ujumbe gani sijui kama wanajua, la muhimu wao wamewajibu wale jamaa wa jirani waliotaka kuiba mlima wetu hahaaaa...hapa kazi tumhh Wanyama wengi kwenye picha moja
Kwamba raisi naye ana hadhi ya ....mkuu ama ....hahahaaAlieandaa hii picha amemkejeli Rais pakubwa sana...
Acha kukariri.... Acha maisha ya kuiga....Ishi maisha yako.... akili za yule na yule changanya na zako.. ndio ufanye maamuzi... usifanye kwa kutumia akili zao...Wanajamvi wa JF,
Wakati Marais wa Africa Mashariki leo WAMEHUTUBIA wananchi wao kupitia Radio na Televisheni wakigusia mafanikio na changamoto na nini wanataka kutimiza mwaka wa 2017.
Mimi sijamsikia rais Magufuli akiongea nasi leo sijui ni kwa nini.
RWANDA:
Rais Kagame aliongea kuhusu mafanikio yake akiwaambia VIONGOZI kuwa WANANCHI wana HAKI ya kuuliza MASWALI na KUPEWA MAJIBU ipasavyo pasipo KUSUMBULIWA ili wewe kiongozi uwasaidie.
Wananchi ni HAKI yao kupata HUDUMA BORA na hilo wewe kama kiongozi ni lazima UWAJIBIKE.
UGANDA:
Rais Museveni alianza kwa kutoa RAMBIRAMBI kwa wananchi wote wa Uganda waliofiwa na wapendwa wao mwaka uliopita wa 2016.
Akizungumzia nini atafanya mwaka huu wa 2017 alisema nchi inachangamoto ya maji safi.Na mwaka huu ataweka Water schemes/Maji MABWAWA/ VISIMA katika sehemu100 alizozitaja zitakazotoondoa TATIZO la maji safi nchini mwake.
Aligusia kufufuliwa kwa shirika la ndege na kuhakikisha maisha ya wananchi yana BOREKA zaidi. Aligusia Uchumi, Mafuta na KUSHUSHA gharama za UMEME nk.
KENYA:
Rais Kenyatta aliwashukuru wananchi na kuwatakia mwaka mpya wa baraka. Huku akiwaambia WAPINZANI, "Tufanye kazi pamoja bila kugonganisha wananchi.CHAGUZI huja na kwenda taifa hubaki"
Aliwaambia kwa kuwa ni mwaka wa uchaguzi watu waombe kura kwa amani bila mivurugano.
Kuhusu UFISADI aliwaambia wananchi "Mtaanza kuona watu WAKIFUNGWA" hasa kwa sababu JAJI MKUU mpya ana ARI na NIA ya kupambana na UFISADI.
TANZANIA:
2017 Rais Magufuli HAKUTUHUTUBIA ili tumsililize kama TAIFA ili KUTUPATIA mwelekeo wa mwaka 2017.
Hata jamani kutuambia TUFANYE nini ama serikali inafanya nini ili kuzikabili changamoto tulizonazo kama taifa na KUTUPA MATUMAINI tunapoingia mwaka 2017?
Ni nini kinaendelea ama it is NOT that important?