Je, Papa ndiye mrithi wa mtakatifu Petro?

Je, Papa ndiye mrithi wa mtakatifu Petro?

Kurunzi

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2009
Posts
10,196
Reaction score
11,623
Je, Papa Ndiye “Mrithi wa Mtakatifu Petro”?

*MNAMO 2002,* Papa Yohana Paulo wa Pili alimwandikia barua askofu wa Limburg, huko Ujerumani, akifutilia mbali uamuzi uliofanywa na askofu huyo kuhusu suala la kutoa mimba. Papa alianza kutoa maagizo yake kwa kusema kwamba anawajibu wa kuhakikisha kuwa “makanisa yote yako katika hali njema na yana umoja kulingana na mapenzi ya Yesu Kristo.” Alidai kuwa ana mamlaka ya kufutilia mbali uamuzi uliofanywa na askofu huyo kwa sababu akiwa papa, yeye ndiye “mrithi wa Mtakatifu Petro.”
Kulingana na tafsiri fulani ya Kanisa Katoliki, “Kristo alimweka rasmi Mt. Petro kuwa mkuu wa mitume wote.” Kanisa Katoliki linaendelea kudai kwamba “Kristo alisema kwamba Petro anapaswa kuwa na watu watakaomrithi katika cheo hicho; na kwamba maaskofu Waroma ndio warithi wake. _”—New Catholic Encyclopedia (2003), Buku la 11, ukurasa wa 495-496._

Hayo ni madai mazito. Je, wewe mwenyewe umewahi kuchunguza ukweli wa madai hayo? Ona majibu ya maswali haya matatu: *(1) Je, Biblia inaunga mkono dai la kwamba Petro alikuwa ndiye papa wa kwanza? (2) Historia inaonyesha nini kuhusu chanzo cha mfuatano wa mapapa? (3) Je, mwenendo na mafundisho ya mapapa yanaunga mkono dai lao la kwamba wao ni warithi wa Petro?*

*Je, Petro Ndiye Aliyekuwa Papa wa Kwanza?*

Ili kuthibitisha kwamba kanisa limejengwa juu ya Petro, kwa muda mrefu Wakatoliki wametegemeza madai yao katika maneno ya Yesu kwenye Mathayo 16:18: “Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu.” (Union Version) Hata maneno hayo yameandikwa kwa Kilatini chini ya dari la kanisa linaloitwa St. Peter’s Basilica huko Rome.

Agustino, Baba wa Kanisa aliyeheshimiwa sana, wakati fulani alisema kanisa limejengwa juu ya Petro. Hata hivyo, mwishoni mwa maisha yake alibadili maoni yake kuhusu maana ya maneno hayo ya Yesu. Kwenye kitabu kinachoitwa Retractations, Agustino alisema kwamba kanisa, yaani, kutaniko la Kikristo, limejengwa juu ya Yesu na si juu ya Petro.*

Ni kweli kwamba mtume Petro anatajwa sana katika vitabu vya Injili. Yesu aliwachagua mitume wake watatu—Yohana, Yakobo, na Petro—wawe pamoja naye kushuhudia matukio kadhaa ya pekee. (Marko 5:37, 38; 9:2; 14:33) Yesu alimkabidhi Petro “funguo za ufalme wa mbinguni,” ambazo alitumia kufungua njia ya kuelekea kwenye Ufalme—kwanza kwa Wayahudi na watu waliogeuzwa imani, kisha Wasamaria, na hatimaye Watu wa Mataifa. (Mathayo 16:19; Matendo 2:5, 41; 8:14-17; 10:45) Kwa sababu Petro alikuwa mchangamfu na alipenda kuongea na watu, mara kwa mara alitumika akiwa msemaji wa mitume wote. (Matendo 1:15; 2:14) Hata hivyo, je, mambo hayo yalimfanya Petro kuwa kiongozi wa kutaniko la kwanza?

Ni kweli kwamba mtume Paulo aliandika kuwa Petro alikabidhiwa “utume kwa wale waliotahiriwa.” (Wagalatia 2:8) Hata hivyo, muktadha wa maneno hayo unaonyesha kwamba Paulo hakuwa akimaanisha kuwa Petro ndiye kiongozi wa kutaniko. Maneno ya Paulo yalihusu jukumu la Petro katika kazi ya kuwahubiria Wayahudi.

Ingawa Petro alipewa majukumu makubwa, hakuna mahali popote katika Biblia ambapo anadai kuwa yeye ndiye kiongozi wa kutaniko, na hivyo kufanya maamuzi kwa ajili ya mitume wale wengine wote. Katika barua zake alijiita “mtume” na “mwanamume mzee,” naye hakuongeza jambo lingine lolote.—1 Petro 1:1; 5:1.

*Historia Inaonyesha Nini Kuhusu Chanzo cha Upapa?*

Wazo la kuwa na mapapa lilianza jinsi gani na wakati gani? Wazo la kwamba ilikuwa sawa kwa mtu mmoja kuwa na madaraka juu ya waamini wenzake lilianza wakati mitume walipokuwa wangali hai. Mitume walikuwa na maoni gani kuhusu jambo hilo?

Mtume Petro mwenyewe aliwaambia wanaume waliokuwa wakiongoza katika makutaniko wasiwe ‘wakipiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu’; walipaswa kuwa wanyenyekevu kwa mmoja na mwenzake. (1 Petro 5:1-5) Mtume Paulo alionya kwamba katika kutaniko, watu wangesimama ambao ‘wangesema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.’ (Matendo 20:30) Mwishoni mwa karne ya kwanza W.K., mtume Yohana aliandika barua ambamo alimshutumu vikali mwanafunzi aliyeitwa Diotrefe. Kwa nini? Sababu moja ni kwamba mwanamume huyo ‘alipenda kuwa na mahali pa kwanza’ kutanikoni. (3 Yohana 9) Shauri kama hilo kutoka kwa mitume lilikuwa kama kizuizi, likizuia kwa muda tamaa ya wale waliotaka kuwa na madaraka.*2 Wathesalonike 2:3-8*.

Muda mfupi baada ya mtume wa mwisho kufa, watu mbalimbali walianza kupata mamlaka. Kitabu The Cambridge History of Christianity kinasema: “Huenda hakukuwa na askofu aliyekuwa na nguvu au mamlaka huko Roma mwanzoni mwa karne ya pili.” Kufikia karne ya tatu, askofu wa Roma alijifanya mwenyewe kuwa ndiye mamlaka kuu, kwenye makanisa fulani.* Ili kuongezea uzito lile dai la kwamba askofu wa Roma ana mamlaka kubwa, watu fulani wamekusanya orodha ya mapapa waliomrithi Petro.

Hata hivyo, orodha hiyo haiwezi kuthibitisha dai hilo. Kwa nini? Kwanza, baadhi ya majina kwenye orodha hiyo hayawezi kuthibitishwa. Zaidi ya hilo, msingi wa orodha hiyo una makosa. Jinsi gani? Hata ikiwa Petro alihubiri jijini Roma, kama baadhi ya vitabu vya kilimwengu vya karne ya pili na ya tatu vinavyodokeza, hakuna uthibitisho wa kwamba alikuwa kiongozi wa kutaniko huko.

Uthibitisho mmoja wa kwamba Petro hakuwa kiongozi wa kutaniko la Roma ni kwamba wakati mtume Paulo alipoandika barua yake kwa Waroma, aliandika orodha ndefu ya Wakristo waliokuwa huko. Hata hivyo, hakumtaja Petro hata kidogo. *(Waroma 16:1-23)* Ikiwa Petro alikuwa kiongozi wa kutaniko, je, tunaweza kuwazia Paulo akimsahau au kumpuuza?

Ona pia kwamba, karibu na wakati ambapo Petro aliongozwa na roho ya Mungu kuandika barua yake ya kwanza, Paulo alimwandikia Timotheo barua ya pili. Katika barua hiyo, Paulo hakusita kutaja Roma. Paulo aliandika barua sita akiwa Roma, na katika barua hizo zote hakumtaja Petro.

Miaka 30 hivi baada ya Paulo kuandika barua zake, mtume Yohana aliandika barua tatu na kitabu cha Ufunuo. Hakuna mahali popote katika maandishi hayo ambapo Yohana anataja kwamba kutaniko la Roma lilikuwa ndilo maarufu zaidi, wala kumtaja yeyote kuwa kiongozi wa kutaniko hilo ambaye alikuwa na mamlaka kubwa na aliyedai kuwa mrithi wa Petro. Hakuna uthibitisho wowote katika Biblia wala katika historia unaounga mkono dai la kwamba Petro alijiweka mwenyewe kuwa askofu wa kwanza wa kutaniko la Roma.

*Je, Mwenendo na Mafundisho ya Mapapa Yanaunga Mkono Dai Lao?*

Tungetarajia kwamba mtu anayedai kuwa “mrithi wa Mtakatifu Petro” na “Mwakilishi wa Kristo” afuate mwenendo na mafundisho ya Petro na Kristo. Kwa mfano, je, Petro alikubali kutendewa kwa njia ya pekee na waamini wenzake? Hapana. Hakukubali kutukuzwa wala kuitwa majina ya cheo. *(Matendo 10:25, 26)* Namna gani Yesu? Alisema kwamba alikuja kuwahudumia wengine na si kuhudumiwa. *(Mathayo 20:28)* Kinyume cha hilo, mapapa wana sifa gani? Je, wanakataa umaarufu, vyeo vya juu, na kuepuka kuonyesha waziwazi utajiri na mamlaka yao?

Petro na Kristo walikuwa safi kiadili na walichangia amani. Linganisha sifa zao na yale ambayo kitabu kimoja cha marejeo cha Wakatoliki, Lexikon für Theologie und Kirche _(Kamusi ya Theolojia na Kanisa),_ kinavyosema kuhusu Papa Leo wa Kumi: “Alijiingiza katika siasa na mara nyingi aliwapendelea watu wake wa ukoo katika shughuli za biashara na kupenda sana anasa. Kwa kufanya hivyo, Leo wa Kumi alipuuza mambo ya kiroho yaliyokuwa muhimu.” Karl Amon, kasisi Mkatoliki ambaye pia ni profesa wa historia ya kanisa, anasema kwamba habari zilizothibitishwa kuhusu Papa Aleksanda wa Sita zinaonyesha “uovu mwingi, matumizi mabaya ya mamlaka, kununua au kuuza vyeo katika kanisa, na upotovu wa maadili.”
Namna gani mafundisho ya mapapa? Je, yanapatana na mafundisho ya Petro na Kristo? Petro hakuamini kwamba watu wote wema wanaenda mbinguni. Akimrejelea Mfalme mwema Daudi, Petro alisema hivi waziwazi: “Daudi hakupanda mbinguni.” (Matendo 2:34) Wala Petro hakufundisha kwamba watoto wachanga wanapaswa kubatizwa. Badala yake alifundisha kwamba ubatizo ni hatua ambayo mwamini anachukua kwa kuongozwa na dhamiri yake.—1 Petro 3:21.

Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kwamba hakuna yeyote kati yao anayepaswa kuwa mkuu kuliko wengine. Yesu alisema: “Ikiwa mtu yeyote anataka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho kati ya wote na mhudumu wa wote.” (Marko 9:35) Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu aliwapa wafuasi wake agizo hili lililo wazi: “Msiitwe Rabi, kwa maana mwalimu wenu ni mmoja, lakini ninyi nyote ni ndugu. Zaidi ya hayo, msimwite mtu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba yenu ni mmoja, Yule wa mbinguni. Wala msiitwe ‘viongozi,’ kwa maana Kiongozi wenu ni mmoja, Kristo.” (Mathayo 23:1, 8-10)
*Je, unafikiri mapapa wamefuata mafundisho ya Petro na Kristo?*

Wengine wanasema kwamba mtu anaweza kuendelea kuwa papa hata ikiwa haishi kulingana na kanuni za Kikristo. Je, unafikiri hoja hiyo inapatana na akili? Yesu alisema: “Kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini kila mti uliooza huzaa matunda yasiyofaa; mti mzuri hauwezi kuzaa matunda yasiyofaa, wala mti uliooza hauwezi kuzaa matunda mazuri.” Ukitegemea uthibitisho ambao umetolewa, je, unafikiri kwamba Petro au Kristo wangependa kuhusianishwa na matunda ambayo mapapa wametokeza?— *Mathayo 7:17, 18, 21-23*.

Mazungumzo ya Yesu na Petro yalihusu kumtambua Kristo na jukumu lake, na si kuhusu jukumu ambalo Petro angetimiza. *(Mathayo 16:13-17)* Baadaye, Petro mwenyewe alisema kwamba Yesu ndiye mwamba ambao juu yake kutaniko lingejengwa. (1 Petro 2:4-8) Mtume Paulo alithibitisha kuwa Yesu, wala si Petro, ndiye “jiwe la msingi la pembeni” la kutaniko la Kikristo.—Waefeso 2:20.

Yesu na mitume walionya kwamba kutaniko la Kikristo lingevamiwa na watu ambao wangefundisha mafundisho ya uasi. (Mathayo 13:24-30, 36-43; 2 Timotheo 4:3; 2 Petro 2:1; 1 Yohana 2:18) Maneno hayo yalitimia wakati kanisa, au kutaniko, la karne ya pili lilipoanza kukubali mapokeo ya kipagani na kuchanganya mafundisho ya Biblia na falsafa za Wagiriki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je, Papa Ndiye “Mrithi wa Mtakatifu Petro”?

*MNAMO 2002,* Papa Yohana Paulo wa Pili alimwandikia barua askofu wa Limburg, huko Ujerumani, akifutilia mbali uamuzi uliofanywa na askofu huyo kuhusu suala la kutoa mimba. Papa alianza kutoa maagizo yake kwa kusema kwamba anawajibu wa kuhakikisha kuwa “makanisa yote yako katika hali njema na yana umoja kulingana na mapenzi ya Yesu Kristo.” Alidai kuwa ana mamlaka ya kufutilia mbali uamuzi uliofanywa na askofu huyo kwa sababu akiwa papa, yeye ndiye “mrithi wa Mtakatifu Petro.”
Kulingana na tafsiri fulani ya Kanisa Katoliki, “Kristo alimweka rasmi Mt. Petro kuwa mkuu wa mitume wote.” Kanisa Katoliki linaendelea kudai kwamba “Kristo alisema kwamba Petro anapaswa kuwa na watu watakaomrithi katika cheo hicho; na kwamba maaskofu Waroma ndio warithi wake. _”—New Catholic Encyclopedia (2003), Buku la 11, ukurasa wa 495-496._

Hayo ni madai mazito. Je, wewe mwenyewe umewahi kuchunguza ukweli wa madai hayo? Ona majibu ya maswali haya matatu: *(1) Je, Biblia inaunga mkono dai la kwamba Petro alikuwa ndiye papa wa kwanza? (2) Historia inaonyesha nini kuhusu chanzo cha mfuatano wa mapapa? (3) Je, mwenendo na mafundisho ya mapapa yanaunga mkono dai lao la kwamba wao ni warithi wa Petro?*

*Je, Petro Ndiye Aliyekuwa Papa wa Kwanza?*

Ili kuthibitisha kwamba kanisa limejengwa juu ya Petro, kwa muda mrefu Wakatoliki wametegemeza madai yao katika maneno ya Yesu kwenye Mathayo 16:18: “Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu.” (Union Version) Hata maneno hayo yameandikwa kwa Kilatini chini ya dari la kanisa linaloitwa St. Peter’s Basilica huko Rome.

Agustino, Baba wa Kanisa aliyeheshimiwa sana, wakati fulani alisema kanisa limejengwa juu ya Petro. Hata hivyo, mwishoni mwa maisha yake alibadili maoni yake kuhusu maana ya maneno hayo ya Yesu. Kwenye kitabu kinachoitwa Retractations, Agustino alisema kwamba kanisa, yaani, kutaniko la Kikristo, limejengwa juu ya Yesu na si juu ya Petro.*

Ni kweli kwamba mtume Petro anatajwa sana katika vitabu vya Injili. Yesu aliwachagua mitume wake watatu—Yohana, Yakobo, na Petro—wawe pamoja naye kushuhudia matukio kadhaa ya pekee. (Marko 5:37, 38; 9:2; 14:33) Yesu alimkabidhi Petro “funguo za ufalme wa mbinguni,” ambazo alitumia kufungua njia ya kuelekea kwenye Ufalme—kwanza kwa Wayahudi na watu waliogeuzwa imani, kisha Wasamaria, na hatimaye Watu wa Mataifa. (Mathayo 16:19; Matendo 2:5, 41; 8:14-17; 10:45) Kwa sababu Petro alikuwa mchangamfu na alipenda kuongea na watu, mara kwa mara alitumika akiwa msemaji wa mitume wote. (Matendo 1:15; 2:14) Hata hivyo, je, mambo hayo yalimfanya Petro kuwa kiongozi wa kutaniko la kwanza?

Ni kweli kwamba mtume Paulo aliandika kuwa Petro alikabidhiwa “utume kwa wale waliotahiriwa.” (Wagalatia 2:8) Hata hivyo, muktadha wa maneno hayo unaonyesha kwamba Paulo hakuwa akimaanisha kuwa Petro ndiye kiongozi wa kutaniko. Maneno ya Paulo yalihusu jukumu la Petro katika kazi ya kuwahubiria Wayahudi.

Ingawa Petro alipewa majukumu makubwa, hakuna mahali popote katika Biblia ambapo anadai kuwa yeye ndiye kiongozi wa kutaniko, na hivyo kufanya maamuzi kwa ajili ya mitume wale wengine wote. Katika barua zake alijiita “mtume” na “mwanamume mzee,” naye hakuongeza jambo lingine lolote.—1 Petro 1:1; 5:1.

*Historia Inaonyesha Nini Kuhusu Chanzo cha Upapa?*

Wazo la kuwa na mapapa lilianza jinsi gani na wakati gani? Wazo la kwamba ilikuwa sawa kwa mtu mmoja kuwa na madaraka juu ya waamini wenzake lilianza wakati mitume walipokuwa wangali hai. Mitume walikuwa na maoni gani kuhusu jambo hilo?

Mtume Petro mwenyewe aliwaambia wanaume waliokuwa wakiongoza katika makutaniko wasiwe ‘wakipiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu’; walipaswa kuwa wanyenyekevu kwa mmoja na mwenzake. (1 Petro 5:1-5) Mtume Paulo alionya kwamba katika kutaniko, watu wangesimama ambao ‘wangesema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.’ (Matendo 20:30) Mwishoni mwa karne ya kwanza W.K., mtume Yohana aliandika barua ambamo alimshutumu vikali mwanafunzi aliyeitwa Diotrefe. Kwa nini? Sababu moja ni kwamba mwanamume huyo ‘alipenda kuwa na mahali pa kwanza’ kutanikoni. (3 Yohana 9) Shauri kama hilo kutoka kwa mitume lilikuwa kama kizuizi, likizuia kwa muda tamaa ya wale waliotaka kuwa na madaraka.*2 Wathesalonike 2:3-8*.

Muda mfupi baada ya mtume wa mwisho kufa, watu mbalimbali walianza kupata mamlaka. Kitabu The Cambridge History of Christianity kinasema: “Huenda hakukuwa na askofu aliyekuwa na nguvu au mamlaka huko Roma mwanzoni mwa karne ya pili.” Kufikia karne ya tatu, askofu wa Roma alijifanya mwenyewe kuwa ndiye mamlaka kuu, kwenye makanisa fulani.* Ili kuongezea uzito lile dai la kwamba askofu wa Roma ana mamlaka kubwa, watu fulani wamekusanya orodha ya mapapa waliomrithi Petro.

Hata hivyo, orodha hiyo haiwezi kuthibitisha dai hilo. Kwa nini? Kwanza, baadhi ya majina kwenye orodha hiyo hayawezi kuthibitishwa. Zaidi ya hilo, msingi wa orodha hiyo una makosa. Jinsi gani? Hata ikiwa Petro alihubiri jijini Roma, kama baadhi ya vitabu vya kilimwengu vya karne ya pili na ya tatu vinavyodokeza, hakuna uthibitisho wa kwamba alikuwa kiongozi wa kutaniko huko.

Uthibitisho mmoja wa kwamba Petro hakuwa kiongozi wa kutaniko la Roma ni kwamba wakati mtume Paulo alipoandika barua yake kwa Waroma, aliandika orodha ndefu ya Wakristo waliokuwa huko. Hata hivyo, hakumtaja Petro hata kidogo. *(Waroma 16:1-23)* Ikiwa Petro alikuwa kiongozi wa kutaniko, je, tunaweza kuwazia Paulo akimsahau au kumpuuza?

Ona pia kwamba, karibu na wakati ambapo Petro aliongozwa na roho ya Mungu kuandika barua yake ya kwanza, Paulo alimwandikia Timotheo barua ya pili. Katika barua hiyo, Paulo hakusita kutaja Roma. Paulo aliandika barua sita akiwa Roma, na katika barua hizo zote hakumtaja Petro.

Miaka 30 hivi baada ya Paulo kuandika barua zake, mtume Yohana aliandika barua tatu na kitabu cha Ufunuo. Hakuna mahali popote katika maandishi hayo ambapo Yohana anataja kwamba kutaniko la Roma lilikuwa ndilo maarufu zaidi, wala kumtaja yeyote kuwa kiongozi wa kutaniko hilo ambaye alikuwa na mamlaka kubwa na aliyedai kuwa mrithi wa Petro. Hakuna uthibitisho wowote katika Biblia wala katika historia unaounga mkono dai la kwamba Petro alijiweka mwenyewe kuwa askofu wa kwanza wa kutaniko la Roma.

*Je, Mwenendo na Mafundisho ya Mapapa Yanaunga Mkono Dai Lao?*

Tungetarajia kwamba mtu anayedai kuwa “mrithi wa Mtakatifu Petro” na “Mwakilishi wa Kristo” afuate mwenendo na mafundisho ya Petro na Kristo. Kwa mfano, je, Petro alikubali kutendewa kwa njia ya pekee na waamini wenzake? Hapana. Hakukubali kutukuzwa wala kuitwa majina ya cheo. *(Matendo 10:25, 26)* Namna gani Yesu? Alisema kwamba alikuja kuwahudumia wengine na si kuhudumiwa. *(Mathayo 20:28)* Kinyume cha hilo, mapapa wana sifa gani? Je, wanakataa umaarufu, vyeo vya juu, na kuepuka kuonyesha waziwazi utajiri na mamlaka yao?

Petro na Kristo walikuwa safi kiadili na walichangia amani. Linganisha sifa zao na yale ambayo kitabu kimoja cha marejeo cha Wakatoliki, Lexikon für Theologie und Kirche _(Kamusi ya Theolojia na Kanisa),_ kinavyosema kuhusu Papa Leo wa Kumi: “Alijiingiza katika siasa na mara nyingi aliwapendelea watu wake wa ukoo katika shughuli za biashara na kupenda sana anasa. Kwa kufanya hivyo, Leo wa Kumi alipuuza mambo ya kiroho yaliyokuwa muhimu.” Karl Amon, kasisi Mkatoliki ambaye pia ni profesa wa historia ya kanisa, anasema kwamba habari zilizothibitishwa kuhusu Papa Aleksanda wa Sita zinaonyesha “uovu mwingi, matumizi mabaya ya mamlaka, kununua au kuuza vyeo katika kanisa, na upotovu wa maadili.”
Namna gani mafundisho ya mapapa? Je, yanapatana na mafundisho ya Petro na Kristo? Petro hakuamini kwamba watu wote wema wanaenda mbinguni. Akimrejelea Mfalme mwema Daudi, Petro alisema hivi waziwazi: “Daudi hakupanda mbinguni.” (Matendo 2:34) Wala Petro hakufundisha kwamba watoto wachanga wanapaswa kubatizwa. Badala yake alifundisha kwamba ubatizo ni hatua ambayo mwamini anachukua kwa kuongozwa na dhamiri yake.—1 Petro 3:21.

Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kwamba hakuna yeyote kati yao anayepaswa kuwa mkuu kuliko wengine. Yesu alisema: “Ikiwa mtu yeyote anataka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho kati ya wote na mhudumu wa wote.” (Marko 9:35) Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu aliwapa wafuasi wake agizo hili lililo wazi: “Msiitwe Rabi, kwa maana mwalimu wenu ni mmoja, lakini ninyi nyote ni ndugu. Zaidi ya hayo, msimwite mtu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba yenu ni mmoja, Yule wa mbinguni. Wala msiitwe ‘viongozi,’ kwa maana Kiongozi wenu ni mmoja, Kristo.” (Mathayo 23:1, 8-10)
*Je, unafikiri mapapa wamefuata mafundisho ya Petro na Kristo?*

Wengine wanasema kwamba mtu anaweza kuendelea kuwa papa hata ikiwa haishi kulingana na kanuni za Kikristo. Je, unafikiri hoja hiyo inapatana na akili? Yesu alisema: “Kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini kila mti uliooza huzaa matunda yasiyofaa; mti mzuri hauwezi kuzaa matunda yasiyofaa, wala mti uliooza hauwezi kuzaa matunda mazuri.” Ukitegemea uthibitisho ambao umetolewa, je, unafikiri kwamba Petro au Kristo wangependa kuhusianishwa na matunda ambayo mapapa wametokeza?— *Mathayo 7:17, 18, 21-23*.

Mazungumzo ya Yesu na Petro yalihusu kumtambua Kristo na jukumu lake, na si kuhusu jukumu ambalo Petro angetimiza. *(Mathayo 16:13-17)* Baadaye, Petro mwenyewe alisema kwamba Yesu ndiye mwamba ambao juu yake kutaniko lingejengwa. (1 Petro 2:4-8) Mtume Paulo alithibitisha kuwa Yesu, wala si Petro, ndiye “jiwe la msingi la pembeni” la kutaniko la Kikristo.—Waefeso 2:20.

Yesu na mitume walionya kwamba kutaniko la Kikristo lingevamiwa na watu ambao wangefundisha mafundisho ya uasi. (Mathayo 13:24-30, 36-43; 2 Timotheo 4:3; 2 Petro 2:1; 1 Yohana 2:18) Maneno hayo yalitimia wakati kanisa, au kutaniko, la karne ya pili lilipoanza kukubali mapokeo ya kipagani na kuchanganya mafundisho ya Biblia na falsafa za Wagiriki.

Sent using Jamii Forums mobile app

ndugu nimesoma hilo andiko lote hapo juu na kugundua yafuatayo.....

HUFAHAMU VYEMA TAMADUNI NA MILA ZA KIYAHUDI KWA WAKATI WA YESU, PIA MAISHA NA WAJIBU WA MARABI ENZI ZA YESU NA HUMFAHAMU VYEMA PETRO MTUME NA KHALIFA WA KRISTO MWENYEWE....

bahati mbaya nasikitika kukwambia kuwa KUNA VITU NA MAMBO YA MSINGI KATIKA MAISHA YA YESU NA UTAMADUNI WA KIYAHUDI (KWA MWALIMU/RABI KUWA NA WANAFUNZI NA MKUBWA WAO) LAZIMA UTAKUWA HUVIFAHAMU.......

na nadhani ndio chanzo hasa cha madai yako kuhusu PETRO NA KANISA KATOLIKI AMBAYO KWA KIASI KIKUBWA UMEDANGANYA NA NI UZUSHI AMBAO UNATAKIWA USAHIHISHWE....

SO, ninapenda kujibu maswali yako na kutolea ufafanuzi uliosahihi wa madai yako kwa kuanza kwanza na MITUME WA YESU JINSI NA KWANINI ALIWACHAGUA NA LENGO LA YEYE KUA NA HAO WANAFUNZI 12 NA MWISHO TUMUONE PETRO MWENYEWE JAPO KIUFUPI (hivyo vitu mkuu hujavizingatia kabisa kabla ya kuleta hiyo thread yako)...........

Basi, ili kupata majibu ya kuridhisha na sahihi kwa maswali yako yote, nimeona ni vyema nitoe kwanza maelezo mafupi juu ya utamaduni wa wayahudi na jambo la uanafunzi au ufuasi na kwa upande wa Yesu tunasikia neno Mitume.......

MITUME WA YESU, KWANINI MITUME 12, NA MALENGO YA YESU JUU YA HAO MITUME 12 NINI HASA

Hivi ndivyo ilivyokuwa kwa Yesu kuchagua idadi ya mitume 12. Yesu ni Mungu na alichokifanya alifanya kwa mapenzi yake

Ndugu tunaposikia wazo wanafunzi, wafuasi au mitume inafaa kwanza tulitangulize wazo la rabi.

Kama ilivyo sisi siku hizi kwamba kama kuna wanafunzi lazima kuwepo pia na mwalimu anayewafundisha hao wanafunzi, au kama kuna wafuasi basi lazima pawepo na mtu wanayemfuata. Hali kadharika, kama kuna mitume lazima pawepo na mtu anayewatuma

Kwa upande wa Wayahudi, rabi ndiye aliyekuwa mwalimu wa wanafunzi na hivyo hao aliowafundisha waliitwa wafuasi; waliitwa wanafunzi

Wakati ule kulikuwa na marabi wengi tu na kila rabi alikuwa na wanafunzi wake, kumbe kila rabi alikuwa na wale waliomfuata na mara nyingi huyo mwalimu yaani rabi alitangulia mbele na hao wanafunzi walimfuata kwa nyuma

Hii ndiyo sababu unaposoma Mk. 8:32 – 34 Yesu anapomwambia Petro kuwa arudi nyuma shetani, maana yake Petro alitangulia mbele.

Kumbe Petro kama mwanafunzi alipaswa kuwa nyuma aone yale ambayo mwalimu wake alikuwa akiyafanya. Alipaswa kufahamu kuwa wakati ule mwalimu alikuwa mmoja tu yaani Yesu.......

Historia ya urabi na uanafunzi kwa wayahudi ilianza rasmi kipindi ambacho wayahudi waliongozwa na Ezra baada ya kutoka utumwani Babiloni.

Kipindi hicho, watu walijitoa rasmi maisha yao yote kujifunza Maandiko Matakatifu, kuyafafanua na kuyazingirisha katika maisha yao ya kila siku.

Sasa, ili mmoja aonekane kuwa mtaalamu, mafunzo hao yalianza utotoni ambapo kijana wa kiume alimtafuta mwalimu wa sheria anayemtaka, na kumwomba ampokee kama mwanafunzi wake

Mwalimu alichunguza uwezo wa mwanafunzi kama anafaa kisha alimchukua. Mwanafunzi huyo alijiaminisha kwa mwalimu huyo kwa miaka kama ishirini hadi thelathini na ili kuonekana kuwa tayari mwanafunzi huyo ameiva kwa ujuzi na hekima, alitakiwa atimize miaka walau 40 na hapo ndipo mwalimu wake alimwekea mikono na jamii ikamtambua kama ni mwalimu wa Maandiko Matakatifu

Ishara ya nje urabi au ualimu ilikuwa ni kuvaa kanzu ndefu (Mk. 12:38 – 40) na hivyo watu walikuwa wanamsalimu kila alipokuwa wanapita. Hao marabi waliheshimiwa sana na watu.

Baada ya kuwa rabi (yaani mtalaamu wa Maandiko Matakatifu) mmoja alitakiwa kushika miiko kama hii;
kutoongea na mwanamke yeyote hadharani,
kutoshindwa swali lolote ambalo angeulizwa na watu, kutogusana na watu walionekana kuwa najisi au wenye dhambi kama vile wakoma, wanawake walio hedhini. n.k.

Kwa upande wa Yesu, Biblia inamtaja kuwa alikuwa rabi (Yoh. 1:38). Pia tunasikia mafarisayo wanamwita Yesu mwalimu pale walipomletea mwanamke aliyefumaniwa kwa uzinzi (Yoh. 8:4).

Hata hivyo, Biblia haituambii kuwa Yesu alipataje kuwa rabi/mwalimu. Na tunaona watu wanashangaa kuwa aliwezaje kupata hekima ile - yaani kuweza kufundisha kama rabi wakati hakupata kuwa mwanafunzi wa rabi yeyote katika Uyahudi. Ukisoma enjili ya Marko 6:2-3 inaonekana watu wa nyumbani kwake wanamshangaa. Cha ajabu zaidi, tunasikia kwamba alipokuwa na miaka 12 tu alishaanza kuuliza na kujibu maswali ya wazee. (Lk, 2:46 – 47).

Ndiyo kusema, alipata urabi wa kuzaliwa nao. Hukuupata urabi kwa kusotea kama walivyofanya marabi wengine.

Kwa hiyo, Yesu alishaonekana kuwa rabi na hivyo alikuwa na wafuasi wake au wanafunzi wake kama ambavyo marabi wengine walikuwa na wanafunzi.

Tofauti ya wanafunzi wa Yesu na wale wa marabi wengine ni kwamba, wale wa marabi wengine kwanza walikuwa wanaume tu na pili wao wenyewe wanafunzi ndiyo waliowachagua marabi;

kumbe kwa upande wa Yesu, Yesu mwenyewe ndiye aliyewachagua na hao wanafunzi walikuwa wa kike na wakiume.

Hata hivyo, tofauti nyingine ya wanafunzi wa marabi wengine na wa Yesu ni kwamba, wanafunzi wa Yesu walikuwa wa makundi mawili:

kulikuwa na wafuasi au wanafunzi wa kawaida (yaani wale ambao walimfuata ili kusikiliza mafundisho yake, kwa vile walivutiwa nayo na walivutiwa pia na alivyokuwa anaishi).

Hawa walikuwa wengi na ni wanaume na wanawake (Lk. 8:2). Mfano wa wanawake wanaotajwa ni Maria Magdarena, Yoana mke wa Kuza, Mfanyakazi Mkuu wa Herode na Susana.

Baada ya kundi hili la wafuasi lilikuwa kundi lingine la pili nalo liliundwa na wanaume 12 waliochaguliwa na Yesu mwenyewe kutoka miongoni mwa wale wafuasi wengi, kama tusomavyo hapa,

“Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akisali. Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akawachagua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume: Simoni (ambaye alimpa jina Petro), na Andrea ndugu yake Yakobo, na Yohane, Filipo na Barthromayo, Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo, na Simoni (aliyeitwa Zelote), Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.” Mwisho wa kunukuu (Lk. 6:12 – 15)

Aliwaita mitume kwa sababu aliwataka si tu wasikilize yale aliyowafundisha na kubaki nayo, bali pia wao aliwataka wakawafundishe na watu wengine. Kwa maneno mengine, aliwataka wajue kusudi awatume wayatangaza yale aliyowaambia; yale waliyoyaona kwake. Anapowaita anasema,
“Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani, Nendeni basi, mkawafanye watu wote kuwa wanafunzi wangu mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Wafundisheni kuyashika maagizo yote niliyowapeni.” (Mt. 28:19 – 20).
(MKUU UPO MPAKA HAPO....)

Kumbe hawa wanafunzi 12 ambao ndiyo tunawaita mitume, hakukuwa na mwanamke hata mmoja. Wote walikuwa wanaume watupu.

TUZIDI KUSONGA MBELE ILI KUUTAFUTA UKWELI ULIO HALISI.....

Kwa nini idadi ya mitume 12 na si vinginevyo na inawakilisha nini ????

idadi 12 ya wale mitume inawakilisha nini au kwa nini wawe 12 na si 24, 40, 50, n.k.......

ndugu yangu idadi hiyo ya kumi na mbili kwa kweli jibu la msingi kabisa ni kwamba Yeye anajua ni kwa nini aliwachagua kwa idadi hiyo kumi na mbili haikuwa kwa ajali tu,

ndiyo maana baada ya kupaa mbinguni mitume walimchagua Mathias achukuea nafasi ya Yuda Iskarioti ili kutimiza idadi hiyo ya kumi na mbili. (Mdo. 1:20 – 26). Huyu Yuda alijinyonga baada ya kumsaliti Yesu. (Mdo. 1:18 – 19).

Namba hiyo 12 ni idadi sawa ya makabila 12 ya wana wa Israeli; wana wa Yakobo ambao toka kwao ndiyo taifa la Israeli lilizaliwa pale mlimani Sinai kwa kupewa zile amri kumi kama katiba.

Wale watoto kumi na mbili wa Yakobo ambao majini yao si mbaya kama nikiyataja hapa: Reubeni, Simeoni, Yuda, Zabuloni, Isakari, Dani, Gadi, Asheri, Naftari, Yosefu, Lawi, na Yosefu. Haya ndiyo makabila kumi na mawili ya watoto wa Yakobo walioingia katika nchi ya Kanaani na kuirithi ila nchi ambayo baba yao Ibrahimu aliahidiwa na Mungu. (Mwa. 13:1 – 18).

Kumbe sasa, anapofika Yesu, anaanzisha taifa jipya la wakristo ambao wanatokana na hao mitume kumi na mbili kama vile taifa la Israeli lilivyoanza na watu 12. Sikia hapa mtume Petro anavyosema.
nanukuu:
“Lakini ninyi ni ukoo mteule, makuhani wa mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani.” (1Pet. 2:9).

Kwa hiyo taifa jipya la wakristo, ambalo urithi wao si tena wa Yerusalemu la Kanaani, bali Yerusalemu ya Mbinguni. (Ufun. 21:9 – 14).

Hivyo idadi yao si 24 au 40 au 50 kwa sababu wanaoashiriwa ni watu 12 wa Agano la Kale na hawa wanaanza Agano Jipya. Watu wa taifa jipya ambalo hatima yake si kama ile ya zamani, bali mpya – mbinguni.

(HICHO KIPANDE HAPO JUUKINAWEZA KUWA NI MOJA JIBU NA UFAFANUZI KATIKA MADAI YAKO)

Mwisho wa hiki kipande cha mitume napenda kufafanua kifupi juu ya uhusiano wa mitume 12 na Kanisa la sasa.(KATOLIKI)

Yesu aliteua mitume wale kumi na mbili ili washiriki ukuhani wake kama viongozi wa Kanisa. Wao walipewa mamlaka hayo chini ya kiongozi wao Simoni Petro (Mt. 16:13 – 19).

Kumbe hao mitume ndiyo maaskofu wakisaidiwa na mapadre wa leo hii chini ya kiongozi wao Baba Mtakatifu kama ndiye halifa wa Petro.

Kwa upande mwingine, wale wote waliompokea Yesu, huitwa wafuasi wake. Hawa ni sawa na wale wafuasi wengine wa Yesu ambao hawakuwa mitume.

Hawa nao wanashiriki ukuhani wa Kristo lakini si kama Kristo mwenyewe katika maaskofu na mapadre.

Wao wanashiriki kwa ushuhuda wa maisha yao na kutangaza neno la Mungu. Kundi hili ni la wabatizwa wote. Wao wana upadre/ukuhani wa wate. Wenzetu waingereza wanauita Common Priesthood. (1Pet. 2:9; Rev. 1:6).

tusonge mbele katika kuutafuta ukweli na uhalisia wa PETRO na kanisa KATOLIKI....

sasa naomba tumtazame MTUME PETRO (KHALIFA WA KWANZA WA KRISTO) JAPO KIUFUPI MAISHA YAKE MPAKA KIFO CHAKE.....


Petro alifia wapi na kwa sababu gani na nini kiliendelea baada ya hapo


Ni kweli kabisa kwamba kama walivyo binadamu wengine, Petro alizaliwa na kuishi, kipindi na muda wake wa kuishi ulipomalizika alikufa.

Petro mtume ndiye alikabidhiwa kanisa na Bwana wetu Yesu Kristo kabla ya kifo na ufufuko wake rej.Mt 16:18.

Jina lake halisi lilikuwa Simon Bar-Yona mwenyeji wa Galilaya.Kazi yake ilikuwa ni uvuvi kabla hajaitwa kuvua watu kama tunavyosoma Mt 4:18-20.

Pamoja na kwamba Petro anatufundisha mambo mengi,Biblia haituelezi mwisho wa maisha yake.Tunachoambiwa ni kwamba,baada ya mitume kumpokea Roho Mtakatifu,siku ile ya pentekoste walianza kazi ya Kutangaza habari za ufufuko wa Yesu.

Kazi ya kutangaza habari za ufufuko wa Yesu ilikuwa ngumu na iliwabidi mitume wasambae huko na huko ili kueneza habari hiyo kwa watu.Habari za mitume na kazi zao baada ya kumpokea Roho Mtakatifu tunazipata kutoka katika kitabu cha Matendo ya mitume.

Sasa,kuhusiana na Petro,maelezo ya wazi kutoka katika Biblia Takatifu yanaanza pale tunapoelezwa juu ya Philip ambaye baada ya kumpokea Roho Mtakatifu alienda hadi Samaria na huko akafanikiwa kupata wafuasi wengi.

Aliporudi kanisa la Yerusalemu likamtuma Petro ili akatoe msaada zaidi huko rej.Mdo 8:14-16,baada ya hapo tunaambiwa kwamba Petro alikwenda hadi Kaisaria akambatiza Kornelio rej.Mdo 9:32,

halafu alipotoka huko Petro alirudi Yerusalemu akakamatwa na Herode Agrippa akafungwa rej Mdo 12:1-3,na baada ya kuokolewa kwa muujiza na malaika toka gerezani,Biblia inatuambia kwamba aliamua kuwa mhubiri wa mataifa rej.Mdo12:17-19.

Maelezo hayo ndiyo yaliyo wazi kabisa kutoka katika Biblia yetu.Hapa ndipo sasa utajiri wa kanisa katoliki unapodhihirishwa wazi linapotumia vyanzo vikuu viwili vya mafundisho ya imani yaani Biblia Takatifu na Mapokeo.Utajiri tulionao kutoka katika mapokeo ndio unaoweza kutufanya kupata na kujua mambo na habari muhimu kuhusu petro.

Watu wa madhehebu mengine yasiyo ya kikatoliki hawana na hawapendi kutumia chanzo hiki cha mafundisho ya imani yaani mapokeo ndiyo maana kwao inaweza kuwa vigumu kujua kama alikufa na kuzikwa mahali fulani ingawa wanaamini kwamba aliishi kwani hilo halimo katika Biblia Takatifu.

Kutokana na mapokeo Petro baada ya kutoka Yerusalemu inasadikika kwamba alikwenda kati ya Antiokia au Alexandria.Ndiyo maana ukisoma Mdo 15:7-11 pale katika mkutano wa Yerusalemu Petro anaongea kama mmisionari na ukisoma pia Gal 2:7-8 Petro anatajwa kama mtu aliyewahubiria wayahudi.

Sasa,alipotoka huko yaani Antiokia au Alexandria ndipo alikwenda Roma na huko akachaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa mitume na Askofu wa kwanza wa Roma.Kama kiongozi wa Roma Petro alifanya kazi katika mazingira magumu maana ilimbidi apingane na utawala wa kirumi uliokuwa chini ya Nero aliyekuwa adui wa wakristo.

Mababa wa kanisa yaani wale ambao walikuwa wanafunzi wa mitume au wafuasi wa wanafunzi wa mitume, wanatupatia habari nyingi zaidi kuhusu Petro.Wa kwanza anayetupatia habari hizo ni Clement wa Roma.Huyu ndiye aliyekuwa askofu wa tatu wa Roma baada ya Petro na Linus.

Katika barua yake kwa wakorintho aliyoiandika mwaka 96 BK aliwataarifu wakorintho kwamba Petro na Paulo waliuawa huko Roma na aliyewaua ni Nero kutokana na wivu na chuki kwa kanisa.Ukitaka kuelewa juu ya mateso waliyoyapata hawa wawili naomba usome 2kor 11:23-27.

Baada ya mateso kutoka kwa Nero kuzidi, Petro aliamua kutoroka kutoka Roma.Mapokeo yanatudhihirishia kwamba alipokuwa akiondoka kutoka mjini Roma, alikutana na Yesu ndipo Petro akamuuliza Yesu akisema, “ QUO VADIS”,tafsiri yake “unakwenda wapi”?.Yesu akamjibu, “nakwenda huko Roma unakotoka nikasulibiwe tena”.

Hapo Petro alijisikia vibaya kuona kwamba anayakimbia mateso aliyokubali kuyapokea siku alipokubali kwa dhati kuwa mfuasi wa Yesu.Akaamua kurudi tena Roma.

Baba wa kanisa Tacitus katika maandishi yake anasema kwamba aliporudi Roma alikamatwa na kusulibiwa akachagua kuteswa msalabani kichwa chini miguu juu maana Petro mwenyewe alisema kwamba hakustahili kusulibiwa kama Bwana wake Yesu Kristo.

Baada ya kifo chake, Petro alizikwa mahali ambapo leo hii kanisa linalojulikana kama kanisa la Mt Petro limejengwa yaani huko Vatican Roma. Kinachotuthibitishia hilo ni kile kilichotokea mwaka 1939 hadi 1949 wakati kanisa hilo la Mt.Petro lilipokuwa likifanyiwa ukarabati.

Wajenzi waliligundua kaburi lake na kwa uhakika wote walielewa kwamba ndilo hasa lenyewe walipokuta ukuta mwekundu wenye maandishi ya kigiriki yaliyosomeka, “PETROS ENI ” tafsiri yake kwa kiingereza ni“PETER IS INSIDE”,na kwa kiswahili,“PETRO YUMO NDANI”.

Mwaka 1950 siku ya Krismasi Baba mtakatifu Papa Pius XII alithibitisha hilo.Mambo haya ya kale sisi tunashindwa kuyaelewa kwa urahisi kwa sababu hatujihusishi sana nayo kama ndugu zetu wa nchi zilizoendelea wale wanaoitwa archeologists.


MWISHO NAOMBA UELEWE KUWA BABA MTAKATIFU AU PAPA NI NANI HASA

naomba nieleze kinagaubaga kuhusu Baba Mtakatifu au Papa ni nani, sawia na mamlaka yake katika Kanisa Katoliki.

P
apa au Baba Mtakatifu ni wakili wa Yesu Kristo, Halifa wa Mtume Petro, Mkuu wa Kanisa Katoliki, Askofu wa jimbo la Roma, na Baba wa Kanisa la Magharibi ambalo kabla ya Mtaguso wa Mkuu wa pili wa Vaticano, lilitumia lugha ya Kilatini katika Ibada zake. Zaidi ya hapo Baba Mtakatifu ni Mkuu wa Jimbo la Kanisa la Italia na ni Rais wa Nchi ndogo ya Vaticani.

Kadiri ya Imani Katoliki, cheo cha Baba Mtakatifu kinatokana na ujumbe aliopewa Mtume Petro na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe. Mtume Petro, kufuatana na ushahidi dhahiri alikufa Roma, na kaburi lake liligunduliwa chini ya Altare kuu ya Kanisa la Mtakatifu Petro huko Roma.

Tukirejea kwenye sheria za Kanisa Katoliki ambazo ni ufafanuzi wa zile amri Kumi za Mungu, sheria namba 331, inasema hivi nanukuu; “Askofu wa Kanisa la Roma ambaye katika yeye inadumu ofisi iliyokabidhiwa na Bwana kwa Petro mwenyewe, wa kwanza katika Mitume na inayopaswa kupitishwa kwa Mahalifa wake ni Mkuu wa jopo la Maaskofu, wakili wa Kristo na mchungaji wa Kanisa zima hapa duniani; hivyo kwa dhati ya ofisi yake anayo madaraka ya kawaida, ya juu, kamili, yanayojitegemea, naya jumla katika Kanisa, ambayo anaweza daima kuyatumia kwa uhuru”. Mwisho wa nukuu.

Pia sheria ya Kanisa Katoliki namba 333, inasema, nanukuu; “Baba Mtakatifu hupata madaraka kamili na ya juu katika Kanisa kwa njia ya uchaguzi halali alioukubali mwenyewe pamoja na kupewa uaskofu. Hivyo Yule aliye Askofu tayari hupata madaraka hayo tangu wakati anapokubali uchaguzi wake kuwa Baba Mtakatifu. Lakini kama Yule aliyechaguliwa hana uaskofu, anabidika kupewa uaskofu mara moja”. Mwisho wa nukuu, hata hivyo kifungu cha pili cha sheria hiyo namba 333, kinasema hivi, nanukuu, “Ikitokea kuwa Baba Mtakatifu anajiuzulu ofisi yake, ili iwe halali inatakiwa ajiuzulu kwa hiari na tendo hilo lidhihirishwe ipaswavyo, lakini si kwamba likubaliwe na yeyote”. Mwisho wa nukuu.

baada ya maelezo hayo mafupi kuhusu Baba Mtakatifu kama ni nani na wadhifa wake katika Kanisa Katoliki, naomba sasa twnde kwenye chimbuko la jina papa

chimbuko la jina hili Papa, hadi wakawa wanapewa viongozi hawa wa dunia wa Kanisa Katoliki, ni kwamba jina hili Papa ni neno la Kiitaliano ambalo limetokana na neno la Kigiriki Pappas, ambalo kwa kiingereza ni Fadher na Baba kwa lugha yetu ya Kiswahili.

Neno hili Papa lilitumiwa na Mapadre wa Makanisa ya Kigiriki. Na hapo ndipo sasa Mababa wa Kanisa Katoliki wakaona ni jina linalofaa apewe kiongozi wa dunia wa Kanisa Katoliki, yaani Baba Mtakatifu, kulingana na hadhi yake kama Baba wa Wakatoliki wote duniani.

Baba Mtakatifu ni kilele cha muundo wote wa daraja za Kanisa, na uwezo wote wa kimuundo katika Kanisa unatoka kwake, na hivyo tunaweza kusema ni sawa na Baba wa familia katika hali ya kawaida, kuwa yeye ni kichwa cha familia na anayo madaraka yote ya ndani ya familia ile. Ndivyo ilivyo kwa

Baba Mtakatifu kama halifa wa Mtume Petro, Askofu wa Roma, wakili wa Yesu Kristo hapa duniani na mkubwa wa Kanisa Katoliki (rej. Mt 16:18-19; Yn 10:16). Nanukuu, “Nami nakuambia: Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga Kanisa langu, wala milango ya kuzimu haitalishinda.
Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lolote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”.
Mwisho wa nukuu (rej. Mt 16:18-19).

Zaidi ya hapo, zamani hizo, jina hili Papa (yaani Baba), lilitolewa kwa Maaskofu, na lilitumiwa sana katika mzingo wa Kimonaki na likawa jina la kawaida kwa Mapadre wa Kanisa la Orthodoksi na pia Mapadre wa sehemu fulani za Kanisa Katoliki la Roma.

Na huko Misri jina hilo Papa lilikuwa ni haki ya Askofu wa Alexandria tu. Lakini kuanzia katikati ya karne ya sita (6th c), na kuendelea hadi hivi leo, jina hilo Papa limewekwa maalumu kwa ajili ya Askofu wa Roma tu, yaani kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani. Na utume huo uliwekwa kisheria na Baba Mtakatifu Gregori wa VII.

Sanjali na hilo kuna sababu za kimazingira kuwa Waitaliano ndiyo waliopokea mafundisho ya Mitume wenye sifa bora, nao ni Mtume Paulo na Mtume Petro ambaye alikuwa kiongozi wa Mitume na halifa wa Yesu Kristo.

Inasadikika kwamba Mitume hao wakuu yaani Perto na Paulo waliacha mafundisho ya Yesu mikononi mwa Waroma na ndiyo maana mpaka leo hii makao makuu ya Kanisa Katoliki yapo Roma. Kutokana na mapokeo ya Kanisa sisi tunajua kwamba Mtume Petro kama kiongozi wa Kanisa la Roma alikamatwa na Mfalme Nero pamoja na Paulo Mtume na Wakristo wengine wengi.

Na baada ya kufungwa katika gereza la Mamertino, Petro alisulubiwa katika shamba la kuzikia lililokuwa katika ukingo wa mlima Vatikano mwaka Sitini na Saba (67), na hivyo Wakristo wa zamani walijenga kumbukumbu hapo.

Tena, mara baada ya Mfalme Mkuu Konstantino kutoa uhuru wa dini, Wakristo kwa msaada wa Kaisari huyo walijenga Kanisa la kwanza juu ya kaburi la Mtume Petro, wakiliacha kaburi chini ya Altare. Na kwa udhibitisho walichimba kwa miaka mingi chini ya Altare ya Kanisa la Mtume Petro, na mwisho wakafika kwenye kaburi lenyewe kwa kukuta maneno “Petro iki” yaani Petro yu hapa.


Ndugu ili kudhibitisha ukuu wa Kanisa la Roma mapokeo yanasema ;

Askofu wa Lione (Ufaransa), mwaka 115, Mt. Ireneo aliyekuwa mfuasi wa Mt. Polycarpi ambaye ni mwanafunzi wa Mtume Yohane, aliandika maneno yafuatayo katika kitabu chake kinachoitwa Dhidi ya Waasi sura ya II.

Nanukuu, “Mafundisho ya Mitume duniani kote yaweza kupatikana katika kila Kanisa, na kila mtu anaweza kuyapata, sisi tunaweza kuleta orodha ya Maaskofu waliopata cheo kutoka kwa mitume na mahalifa wao, mfuatano hadi siku hizi zetu. Lakini ingekuwa kazi ya kuchosha mno kuleta katika kitabu hiki mfuatano huo wa Mitume katika Kanisa. Ni bora nilete mapokea ya kitume na mafundisho ya imani ya Kanisa kubwa zaidi, ya zamani zaidi na lililojulikana kwa watu wote, ambalo liliwekwa kwa kimsingi huko Roma na Mitume wenye sifa bora, yaani Petro na Paulo. Kanisa hili limefika kwetu hadi leo kwa njia ya mfuatano wa Maaskofu na Mahalifa wao. Sasa basi kila Kanisa, yaani waamini wa duniani kote lazima wakubaliane na kushirikiana na Kanisa la Roma, kwa sababu ya cheo chake bora sana”. Mwisho wa nukuu.

Na zaidi ya hapo kuna uhakika kuwa mapokeo ya Mitume yanahifadhiwa huko Roma na baada ya Mitume waadhama kuweka misingi ya Kanisa la Roma na kuliongoza, uaskofu walipitisha wao kwa Linus kwa ajili ya uongozi wa Kanisa zima. Linus huyu ni Yule anayekumbukwa na Mtume Paulo katika waraka wake wa pili kwa Timotheo, (rej. 2Tim 4:21).

ndugu kutokana na ukweli huo kuwa misingi ya Kanisa Katoliki iliwekwa Roma na Mitume hao maarufu, yaani Petro na Paulo, bila shaka utakubaliana nami kuwa Waitaliano ni moja ya watu walioachiwa Kanisa na kuchukua jukumu la kuendeleza kazi ya uenezaji wa neno la Mungu duniani kote, kama ilivyokuwa ujumbe wa Kristo mwenyewe kwa Mitume wake.
Nanukuu, “Basi, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi. Na tazama mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”. Mwisho wa nukuu (rej. Mt 28:19-20).

Kwa udhibitisho wa hilo na mengi zaidi ya hayo nilio kueleza toka mwanzo unaweza kutafuta na kukisoma kitabu chenye kichwa cha habari PAPA NI NANI, kilichoandikwa na Padre Medri na Padre Magnus Lunyungu ambaye

MKUU NAAMINI KUWA NITAKUWA NIMEKUJIBU VEMA KABISA HAYO MASWALI YAKO NA KUKUPATIA UFAFANUZI WA KWELI NA ILIO HALISI

AHSANTE..............
 
ndugu nimesoma hilo andiko lote hapo juu.......

bahati mbaya nasikitika kukwambia kuwa KUNA VITU NA MAMBO YA MSINGI KATIKA MAISHA YA YESU NA UTAMADUNI WA KIYAHUDI (KWA MWALIMU/RABI KUWA NA WANAFUNZI NA MKUBWA WAO) LAZIMA UTAKUWA HUVIFAHAMU.......

na nadhani ndio chanzo hasa cha madai yako kuhusu PETRO NA KANISA KATOLIKI AMBAYO KWA KIASI KIKUBWA UMEDANGANYA NA NI UZUSHI AMBAO UNATAKIWA USAHIHISHWE....

SO, ninapenda kujibu maswali yako na kutolea ufafanuzi uliosahihi wa madai yako kwa kuanza kwanza na MITUME WA YESU JINSI NA KWANINI ALIWACHAGUA NA LENGO LA YEYE KUA NA HAO WANAFUNZI 12 NA MWISHO TUMUONE PETRO MWENYEWE JAPO KIUFUPI (hivyo vitu mkuu hujavizingatia kabisa kabla ya kuleta hiyo thread yako)...........

Basi, ili kupata majibu ya kuridhisha na sahihi kwa maswali yako yote, nimeona ni vyema nitoe kwanza maelezo mafupi juu ya utamaduni wa wayahudi na jambo la uanafunzi au ufuasi na kwa upande wa Yesu tunasikia neno Mitume.......

MITUME WA YESU, KWANINI 12, NA MALENGO YA YESU JUU YA HAO MITUME 12

Hivi ndivyo ilivyokuwa kwa Yesu kuchagua idadi ya mitume 12. Yesu ni Mungu na alichokifanya alifanya kwa mapenzi yake.............

Ndugu tunaposikia wazo wanafunzi, wafuasi au mitume inafaa kwanza tulitangulize wazo la rabi. Kama ilivyo sisi siku hizi kwamba kama kuna wanafunzi lazima kuwepo pia na mwalimu anayewafundisha hao wanafunzi, au kama kuna wafuasi basi lazima pawepo na mtu wanayemfuata. Hali kadharika, kama kuna mitume lazima pawepo na mtu anayewatuma...

Kwa upande wa Wayahudi, rabi ndiye aliyekuwa mwalimu wa wanafunzi na hivyo hao aliowafundisha waliitwa wafuasi; waliitwa wanafunzi.......


Wakati ule kulikuwa na marabi wengi tu na kila rabi alikuwa na wanafunzi wake, kumbe kila rabi alikuwa na wale waliomfuata na mara nyingi huyo mwalimu yaani rabi alitangulia mbele na hao wanafunzi walimfuata kwa nyuma......

Hii ndiyo sababu unaposoma Mk. 8:32 – 34 Yesu anapomwambia Petro kuwa arudi nyuma shetani, maana yake Petro alitangulia mbele. Kumbe Petro kama mwanafunzi alipaswa kuwa nyuma aone yale ambayo mwalimu wake alikuwa akiyafanya. Alipaswa kufahamu kuwa wakati ule mwalimu alikuwa mmoja tu yaani Yesu.......

Historia ya urabi na uanafunzi kwa wayahudi ilianza rasmi kipindi ambacho wayahudi waliongozwa na Ezra baada ya kutoka utumwani Babiloni. .....

Kipindi hicho, watu walijitoa rasmi maisha yao yote kujifunza Maandiko Matakatifu, kuyafafanua na kuyazingirisha katika maisha yao ya kila siku. Sasa, ili mmoja aonekane kuwa mtaalamu, mafunzo hao yalianza utotoni ambapo kijana wa kiume alimtafuta mwalimu wa sheria anayemtaka, na kumwomba ampokee kama mwanafunzi wake......

Mwalimu alichunguza uwezo wa mwanafunzi kama anafaa kisha alimchukua. Mwanafunzi huyo alijiaminisha kwa mwalimu huyo kwa miaka kama ishirini hadi thelathini na ili kuonekana kuwa tayari mwanafunzi huyo ameiva kwa ujuzi na hekima, alitakiwa atimize miaka walau 40 na hapo ndipo mwalimu wake alimwekea mikono na jamii ikamtambua kama ni mwalimu wa Maandiko Matakatifu

Ishara ya nje urabi au ualimu ilikuwa ni kuvaa kanzu ndefu (Mk. 12:38 – 40) na hivyo watu walikuwa wanamsalimu kila alipokuwa wanapita. Hao marabi waliheshimiwa sana na watu.

Baada ya kuwa rabi (yaani mtalaamu wa Maandiko Matakatifu) mmoja alitakiwa kushika miiko kama hii; kutoongea na mwanamke yeyote hadharani, kutoshindwa swali lolote ambalo angeulizwa na watu, kutogusana na watu walionekana kuwa najisi au wenye dhambi kama vile wakoma, wanawake walio hedhini. n.k.

Kwa upande wa Yesu, Biblia inamtaja kuwa alikuwa rabi (Yoh. 1:38). Pia tunasikia mafarisayo wanamwita Yesu mwalimu pale walipomletea mwanamke aliyefumaniwa kwa uzinzi (Yoh. 8:4).

Hata hivyo, Biblia haituambii kuwa Yesu alipataje kuwa rabi/mwalimu. Na tunaona watu wanashangaa kuwa aliwezaje kupata hekima ile - yaani kuweza kufundisha kama rabi wakati hakupata kuwa mwanafunzi wa rabi yeyote katika Uyahudi. Ukisoma enjili ya Marko 6:2-3 inaonekana watu wa nyumbani kwake wanamshangaa. Cha ajabu zaidi, tunasikia kwamba alipokuwa na miaka 12 tu alishaanza kuuliza na kujibu maswali ya wazee. (Lk, 2:46 – 47).

Ndiyo kusema, alipata urabi wa kuzaliwa nao. Hukuupata urabi kwa kusotea kama walivyofanya marabi wengine.

Kwa hiyo, Yesu alishaonekana kuwa rabi na hivyo alikuwa na wafuasi wake au wanafunzi wake kama ambavyo marabi wengine walikuwa na wanafunzi.

Tofauti ya wanafunzi wa Yesu na wale wa marabi wengine ni kwamba, wale wa marabi wengine kwanza walikuwa wanaume tu na pili wao wenyewe wanafunzi ndiyo waliowachagua marabi;

kumbe kwa upande wa Yesu, Yesu mwenyewe ndiye aliyewachagua na hao wanafunzi walikuwa wa kike na wakiume.

Hata hivyo, tofauti nyingine ya wanafunzi wa marabi wengine na wa Yesu ni kwamba, wanafunzi wa Yesu walikuwa wa makundi mawili: kulikuwa na wafuasi au wanafunzi wa kawaida (yaani wale ambao walimfuata ili kusikiliza mafundisho yake, kwa vile walivutiwa nayo na walivutiwa pia na alivyokuwa anaishi).

Hawa walikuwa wengi na ni wanaume na wanawake (Lk. 8:2). Mfano wa wanawake wanaotajwa ni Maria Magdarena, Yoana mke wa Kuza, Mfanyakazi Mkuu wa Herode na Susana.

Baada ya kundi hili la wafuasi lilikuwa kundi lingine la pili nalo liliundwa na wanaume 12 waliochaguliwa na Yesu mwenyewe kutoka miongoni mwa wale wafuasi wengi, kama tusomavyo hapa,

“Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akisali. Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akawachagua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume: Simoni (ambaye alimpa jina Petro), na Andrea ndugu yake Yakobo, na Yohane, Filipo na Barthromayo, Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo, na Simoni (aliyeitwa Zelote), Yuda wa Yakobo na

Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.” Mwisho wa kunukuu (Lk. 6:12 – 15)
Aliwaita mitume kwa sababu aliwataka si tu wasikilize yale aliyowafundisha na kubaki nayo, bali pia wao aliwataka wakawafundishe na watu wengine. Kwa maneno mengine, aliwataka wajue kusudi awatume wayatangaza yale aliyowaambia; yale waliyoyaona kwake. Anapowaita anasema,

“Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani, Nendeni basi, mkawafanye watu wote kuwa wanafunzi wangu mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Wafundisheni kuyashika maagizo yote niliyowapeni.” (Mt. 28:19 – 20).

Kumbe hawa wanafunzi 12 ambao ndiyo tunawaita mitume, hakukuwa na mwanamke hata mmoja. Wote walikuwa wanaume watupu.

“Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akisali. Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao waliwachagua watu kumi na mbili ambao aliwaita mitume.”

Kwa nini idadi ya mitume 12 na si vinginevyo na inawakilisha nini ????
idadi 12 ya wale mitume inawakilisha nini au kwa nini wawe 12 na si 24, 40, 50, n.k.......

ndugu yangu idadi hiyo ya kumi na mbili kwa kweli jibu la msingi kabisa ni kwamba Yeye anajua ni kwa nini aliwachagua kwa idadi hiyo kumi na mbili haikuwa kwa ajali tu, ndiyo maana baada ya kupaa mbinguni mitume walimchagua Mathias achukuea nafasi ya Yuda Iskarioti ili kutimiza idadi hiyo ya kumi na mbili.

(Mdo. 1:20 – 26). Huyu Yuda alijinyonga baada ya kumsaliti Yesu. (Mdo. 1:18 – 19).

Namba hiyo 12 ni idadi sawa ya makabila 12 ya wana wa Israeli; wana wa Yakobo ambao toka kwao ndiyo taifa la Israeli lilizaliwa pale mlimani Sinai kwa kupewa zile amri kumi kama katiba.

Wale watoto kumi na mbili wa Yakobo ambao majini yao si mbaya kama nikiyataja hapa: Reubeni, Simeoni, Yuda, Zabuloni, Isakari, Dani, Gadi, Asheri, Naftari, Yosefu, Lawi, na Yosefu. Haya ndiyo makabila kumi na mawili ya watoto wa Yakobo walioingia katika nchi ya Kanaani na kuirithi ila nchi ambayo baba yao Ibrahimu aliahidiwa na Mungu. (Mwa. 13:1 – 18).

Kumbe sasa, anapofika Yesu, anaanzisha taifa jipya la wakristo ambao wanatokana na hao mitume kumi na mbili kama vile taifa la Israeli lilivyoanza na watu 12. Sikia hapa mtume Petro anavyosema.

“Lakini ninyi ni ukoo mteule, makuhani wa mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani.” (1Pet. 2:9).

Kwa hiyo taifa jipya la wakristo, ambalo urithi wao si tena wa Yerusalemu la Kanaani, bali Yerusalemu ya Mbinguni. (Ufun. 21:9 – 14).

Hivyo idadi yao si 24 au 40 au 50 kwa sababu wanaoashiriwa ni watu 12 wa Agano la Kale na hawa wanaanza Agano Jipya. Watu wa taifa jipya ambalo hatima yake si kama ile ya zamani, bali mpya – mbinguni.

Mwisho wa hiki kipande cha mitume napenda kufafanua kifupi juu ya uhusiano wa mitume 12 na Kanisa la sasa.

Yesu aliteua mitume wale kumi na mbili ili washiriki ukuhani wake kama viongozi wa Kanisa. Wao walipewa mamlaka hayo chini ya kiongozi wao Simoni Petro (Mt. 16:13 – 19).

Kumbe hao mitume ndiyo maaskofu wakisaidiwa na mapadre wa leo hii chini ya kiongozi wao Baba Mtakatifu kama ndiye halifa wa Petro.

Kwa upande mwingine, wale wote waliompokea Yesu, huitwa wafuasi wake. Hawa ni sawa na wale wafuasi wengine wa Yesu ambao hawakuwa mitume. Hawa nao wanashiriki ukuhani wa Kristo lakini si kama Kristo mwenyewe katika maaskofu na mapadre. Wao wanashiriki kwa ushuhuda wa maisha yao na kutangaza neno la Mungu. Kundi hili ni la wabatizwa wote. Wao wana upadre/ukuhani wa wate. Wenzetu waingereza wanauita Common Priesthood. (1Pet. 2:9; Rev. 1:6).

ATAEFUATA HAPO NI PETRO MWENYEWE......
NA MWISHO UFAFANUZI HALISI/KWELI WA MASWALI NA MAMAELEZO YAKO
Naomba number yako Tafadhali... Nimependezwa na Ufafanuzi.. Mzuri Naweza kujifunza mengi kutoka kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je, Papa Ndiye “Mrithi wa Mtakatifu Petro”?

*MNAMO 2002,* Papa Yohana Paulo wa Pili alimwandikia barua askofu wa Limburg, huko Ujerumani, akifutilia mbali uamuzi uliofanywa na askofu huyo kuhusu suala la kutoa mimba. Papa alianza kutoa maagizo yake kwa kusema kwamba anawajibu wa kuhakikisha kuwa “makanisa yote yako katika hali njema na yana umoja kulingana na mapenzi ya Yesu Kristo.” Alidai kuwa ana mamlaka ya kufutilia mbali uamuzi uliofanywa na askofu huyo kwa sababu akiwa papa, yeye ndiye “mrithi wa Mtakatifu Petro.”
Kulingana na tafsiri fulani ya Kanisa Katoliki, “Kristo alimweka rasmi Mt. Petro kuwa mkuu wa mitume wote.” Kanisa Katoliki linaendelea kudai kwamba “Kristo alisema kwamba Petro anapaswa kuwa na watu watakaomrithi katika cheo hicho; na kwamba maaskofu Waroma ndio warithi wake. _”—New Catholic Encyclopedia (2003), Buku la 11, ukurasa wa 495-496._

Hayo ni madai mazito. Je, wewe mwenyewe umewahi kuchunguza ukweli wa madai hayo? Ona majibu ya maswali haya matatu: *(1) Je, Biblia inaunga mkono dai la kwamba Petro alikuwa ndiye papa wa kwanza? (2) Historia inaonyesha nini kuhusu chanzo cha mfuatano wa mapapa? (3) Je, mwenendo na mafundisho ya mapapa yanaunga mkono dai lao la kwamba wao ni warithi wa Petro?*

*Je, Petro Ndiye Aliyekuwa Papa wa Kwanza?*

Ili kuthibitisha kwamba kanisa limejengwa juu ya Petro, kwa muda mrefu Wakatoliki wametegemeza madai yao katika maneno ya Yesu kwenye Mathayo 16:18: “Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu.” (Union Version) Hata maneno hayo yameandikwa kwa Kilatini chini ya dari la kanisa linaloitwa St. Peter’s Basilica huko Rome.

Agustino, Baba wa Kanisa aliyeheshimiwa sana, wakati fulani alisema kanisa limejengwa juu ya Petro. Hata hivyo, mwishoni mwa maisha yake alibadili maoni yake kuhusu maana ya maneno hayo ya Yesu. Kwenye kitabu kinachoitwa Retractations, Agustino alisema kwamba kanisa, yaani, kutaniko la Kikristo, limejengwa juu ya Yesu na si juu ya Petro.*

Ni kweli kwamba mtume Petro anatajwa sana katika vitabu vya Injili. Yesu aliwachagua mitume wake watatu—Yohana, Yakobo, na Petro—wawe pamoja naye kushuhudia matukio kadhaa ya pekee. (Marko 5:37, 38; 9:2; 14:33) Yesu alimkabidhi Petro “funguo za ufalme wa mbinguni,” ambazo alitumia kufungua njia ya kuelekea kwenye Ufalme—kwanza kwa Wayahudi na watu waliogeuzwa imani, kisha Wasamaria, na hatimaye Watu wa Mataifa. (Mathayo 16:19; Matendo 2:5, 41; 8:14-17; 10:45) Kwa sababu Petro alikuwa mchangamfu na alipenda kuongea na watu, mara kwa mara alitumika akiwa msemaji wa mitume wote. (Matendo 1:15; 2:14) Hata hivyo, je, mambo hayo yalimfanya Petro kuwa kiongozi wa kutaniko la kwanza?

Ni kweli kwamba mtume Paulo aliandika kuwa Petro alikabidhiwa “utume kwa wale waliotahiriwa.” (Wagalatia 2:8) Hata hivyo, muktadha wa maneno hayo unaonyesha kwamba Paulo hakuwa akimaanisha kuwa Petro ndiye kiongozi wa kutaniko. Maneno ya Paulo yalihusu jukumu la Petro katika kazi ya kuwahubiria Wayahudi.

Ingawa Petro alipewa majukumu makubwa, hakuna mahali popote katika Biblia ambapo anadai kuwa yeye ndiye kiongozi wa kutaniko, na hivyo kufanya maamuzi kwa ajili ya mitume wale wengine wote. Katika barua zake alijiita “mtume” na “mwanamume mzee,” naye hakuongeza jambo lingine lolote.—1 Petro 1:1; 5:1.

*Historia Inaonyesha Nini Kuhusu Chanzo cha Upapa?*

Wazo la kuwa na mapapa lilianza jinsi gani na wakati gani? Wazo la kwamba ilikuwa sawa kwa mtu mmoja kuwa na madaraka juu ya waamini wenzake lilianza wakati mitume walipokuwa wangali hai. Mitume walikuwa na maoni gani kuhusu jambo hilo?

Mtume Petro mwenyewe aliwaambia wanaume waliokuwa wakiongoza katika makutaniko wasiwe ‘wakipiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu’; walipaswa kuwa wanyenyekevu kwa mmoja na mwenzake. (1 Petro 5:1-5) Mtume Paulo alionya kwamba katika kutaniko, watu wangesimama ambao ‘wangesema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.’ (Matendo 20:30) Mwishoni mwa karne ya kwanza W.K., mtume Yohana aliandika barua ambamo alimshutumu vikali mwanafunzi aliyeitwa Diotrefe. Kwa nini? Sababu moja ni kwamba mwanamume huyo ‘alipenda kuwa na mahali pa kwanza’ kutanikoni. (3 Yohana 9) Shauri kama hilo kutoka kwa mitume lilikuwa kama kizuizi, likizuia kwa muda tamaa ya wale waliotaka kuwa na madaraka.*2 Wathesalonike 2:3-8*.

Muda mfupi baada ya mtume wa mwisho kufa, watu mbalimbali walianza kupata mamlaka. Kitabu The Cambridge History of Christianity kinasema: “Huenda hakukuwa na askofu aliyekuwa na nguvu au mamlaka huko Roma mwanzoni mwa karne ya pili.” Kufikia karne ya tatu, askofu wa Roma alijifanya mwenyewe kuwa ndiye mamlaka kuu, kwenye makanisa fulani.* Ili kuongezea uzito lile dai la kwamba askofu wa Roma ana mamlaka kubwa, watu fulani wamekusanya orodha ya mapapa waliomrithi Petro.

Hata hivyo, orodha hiyo haiwezi kuthibitisha dai hilo. Kwa nini? Kwanza, baadhi ya majina kwenye orodha hiyo hayawezi kuthibitishwa. Zaidi ya hilo, msingi wa orodha hiyo una makosa. Jinsi gani? Hata ikiwa Petro alihubiri jijini Roma, kama baadhi ya vitabu vya kilimwengu vya karne ya pili na ya tatu vinavyodokeza, hakuna uthibitisho wa kwamba alikuwa kiongozi wa kutaniko huko.

Uthibitisho mmoja wa kwamba Petro hakuwa kiongozi wa kutaniko la Roma ni kwamba wakati mtume Paulo alipoandika barua yake kwa Waroma, aliandika orodha ndefu ya Wakristo waliokuwa huko. Hata hivyo, hakumtaja Petro hata kidogo. *(Waroma 16:1-23)* Ikiwa Petro alikuwa kiongozi wa kutaniko, je, tunaweza kuwazia Paulo akimsahau au kumpuuza?

Ona pia kwamba, karibu na wakati ambapo Petro aliongozwa na roho ya Mungu kuandika barua yake ya kwanza, Paulo alimwandikia Timotheo barua ya pili. Katika barua hiyo, Paulo hakusita kutaja Roma. Paulo aliandika barua sita akiwa Roma, na katika barua hizo zote hakumtaja Petro.

Miaka 30 hivi baada ya Paulo kuandika barua zake, mtume Yohana aliandika barua tatu na kitabu cha Ufunuo. Hakuna mahali popote katika maandishi hayo ambapo Yohana anataja kwamba kutaniko la Roma lilikuwa ndilo maarufu zaidi, wala kumtaja yeyote kuwa kiongozi wa kutaniko hilo ambaye alikuwa na mamlaka kubwa na aliyedai kuwa mrithi wa Petro. Hakuna uthibitisho wowote katika Biblia wala katika historia unaounga mkono dai la kwamba Petro alijiweka mwenyewe kuwa askofu wa kwanza wa kutaniko la Roma.

*Je, Mwenendo na Mafundisho ya Mapapa Yanaunga Mkono Dai Lao?*

Tungetarajia kwamba mtu anayedai kuwa “mrithi wa Mtakatifu Petro” na “Mwakilishi wa Kristo” afuate mwenendo na mafundisho ya Petro na Kristo. Kwa mfano, je, Petro alikubali kutendewa kwa njia ya pekee na waamini wenzake? Hapana. Hakukubali kutukuzwa wala kuitwa majina ya cheo. *(Matendo 10:25, 26)* Namna gani Yesu? Alisema kwamba alikuja kuwahudumia wengine na si kuhudumiwa. *(Mathayo 20:28)* Kinyume cha hilo, mapapa wana sifa gani? Je, wanakataa umaarufu, vyeo vya juu, na kuepuka kuonyesha waziwazi utajiri na mamlaka yao?

Petro na Kristo walikuwa safi kiadili na walichangia amani. Linganisha sifa zao na yale ambayo kitabu kimoja cha marejeo cha Wakatoliki, Lexikon für Theologie und Kirche _(Kamusi ya Theolojia na Kanisa),_ kinavyosema kuhusu Papa Leo wa Kumi: “Alijiingiza katika siasa na mara nyingi aliwapendelea watu wake wa ukoo katika shughuli za biashara na kupenda sana anasa. Kwa kufanya hivyo, Leo wa Kumi alipuuza mambo ya kiroho yaliyokuwa muhimu.” Karl Amon, kasisi Mkatoliki ambaye pia ni profesa wa historia ya kanisa, anasema kwamba habari zilizothibitishwa kuhusu Papa Aleksanda wa Sita zinaonyesha “uovu mwingi, matumizi mabaya ya mamlaka, kununua au kuuza vyeo katika kanisa, na upotovu wa maadili.”
Namna gani mafundisho ya mapapa? Je, yanapatana na mafundisho ya Petro na Kristo? Petro hakuamini kwamba watu wote wema wanaenda mbinguni. Akimrejelea Mfalme mwema Daudi, Petro alisema hivi waziwazi: “Daudi hakupanda mbinguni.” (Matendo 2:34) Wala Petro hakufundisha kwamba watoto wachanga wanapaswa kubatizwa. Badala yake alifundisha kwamba ubatizo ni hatua ambayo mwamini anachukua kwa kuongozwa na dhamiri yake.—1 Petro 3:21.

Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kwamba hakuna yeyote kati yao anayepaswa kuwa mkuu kuliko wengine. Yesu alisema: “Ikiwa mtu yeyote anataka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho kati ya wote na mhudumu wa wote.” (Marko 9:35) Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu aliwapa wafuasi wake agizo hili lililo wazi: “Msiitwe Rabi, kwa maana mwalimu wenu ni mmoja, lakini ninyi nyote ni ndugu. Zaidi ya hayo, msimwite mtu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba yenu ni mmoja, Yule wa mbinguni. Wala msiitwe ‘viongozi,’ kwa maana Kiongozi wenu ni mmoja, Kristo.” (Mathayo 23:1, 8-10)
*Je, unafikiri mapapa wamefuata mafundisho ya Petro na Kristo?*

Wengine wanasema kwamba mtu anaweza kuendelea kuwa papa hata ikiwa haishi kulingana na kanuni za Kikristo. Je, unafikiri hoja hiyo inapatana na akili? Yesu alisema: “Kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini kila mti uliooza huzaa matunda yasiyofaa; mti mzuri hauwezi kuzaa matunda yasiyofaa, wala mti uliooza hauwezi kuzaa matunda mazuri.” Ukitegemea uthibitisho ambao umetolewa, je, unafikiri kwamba Petro au Kristo wangependa kuhusianishwa na matunda ambayo mapapa wametokeza?— *Mathayo 7:17, 18, 21-23*.

Mazungumzo ya Yesu na Petro yalihusu kumtambua Kristo na jukumu lake, na si kuhusu jukumu ambalo Petro angetimiza. *(Mathayo 16:13-17)* Baadaye, Petro mwenyewe alisema kwamba Yesu ndiye mwamba ambao juu yake kutaniko lingejengwa. (1 Petro 2:4-8) Mtume Paulo alithibitisha kuwa Yesu, wala si Petro, ndiye “jiwe la msingi la pembeni” la kutaniko la Kikristo.—Waefeso 2:20.

Yesu na mitume walionya kwamba kutaniko la Kikristo lingevamiwa na watu ambao wangefundisha mafundisho ya uasi. (Mathayo 13:24-30, 36-43; 2 Timotheo 4:3; 2 Petro 2:1; 1 Yohana 2:18) Maneno hayo yalitimia wakati kanisa, au kutaniko, la karne ya pili lilipoanza kukubali mapokeo ya kipagani na kuchanganya mafundisho ya Biblia na falsafa za Wagiriki.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndugu yangu kuna udhaifu mkubwa sana kwenye maelezo yako.Nimeshindwa hata nikusaidieje.Kwanza tujikumbushe.

JE,UNAFAHAMU ALIYEANZISHA DHEHEBU LAKO?

Kabla ya Mwaka 1517,Kila Mkristo aliuwa Mkatoliki.

Tunafahamu leo ukristo uko hivi:

1.Kama wewe ni Mlutheri ufahamu kwamba Kanisa lako lilianzishwa na Baba Martin Luther,Ujerumani Mwaka 1517 akiwa na Daraja la Upadre Katoliki.

2.Wewe kama ni Mennonite,Fahamu kuwa Kanisa lako lilianzishwa na ndugu Grebel,Mantz na Blaurock mwaka 1525

3.Wewe kama ni Anglikana,Kanisa lako lilianzishwa na Mfalme Henry XIII Mwaka 1534.

4.Kama wewe ni Presbyterian,Kanisa lako lilianzishwa na ndugu John Knox Mwaka 1960.

5.Kama wewe ni Congregationist(Kanisa la Mtaa) Kanisa lako lilianzishwa na ndugu Robert Brown,Uholanzi Mwaka 1583.

6.Kama wewe ni Baptist(Kanisa la Ubatizo),Fahamu kuwa Kanisa lako lilianzishwa na ndugu John Smith,Amsterdam,UholanziMwaka 1606.

7.Kama wewe ni Methodist,Kanisa lako lilianzishwa na John Murray,New jersey,Marekani mwaka 1770.

8.Kama wewe ni Mormo au Malaika Wajao Kanisa lako lilianzishwa na ndugu Joseph,New York,Marekani mwaka 1829.

9.Kama wewe ni Seven Day Adventist(Sabato) fahamu kuwa kanisa lako lilianzishwa Willium Miller Mwaka 1831.

10.Kama wewe ni Jeshi la Wokovu(Salvation Army),Kanisa lako lilianzishwa na ndugu Willium Booth Mwaka 1865.

11.Kama wewe ni Mashahidi wa Yehovah(Jehovah Witness) Kanisa lako lilianzishwa na Charles Russel Mwaka 1872.

12.Kama wewe ni Redeemed Christian Church of God(Marejeo ya Kikristo ya Kanisa la Mungu) unatakiwa kufahamu Kanisa lako lilianzishwa Mwaka 1952 na Josiah Akinayomi.

13.Kama Muumini wa Deeper Lige Bible Church,Kanisa lako lilianzishwa na Pastor William Kumuyi,Lagos Nigeria Mwaka 1973.

14.Kama wewe ni Mountain of Fire(Mlima wa Moto) Kanisa lako lilianzishwa na Daniel Olokoya Mwaka 1952.

15.Kama wewe ni Muumini wa Makanisa ya Askofu Zakaria Kakobe,Mtume na Nabii Josephat Mwingira,Mchungaji Hernandes,Askofu Gwajima nk,ujue kwamba Makanisa hayo yameanzishwa Dar es Salaam miaka ya hivi karibuni.

16.Hapa unaweza kuendelea na kuendelea mpaka Makanisa 43,000 yaliyopo leo.

17.Lakini kama wewe ni Mkatoliki unafahamu kabisa Imani na Kanisa lako vilianzishwa na Yesu Kristo mwenyewe Mwaka 33 kabla ya kupaa kwenda Mbinguni soma Mathayo 16:18 na kuliacha chini ya wanafunzi wake wakiongozwa na Mtume Petro na kutokea kipindi hicho kumekuwa na ukasimishaji wa Baba Watakatifu 266 wa kwanza akiwa Mtume Petro(soma Matendo ya Mitume 2:1) mpaka Yesu atakaporudi tena kadiri ya Maandiko Matakatifu.
Nimeorodhesha historia hii si kudharau Imani yoyote ila kufundisha Historia ya Imani ya Kikristo na kuweka Kumbukumbu sawa.
Kanisa Katoliki linabaki kuwa lilelile aliloanzisha Yesu Kristo na kuliwekea Ekaristi Takatifu kama Baraka ya Mwisho.Tunaendelea kufanya alichoagiza Bwana wetu Yesu Kristo kama alivyoyatoa maneno haya Matakatifu juu ya Mkate na Divai,kuwa tuule Mwili wake na Kuinywa Damu yake na aliagiza kufanya haya kwa kumkumbuka yeye mpaka atakapokuja tena(Mathayo 26:26).
Neno Katoliki maana yake kitu kizima au chote au wote.
Eneza Upendo,Eneza Utengamano na Umoja wa Kiroho aliotuacha nao Yesu Kristo na sio Mgawanyiko.
 
Achana na tunzi za kufikirika za wazungu..soma hapa chini.



UKRISTO

ALEXANDER,THE GREAT(actually the invader/barbarian)

Alexander,The Great(the barbarian,the invader) aliivamia Kemet(Misri) mwaka 332 BC na kumuondoa mfalme(farao) na yeye kuchukua kiti cha ufalme akiwa hajui chochote kuhusu mila na desturi za Misri.

Aliwalazimisha viongozi wa “dini” iliyokuwa inaabudiwa wamkubali katika dini yao,lakini walimkatalia.Alexander mvamizi alikufa mwaka 323 BC.

Mrithi wa Alexander ,Ptolemy I au Soter(maana ya soter ni mwokozi) naye alikataliwa kuwa sehemu ya “dini” ya wamisri wa kipindi hicho lakini katika mji wa Memphis alipata baadhi ya viongozi wa dini waliosaliti na kumkubali.Walimpa jina la SERAPIS kwa kuunganisha majina Osiris na hepis.Huyu Ptelomy I ndiye aliyetibua misingi ya imani ya wamisri wa kipindi hicho.

Ptolemy I au Soter au Serapis au Christus alijipa cheo cha farao,alitengeneza sanamu ya kichwa yenye sura yake na watu wote walilazimishwa kuabudu lile sanamu.Waliomwabudu serapis walikuwa wanaitwa wakristo(neon la Kigiriki Christus)

SERAPIS 350 BC



ARIUS(256-336 A.D)

Alikuwa mmoja wa viongozi wa dini chini ya utawala wa warumi aliyepaza sauti kuwa kuabudu sanamu la serapis haikuwa sawa hivyo watu wote waache kuliabudu.

MKUTANO WA NICEA 325 A.D(the council of nicea)

Uliwakutanisha viongozi wa juu wa dini chini ya uenyekiti wa mfalme Constantine na ajenda kuu ya kwanza ilikuwa ni kumnyamazisha Arius asiendelee kueneza sumu ya kupinga kumuabudu serapis.Katika kipindi chote kulikuwa hakuna mtu anayeitwa yesu(jesus),aliyeabudiwa alikuwa ni serapis soter au mwokozi kwa Kiswahili.

MAAZIMIO YA MKUTANO WA NICEA 325 A.D

Ambapo ilitolewa “statement” ya imani ya kikristo iliandikwa na makasisi(bishops?) wa kanisa la roma wapatao 318.statement(ambayo ni kanuni ya imani kwenye kanisa katoliki la roma) inasomwa ‘nasadiki kwa mungu baba mwenyezi muumba mbingu na dunia,na kwa yesu kristo mwanae wa pekee’(hapa anaongelewa serapis sanamu).

1.Kubadilisha sanamu la serapis na kuweka la yesu

2. Kumfukuza Arius(exile) asiendelee kupinga imani ya warumi




BIBLE’S CONTRADICTIONS

1. Genesis chapter 1

God created adam and eve

Genesis chapter 2

God created adam and then eve later


2. Genesis 2:7 and 2:19

God created a man and then the animals

Genesis 1:24-27

God created the animals first and then a man


3. Genesis 32:30 and numbers 14:14

Men have seen god

John 1:18

No man has seen god


4. Jeremiah 3:12

God does not keep anger forever

Jeremiah 17:4

God does keep anger forever


5. Mathew 1:20

Angel appeared to joseph

Luke 1:28

Angel appeared to mary


6. Mathew 8:5

Centurion came to jesus

Luke 7:3

Centurion sent his elders


7. Mathew 4:5-8

Satan took jesus to temple and then mountain

Luke 4:5-9

Satan took jesus to mountain and then temple


8. Mathew 20:29

9. Two blind men were healed on the road

Mark 10:46-47

One blind man was healed on the road
 
Ndugu yangu kuna udhaifu mkubwa sana kwenye maelezo yako.Nimeshindwa hata nikusaidieje.Kwanza tujikumbushe.

JE,UNAFAHAMU ALIYEANZISHA DHEHEBU LAKO?

Kabla ya Mwaka 1517,Kila Mkristo aliuwa Mkatoliki.

Tunafahamu leo ukristo uko hivi:

1.Kama wewe ni Mlutheri ufahamu kwamba Kanisa lako lilianzishwa na Baba Martin Luther,Ujerumani Mwaka 1517 akiwa na Daraja la Upadre Katoliki.

2.Wewe kama ni Mennonite,Fahamu kuwa Kanisa lako lilianzishwa na ndugu Grebel,Mantz na Blaurock mwaka 1525

3.Wewe kama ni Anglikana,Kanisa lako lilianzishwa na Mfalme Henry XIII Mwaka 1534.

4.Kama wewe ni Presbyterian,Kanisa lako lilianzishwa na ndugu John Knox Mwaka 1960.

5.Kama wewe ni Congregationist(Kanisa la Mtaa) Kanisa lako lilianzishwa na ndugu Robert Brown,Uholanzi Mwaka 1583.

6.Kama wewe ni Baptist(Kanisa la Ubatizo),Fahamu kuwa Kanisa lako lilianzishwa na ndugu John Smith,Amsterdam,UholanziMwaka 1606.

7.Kama wewe ni Methodist,Kanisa lako lilianzishwa na John Murray,New jersey,Marekani mwaka 1770.

8.Kama wewe ni Mormo au Malaika Wajao Kanisa lako lilianzishwa na ndugu Joseph,New York,Marekani mwaka 1829.

9.Kama wewe ni Seven Day Adventist(Sabato) fahamu kuwa kanisa lako lilianzishwa Willium Miller Mwaka 1831.

10.Kama wewe ni Jeshi la Wokovu(Salvation Army),Kanisa lako lilianzishwa na ndugu Willium Booth Mwaka 1865.

11.Kama wewe ni Mashahidi wa Yehovah(Jehovah Witness) Kanisa lako lilianzishwa na Charles Russel Mwaka 1872.

12.Kama wewe ni Redeemed Christian Church of God(Marejeo ya Kikristo ya Kanisa la Mungu) unatakiwa kufahamu Kanisa lako lilianzishwa Mwaka 1952 na Josiah Akinayomi.

13.Kama Muumini wa Deeper Lige Bible Church,Kanisa lako lilianzishwa na Pastor William Kumuyi,Lagos Nigeria Mwaka 1973.

14.Kama wewe ni Mountain of Fire(Mlima wa Moto) Kanisa lako lilianzishwa na Daniel Olokoya Mwaka 1952.

15.Kama wewe ni Muumini wa Makanisa ya Askofu Zakaria Kakobe,Mtume na Nabii Josephat Mwingira,Mchungaji Hernandes,Askofu Gwajima nk,ujue kwamba Makanisa hayo yameanzishwa Dar es Salaam miaka ya hivi karibuni.

16.Hapa unaweza kuendelea na kuendelea mpaka Makanisa 43,000 yaliyopo leo.

17.Lakini kama wewe ni Mkatoliki unafahamu kabisa Imani na Kanisa lako vilianzishwa na Yesu Kristo mwenyewe Mwaka 33 kabla ya kupaa kwenda Mbinguni soma Mathayo 16:18 na kuliacha chini ya wanafunzi wake wakiongozwa na Mtume Petro na kutokea kipindi hicho kumekuwa na ukasimishaji wa Baba Watakatifu 266 wa kwanza akiwa Mtume Petro(soma Matendo ya Mitume 2:1) mpaka Yesu atakaporudi tena kadiri ya Maandiko Matakatifu.
Nimeorodhesha historia hii si kudharau Imani yoyote ila kufundisha Historia ya Imani ya Kikristo na kuweka Kumbukumbu sawa.
Kanisa Katoliki linabaki kuwa lilelile aliloanzisha Yesu Kristo na kuliwekea Ekaristi Takatifu kama Baraka ya Mwisho.Tunaendelea kufanya alichoagiza Bwana wetu Yesu Kristo kama alivyoyatoa maneno haya Matakatifu juu ya Mkate na Divai,kuwa tuule Mwili wake na Kuinywa Damu yake na aliagiza kufanya haya kwa kumkumbuka yeye mpaka atakapokuja tena(Mathayo 26:26).
Neno Katoliki maana yake kitu kizima au chote au wote.
Eneza Upendo,Eneza Utengamano na Umoja wa Kiroho aliotuacha nao Yesu Kristo na sio Mgawanyiko.

UKRISTO

ALEXANDER,THE GREAT(actually the invader/barbarian)

Alexander,The Great(the barbarian,the invader) aliivamia Kemet(Misri) mwaka 332 BC na kumuondoa mfalme(farao) na yeye kuchukua kiti cha ufalme akiwa hajui chochote kuhusu mila na desturi za Misri.

Aliwalazimisha viongozi wa “dini” iliyokuwa inaabudiwa wamkubali katika dini yao,lakini walimkatalia.Alexander mvamizi alikufa mwaka 323 BC.

Mrithi wa Alexander ,Ptolemy I au Soter(maana ya soter ni mwokozi) naye alikataliwa kuwa sehemu ya “dini” ya wamisri wa kipindi hicho lakini katika mji wa Memphis alipata baadhi ya viongozi wa dini waliosaliti na kumkubali.Walimpa jina la SERAPIS kwa kuunganisha majina Osiris na hepis.Huyu Ptelomy I ndiye aliyetibua misingi ya imani ya wamisri wa kipindi hicho.

Ptolemy I au Soter au Serapis au Christus alijipa cheo cha farao,alitengeneza sanamu ya kichwa yenye sura yake na watu wote walilazimishwa kuabudu lile sanamu.Waliomwabudu serapis walikuwa wanaitwa wakristo(neon la Kigiriki Christus)

SERAPIS 350 BC



ARIUS(256-336 A.D)

Alikuwa mmoja wa viongozi wa dini chini ya utawala wa warumi aliyepaza sauti kuwa kuabudu sanamu la serapis haikuwa sawa hivyo watu wote waache kuliabudu.

MKUTANO WA NICEA 325 A.D(the council of nicea)

Uliwakutanisha viongozi wa juu wa dini chini ya uenyekiti wa mfalme Constantine na ajenda kuu ya kwanza ilikuwa ni kumnyamazisha Arius asiendelee kueneza sumu ya kupinga kumuabudu serapis.Katika kipindi chote kulikuwa hakuna mtu anayeitwa yesu(jesus),aliyeabudiwa alikuwa ni serapis soter au mwokozi kwa Kiswahili.

MAAZIMIO YA MKUTANO WA NICEA 325 A.D

Ambapo ilitolewa “statement” ya imani ya kikristo iliandikwa na makasisi(bishops?) wa kanisa la roma wapatao 318.statement(ambayo ni kanuni ya imani kwenye kanisa katoliki la roma) inasomwa ‘nasadiki kwa mungu baba mwenyezi muumba mbingu na dunia,na kwa yesu kristo mwanae wa pekee’(hapa anaongelewa serapis sanamu).

1.Kubadilisha sanamu la serapis na kuweka la yesu

2. Kumfukuza Arius(exile) asiendelee kupinga imani ya warumi
 
UKRISTO

ALEXANDER,THE GREAT(actually the invader/barbarian)

Alexander,The Great(the barbarian,the invader) aliivamia Kemet(Misri) mwaka 332 BC na kumuondoa mfalme(farao) na yeye kuchukua kiti cha ufalme akiwa hajui chochote kuhusu mila na desturi za Misri.

Aliwalazimisha viongozi wa “dini” iliyokuwa inaabudiwa wamkubali katika dini yao,lakini walimkatalia.Alexander mvamizi alikufa mwaka 323 BC.

Mrithi wa Alexander ,Ptolemy I au Soter(maana ya soter ni mwokozi) naye alikataliwa kuwa sehemu ya “dini” ya wamisri wa kipindi hicho lakini katika mji wa Memphis alipata baadhi ya viongozi wa dini waliosaliti na kumkubali.Walimpa jina la SERAPIS kwa kuunganisha majina Osiris na hepis.Huyu Ptelomy I ndiye aliyetibua misingi ya imani ya wamisri wa kipindi hicho.

Ptolemy I au Soter au Serapis au Christus alijipa cheo cha farao,alitengeneza sanamu ya kichwa yenye sura yake na watu wote walilazimishwa kuabudu lile sanamu.Waliomwabudu serapis walikuwa wanaitwa wakristo(neon la Kigiriki Christus)

SERAPIS 350 BC



ARIUS(256-336 A.D)

Alikuwa mmoja wa viongozi wa dini chini ya utawala wa warumi aliyepaza sauti kuwa kuabudu sanamu la serapis haikuwa sawa hivyo watu wote waache kuliabudu.

MKUTANO WA NICEA 325 A.D(the council of nicea)

Uliwakutanisha viongozi wa juu wa dini chini ya uenyekiti wa mfalme Constantine na ajenda kuu ya kwanza ilikuwa ni kumnyamazisha Arius asiendelee kueneza sumu ya kupinga kumuabudu serapis.Katika kipindi chote kulikuwa hakuna mtu anayeitwa yesu(jesus),aliyeabudiwa alikuwa ni serapis soter au mwokozi kwa Kiswahili.

MAAZIMIO YA MKUTANO WA NICEA 325 A.D

Ambapo ilitolewa “statement” ya imani ya kikristo iliandikwa na makasisi(bishops?) wa kanisa la roma wapatao 318.statement(ambayo ni kanuni ya imani kwenye kanisa katoliki la roma) inasomwa ‘nasadiki kwa mungu baba mwenyezi muumba mbingu na dunia,na kwa yesu kristo mwanae wa pekee’(hapa anaongelewa serapis sanamu).

1.Kubadilisha sanamu la serapis na kuweka la yesu

2. Kumfukuza Arius(exile) asiendelee kupinga imani ya warumi
Duuuuu kweli wee mwenzetu upo nyuma sana.hapo tuu juu umeshachanganya mambo kweli kweli. Eti alivamia 332 na akafa 323 inamaana miaka ilikuwa inarudi nyuma au alivamia akiwa maiti. Uongo hujitenga na ukwel mkuu.... Hivi ubishani wa dini utawasaidia nn? Mm naamini kama kanisa katoliki lingekuwa si la kristo lingekuwa lilishajifia siku nyingi maana linavyopigwa mawe na nyundo si mchezo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuuuu kweli wee mwenzetu upo nyuma sana.hapo tuu juu umeshachanganya mambo kweli kweli. Eti alivamia 332 na akafa 323 inamaana miaka ilikuwa inarudi nyuma au alivamia akiwa maiti. Uongo hujitenga na ukwel mkuu.... Hivi ubishani wa dini utawasaidia nn? Mm naamini kama kanisa katoliki lingekuwa si la kristo lingekuwa lilishajifia siku nyingi maana linavyopigwa mawe na nyundo si mchezo

Sent using Jamii Forums mobile app
for you info,miaka zamani ilikuwa inahesabiwa kwa kurudi nyuma...kanisa na ukristo ni uzushi..hakuna ushahidi wowote kuwa mambo ya kwenye biblia yalitokea zaidi ya kucopy mambo ya mataifa mengine
 
Papa ndiye mrithi wa Petro ndio, sasa unachobisha ni nini....
 
SALA NA KAZI

Nilitaka nikuulize maswali kadhaa kutokana na bandiko lako lakini nimeona niache kwanza....

Nina malengo ya kuja kuandika kuhusu kanisa katoliki,nitakachoandika kitakuwa tofauti na hiki alichoandika huyu mleta thread na nadhani tutaweza kubadilishana mawazo huko....

Nimeamua kuacha kukuuliza kwasababu nitakuwa sina haja ya kuja kuandika uzi na kwenye mjadala wa namna hii sitaweza kuandika yote kwa kirefu na kwa kina....

Tuombeane uzima tu mkuu tuje tuwe na mjadala wenye tija wakati huo na tumuombe Mungu atujalie hekima yake....

Kanisa katoliki ni kanisa la aina yake na linavutia sana kwakweli.Kuna mambo mengi sana kulihusu,yapo hasi na chanya....

Ni kanisa linaloonekana kuhusika na Ukristo kwa kiwango kikubwa kabisa....

Lets hope for the best mkuu.....

Tumuombe Mungu atujaalie uzima...

Mungu ni mwema sana....
 
UKRISTO

ALEXANDER,THE GREAT(actually the invader/barbarian)

Alexander,The Great(the barbarian,the invader) aliivamia Kemet(Misri) mwaka 332 BC na kumuondoa mfalme(farao) na yeye kuchukua kiti cha ufalme akiwa hajui chochote kuhusu mila na desturi za Misri.

Aliwalazimisha viongozi wa “dini” iliyokuwa inaabudiwa wamkubali katika dini yao,lakini walimkatalia.Alexander mvamizi alikufa mwaka 323 BC.

Mrithi wa Alexander ,Ptolemy I au Soter(maana ya soter ni mwokozi) naye alikataliwa kuwa sehemu ya “dini” ya wamisri wa kipindi hicho lakini katika mji wa Memphis alipata baadhi ya viongozi wa dini waliosaliti na kumkubali.Walimpa jina la SERAPIS kwa kuunganisha majina Osiris na hepis.Huyu Ptelomy I ndiye aliyetibua misingi ya imani ya wamisri wa kipindi hicho.

Ptolemy I au Soter au Serapis au Christus alijipa cheo cha farao,alitengeneza sanamu ya kichwa yenye sura yake na watu wote walilazimishwa kuabudu lile sanamu.Waliomwabudu serapis walikuwa wanaitwa wakristo(neon la Kigiriki Christus)

SERAPIS 350 BC



ARIUS(256-336 A.D)

Alikuwa mmoja wa viongozi wa dini chini ya utawala wa warumi aliyepaza sauti kuwa kuabudu sanamu la serapis haikuwa sawa hivyo watu wote waache kuliabudu.

MKUTANO WA NICEA 325 A.D(the council of nicea)

Uliwakutanisha viongozi wa juu wa dini chini ya uenyekiti wa mfalme Constantine na ajenda kuu ya kwanza ilikuwa ni kumnyamazisha Arius asiendelee kueneza sumu ya kupinga kumuabudu serapis.Katika kipindi chote kulikuwa hakuna mtu anayeitwa yesu(jesus),aliyeabudiwa alikuwa ni serapis soter au mwokozi kwa Kiswahili.

MAAZIMIO YA MKUTANO WA NICEA 325 A.D

Ambapo ilitolewa “statement” ya imani ya kikristo iliandikwa na makasisi(bishops?) wa kanisa la roma wapatao 318.statement(ambayo ni kanuni ya imani kwenye kanisa katoliki la roma) inasomwa ‘nasadiki kwa mungu baba mwenyezi muumba mbingu na dunia,na kwa yesu kristo mwanae wa pekee’(hapa anaongelewa serapis sanamu).

1.Kubadilisha sanamu la serapis na kuweka la yesu

2. Kumfukuza Arius(exile) asiendelee kupinga imani ya warumi
Kama mtu alivamia mwaka 332 alafu akafa 323 huo pia ni muujiza.
Kwa akili za kibinadamu.hatuwezi kukuelewa.

sent from my BBC using JamiiForums mobile app
 
for you info,miaka zamani ilikuwa inahesabiwa kwa kurudi nyuma...kanisa na ukristo ni uzushi..hakuna ushahidi wowote kuwa mambo ya kwenye biblia yalitokea zaidi ya kucopy mambo ya mataifa mengine
Miaka ilihesabiwa hivyo Mara tu baada ya benchmark ya Yesu kuzaliwa na kufa. Uliyoeleza hapo unamaanisha ilikuwa ni miaka 332 kabla huyo Yesu hajawepo. Lakini unasema Yesu alinganganizwa. Kivipi Wakati hakuwa hata kazaliwa?

sent from my BBC using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom