Je, Rais Magufuli hajali haki za wananchi?

Kessy Wa Kilimanjaro

JF-Expert Member
Jan 23, 2016
327
208
Je, Magufuli hajali haki za wananchi? Kama anajali na kama kuna mwenye uwezo wa kumfikia Rais au offisi yake awaambiye hivi:

KABLA YA KUTENGENEZA KATIBA MPYA TUJENGE MSWADA WA HAKI!

Mswada huu utahakikisha kwamba uhuru, haki, na mali za wananchi zitalindwa pale kila sheria mpya inapotungwa na sheria yeyote itakayo tungwa baada ya mswada huu kuandikwa, kama hiyo sheria inapinga hata haki moja ya mswada ifutwe au ibadilishwe.

Zifuatazo ndiyo hizo haki zakulinda na MSWADA WA HAKI.

I. Kila binadamu anaeishi Tanzania awe mgeni au mwenyeji, ana uhuru wa kuishi, kumiliki mali, na kusema kwa uhuru ili mradi asi vunje, asiingilie na asidhuru maisha, uhuru, na mali za binadamu wengine.

II. Serikali haina madaraka ya kuamua, kulazimisha au kupitisha sheria ya jinsi binadamu atakovyoishi, sema, kipi atakacho miliki na nini atakacho fanya na mwili au mali yake mtu yeyote ambaye anaishi kwenye ardhi ya jumuia ya muungano wa Tanzania, ili mradi binadamu huyo hamdhuru binadamu mwingine yeyote wala mali zake, au uhuru na hali yake ya maisha.

III. Kila binadamu anayeishi kwenye ardhi ya Tanzania ana madaraka, uwajibu na uhuru wakulinda mali, uhuai na uhuru wake iwe kutokana na adui yeyote, awe mwenyeji, mgeni au kiongozi anayekiuka mswada huu wa haki na anayeingilia kati ya uhuru wa huyo binadamu, au mali yake au aina yake ya maisha.

IV. Kila binadamu anayemiliki mali kwenye ardhi ya muungano wa jamuhuri ya Tanzania ana madaraka, uwajibu na uhuru wa kumiliki silaa ili aweze kujilinda yeye na nchi yake ikibidi kutokana na yeyote anayetaka kudhuru uhuru, mali au hali ya maisha ya yeye au wananchi wenzake hatakama huyo adui ni kiongozi anayeipinga Mswada wa Haki. Kama mwananchi atatumia silaa yake kwajili ya uhalifu na ikathibitiswa, serikali ina madaraka ya kumnyang'anya huyo binadamu hiyo silaa.

V. Kila binadamu anayeishi kwenye ardhi ya Tanzania ana uhuru wa kuamua cha kufanya na mali yake, na ana madaraka ya kuamua nani anaweza kuingia, kuigusa au kujihusisha kwenye mali yake. Mali yeyote iliyopatikana kihalali na kama mmiliki anaweza kuthibitisha umiliki wake wa hii mali, serikali haina madaraka ya kunyang'anya, kuingilia, kujihusisha au kuitaifisha hii mali.

VI. Serikali haina madaraka ya kumuweka jela au kumchukulia hatua za nguvu mtuhumiwa yeyote ambaye hajamdhuru binadamu mwingine wala kumuumiza. Makosa yote ambayo hayajawaathiri binadamu wengine, wala mali zao, wala uhuru wao na maisha yao yatachukuliwa hatua za adhabu ya kutozwa fedha.

VII. Serikali ina wajibu wa kuwajulisha binadamu wote wanaoishi kwenye ardhi ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuhusu sheria yeyote inayotaka kuitekeleza na matumizi ya hela za kodi mwezi mmoja kabla ya kuipitisha hizo sheria na mipango, kupitia mitandao ya mawasiliano.

VIII. Kama binadamu wanaoishi kwenye ardhi ya Tanzania na wanolipa kodi wakapiga kura kwenye kura ya maoni au dua ili waiondoe sheria ambayo wanaiona siyo halali na katika hizo kura zaidi ya asilimia 60% wakaamua kuiondoa hiyo sheria, serikali ina wajibu wa kuiondoa hiyo sheria.

IX. Raisi hana madaraka ya kuanzisha vita, kuupinga Mswada wa haki, kumnyang'anya binadamu yeyote kwenye ardhi ya Tanzania mali yake, wala uhuru wake, wala kupitisha sheria ya kulazimisha aina ya kuishi kwa mtu yeyote Tanzania.

X. Kiongozi, yeyote, sheria yeyote na mwananchi yeyote wa Tanzania anaye upinga mswada huu wa haki au anayeingilia haki yeyote ya binadamu yeyote wa Tanzania kwa kutumia nguvu, uhalifu au njia za vitisho anapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria.
 
Je, Magufuli hajali haki za wananchi? Kama anajali na kama kuna mwenye uwezo wa kumfikia Rais au offisi yake awaambiye hivi:

KABLA YA KUTENGENEZA KATIBA MPYA TUJENGE MSWADA WA HAKI!

Mswada huu utahakikisha kwamba uhuru, haki, na mali za wananchi zitalindwa pale kila sheria mpya inapotungwa na sheria yeyote itakayo tungwa baada ya mswada huu kuandikwa, kama hiyo sheria inapinga hata haki moja ya mswada ifutwe au ibadilishwe.

Zifuatazo ndiyo hizo haki zakulinda na MSWADA WA HAKI.

I. Kila binadamu anaeishi Tanzania awe mgeni au mwenyeji, ana uhuru wa kuishi, kumiliki mali, na kusema kwa uhuru ili mradi asi vunje, asiingilie na asidhuru maisha, uhuru, na mali za binadamu wengine.

II. Serikali haina madaraka ya kuamua, kulazimisha au kupitisha sheria ya jinsi binadamu atakovyoishi, sema, kipi atakacho miliki na nini atakacho fanya na mwili au mali yake mtu yeyote ambaye anaishi kwenye ardhi ya jumuia ya muungano wa Tanzania, ili mradi binadamu huyo hamdhuru binadamu mwingine yeyote wala mali zake, au uhuru na hali yake ya maisha.

III. Kila binadamu anayeishi kwenye ardhi ya Tanzania ana madaraka, uwajibu na uhuru wakulinda mali, uhuai na uhuru wake iwe kutokana na adui yeyote, awe mwenyeji, mgeni au kiongozi anayekiuka mswada huu wa haki na anayeingilia kati ya uhuru wa huyo binadamu, au mali yake au aina yake ya maisha.

IV. Kila binadamu anayemiliki mali kwenye ardhi ya muungano wa jamuhuri ya Tanzania ana madaraka, uwajibu na uhuru wa kumiliki silaa ili aweze kujilinda yeye na nchi yake ikibidi kutokana na yeyote anayetaka kudhuru uhuru, mali au hali ya maisha ya yeye au wananchi wenzake hatakama huyo adui ni kiongozi anayeipinga Mswada wa Haki. Kama mwananchi atatumia silaa yake kwajili ya uhalifu na ikathibitiswa, serikali ina madaraka ya kumnyang'anya huyo binadamu hiyo silaa.

V. Kila binadamu anayeishi kwenye ardhi ya Tanzania ana uhuru wa kuamua cha kufanya na mali yake, na ana madaraka ya kuamua nani anaweza kuingia, kuigusa au kujihusisha kwenye mali yake. Mali yeyote iliyopatikana kihalali na kama mmiliki anaweza kuthibitisha umiliki wake wa hii mali, serikali haina madaraka ya kunyang'anya, kuingilia, kujihusisha au kuitaifisha hii mali.

VI. Serikali haina madaraka ya kumuweka jela au kumchukulia hatua za nguvu mtuhumiwa yeyote ambaye hajamdhuru binadamu mwingine wala kumuumiza. Makosa yote ambayo hayajawaathiri binadamu wengine, wala mali zao, wala uhuru wao na maisha yao yatachukuliwa hatua za adhabu ya kutozwa fedha.

VII. Serikali ina wajibu wa kuwajulisha binadamu wote wanaoishi kwenye ardhi ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuhusu sheria yeyote inayotaka kuitekeleza na matumizi ya hela za kodi mwezi mmoja kabla ya kuipitisha hizo sheria na mipango, kupitia mitandao ya mawasiliano.

VIII. Kama binadamu wanaoishi kwenye ardhi ya Tanzania na wanolipa kodi wakapiga kura kwenye kura ya maoni au dua ili waiondoe sheria ambayo wanaiona siyo halali na katika hizo kura zaidi ya asilimia 60% wakaamua kuiondoa hiyo sheria, serikali ina wajibu wa kuiondoa hiyo sheria.

IX. Raisi hana madaraka ya kuanzisha vita, kuupinga Mswada wa haki, kumnyang'anya binadamu yeyote kwenye ardhi ya Tanzania mali yake, wala uhuru wake, wala kupitisha sheria ya kulazimisha aina ya kuishi kwa mtu yeyote Tanzania.

X. Kiongozi, yeyote, sheria yeyote na mwananchi yeyote wa Tanzania anaye upinga mswada huu wa haki au anayeingilia haki yeyote ya binadamu yeyote wa Tanzania kwa kutumia nguvu, uhalifu au njia za vitisho anapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria.

Hakuna point ambayo haijazingumziwa kwenye katiba na kanuni mbalimbali ambazo Kwa sasa zipo... Tatizo ni kutozifahamu na kufanya mambo bila kujali mipaka kisha kulalamika Haki zinakukwa.....
 
Nafikiri mwandishi sio msomi wa sheria, kama ukipata nafasi tafuta hata certificate ya sheria itakusaidia kujua uandike nini juu ya mambo yahusuyo sheria
 
Back
Top Bottom