babukijana
JF-Expert Member
- Jul 21, 2009
- 13,068
- 15,923
wakuu,nakumbuka kipindi nasoma hasa history vitabu viliandikwa jinsi mwanadamu hasa mwafrika alivyobadilika badilika mpaka kufikia kuwa kama hivi tulivyo,na mpaka sasa kuna documentary nyingi sana tu wanaonyesha ktk tv jinsi mwafrika alipokuwa nyani mpaka kuwa mwanadamu,juzijuzi hapa naangalia documentary moja ilikua inaonyesha kama hayo manyani(sisi) hapo nyuma tulikua tunaishi na wanyama na chakula chetu kilikua mifupa kabla hatujaweza kuwinda,yaani ilikuwa simba akiua mnyama akila akabakisha fisi nao wanakula kisha manyani hayo(sisi)tunawafukuza fisi tunakula masalia!,ni documentary nyingi zinaonyesha haya mambo,sasa je swali ambalo najiuliza ni kwamba je ni kweli sisi waafrika tulitokana na manyani?kivipi binadamu atoke kuwa nyani mpaka awe binadamu?na kama ingekuwa hivyo manyani si bado yapo si tungeendelea kuona jinsi nayo yanavyobadilika na kuwa binadamu?halafu sijui kama watoto bado mpaka sasa wanafundishiwa hivyo vitabu vya historia kwamba tulikua manyani,haya wanasayansi na wandugu nawasilisha hoja hapa tuijadili.