Je ni kweli marekani walilenga kuwakomboa walibia au kuwalea maafa kwa faida yao?

kamili

JF-Expert Member
Feb 10, 2011
1,213
849
Tangu Muammar Gaddafi auawe kikatili na utawala kuchukuliwa na NTC wananchi wa Libya wameingia katika dhama mpya ya mateso yasiyoelezeka, kama ambavyo taweka baadhi ya ushahidi huo hapa.
Tuliona baada ya vita ya Iraq jinsi Marekani walivyomkabidhi Saddam kwenye mahakama ambayo walijua mwishowe itamhukumu kunyongwa, na jinsi kulivyozuka vitendo vya kigaidi ambavyo havikuwahi kutoke Iraq kabla haijavamiwa na Marekani. Tumeona pia uvamizi wa Afghanistani mwisho wake kumetokea vitendo vya kigaidi vya kujitoa mhanga, ambavyo Kabla ya uvamizi huo havikuwahi kuwepo.
Kwa kuwa Tanzani tuliwahi kuwasaidia Waganda kutoka mikono dhalimu ya Idd Amin na hakukuwahi kutoke visa vyovyote vya kigaidi.
Je itakuwa ni makosa kuamini kuwa uvamizi wa Marekani kwa kisingizio cha kuleta demokrasia, kupigana na magaidi, au kutaka kuondoa silaha kali kama walivyofanya kwa Iraq na sasa wanaitaka Iran, kuna lengo la kuzivuruga nchi na kuleta mauaji ya kikatili yasiyo na msingi?.
Na je kwanini vyomba vya habari vya magharibi havitangazi yale mateso yanayowapata Walibya kwa sasa?
Na je kwanini wauwaji wakubwa kama Charles Taylor kaua zaidi ya watu 200,000, Slovodan Milosovich aliyeuwa zaidi ya watu 100,000, na wauaji wa Rwanda walioua zaidi ya watu 800,000, wamefikishwa mahakama ya kimataifa ambayo licha ya kesi kusikilizwa kwa haki na uwazi haina hukumu ya kifo. Lakini watu kama Saddam, Osama aliyeuwa 3,500, Gaddafi (na sasa Seif al Islam) hawa ama waliuawa kikatili au walikabidhiwa kwenye mikono ya wanyongaji. Na kwa upande mwingine Joseph Kony anatafutwa ili akashtakiwe kwenye mahakama ya ICC. Je tofauti hii inaletwa na nini?
zaidi hapa. Libya S.O.S.: Torture in Libya [ WARNING: THESE IMAGES MAY SHOCK VIEWERS]

Wana JF naomba mjadala maana mwenzako akinyolewa wewe tia maji.
 
suala zima ni kuwa kila nchi inamaslahi yake,

ukisha jua hicho kitu jiulize kwann marekani ni mwepesi kutoa hela au kufadhili vikundi flani na kuacha vitu muhimu kama vile watu wake vijana asilimia tisa hawana kazi wala pesa za kutosha za kumudu maisha yao,


tatizo kubwa tulio nao ulimwengu huu tangu zama hizi za teknolojia ya tv, redio na njia zingine za usambazaji wa habari umekuwa wakuegemea upande mmoja wa wenye nguvu au pesa zaidi.

Mimi kinacho nisikitisha ni ile sababu ya marekani na jamaa zake kuingia iraq bila ya sababu muhimu, na kulipigwa kura na kuone kana ulimwengu ulikuwa haukubaliani na vitendo na njia waliotaka kuchukua marekani na jamaa zake lkn vyombo vya habari vili fuata kwa kugemea na kueneza taarifa za uongo kuwa iraq ina mabobu ya kuandamiza (ambayo hadi sasa tangu vita iishe mabomu hayo haja onesha na wala hakuna msamaha au majuto walio yaonesha kwa kueneza taarifa hizi za uwongo)

huwa siku zote naamini hakuna mtu anafanya kazi kubwa ya kuhatarisha maisha ya vijana wao bila ya sababu muhimu mno na hii hadi sasa tunafichwa.
 
suala zima ni kuwa kila nchi inamaslahi yake,

ukisha jua hicho kitu jiulize kwann marekani ni mwepesi kutoa hela au kufadhili vikundi flani na kuacha vitu muhimu kama vile watu wake vijana asilimia tisa hawana kazi wala pesa za kutosha za kumudu maisha yao,


tatizo kubwa tulio nao ulimwengu huu tangu zama hizi za teknolojia ya tv, redio na njia zingine za usambazaji wa habari umekuwa wakuegemea upande mmoja wa wenye nguvu au pesa zaidi.

Mimi kinacho nisikitisha ni ile sababu ya marekani na jamaa zake kuingia iraq bila ya sababu muhimu, na kulipigwa kura na kuone kana ulimwengu ulikuwa haukubaliani na vitendo na njia waliotaka kuchukua marekani na jamaa zake lkn vyombo vya habari vili fuata kwa kugemea na kueneza taarifa za uongo kuwa iraq ina mabobu ya kuandamiza (ambayo hadi sasa tangu vita iishe mabomu hayo haja onesha na wala hakuna msamaha au majuto walio yaonesha kwa kueneza taarifa hizi za uwongo)

huwa siku zote naamini hakuna mtu anafanya kazi kubwa ya kuhatarisha maisha ya vijana wao bila ya sababu muhimu mno na hii hadi sasa tunafichwa.

Kama maamuzi makubwa na ya hatari yanategemea ushawishi tu wa hao wakubwa, na siyo kuegemea ukweli au haki yaani mwenye nafasi ya fedha na vyombo vya habari ndiye anaye win kufanya lolote analotaka ndio kusema safari ya kutafuta haki bado ni ndefu sana?
 
Kama maamuzi makubwa na ya hatari yanategemea ushawishi tu wa hao wakubwa, na siyo kuegemea ukweli au haki yaani mwenye nafasi ya fedha na vyombo vya habari ndiye anaye win kufanya lolote analotaka ndio kusema safari ya kutafuta haki bado ni ndefu sana?

safari ya kutafuta haki haikuazia jana wala juzi. vyombo vya habari vimekuwa na matatizo mengi sana kwenye kueneza ukweli. kuna vyombo vingine vinapigani haki sana lkn havina uwezo wa kifedha au support toka kwa wakubwa.

kwa mfano nilio utoa hapo juu kuhusu iraq kusingiziwa kuwa ana mabomu makubwa. ukiangalia kwa undani ni kuwa vyombo vili support bila kuwa na ushahidi wowote na hatimaye wao walikuwa ni moja wa masuprt wakubwa wakitendo cha marekani kuingia iraq.

sasa kama media(cnn,aljazeera,BBC) wameweza kudanganya watu kirahisi hivi kuhusu ile ishu,je hawatudanganyi mambo mengine kwa maslahi ya mabosi wao?
 
Back
Top Bottom