Weston Songoro
JF-Expert Member
- Feb 17, 2014
- 2,793
- 1,083
Kuna taarifa zinasikitisha na kuhuzunisha. Zinaleta simanzi kwa wasomaji wa taarifa hizo hasa ndugu wa marehemu.
Kwamba, msiba wa Alphonce Mawazo, aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Geita umekuwa na sura mbili kwa CHADEMA. Sura ya kwanza ni kujijenga kisiasa baada ya kufanya vibaya kwenye uchaguzi Mkuu uliomalizika ambapo CCM kimeibuka mshindi kwa nafasi zote yaani Urais, Ubunge na Udiwani.
Sura ya pili ni ya kiuchumi. Kumbe kuna jamaa ndani ya CHADEMA wamepiga mpunga wa maana kwenye msiba huo. Taarifa nilizopata hivi punde kutoka kwa mtonyaji wangu ndani ya makao makuu ya CHADEMA zinasema kuwa shilingi milioni 400 zimeidhinishwa kutumika kwa ajili ya msiba wa Mawazo. Kwamba, fedha hizo ni kwa ajili ya kugharamia usafiri, chakula na malazi kwa viongozi wa CHADEMA walioenda kwenye msiba huo. Aidha, fedha hizo pia ni kwa ajili ya kuandaa mikutano au kwa jina jingine mikusanyiko ya kuuaga mwili wa Mawazo. Vile vile mtonyaji amesema kuwa fedha hizo pia zimetumika kutoa rambirambi kwa wafiwa ambapo hata hivyo, haijabainishwa ni kiasi gani cha fedha kimetengwa kwa madhumuni hayo
Taarifa zaidi zinasema kuwa wakati makao makuu wakiidhinisha fedha hizo, Mwenyekiti wa CHADEMA, FREEMAN MBOWE aliwasilisha maombi binafsi kwa Edward Lowasa ili aweze kutoa shilingi milioni 200 zisaidie kuratibu shughuli za kuuaga mwili wa Alphonce Mawazo. Inadaiwa kuwa, Lowasa ametoa kiasi hicho cha fedha ambacho hata hivyo, haijulikani wapi kimepelekwa.
Mtonyaji wangu amenitonya kuwa, imekuwa ni desturi ya viongozi wa CHADEMA kutumia misiba ama matukio mengine ya majanga kujinufaisha. Anasema kuwa hata alipofariki Mohamed Mtoi, zaidi ya shilingi milioni 170 ziliidhinishwa Makao Makuu kwa ajili msiba huo. Hata hivyo, imeelezwa kuwa ni shilingi milioni 12 tu ndizo zilizotumika tena kwa matumizi ambayo hayana uthibitisho wa dhahiri.:angry:
Kwamba, msiba wa Alphonce Mawazo, aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Geita umekuwa na sura mbili kwa CHADEMA. Sura ya kwanza ni kujijenga kisiasa baada ya kufanya vibaya kwenye uchaguzi Mkuu uliomalizika ambapo CCM kimeibuka mshindi kwa nafasi zote yaani Urais, Ubunge na Udiwani.
Sura ya pili ni ya kiuchumi. Kumbe kuna jamaa ndani ya CHADEMA wamepiga mpunga wa maana kwenye msiba huo. Taarifa nilizopata hivi punde kutoka kwa mtonyaji wangu ndani ya makao makuu ya CHADEMA zinasema kuwa shilingi milioni 400 zimeidhinishwa kutumika kwa ajili ya msiba wa Mawazo. Kwamba, fedha hizo ni kwa ajili ya kugharamia usafiri, chakula na malazi kwa viongozi wa CHADEMA walioenda kwenye msiba huo. Aidha, fedha hizo pia ni kwa ajili ya kuandaa mikutano au kwa jina jingine mikusanyiko ya kuuaga mwili wa Mawazo. Vile vile mtonyaji amesema kuwa fedha hizo pia zimetumika kutoa rambirambi kwa wafiwa ambapo hata hivyo, haijabainishwa ni kiasi gani cha fedha kimetengwa kwa madhumuni hayo
Taarifa zaidi zinasema kuwa wakati makao makuu wakiidhinisha fedha hizo, Mwenyekiti wa CHADEMA, FREEMAN MBOWE aliwasilisha maombi binafsi kwa Edward Lowasa ili aweze kutoa shilingi milioni 200 zisaidie kuratibu shughuli za kuuaga mwili wa Alphonce Mawazo. Inadaiwa kuwa, Lowasa ametoa kiasi hicho cha fedha ambacho hata hivyo, haijulikani wapi kimepelekwa.
Mtonyaji wangu amenitonya kuwa, imekuwa ni desturi ya viongozi wa CHADEMA kutumia misiba ama matukio mengine ya majanga kujinufaisha. Anasema kuwa hata alipofariki Mohamed Mtoi, zaidi ya shilingi milioni 170 ziliidhinishwa Makao Makuu kwa ajili msiba huo. Hata hivyo, imeelezwa kuwa ni shilingi milioni 12 tu ndizo zilizotumika tena kwa matumizi ambayo hayana uthibitisho wa dhahiri.:angry: