Je! Nitakosea nikisema kuna tatizo IKULU?

Je! Nitakosea nikisema kuna tatizo IKULU?

Maadam Rais amewarudisha mizigo tafsiri nyepesi siyo mizigo kwake. wale waliokuwa wakitangazia umma kuwa mawaziri hao ni mizigo (Nape Mnauye na Abdulhaman Kinana) basi rais aangalie kwenye chama chake inawezekana wao (Nape na Kinana) ndiyo mizigo awatue mapema
 
B.JPG mwigulu_msigwa1.jpg download.jpg
Baadhi ya wateule wa Kikwete baraza la mawaziri

Mnyamahodzo,
Msahafu wa Biblia toka Agano Jipya kuna maneno yasemayo, mti mbaya huzaa matunda mabaya na mti mwema huzaa matunda mema. Ulichoongea Mnyamahocho ni ukweli mtupu. Kuna tatizo lisilo la kawaida Ikulu na ndio maana kinachoendelea ni sawa na kupanda mchungwa yeye atapandikiza (budding) mlimau ndicho kinachoendelea.

Siamini kwamba pamoja na wabovu waliochaguliwa kama akina Mchemba, Jenista, Pindi Chana na wengineo ambao tumeshuhudia pumba zao bungeni hadi kuharibu mwelekeo wa vikao vya bunge leo ndio anaowapandisha kwenda kuwa pambo tu pale kwenye baraza la mawaziri badala ya kuwaweka wachapa kazi.

Haitanishangaza kwamba kuna baadhi ya watu ambao ni waadilifu aliotegemea kuwaingiza ndani ya baraza hilo la mawaziri wakamkatalia ndio sababu ya kuchukua muda mrefu kutangazwa, hata ningekuwa mie kwa uchungu wa nchi yangu siko tayari kuwamo ndani ya baraza hilo kwa uchungu nilio nao kwa nchi hii, wenye uchu na wamoja wa Mkulu ndio wanaopaparikia na sasa wako kusherehekea kuingia ndani ya baraza hilo badala ya kuhuzunikia yatakayowapata.

Nikuunge mkono kwa hilo, nakumbuka siku za karibuni niliandika hapa JF kuwa jambo linaloendelea sasa hivi ni kuyajadili matawi badala ya shina linaloshikilia matawi hayo. Uimara wa matawi na usitawi wake unategemea tu source kutoka shinani. Sidhani kama nchi itaongozwa na Rais toka angani akiwe kwenye ndege kila siku.
 
Maadam Rais amewarudisha mizigo tafsiri nyepesi siyo mizigo kwake. wale waliokuwa wakitangazia umma kuwa mawaziri hao ni mizigo (Nape Mnauye na Abdulhaman Kinana) basi rais aangalie kwenye chama chake inawezekana wao (Nape na Kinana) ndiyo mizigo awatue mapema



  1. Pamoja na aliyosema Mnyamahocho, haijatokea Tanzania kuwa kituo cha kimataifa cha Madawa ya kulevya na sikutegemea siku itakuwa hivyo ila katika awamu hii.
  2. Haijatokea Tanzania kufurika utitiri wa viongozi wa mataifa makubwa wakisindikizana rais wa Marekani na wastaafu wawili kwa wakati mmoja kwa vyo vyote kuna jambo.

Je, ile mikataba ya biashara na mataifa hayo itakuwa wazi lini wakati ushirikiano wa biashara hizo hatuuoni kwa uwazi ila kushamiri kwa biashara ya madawa ya kulevya? Tumeshuhdia Rais wa Marekani na marasi waistaafu wake na familia zao Tanzania imekuna kituo cha kukutania kuliko huko kwao Marekani.
 
Tunachotakiwa watanzania ni kujihadhari tu sasa, maana CCM kama gari, gia zake za mbele zote hazifanyi kazi na sasa linatumia gia ya rivasi kujiendesha. Hapo tutegemee chochote kile.
 
Pia tukumbuke ni katika kipindi hiki tumeshuhudia yafuatayo pale IKULU
1. Kualikwa kwa TEJA RAY C
2. Kualikwa kwa MATEJA na kufanya sherehe pale IKULU
3. Kualikwa wanamziki wa BONGOFLAVA na BONGO MOVIE kula bata pale IKULU
4. FBI kuishikiria IKULU kwa siku 3 wakati wa ziara ya OBAMA

Hayo niliyoyaorodhesha hayajawahi kufanywa na Marais wa awamu zote 3 zilizopita isipokuwa kwa huyu wa awamu ya 4

Umesahau na kufuturisha watu .
 
Nimeandika post nyingi sana zinazopingana na uteuzi wa mawaziri uliofanywa juzi na Raisi kikwete. Lakini sasa inabidi nikubaliane na matokeo kwa kuwa ni vigumu kuibadili historia.

Kwa watu wanaozikumbuka baadhi ya kauli za Baba wa Taifa Mw. J.K.Nyerere aliposema "Ikulu ni mzigo, sio mahali pa kukimbilia hata kidogo" Kutokana na kauli hiyo imenibidi ninyooshe mikono juu.
 
Naitazama Ikulu kama Taasisi ya juu sana hapa nchini kwetu na ndivyo ukweli halisi ulivyo. Lipo tatizo kubwa katika Taasisi hii hasa katika awamu hii ya nne ya Urais wa Tanzania. Ikumbukwe kuwa hii ni Taasisi yenye wataalamu mbalimbali wanaofanya/wanaotakiwa kufanya kazi kwa kumsaidia na kumwongoza Rais kufanya jambo jema kwa mustkabali wa Taifa hili kwa faida ya kizazi cha sasa na vijavyo.

Tangu rais wa Awamu ya Nne aingie madarakani amefanya uteuzi wa Mawaziri (Baraza la Mawaziri) takribani mara kadhaa:- Mwaka 2005 (mara baada ya uchaguzi), 2008 (Kashfa ya Richmond), 2010 (mara baada ya Uchaguzi), 2012 ( kashfa ya Nishati na Madini, Mgogoro wa Wizara ya Afya), na sasa 2014 (Kashfa ya Operesheni Tokomeza) (…….ikiwa pana mwaka nimeruka au tukio halijakaa sawa I stand to corrected)

Katika mara zote baraza la Mawaziri halijawahi kutangazwa lile lililo/litakaloleta tija kwa watanzania kwa mwonekano (machoni pa wasomi wengi) hata utendaji achilia mbali gharama linazotumia. Kitu cha ajabu ambacho mara kadhaa nimekuwa najiuliza hivi ni kweli kuwa Rais anachagua Mawaziri peke yake? Jibu ni hapana. Anapochagua mawaziri lazima ashirikiane na Makamu wa Rais na Waziri Mkuu. Lakini hao wawili hawatoshi bila kupata taarifa za Mawaziri wanaowapendekeza toka kwa Maafisa wa Ikulu kwa kuzingatia Dira, Maono, Vipaumbele katika Mipango Mkakati na Sera ambazo Ikulu inapaswa kuzisimamia kwa mustakabali wa nchi. Sasa, unajiuliza huwa wana-shauri nini?

Hivi pamoja na makosa yote yalifanyika huko nyuma, basi kwenye kuelekea mwisho wa awamu hii wameshindwa kabisa kufikiri vyema hata kuchagua Baraza la Mawaziri bora? Hivi inahitaji kuwa na Phd kujua kuwa kuwa Shukuru Kawambwa hafai kuwa kuwaWaziri kwani katika Wizara zote alizopitia hakuna aliyo-deliver? Kama haitoshi, ikiwa ameleta majanga kwenye Wizara ya Elimu, kuna sababu gani kuendelea kumbakiza mtu anayesababisha majanga zaidi? Ofisi yenyewe ya Ikulu katika nukuu ya leo wameweka "Human history becomes more and more a race between education and catastrophe."H. G. Wells (1866-1946). Sasa ninajiuliza Kawambwa wa nini? Hebu tafakari orodha ya Mawaziri ambao wanaoitwa ni mizigo; kama haitoshi mnaongezewa mawaziri majanga wengine yaani Mwigulu Nchemba na Juma Nkamia (…hata Jenister Mhagama wanaomfahamu wanasema ni bomu hilo). Wanavyochagua wanazingatia dira, dhima na Maono ya ofisis ya Rais kweli? Ndiyo maana nasema Ikulu lipo Tatizo. Kama mtasema hakuna tatizo basi Ikulu ni Tatizo kwa watanzania.

Mwaka 2010 wakati viongozi na wazee mablimbali (akiwemo Butiku, Warioba na Salim) walipokuwa wanalalamikia juu ya ombwe la uongozi, walifika mbali kidogo na kusema “Washauri wa Rais hawamshauri vizuri”, japo wengine tukajiuliza, kama rais anashauriwa vibaya kwanini apokee kila ushauri mbaya ikiwa mwenyewe haupendi? Je hajui kuwa hawa watu/washauri wanaweza kumdharau kwasababu kila mara wanampa ushauri mbovu naye anaukubali? (zingatia kauli ya Mwalimu Nyerere pale New Africa Hotel,akizungumzia sifa za Rais ajaye, 1995).

Nikifanya marejeo ya Baraza Jipya la Mawaziri lilitangazwa jana, ninafikiri hadi sasa kuwa lipo tatizo kwenye Taasisi ya Ikulu yetu nikilinganisha na maandishi juu ya Dira, Maono na Dhamira ya Ofisi ya Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, ni la kiuongozi au kiutendaji? Sijui, ila karibu kuchangia.

Tanzania ni nchi yangu sina pakwenda zaidi ya nchi yangu hii ninayoipenda sana, ndiyo sababu nimeandika haya.
huo ni mtazamo wako. na hao wasomi unaoongelea ni kina nanini? au ni wivu tu unaokusumbua. acha wivu fanya kazi ulishe familia yako.
 
Back
Top Bottom