Je, nikimuacha nitakuwa nakosea?

new gal

JF-Expert Member
May 4, 2021
1,474
2,716
Habari wadau, ama kweli yakikufika huna namna utazungumza tu. Mwenzenu yamenifika shingoni na sijui kama nikichukua maamuzi ya kumuacha nitakua nakosea au lah.

Nikiri katika mahusiano yote niliyopitia sijawahi kuwa na mwanaume anayenifanya nijisikie furaha kama huyu kaka.Uhusiano wetu una mwaka sasa. Ni mkaka anayepambana sana, anajali, anahudumia pale anapoweza na kule 6*6 ndo usiseme. Hamna kitu ananificha. In short he is a man in every woman's dream mpaka nikawa naogopa kumpoteza bwana.

Mbembe ikaja baada ya kunitambulisha kwa mama yake mzazi (Eh Mungu). Mama alinipokea vizuri tu lakini siku ya kwanza tu akaniambia ukija niletee bia, mtoto wa kike nikapeleka. Baada ya hapo kila nikiona simu ya yule mama yeye ni kutaka hela tu kwangu. Nikajiuliza ni kisa kaniona na gari au ni nini?

On top of that mama yake hatak apange, kashikilia akae nyumbani eti asiharibu hela kwa kulipa kodi. Mshahara wake wote unatumika kwenye matumizi ya nyumbani, kama anabakiza ni kiasi kdg sana. Sasa kutokana na ukaribu huo kati yao naogopa hata kumshauri asije ona nawaingilia maisha yao.

Napata hofu kuwa ntakua adui kwa yule mama, maana akibadilika kimatumizi ataona mimi ndo kisababishi. Jamaa anapanga mipango ya ndoa lakini naogopa sana kuingia kwenye ile familia. Maana hata akiongea nae kwenye simu akiomba hela akimwambia hana anamwambia ahakikishe anaipata anampa na kijana anafanya hivyo.

Je, nikimuacha huyu kijana mapema nitakuwa nakosea?
 
Utakuwa unakosea kama hutojaribu kumshauri uone muitikio wake,nini tofauti ya yeye kuwa single na kuwa nawewe kama hata kushauri kama mwanamke shujaa unashindwa? mshauri kwanza akigoma hapo sasa waweza chukua maamuzi.
Nashindwa kumshauri as ntaonekana namchukia mama yake, cause alisema mama yake anapenda kudekezwa. Ila mm sikujua kudekezwa yenyewe ni aina hii.

Kitendo cha yeye kufata kila anachoambiwa na mama ni tatizo tayari ndo mana nakosa hyo nguvu ya kushauri. na akifata ushauri wangu jua nipo kwenye hatari ya kuingia vita na mama mkwe
 
Ebu angalia mfano wangu huu: Je unaonaje ni kheri kuondoka kimya kimya uyu bwana ako asijue sababu ya kukuondoa kimya kimya au ni kheri uondoke na uku ukiwa umejua ya kwamba umemshauri ila kwa upande wake umeona imeshindikana na ata ukiondoka anajua umeondokana kwa kuwa kuna mambo umeona uko mbele hayata enda, nina mfano kama wako copy and paste,,, njoo pm nikusimulie na nikupe mkanda ilivyo kuwa.
 
Nashindwa kumshauri as ntaonekana namchukia mama yake, cause alisema mama yake anapenda kudekezwa. Ila mm sikujua kudekezwa yenyewe ni aina hii. Kitendo cha yeye kufata kila anachoambiwa na mama ni tatizo tayari ndo mana nakosa hyo nguvu ya kushauri. na akifata ushauri wangu jua nipo kwenye hatari ya kuingia vita na mama mkwe
Hapo dada tafuta lugha nzuri isiyo elemea upande wowote umwambie awe mwanaume..ili ukiondoka usije jihis kuwa na hatia,huenda atakuelewa tumia tafsida usiweke lugha zitakazo mkwaza na kujenga chuki
 
Ebu angalia mfano wangu huu: Je unaonaje ni kheri kuondoka kimya kimya uyu bwana ako asijue sababu ya kukuondoa kimya kimya au ni kheri uondoke na uku ukiwa umejua ya kwamba umemshauri ila kwa upande wake umeona imeshindikana na ata ukiondoka anajua umeondokana kwa kuwa kuna mambo umeona uko mbele hayata enda, nina mfano kama wako copy and paste,,, njoo pm nikusimulie na nikupe mkanda ilivyo kuwa.
Naja haraka sana
 
Kila kitu lazima kiwe na kiasi.

Kila kitu lazima kiwe na mpaka.

Haiwezekani kila anachoomba mama basi anakipewa hata kama hakifai.

Haiwezekani mama ndio anakuwa ultimatum ya maisha ya kijana wake, kwamba akisemacho yeye ndio alfa & omega.

Hivyo mueleze waziwazi mwenzio kwamba maisha yenu nyie wawili lazima yawe na defined limit.

Pia usikubali kamwe kuishi nyumba ya mama mkwe unless muwe hamna uwezo wa kupanga.

Mueleze wazi jamaa yako kwamba humchukii mama mkwe, kama anataka muishi na mama mkwe basi mkijenga mama mkwe aje aishi kwenye makazi yenu ila sio nyie mkaishi kwa mama mkwe.
 
Jisepee kwa huyo mama boy wako.. Wazazi walewa, watoto wakifikisha umri fulani, huwa wanawaondoa watoto wao home ili wakajijengee uwezo wa kujitegemea kwa kila nyanja.

Jingine ni kwamba mama anakutazama wewe kama source ya pili ya income kwake... Ndo maana anakutaka umpelekee bia kila ukienda.

KABLA YA KUONDOKA, MSHAURI JAMAA AHAME KWAO AKAPANGE... AKIGOMA NDO USEPE
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom