Je nikweli shetani ni kiumbe au roho yenye ubaya?

Je nikweli shetani ni kiumbe au roho yenye ubaya?

nodetz

Senior Member
Joined
May 4, 2024
Posts
173
Reaction score
156
Habari wana jf

ANGALIZO.
UZI HUU HAUUSIANI NA DINI KABISA.

NI KWAAJILI YA WATU WANAOWEZA KUFIKIRI NA KUTAFAKARI MAMBO.

Kila mtu amewai kusikia, kuona au ata kuhisi uwepo wa nguvu ya shetani.

Je nikweli kwamba shetani yupo na anafanya kazi au ni mindset zetu zimekaa ivo.

Kila jamii iliyowai kuishi au inayoishi hapa duniani ina namna ya kufana ya kuitambua nguvu hasi yaani wote tunaitambua kama ni nguvu ya shetani.

Lakini baadhi ya watu ikiwemo mimi naona mtizamo huu hauko sawa maana kila jambo positive basi lazima liwe na negative
Mfano

Mchana - usiku
Utajiri - umasikini
Kupenda - kuchukia
Kuzaliwa - kufa
Furaha - hasira

Na mengine mengi.

Jambo moja ambalo karibia binadamu wote tunafana nikua nguvu chanya tunaziona kama nguvu za mungu na nguvu hasi tunaziona kama nguvu za shetani

Tunashindwa kuelewa pia kuwa hicho tunacho kiita shetani kinaweza zalisha nguvu chanya
Mfano. Mwizi masikini anaweza iba pesa na akawa tajiri.

Pia ata nguvu chanya inaweza zalisha nguvu hasi
Mfano. Kutokana na tabia za mtu tajiri kupenda sifa na kuwafurahisha watu anaweza jikuta anarudi kwenye umasikini.

Pia kuna aina ya ushetani ambayo ni mawazo ambayo mtu anayawaza na kumperekea kufanya jambo la ovyo.

Kwa maoni yangu naona shetani ni kitu ambacho hakipo ila sisi tunamfanya awepo ili tunapotenda mabaya tupate wa kumlaumu.

Je unaona niko sahihi??
 
Huo ni kulingana na mtazamo wako ila shetani ni roho tena yupo, sema inakuwa ngumu kukuelezea sababu ushasema hautaki suala la dini na mimi shetani siwezi muelezea tofauti na nilivyofundishwa katika dini yangu sababu sijawahi kumsoma katika uchawi au elimu dunia.
 
Hata kama shetani yupo kweli ila me naamini kuwa matendo mengi mabaya nayafanya kutokana na matamanio

Kwa Mfano labda kulala na mwanamke siwezi kumsingizia shetani wakati nimetamani mwenyew na kama kujizuia nilikuwa na uwezo wa kujizuia nisifanye hivyo

Ila shetani hupewa lawama pale ambapo unahitaji kuitetea nafsi yako kuwa haishiriki uovu uliofanya mwenyew baada ya kutokea madhara
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom