wa zion
JF-Expert Member
- Mar 23, 2013
- 223
- 486
Ilianza kama utani kutumiana message za kirafiki,kuchekeshana hadi leo ninavyoandika hivi.
Mwaka jana ilitokea nimetokea kumpenda mkaka ambaye tulikua marafiki na alikua ananishauri kwenye mambo mengi tofauti ya maana, urafiki uliendelea huku akionesha kuwa hana mahusiano yoyote yale hadi siku nlipogundua kuwa yupo kwenye mahusiano na mdada mwingine.
Baada ya kugundua na kumuuliza alisema nimvumilie ananipenda kwa dhati na mimi ndio mwanamke wa maisha yake,kwa kua nilimpenda nilivumilia yote aliniambia aliangukia mikononi mwa huyo dada mwingine baada ya kuumizwa na binti aliekua akimpenda kwa dhati nikaona sababu amekua wazi na kumpenda nampenda kumpoteza sitaki nikavumilia hadi pale maji yalipofika shingoni....
Pale ambapo yule dada alipoanza vitimbwi nikaona sio kesi nikamwambia kaka chagua moja kama ni mimi au huyo mwenzangu nikampa muda wa kukaa kutafakari yupi anaona kwake atamfaa kwenye maisha yake siwezi kuficha niliumia sana kutowasiliana naye kwa kipindi kile hadi siku atakayotoa maamuzi.
Siku ikafika kaka akasema nimeona bora kuwa na wewe na sasa tupo kwenye mahusiano halali nilifurahi sana nikaona sasa nimepata mtu wa kufa na kuzikana.
Kwa kufupisha sasa amesema hawezi kuwa na mimi kwa sasa maana hatafanikisha malengo yake kwa kua akiwa na mimi namdekeza,namfanya aone kama yupo likizo anaomba arudi kwa x wake akakamilishe mipango yake baada ya hapo turejeshe mahusiano yetu rasmi hadi sasa tunaonana,hatujaachana rasmi ingawa huyo dada hajui hiki kitu imekua siri kubwa kati yetu sisi.
Maumivu ninayopitia kumuona yupo na huyo dada mwingine ni makubwa na mazito nimejaribu kila njia labda atatoka kichwani nimeshindwa..nampenda kutoka moyoni sio siri.
Moyo unaniambia mvumilivu hula mbivu akili inaniambia niondoke Uran amefanya nifunguke hapa Bado najiuliza je nivumilie maana aliniambia hadi mwezi wa saba mambo yatakuwa sawa atarudi rasmi kwangu baada ya kupata anachokitaka huko Kwa kua nakijua anachokitaka naona kama ana point maana mimi sitamsaidia na sina uwezo wa kumsaidia hicho anachokitaka kwa huyo dada.
JE NIMSUBIRI?
Mwaka jana ilitokea nimetokea kumpenda mkaka ambaye tulikua marafiki na alikua ananishauri kwenye mambo mengi tofauti ya maana, urafiki uliendelea huku akionesha kuwa hana mahusiano yoyote yale hadi siku nlipogundua kuwa yupo kwenye mahusiano na mdada mwingine.
Baada ya kugundua na kumuuliza alisema nimvumilie ananipenda kwa dhati na mimi ndio mwanamke wa maisha yake,kwa kua nilimpenda nilivumilia yote aliniambia aliangukia mikononi mwa huyo dada mwingine baada ya kuumizwa na binti aliekua akimpenda kwa dhati nikaona sababu amekua wazi na kumpenda nampenda kumpoteza sitaki nikavumilia hadi pale maji yalipofika shingoni....
Pale ambapo yule dada alipoanza vitimbwi nikaona sio kesi nikamwambia kaka chagua moja kama ni mimi au huyo mwenzangu nikampa muda wa kukaa kutafakari yupi anaona kwake atamfaa kwenye maisha yake siwezi kuficha niliumia sana kutowasiliana naye kwa kipindi kile hadi siku atakayotoa maamuzi.
Siku ikafika kaka akasema nimeona bora kuwa na wewe na sasa tupo kwenye mahusiano halali nilifurahi sana nikaona sasa nimepata mtu wa kufa na kuzikana.
Kwa kufupisha sasa amesema hawezi kuwa na mimi kwa sasa maana hatafanikisha malengo yake kwa kua akiwa na mimi namdekeza,namfanya aone kama yupo likizo anaomba arudi kwa x wake akakamilishe mipango yake baada ya hapo turejeshe mahusiano yetu rasmi hadi sasa tunaonana,hatujaachana rasmi ingawa huyo dada hajui hiki kitu imekua siri kubwa kati yetu sisi.
Maumivu ninayopitia kumuona yupo na huyo dada mwingine ni makubwa na mazito nimejaribu kila njia labda atatoka kichwani nimeshindwa..nampenda kutoka moyoni sio siri.
Moyo unaniambia mvumilivu hula mbivu akili inaniambia niondoke Uran amefanya nifunguke hapa Bado najiuliza je nivumilie maana aliniambia hadi mwezi wa saba mambo yatakuwa sawa atarudi rasmi kwangu baada ya kupata anachokitaka huko Kwa kua nakijua anachokitaka naona kama ana point maana mimi sitamsaidia na sina uwezo wa kumsaidia hicho anachokitaka kwa huyo dada.
JE NIMSUBIRI?