Je, ni kweli Ugali wa Dona ni bora kuliko wa Sembe?

Kwaiyo sembe ni bora kama unakula na kufanya mazoezi na kutumia ile grucos yote?

Ndio kwa upande wa kupunguz sukari....
Lkn dona ina fibres zinazosaidia kupunguza choo kikavu/ pia constipation.

Vilevile virutubisho vidogo kama protini vipo kwenye dona
 
We janaa unatumia ujuzi wako kuwadanganya watu panya mwenyewe ana akili sana maana hayo mahindi yeye hula kiini pekee na kuacha hayo masalia mengine.
Ila we kazana na sembe tuu siye tuachie dona
Hoja yako bado haina mashiko mkuu, maana mleta uzi amejaribu kuchambua tena kwa kina na hajatoa mapendekezo watu wale nini ila alichosema kuwa ni vema kula dona ya mahindi yaliyotoka moja kwa moja kutoka shambani ambayo hayajahifadhiwa kwa muda mrefu na kupuliziwa madawa.

Sasa hapo uongo wake upo wapi? Kwa maoni yangu amechambua vema, mimi naona sembe ni bora kwa sababu ni unga safi na pia ukichanganya na mboga mboga mchanganyiko basi unakamilisha mlo kamili.
 
Hoja yako bado haina mashiko mkuu, maana mleta uzi amejaribu kuchambua tena kwa kina na hajatoa mapendekezo watu wale nini ila alichosema kuwa ni vema kula dona ya mahindi yaliyotoka moja kwa moja kutoka shambani ambayo hayajahifadhiwa kwa muda mrefu na kupuliziwa madawa.

Sasa hapo uongo wake upo wapi? Kwa maoni yangu amechambua vema, mimi naona sembe ni bora kwa sababu ni unga safi na pia ukichanganya na mboga mboga mchanganyiko basi unakamilisha mlo kamili.

Absolutely
 
Mjadala...
------------
Sehemu kubwa ya jamii ya kitanzania inaamini kwamba ugali unaopikwa kwa kutumia unga wa dona ni bora kuliko ugali unaopikwa kwa kutumia unga wa sembe! Je! Ni kweli?

Twende Taratibu; wanaoamini kuwa dona ni bora zaidi wanatoa sababu kuu mbili; moja ni kuwa ugali wa dona unamfanya mtu awe na nguvu zaidi, pili una virutubisho zaidi kwa sababu haujakobolewa na hivyo kubaki na kiini chake. Je! Sababu hizo mbili zinatosha kuufaya ugali wa dona kuwa bora zaidi?

Kabla ya kutoa majibu yangu, nieleze kwa ufupi namna mfumo wa mmeng'enyo wa chakula unavyofanya kazi.

Binadamu anatakiwa kula ili aishi, na ameumbwa kusikia njaa ili 'akumbuke' kula kwa wakati. Mfumo wa fahamu (ubongo, ugwe mgongo na neva za fahamu) ndiwo unaongoza mifumo mingine ya mwiki ukiwemo mfumo wa mmeng'enyo wa chakula...ili mifumo hiyo ifanye kazi kwa ufasaha na kiumbe (binadamu) apate kuishi.

Kuna sababu nyingi zinazomfanya binadamu aanze kusikia njaa...lakini sababu kubwa kuliko zote ni kusinyaa kwa kuta za mfuko wa chakula (tumbo) kunakosababishwa na kutokuwapo kwa 'kitu' tumboni. Nimesema kutokuwapo kwa 'kitu' tumboni -sio kutokuwapo kwa chakula, kuna sababu za kusema hivyo.

Mtu anapotia 'kitu' tumboni iwe ni chakula au kitu kinachofanana na chakula kisicho na madhara, kuta za mfuko wa chakula (tumbo) zitavutika (stretch) kwa sababu mfuko huo umeumbwa kutanuka na kusinyaa - mithili ya 'elastiki'. Kutanuka huko husababisha mishipa ya neva za fahamu kupeleka taarifa kwenye mfumo mkuu wa fahamu (ubongo na ugwe mgongo/spinal cord) ili mfumo mkuu uanze kuratibu matukio muhimu ya mmeng'enyo wa chakula huko tumboni.

Moja kati ya matukio hayo ni kupunguza hamu ya kula (au njaa) taratibu hadi pale tumbo linapovutika kwa kiasi cha kutosha na njaa hukoma.

Kumbuka - kinachofanya kuta za mfuko wa chakula zivutike ni 'kitu' kilichopo tumboni, sio lazima iwe chakula. Kwa lugha nyingine - ni kuwa mtu anaweza kusikia ameshiba kwa sababu kuna kitu tumboni...hata kama kitu hicho si chakula.
Ukiyaelewa maelezo haya machache tutakuwa tumevuka hatua ya kwanza katika kutafuta jibu la swali letu; dona ni bora kuliko sembe?

Pointi ya Kwanza: Ingawa Ni kweli ugali wa dona unaweza kumfanya mtu ajisikie ameshiba zaidi kuliko kiasi sawa cha ugali wa sembe, bado haitoshi kusema ugali wa dona ni chakula bora kuliko ugali wa sembe, kwa sababu si kila kinachompa mtu hisia za kushiba ni chakula.

Dona ni nini?
Dona ni jina linalopewa unga usiokobolewa. Pamoja na kwamba unga wa dona unabaki na kiini cha punje ya hindi chenye protini, vilevile unabaki na ganda la nje la punje ya hindi - ganda ambalo huitwa pumba endapo mahindi yatakobolewa.

Sembe ni unga unaotokana na mahindi yaliyosagwa baada ya kukobolewa, na hivyo hauna kiini na maganda ya nje ya punje za hindi (pumba).

Je, Dona ni bora kuliko sembe?

Sehemu kubwa ya unga wa mahindi ni wanga (carbohydrate) aina ya hamirojo (starch). Wakati kiwango cha hamirojo kwenye dona kinafikia 75% na 25% za protini, virutubisho-madini na vitamini, kiwango cha hamirojo kwenye unga wa sembe kinakaribia 90%, na 10% inabaki kuwa ya virutubisho-madini na baadhi ya vitamin na protini kwa kiwango kidogo sana.

Protini iliyopo kwenye kiini cha punje ya hindi ambayo hubaki kwenye unga wa dona ni protini isiyo timilifu kwa sababu imepungukiwa baadhi ya viungo vya lazima vinavyofanya protini iwe timilifu. 'Viungo' hivi huitwa 'amino acids', na vimegawanyika katika makundi makuu mawili - Essentials amino acids (EAA) na Non - essential amino acids (NAA).

Tofauti kubwa ya virutubisho hivi ni kuwa EAA hazitengenezwi ndani ya mwili na hivyo ni lazima zipatikane kutoka nje kwenye vyakula mbalimbali, wakati NAA zinaweza kutengenezwa ndani ya mwili kutokana na virutubisho vya aina nyingine. Protini iliyopo kwenye punje ya hindi haina idadi ya kutosha ya EAA, (ambazo ni lazima zipatikane nje ya mwili).

Virutubisho vingine vilivyomo kwenye dona ni Vitamin B, madini ya chuma, madini ya Calcium, Magnesium, Potash nk, ambavyo vina umuhimu wake mwilini.

Pointi ya pili: Ugali wa dona una kiasi kidogo cha wanga kulinganisha na kiasi kilekile cha ugali wa sembe. Hata hivyo ugali wa dona una virutubisho zaidi ya ugali wa sembe.

Kumbuka, kila aina ya chakula ina kazi zake mwilini. Itoshe kurudia elimu ya sayansi kimu ya darasa la tano hata kama haitoi picha halisi, kwamba Protini hujenga mwili, Wanga (carbohydrate) unasidia mwili kupata nguvu, na Fat & Oil (mafuta) husaidia kudumisha jotoridi la mwili. Muhimu hapa ni hiyo pointi ya -wanga unasaidia mwili kupata nguvu.

Ndio. Vyakula aina ya wanga huanza kumeng'enywa kuanzia mdomoni kwa nguvu ya 'enzyme' iliyopo kwenye mate (salivary amylase) ambayo huvunjavunja molekyuli zinazounda wanga na kupata aina nyingine ya wanga nyepesi iitwayo Maltose. Zao hilo linapofika tumboni na baadae kwenye utumbo mwembamba huendelea kumeng'enywa kwa nguvu ya enzyme nyingine iitwayo 'Maltase' na kupatikana wanga nyepesi zaidi inayoitwa 'Glucose'. Hiyo glucose ndio inanyonywa na kuingia kwenye mzunguko wa damu na kusambazwa sehemu zote za mwili -na huko hutumika kama malighafi ya kuzalisha nguvu zinazohitajika ili binadamu andelee kuwa hai.

Pointi ya tatu: Glucose, ndiyo malighafi inayohitajika kuzalisha nguvu mwilini, glucose ni zao la wanga - ambao upo kwa wingi zaidi kwenye unga wa sembe kuliko wanga uliyopo kwenye kiasi sawa cha unga wa dona.

Hitimisho
Kwanza, si kweli kwamba ugali wa dona unamfanya mtu apate nguvu kuliko sembe kwa sababu ugali wa sembe una zalisha glucose kwa haraka zaidi na kwa wingi zaidi kuliko dona. Glucose ndio zao la ugali wa mahindi ambalo ndio malighafi ya kwanza inayohitajika kuzalisha nguvu za mwili.
Kinachotokea kwa dona ni kuchelewa kumeng'enywa na kukaa tumboni muda mrefu na hivyo kufanya mfumo wa chakula na mfumo wa fahamu 'ujue' bado kuna kitu kwenye mfumo wa chakula. Hali hii hufanya mfumo wa fahamu uridhike kwa muda mrefu na mtu kutopata hisia ya njaa...

Kwanini dona linakaa muda mrefu kwenye mfumo wa mmeng'enyo wa chakula? Ni kwa sababu ya uwepo wa maganda ya punje za hindi (ambayo yangekuwa pumba endapo mahindi yangekobolewa). Maganda haya hutengenezwa kwa aina nyingine ya wanga inayoutwa Cellulose ambayo haiwezi kumeng'enywa mwilini. Mwili wa binadamu hauna enzyme aina ya cellulase inayohitajika kwa ajili ya kumeng'enya Cellulose. Homoni hii hupatikana kwa wanyama aina ya 'ruminants' kama Ng'ombe, Mbuzi, Kondoo nk.
Hata hivyo kuna faida moja ya 'pumba' zilizopo kwenye dona - nayo ni kupata choo chepesi.

Pili, Dona lina virutubisho vingi kuliko sembe, ingawa faida si ya maana Sana kwa sababu mtu hali ugali wa dona bila kitoweo. Protini iliyopo kwenye mboga kama maharage, samaki/dagaa au nyama ni nyingi mno kiasi cha kufanya protini ya kwenye dona isiwe na maana yoyote. Madini ya chuma, calcium, potash magnesium nk yanapatikana kwenye mboga za majani kwa wingi kiasi kwamba kiwango kilichopo kwenye dona hakina maana. Vitamini zilizopo kwenye matunda zinafanya vitamini za kwenye dona zisiwe na maana. Zaidi, pamoja na kuwa na virutubisho vya ziada, Bado virutubisho hivyo vya ziada vinavyopatikana kwenye dona - si vya kiwango cha kutosha kuusaidia mwili wa binadamu kama hatakula vyakula vingine. Kwahiyo; uwepo wa virutubisho vya ziada kwenye dona si faida ya kujivunia juu ya sembe. Mwili hauwezi kutegemea protini, madini na vitamini zilizopo kwenye dona.

Tatu. Kuhusu sumu kavu. Ingawa hili si suala la ki-baiolojia lakini pengine ndio muhimu kuliko yote niliyoandika. Mahindi mengi huhifadhiwa kwa kupuliziwa madawa ya kuzuia wadudu ili yasiharibike. Ukiacha madawa hayo (kemikali) bado kuna vumbi na vitu vingine vinavyoambatana na mahindi tangu kuvunwa, kupukuchuliwa na kuhifadhiwa. Mashine ya kusaga haiondoi kemikali au vumbi au vitu vingine vilivyogandamana na mahindi, lakini ikiwa mahindi yatakobolewa angalau vitu hivyo vitapungua kwa kiasi kikubwa.

Vipi? Dona ni bora kuliko sembe?

Tazama zile pumba zinazopatikana baada ya kukoboa mahindi, zitazame tena. Unapokula dona unakula pamoja na hizo pumba. Faida yake ni moja - kupata choo bila shida. Lakini matunda yenye nyuzinyuzi/roughages (mfano; maganda ya ndani ya chungwa) mapapai, maji ya kutosha, kushughulisha mwili, vitasaidia kupata choo chepesi.

Ushauri.
Hakuna shida kula unga wa dona ikiwa mahindi yametoka shambani na kusagwa mara moja. Lakini ikiwa mahindi yametunzwa kwa muda mrefu na kwa dawa za kuzuia wadudu - ni jambo la kutafakari kuyasaga bila kukoboa. Sumu kavu - vumbi na dawa za kuzuia wadudu waharibifu vinaweza kuleta madhara ya kiafya mwilini. Nirudie tena, faida pekee ya ziada na maana ya dona juu sembe ni kupata choo chepesi...
-Sio kweli kwamba Dona linaleta nguvu kuliko sembe (neno 'nguvu' linaweza kuhutaji ufafanuzi zaidi)
-Ziada ya virutubisho vya dona haina faida ya maana juu ya sembe kwa sababu havitoshi kuunufaisha mwili bila kuongeza kutoka vyakula vingine...

Dona ni bora kuliko sembe?
Amua...
utafiti huu wa kisayansi labda ni wa darasa la 5. haiwezekani useme
Mjadala...
------------
Sehemu kubwa ya jamii ya kitanzania inaamini kwamba ugali unaopikwa kwa kutumia unga wa dona ni bora kuliko ugali unaopikwa kwa kutumia unga wa sembe! Je! Ni kweli?

Twende Taratibu; wanaoamini kuwa dona ni bora zaidi wanatoa sababu kuu mbili; moja ni kuwa ugali wa dona unamfanya mtu awe na nguvu zaidi, pili una virutubisho zaidi kwa sababu haujakobolewa na hivyo kubaki na kiini chake. Je! Sababu hizo mbili zinatosha kuufaya ugali wa dona kuwa bora zaidi?

Kabla ya kutoa majibu yangu, nieleze kwa ufupi namna mfumo wa mmeng'enyo wa chakula unavyofanya kazi.

Binadamu anatakiwa kula ili aishi, na ameumbwa kusikia njaa ili 'akumbuke' kula kwa wakati. Mfumo wa fahamu (ubongo, ugwe mgongo na neva za fahamu) ndiwo unaongoza mifumo mingine ya mwiki ukiwemo mfumo wa mmeng'enyo wa chakula...ili mifumo hiyo ifanye kazi kwa ufasaha na kiumbe (binadamu) apate kuishi.

Kuna sababu nyingi zinazomfanya binadamu aanze kusikia njaa...lakini sababu kubwa kuliko zote ni kusinyaa kwa kuta za mfuko wa chakula (tumbo) kunakosababishwa na kutokuwapo kwa 'kitu' tumboni. Nimesema kutokuwapo kwa 'kitu' tumboni -sio kutokuwapo kwa chakula, kuna sababu za kusema hivyo.

Mtu anapotia 'kitu' tumboni iwe ni chakula au kitu kinachofanana na chakula kisicho na madhara, kuta za mfuko wa chakula (tumbo) zitavutika (stretch) kwa sababu mfuko huo umeumbwa kutanuka na kusinyaa - mithili ya 'elastiki'. Kutanuka huko husababisha mishipa ya neva za fahamu kupeleka taarifa kwenye mfumo mkuu wa fahamu (ubongo na ugwe mgongo/spinal cord) ili mfumo mkuu uanze kuratibu matukio muhimu ya mmeng'enyo wa chakula huko tumboni.

Moja kati ya matukio hayo ni kupunguza hamu ya kula (au njaa) taratibu hadi pale tumbo linapovutika kwa kiasi cha kutosha na njaa hukoma.

Kumbuka - kinachofanya kuta za mfuko wa chakula zivutike ni 'kitu' kilichopo tumboni, sio lazima iwe chakula. Kwa lugha nyingine - ni kuwa mtu anaweza kusikia ameshiba kwa sababu kuna kitu tumboni...hata kama kitu hicho si chakula.
Ukiyaelewa maelezo haya machache tutakuwa tumevuka hatua ya kwanza katika kutafuta jibu la swali letu; dona ni bora kuliko sembe?

Pointi ya Kwanza: Ingawa Ni kweli ugali wa dona unaweza kumfanya mtu ajisikie ameshiba zaidi kuliko kiasi sawa cha ugali wa sembe, bado haitoshi kusema ugali wa dona ni chakula bora kuliko ugali wa sembe, kwa sababu si kila kinachompa mtu hisia za kushiba ni chakula.

Dona ni nini?
Dona ni jina linalopewa unga usiokobolewa. Pamoja na kwamba unga wa dona unabaki na kiini cha punje ya hindi chenye protini, vilevile unabaki na ganda la nje la punje ya hindi - ganda ambalo huitwa pumba endapo mahindi yatakobolewa.

Sembe ni unga unaotokana na mahindi yaliyosagwa baada ya kukobolewa, na hivyo hauna kiini na maganda ya nje ya punje za hindi (pumba).

Je, Dona ni bora kuliko sembe?

Sehemu kubwa ya unga wa mahindi ni wanga (carbohydrate) aina ya hamirojo (starch). Wakati kiwango cha hamirojo kwenye dona kinafikia 75% na 25% za protini, virutubisho-madini na vitamini, kiwango cha hamirojo kwenye unga wa sembe kinakaribia 90%, na 10% inabaki kuwa ya virutubisho-madini na baadhi ya vitamin na protini kwa kiwango kidogo sana.

Protini iliyopo kwenye kiini cha punje ya hindi ambayo hubaki kwenye unga wa dona ni protini isiyo timilifu kwa sababu imepungukiwa baadhi ya viungo vya lazima vinavyofanya protini iwe timilifu. 'Viungo' hivi huitwa 'amino acids', na vimegawanyika katika makundi makuu mawili - Essentials amino acids (EAA) na Non - essential amino acids (NAA).

Tofauti kubwa ya virutubisho hivi ni kuwa EAA hazitengenezwi ndani ya mwili na hivyo ni lazima zipatikane kutoka nje kwenye vyakula mbalimbali, wakati NAA zinaweza kutengenezwa ndani ya mwili kutokana na virutubisho vya aina nyingine. Protini iliyopo kwenye punje ya hindi haina idadi ya kutosha ya EAA, (ambazo ni lazima zipatikane nje ya mwili).

Virutubisho vingine vilivyomo kwenye dona ni Vitamin B, madini ya chuma, madini ya Calcium, Magnesium, Potash nk, ambavyo vina umuhimu wake mwilini.

Pointi ya pili: Ugali wa dona una kiasi kidogo cha wanga kulinganisha na kiasi kilekile cha ugali wa sembe. Hata hivyo ugali wa dona una virutubisho zaidi ya ugali wa sembe.

Kumbuka, kila aina ya chakula ina kazi zake mwilini. Itoshe kurudia elimu ya sayansi kimu ya darasa la tano hata kama haitoi picha halisi, kwamba Protini hujenga mwili, Wanga (carbohydrate) unasidia mwili kupata nguvu, na Fat & Oil (mafuta) husaidia kudumisha jotoridi la mwili. Muhimu hapa ni hiyo pointi ya -wanga unasaidia mwili kupata nguvu.

Ndio. Vyakula aina ya wanga huanza kumeng'enywa kuanzia mdomoni kwa nguvu ya 'enzyme' iliyopo kwenye mate (salivary amylase) ambayo huvunjavunja molekyuli zinazounda wanga na kupata aina nyingine ya wanga nyepesi iitwayo Maltose. Zao hilo linapofika tumboni na baadae kwenye utumbo mwembamba huendelea kumeng'enywa kwa nguvu ya enzyme nyingine iitwayo 'Maltase' na kupatikana wanga nyepesi zaidi inayoitwa 'Glucose'. Hiyo glucose ndio inanyonywa na kuingia kwenye mzunguko wa damu na kusambazwa sehemu zote za mwili -na huko hutumika kama malighafi ya kuzalisha nguvu zinazohitajika ili binadamu andelee kuwa hai.

Pointi ya tatu: Glucose, ndiyo malighafi inayohitajika kuzalisha nguvu mwilini, glucose ni zao la wanga - ambao upo kwa wingi zaidi kwenye unga wa sembe kuliko wanga uliyopo kwenye kiasi sawa cha unga wa dona.

Hitimisho
Kwanza, si kweli kwamba ugali wa dona unamfanya mtu apate nguvu kuliko sembe kwa sababu ugali wa sembe una zalisha glucose kwa haraka zaidi na kwa wingi zaidi kuliko dona. Glucose ndio zao la ugali wa mahindi ambalo ndio malighafi ya kwanza inayohitajika kuzalisha nguvu za mwili.
Kinachotokea kwa dona ni kuchelewa kumeng'enywa na kukaa tumboni muda mrefu na hivyo kufanya mfumo wa chakula na mfumo wa fahamu 'ujue' bado kuna kitu kwenye mfumo wa chakula. Hali hii hufanya mfumo wa fahamu uridhike kwa muda mrefu na mtu kutopata hisia ya njaa...

Kwanini dona linakaa muda mrefu kwenye mfumo wa mmeng'enyo wa chakula? Ni kwa sababu ya uwepo wa maganda ya punje za hindi (ambayo yangekuwa pumba endapo mahindi yangekobolewa). Maganda haya hutengenezwa kwa aina nyingine ya wanga inayoutwa Cellulose ambayo haiwezi kumeng'enywa mwilini. Mwili wa binadamu hauna enzyme aina ya cellulase inayohitajika kwa ajili ya kumeng'enya Cellulose. Homoni hii hupatikana kwa wanyama aina ya 'ruminants' kama Ng'ombe, Mbuzi, Kondoo nk.
Hata hivyo kuna faida moja ya 'pumba' zilizopo kwenye dona - nayo ni kupata choo chepesi.

Pili, Dona lina virutubisho vingi kuliko sembe, ingawa faida si ya maana Sana kwa sababu mtu hali ugali wa dona bila kitoweo. Protini iliyopo kwenye mboga kama maharage, samaki/dagaa au nyama ni nyingi mno kiasi cha kufanya protini ya kwenye dona isiwe na maana yoyote. Madini ya chuma, calcium, potash magnesium nk yanapatikana kwenye mboga za majani kwa wingi kiasi kwamba kiwango kilichopo kwenye dona hakina maana. Vitamini zilizopo kwenye matunda zinafanya vitamini za kwenye dona zisiwe na maana. Zaidi, pamoja na kuwa na virutubisho vya ziada, Bado virutubisho hivyo vya ziada vinavyopatikana kwenye dona - si vya kiwango cha kutosha kuusaidia mwili wa binadamu kama hatakula vyakula vingine. Kwahiyo; uwepo wa virutubisho vya ziada kwenye dona si faida ya kujivunia juu ya sembe. Mwili hauwezi kutegemea protini, madini na vitamini zilizopo kwenye dona.

Tatu. Kuhusu sumu kavu. Ingawa hili si suala la ki-baiolojia lakini pengine ndio muhimu kuliko yote niliyoandika. Mahindi mengi huhifadhiwa kwa kupuliziwa madawa ya kuzuia wadudu ili yasiharibike. Ukiacha madawa hayo (kemikali) bado kuna vumbi na vitu vingine vinavyoambatana na mahindi tangu kuvunwa, kupukuchuliwa na kuhifadhiwa. Mashine ya kusaga haiondoi kemikali au vumbi au vitu vingine vilivyogandamana na mahindi, lakini ikiwa mahindi yatakobolewa angalau vitu hivyo vitapungua kwa kiasi kikubwa.

Vipi? Dona ni bora kuliko sembe?

Tazama zile pumba zinazopatikana baada ya kukoboa mahindi, zitazame tena. Unapokula dona unakula pamoja na hizo pumba. Faida yake ni moja - kupata choo bila shida. Lakini matunda yenye nyuzinyuzi/roughages (mfano; maganda ya ndani ya chungwa) mapapai, maji ya kutosha, kushughulisha mwili, vitasaidia kupata choo chepesi.

Ushauri.
Hakuna shida kula unga wa dona ikiwa mahindi yametoka shambani na kusagwa mara moja. Lakini ikiwa mahindi yametunzwa kwa muda mrefu na kwa dawa za kuzuia wadudu - ni jambo la kutafakari kuyasaga bila kukoboa. Sumu kavu - vumbi na dawa za kuzuia wadudu waharibifu vinaweza kuleta madhara ya kiafya mwilini. Nirudie tena, faida pekee ya ziada na maana ya dona juu sembe ni kupata choo chepesi...
-Sio kweli kwamba Dona linaleta nguvu kuliko sembe (neno 'nguvu' linaweza kuhutaji ufafanuzi zaidi)
-Ziada ya virutubisho vya dona haina faida ya maana juu ya sembe kwa sababu havitoshi kuunufaisha mwili bila kuongeza kutoka vyakula vingine...

Dona ni bora kuliko sembe?
Amua...
utafiti huu wa kisayansi labda ni wa darasa la 5. haiwezekani useme maganda ya mahindi ni pumba kama vile maganda hayo hayana kazi, ukiacha virutubisho vilivyomo, ni roughage, husaidia kupata choo na kuondoa tatizo la constipation. Hizo unazoita pumba ndiyo zinanenepesha mifugo, kutagisha kuku, kuongeza maziwa kwa ng'ombe n.k. Huwezi linganisha uchafu sembe na special diet dona.
 
utafiti huu wa kisayansi labda ni wa darasa la 5. haiwezekani useme

utafiti huu wa kisayansi labda ni wa darasa la 5. haiwezekani useme maganda ya mahindi ni pumba kama vile maganda hayo hayana kazi, ukiacha virutubisho vilivyomo, ni roughage, husaidia kupata choo na kuondoa tatizo la constipation. Hizo unazoita pumba ndiyo zinanenepesha mifugo, kutagisha kuku, kuongeza maziwa kwa ng'ombe n.k. Huwezi linganisha uchafu sembe na special diet dona.

Kaka shida ni kupata choo basi kula papai, point yake ni kuwa, mahindi yanakaa gharani miaka 2, yanapigwa na dawa za kuzuia wadudu, Then unaenda kuyasaga tu, madhara yake ni makubwa kuliko faida,
 
Kaka shida ni kupata choo basi kula papai, point yake ni kuwa, mahindi yanakaa gharani miaka 2, yanapigwa na dawa za kuzuia wadudu, Then unaenda kuyasaga tu, madhara yake ni makubwa kuliko faida,
Kabla ya kusaga unaweza kusafisha, kisha kuanika, yakikauka unasaga, kama vile wafanyavyo wamama wanaopika vitumbua. Ktk pointi yangu nimeainisha faida za dona, ila ww umeona kupata choo tu! Niseme hujasoma ama ni shida ya wengi ku.underrate vitu, kama huyu mtoa post.
 
Kabla ya kusaga unaweza kusafisha, kisha kuanika, yakikauka unasaga, kama vile wafanyavyo wamama wanaopika vitumbua. Ktk pointi yangu nimeainisha faida za dona, ila ww umeona kupata choo tu! Niseme hujasoma ama ni shida ya wengi ku.underrate vitu, kama huyu mtoa post.
Miye toka nizaliwe now nina zaidi ya miaka 30 ninakula sembe nikila dona tumbo linasumbua nadhani nikutokana na hizo pumba unazozitetea sijui unanishaurije
 
Kabla ya kusaga unaweza kusafisha, kisha kuanika, yakikauka unasaga, kama vile wafanyavyo wamama wanaopika vitumbua. Ktk pointi yangu nimeainisha faida za dona, ila ww umeona kupata choo tu! Niseme hujasoma ama ni shida ya wengi ku.underrate vitu, kama huyu mtoa post.

Sasa kwa maelezo hayo ni kwamba ww ni mkulima, sasa je unapoenda restaurant ukasema wakupe ugali wa dona unajua hayo mahindi yalikaa muda gani gharani? Hiyo ndio point ya msingi
 
Da nimekaribia kufika mwishoni but sijamaliza maana nimeona mengi umeyarudia kwa kutumia lugha tofauti,swali langu ni moja kwa nini unga wa sembe uzalishe glucose nyingi kuliko dona huku sembe imetokana na dona??? na katika maelezo yako hujaseme kama kuna virutubisho vyovyote labda vinaongezwa kwenye sembe??
Ni hivii kilo moja ya sembe ina wanga tu wote na wanga ndo chanzo cha glocose na kilo moja ya dona ina wanga pamoja ni vitu vingine kama protein ganda la nje la hindi, Hapo sijui nimeeleweka?
 
Ni hivii kilo moja ya sembe ina wanga tu wote na wanga ndo chanzo cha glocose na kilo moja ya dona ina wanga pamoja ni vitu vingine kama protein ganda la nje la hindi, Hapo sijui nimeeleweka?

Which means ni kila sembe na samaki na mchicha mambo ni mswano
 
Da nimekaribia kufika mwishoni but sijamaliza maana nimeona mengi umeyarudia kwa kutumia lugha tofauti,swali langu ni moja kwa nini unga wa sembe uzalishe glucose nyingi kuliko dona huku sembe imetokana na dona??? na katika maelezo yako hujaseme kama kuna virutubisho vyovyote labda vinaongezwa kwenye sembe??
Kwa sababu Sembe ina meng'enywa kwa urahisi a upesi zaidi kuliko Dona
 
Wanaume wa Dar na Madaktari wenu wa Dar endeleeni kula sembe. Mjue kuwa kwenye dona kuna zaidi ya glucose. Kuna madini ya zinc kwa wingi, kuna fibres kwa wingi, kuna aina ya protein ambayo haipo kwenye source zingine. Ila ninyi endeleeni tu, hatubishani. Nimeona kuna mpendwa hapo awali kawapa darasa la nutrition, wengine mnajifanya wajuaji, endeleeni tu, kula sembe zenu, mnazidiwa akili na panya, aaaaaaahhh!!! kwi kwi!!!! sio ajabu mpo kwenye kundi la wanunua dagaa na samaki za kopo in the name of modernization. wakati kuna samaki wa ziwani wapo. Endeleeni tu kula, it is your choice
 
Wanaume wa Dar na Madaktari wenu wa Dar endeleeni kula sembe. Mjue kuwa kwenye dona kuna zaidi ya glucose. Kuna madini ya zinc kwa wingi, kuna fibres kwa wingi, kuna aina ya protein ambayo haipo kwenye source zingine. Ila ninyi endeleeni tu, hatubishani. Nimeona kuna mpendwa hapo awali kawapa darasa la nutrition, wengine mnajifanya wajuaji, endeleeni tu, kula sembe zenu, mnazidiwa akili na panya, aaaaaaahhh!!! kwi kwi!!!! sio ajabu mpo kwenye kundi la wanunua dagaa na samaki za kopo in the name of modernization. wakati kuna samaki wa ziwani wapo. Endeleeni tu kula, it is your choice

Kabisa panya anatuzidi yy anakula mpaka mifupa ya chakula kilichotupwa, anakula nguo na godoro
 
Dona lina sumu kuvu na hilo limethibitishwa na jopo la wataalamu. Tatizo mnaendekeza ubishi kama wanzuki
Nadhani hilo andiko la sumu ya kuvu hukulielewa vizuri. Nenda kalisome tena kwa jicho la kitaaluma. sio kilaymen. Kama ungekuwa sahihi, basi mimi ningekuwa marehemu sasa, Maana dozi yangu ya ugali ni aina ya dona
 
Back
Top Bottom