Kesi ya mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (
CHADEMA),
Tundu Lissu kuhusu mashitaka ya uhaini, imeendelea katika mahakama kuu huku
mashahidi wa Jamhuri wakitoa ushahidi wao.
Madai
Kumekuwapo na nakala ya ukarasa wa mbele wa gazeti la Mwananchi la Februari 17, 2026 lenye habari kubwa ukurasa wa mbele ikidai kuwa Shahidi ameeleza makatibu wa wilaya Chadema walipewa Milioni 10 kukinukisha nchi nzima.
Uhalisia wa madai hayo
JamiiCheck imefuatilia nakala hiyo na kubaini kuwa inapotosha uhalisia.
Nakala hiyo yenye ujumbe wa kuwa shahidi amesema vingozi wa Chadema walilipwa kukinukisha ni potoshi kwani ni maneno ambayo hayapo katika nakala halisi ya Februari 17, 2026 ya gazeti la Mwananchi.
Ufuatiliaji umebaini kuwa
nakala halisi ilikuwa na ujumbe unaoseomeka;
"Mnyukano wa shahidi, Lissu" na siyo
"Shahidi: Makatibu wa wilaya Chadema walipewa milioni 10 kukinukisha nchi nzima"
Aidha, Februari 17, 2026 kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Taifa, Tundu Lissu iliendelea katika mahakama kuu ambapo mashahidi wawili wa Jamhuri walitoa ushahidi wao.
Mashahidi hao walikuwa ni ASP Geofrey Agrey Lutufye pamoja na shahidi wa kificho P4 ambao
walitoa ushahidi wao bila kutaja suala hilo la Makatibu wa Chadema wilaya kupewa pesa ili wakinukishe.
Hivyo nakala hiyo yenye ujumbe tofauti ilihariririwa kutoka kwenye nakala halisi ili kupotosha uhalisia.