Je, ni kweli CCM wanaiba kura?

Je, ni kweli CCM wanaiba kura?

Mshumaa_Tz

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2020
Posts
681
Reaction score
2,503
Watanzania naomba tuzungumze ukweli kuhusu suala la wizi wa kura ,

Je, nikweli CCM wanaiba kura?

Tujikite kwenye hoja maana kati ya sifa mbaya zinazitumika kuichafua ccm mojawapo niwizi wa kura je ? Cccm wanaiba kweli kura?
 
1. Wizi wa kura ni tukio la kufikirika tu halina uhalisia wowote na madai yoyote yanayotolewa na upinzani.

2. Kama kura singekuwa zinaibiwa nafikiri isingekuwa rahisi upinzani kushinda kwa majimbo mengi.

3. Upinzani bado haupo katika mizani ya kujilinganisha na CCM kwa kupendwa na watu wengi, hivyo suala la wizi wa kura ni la kufikirika.

4. Mpaka uchaguzi unafanyika, CCM inakuwa na uhakika wa ushindi wa kishindo kutokana na maandalizi inayofanya.

5. CCM Kuna hazina ya uongozi na Viongozi wa kustawisha uongozi wa nchi yetu kwa Karne kadhaa zijazo, hivyo hakiwezi kutumia njia ya mkato namna hiyo

CCM raha jamani, kampeni kidogo ushindi mwingi
 
Kama hawaibi basi waruhusu matokeo yote yakiwemo ya Urais kupingwa mahakamani kama ilivyo kwa Nchi za wenzetu,
Pia waruhusu mawakala wa vyama vya siasa kutoka vituoni na fomu za matokeo.

na pia vile vituo vinavyo funguliwa na wagombea (kama kile cha Lowasa mwaka 2015) viruhusiwe kukusanya takwimu za matokeo yote! Badala ya kuviharibu na hivyo kuachwa Tume ya Taifa tu ya uchaguzi kukusanya yenyewe tu.

Pia polisi waache kuwatisha wananchi wakati wa uchaguzi kwa namna yoyote ile, na mwisho Wakurugenzi wa Halmashauri waondolewe kuwa wasimamizi wa uchaguzi kutokana na ukweli kwamba wao ni makada wa chama tawala! Na hii inatengeneza kile kitu kinachoitwa 'double standard'
 
Ccm hatujawahi kuiba kura ni kelele tu hakuna ushahidi ila rais kikwete aliwahi kusema afrika mtu akishinda anasema hakuibiwa kura akishindwa anasema ameibiwa kura
Watanzania naomba tuzungumze ukweli kuhusu swala la wizi wa kura,

Je, nikweli CCM wanaiba kura?


Tujikite kwenye hoja maana kati ya sifa mbaya zinazitumika kuichafua ccm mojawapo niwizi wa kura je ? Cccm wanaiba kweli kura?
 
CCM wakielemewa wanafanya lolote kuzidi hata hilo la kuiba kura! Linapokuja suala la uchaguzi, Genge la CCM ni Genge la Maharamia lililo tayari kufanya lolote kujihakikishia "ushindi"!!

Sehemu nyepesi nyepesi, wakiona wanataka kuingia shimoni; CCM wataiba kura!

Mahali ambapo sio kazi nyepesi kuiba kura, CCM hawaoni aibu kukimbia na masanduku ya kura!!

Sehemu ambayo kukimbia na masanduku ya kura sio jambo jepesi, CCM hawaoni aibu kuzima umeme wakati zoezi la kuhesabu kura likiendelea!

Yote hayo yakishindikana, CCM hawaoni aibu kuvuruga zoezi zima la uchaguzi kama ambavyo walifanya Zanzibar mwaka 2015 kwa Jecha kumtangaza aliyemtaka yeye na Mabwana zake wa CCM!
 
Wizi wa kura upo.Kuanzia na sheria kandamizi,usimamizi,uhesabu kura na kutangaza matokeo. Pale wapinzani wanapongazwa inakuwa imetumika hekima na nguvu,umoja wapinzani.
 
Hujawahi kuwaona wakikimbia na masanduku ya kura usiku?!

Ni wezi kweli, hawasingiziwi, tena wakati mwingine na polisi wanakuwepo lakini wanatazama tu.
 
Watz naomba tuzungumze ukweli kuhusu swala la wizi wa kura ,

Je nikweli ccm wanaiba kura?


Tujikite kwenye hoja maana kati ya sifa mbaya zinazitumika kuichafua ccm mojawapo niwizi wa kura je ? Cccm wanaiba kweli kura?
Kura wanaiba sana tu.

Na ujinga mwengine wananchi wao huwapigisha Kura zaidi ya mara moja na kwa vituo tofauti nishashuhudia.
 
Ni aibu
leo 2020 mwenzi wa sita mtanzania Kuuliza swali la wizi wa kura
 
1. Wizi wa kura ni tukio la kufikirika tu halina uhalisia wowote na madai yoyote yanayotolewa na upinzani.

2. Kama kura singekuwa zinaibiwa nafikiri isingekuwa rahisi upinzani kushinda kwa majimbo mengi.

3. Upinzani bado haupo katika mizani ya kujilinganisha na CCM kwa kupendwa na watu wengi, hivyo suala la wizi wa kura ni la kufikirika.

4. Mpaka uchaguzi unafanyika, CCM inakuwa na uhakika wa ushindi wa kishindo kutokana na maandalizi inayofanya.

5. CCM Kuna hazina ya uongozi na Viongozi wa kustawisha uongozi wa nchi yetu kwa Karne kadhaa zijazo, hivyo hakiwezi kutumia njia ya mkato namna hiyo

CCM raha jamani, kampeni kidogo ushindi mwingi
We nikada kura zinaibiwa vizuri tu, rejea kipindi cha kikwete mabox mangapi yalikamatwa ambayo hayakuesabiwa, rudi shule!
 
Mkuu nakupa Siri za Wizi wa Kura ,CCM wana mbinu kibao za wizi, moja wapo ni kuweka Masanduku ya kura waliyompigia mgombea wao kura za ndio juu ya dali kukiwa na watu, mkishamaliza mkishaingiza ndani ,wanafungua dali wanayatoa ya ukweli wanashusha feki chini.
 
Ccm hatujawahi kuiba kura ni kelele tu hakuna ushahidi ila rais kikwete aliwahi kusema afrika mtu akishinda anasema hakuibiwa kura akishindwa anasema ameibiwa kura
Kura zinaweza kuibwa? Kama ndio basi huwezi kukataa.. mimi nasema kura zinawrza kuibwa na zinsibwa. Mwenye kuiba ana sababu
 
Kama hawaibi kura kwanini WAHOFIE TUME HURU ambayo haitakuwa answerable kwa dikteta? Kwanini Mkapa atoe wito wa kuwepo TUME HURU ili kuhakikisha Uchaguzi HURU na wa HAKI?

Watz naomba tuzungumze ukweli kuhusu swala la wizi wa kura ,

Je nikweli ccm wanaiba kura?


Tujikite kwenye hoja maana kati ya sifa mbaya zinazitumika kuichafua ccm mojawapo niwizi wa kura je ? Cccm wanaiba kweli kura?
 
1. Wizi wa kura ni tukio la kufikirika tu halina uhalisia wowote na madai yoyote yanayotolewa na upinzani.

2. Kama kura singekuwa zinaibiwa nafikiri isingekuwa rahisi upinzani kushinda kwa majimbo mengi.

3. Upinzani bado haupo katika mizani ya kujilinganisha na CCM kwa kupendwa na watu wengi, hivyo suala la wizi wa kura ni la kufikirika.

4. Mpaka uchaguzi unafanyika, CCM inakuwa na uhakika wa ushindi wa kishindo kutokana na maandalizi inayofanya.

5. CCM Kuna hazina ya uongozi na Viongozi wa kustawisha uongozi wa nchi yetu kwa Karne kadhaa zijazo, hivyo hakiwezi kutumia njia ya mkato namna hiyo

CCM raha jamani, kampeni kidogo ushindi mwingi
Wanaibaa
 
Back
Top Bottom