Je! Ni anguko la ccm?

Je! Ni anguko la ccm?

falesy

Senior Member
Joined
Mar 15, 2006
Posts
105
Reaction score
17
TANZANIA NA CCM TUNAKOELEKEA (Kuna makosa ya kutofumbia macho)

Niliwahi kusema (miongoni mwa post zangu kuhusu uchaguzi wa Arumeru Mashariki) katika mtandao wa jamii wa Face book (FB) kuwa "ARUMERU ndo start point ya COUNTDOWN ya vitu viwili ama;
1. Ukombozi wa Nchi kwa njia ya BARROT; Ama
2. Tungeanzia hapo kuhesabu siku za mwisho wa CCM hii ya sasa;
Sasa kwa yale yaliyotokea huko (Lusinde issue na mengine); ni wazi tumeanzia pazuri maana kwa sehemu zingine za Tanzania watasema "kwani Arumeru wameweza wana nini; na sisi tushindwe tuna nini?"
Pia watasema "tumejua sasa CCm si mahali salama maana wamekuja watatukana wazee wetu (Maana Slaa kwa kule si tu mwanasiasa bali ni mtu wa heshima kwao kama wengine kina Lowassa) Kwa hiyo; kuanzia sasa; CCM wakiwa na mkutano wakileta mjumbe wa NEC wategemee kutokuona mtu mkutanoni maana watu hawako tayari kuona wanatukanwa Pia CCM wakimpeleka Mkapa popote; wasitegemee kuona mtu maana wanaogopa kutangaziwa kuwa wao si wa ukoo walioko
Kwa sasa nguvu pekee ya CCM iliyobaki (naomba nistaje) pekee ambaye wakimtumia bila hila watafika mbali. Pia hakukuwa na ubaya wowote kuendelea kumtumia Mzee Malecela kwani ni Mjumbe wa kudumu CC na NEC
Lakini; Am sorry to say: CCM, it is too late; and in the end only the true Legends of the party wll remain in others (most of them) will go to their new parties (CCK---CCJ); join other weak parties now like AFP and form their new parties kama hiki cha juzi from CUF (is another CCm follower)
Wito kwa mwenyekiti wangu; Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete;
i. Ni wakati wa kuwajibisha wahujumu ndani ya Chama; maana kwa jinsi ambavyo mambo yameendeshwa Arumeru na kwingine(kama Kirumba Mwanza); ni wazi wajumbe wa Chama hawakuwa kwa ajili ya kutafuta ushindi wa Chama bali ama kukoroga mapishi ya kubomoa chama, ama kujijenga wao wenyewe kwa siasa zao
ii. Kamati kuu ya NEC ya CCM lazima itoe maamuzi na tamko dhidi ya kauli za viongozi wa Chama wawili ambao wamesababisha upotevu wa kura; ya kwanza ni ile ya Mwenyekiti wa Chama Mstaafu juu ya ukoo wa Nyerere, jambo ambalo halikuwa na tija kwa kampeni za Arumeru na la pili ni ile hotuba ya Livingstone Lusinde ambayo imetuchafua na itaendelea kutuchafua kila tunakopita
iii. Ushiriki wa kampeni wa Mh. Lowassa na Mh. Sitta Arumeru na Kirumba (kwa mfuatano huo) haukuwa kwa ajili ya kampeni za waliyoendea bali walifanya kampeni zao binafsi (wanatakiwa watoe maelezo kwa nini walifanya hivyo)
iv. Je! mh. mwenyekiti; kwa nafasi yako kama rais wa jamhuri una kisasi kuwa huwezi kushirikiana na wabunge wa upinzani? Ninavyokuelewa la hasha; ila kwa kampeni za Arumeru imeonekana kuwa utakuwa tayari pamoja na mawaziri (hasa wa ardhi) kusuluhisha matatizo ya wana Arumeru iwapo tu wangemchagua Siyoi; je huo ndiyo msimamo wako?
v. Kwa hali ilivyo sasa; na hasa kuzingatia kuwa wananchi wa Tanzania hatuna tena imani na CCM; CC ya NEC ya CCM ifikie uamuzi kuwa; ikitokea kuna uchaguzi mdogo umetokea hapa katikati kabla ya 2015, basi CCM isisimamishe mgombea ili kuwasahaulisha watanzania (angalau kwa kipindi) yaliyotokea Arumeru, ama kama itashiriki basi viongozi wa kitaifa waende tu wale wa sekretariet na si wengine kama hawa kina Lusinde, Pia kwa wakti huu kwa vile wapiga kura wengi ni vijana basi tuwaamini vijana kama (mimi Falesy Mohamed kibassa), January Makamba, mwigulu Nchemba; Hussein Bashe maana ndo wenye mvuto (usiniulize mimi mvuto nimeutoa wapi, wewe nipe kazi)
v. CCM tumekuwa na kampeni saidizi kwa CHADEMA na kwa muda mrefu hakuna aliyelisemea isipokuwa kwenye miongoni mwa vikao Mh. Lowassa aliligusia kwa kusema "Kampeni dhidi ya UFISADI ilikuwa ni ya CHADEMA hivyo kuibeba kama ya ccm ni hatari (maneno nimehaulisha); na NEC haijatoa msimamo juu ya hii kampeni; hivi hatujui kuwa kutaja hilo neno tu UFISADI lina link na CHADEMA? Au tumeisahau Operesheni SANGARA ambayo mzee wangu Makamba aliwahi kuibeza na kuiita Operesheni Dagaa? Au tumesahau kuwa CDM walishafanya hii kampeni hadi ikaingia vichwani mwa watanzania na wakaelewa? Au tumesahau kuwa hii ina hatimilki ya CDM? Au hatujui kuwa wao wakiisema kwa maneno mepesi wanaeleweka kuliko sisi? Ninakuomba mwongozo mwenyekiti!
Mwisho; natoa mwito kuwa CCM ijiimarishe kwa kuchukua wataalamu wa kweli na kuwaweka hadharani badala ya kufanya nao kazi kwa siri ili wasaidie chama katika mipango mikakati na watakaofanya tafiti yakinifu kuelekea maeneo ya mapambano (Angalia CDM wana maprofessor makini kama Prof Safari, Prof Baregu na vijana wasomi makini). Kwa nini CCM tumefanya siri wakati siri za chama zinavuja kila siku? Ninalipenda wazo lako la kutumia vijana wasomi lakini kujitegemeza sana na walioko vyuoni si wakati wake maana hawana "mentors" wa uhakika!!! napenda tuwe na maprofessor ambao tutawatumia kwa ajili ya Coaching na Mentoring ya vijana kutoka vyuoni si kiitikadi tu bali kitafiti kitaifa na Chama ili wanapokuwa na ukada wa Chama wanjua Taifa ndo namba moja!

I remain Royal to my party CCM and my Nation TANZANIA
 

Attachments

Hisiahazipo tena kaka. Kuna realities and facts. Salamu zenyu sana.
 
Mawazo yako ni tofauti sana na wale waliopewa dhamana kwenye chama.,chama hicho sasa hakina mwenyewe,kila mtu kivyake
 
TANZANIA NA CCM TUNAKOELEKEA (Kuna makosa ya kutofumbia macho)

Niliwahi kusema (miongoni mwa post zangu kuhusu uchaguzi wa Arumeru Mashariki) katika mtandao wa jamii wa Face book (FB) kuwa "ARUMERU ndo start point ya COUNTDOWN ya vitu viwili ama;
1. Ukombozi wa Nchi kwa njia ya BARROT; Ama
2. Tungeanzia hapo kuhesabu siku za mwisho wa CCM hii ya sasa;
Sasa kwa yale yaliyotokea huko (Lusinde issue na mengine); ni wazi tumeanzia pazuri maana kwa sehemu zingine za Tanzania watasema "kwani Arumeru wameweza wana nini; na sisi tushindwe tuna nini?"
Pia watasema "tumejua sasa CCm si mahali salama maana wamekuja watatukana wazee wetu (Maana Slaa kwa kule si tu mwanasiasa bali ni mtu wa heshima kwao kama wengine kina Lowassa) Kwa hiyo; kuanzia sasa; CCM wakiwa na mkutano wakileta mjumbe wa NEC wategemee kutokuona mtu mkutanoni maana watu hawako tayari kuona wanatukanwa Pia CCM wakimpeleka Mkapa popote; wasitegemee kuona mtu maana wanaogopa kutangaziwa kuwa wao si wa ukoo walioko
Kwa sasa nguvu pekee ya CCM iliyobaki (naomba nistaje) pekee ambaye wakimtumia bila hila watafika mbali. Pia hakukuwa na ubaya wowote kuendelea kumtumia Mzee Malecela kwani ni Mjumbe wa kudumu CC na NEC
Lakini; Am sorry to say: CCM, it is too late; and in the end only the true Legends of the party wll remain in others (most of them) will go to their new parties (CCK---CCJ); join other weak parties now like AFP and form their new parties kama hiki cha juzi from CUF (is another CCm follower)
Wito kwa mwenyekiti wangu; Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete;
i. Ni wakati wa kuwajibisha wahujumu ndani ya Chama; maana kwa jinsi ambavyo mambo yameendeshwa Arumeru na kwingine(kama Kirumba Mwanza); ni wazi wajumbe wa Chama hawakuwa kwa ajili ya kutafuta ushindi wa Chama bali ama kukoroga mapishi ya kubomoa chama, ama kujijenga wao wenyewe kwa siasa zao
ii. Kamati kuu ya NEC ya CCM lazima itoe maamuzi na tamko dhidi ya kauli za viongozi wa Chama wawili ambao wamesababisha upotevu wa kura; ya kwanza ni ile ya Mwenyekiti wa Chama Mstaafu juu ya ukoo wa Nyerere, jambo ambalo halikuwa na tija kwa kampeni za Arumeru na la pili ni ile hotuba ya Livingstone Lusinde ambayo imetuchafua na itaendelea kutuchafua kila tunakopita
iii. Ushiriki wa kampeni wa Mh. Lowassa na Mh. Sitta Arumeru na Kirumba (kwa mfuatano huo) haukuwa kwa ajili ya kampeni za waliyoendea bali walifanya kampeni zao binafsi (wanatakiwa watoe maelezo kwa nini walifanya hivyo)
iv. Je! mh. mwenyekiti; kwa nafasi yako kama rais wa jamhuri una kisasi kuwa huwezi kushirikiana na wabunge wa upinzani? Ninavyokuelewa la hasha; ila kwa kampeni za Arumeru imeonekana kuwa utakuwa tayari pamoja na mawaziri (hasa wa ardhi) kusuluhisha matatizo ya wana Arumeru iwapo tu wangemchagua Siyoi; je huo ndiyo msimamo wako?
v. Kwa hali ilivyo sasa; na hasa kuzingatia kuwa wananchi wa Tanzania hatuna tena imani na CCM; CC ya NEC ya CCM ifikie uamuzi kuwa; ikitokea kuna uchaguzi mdogo umetokea hapa katikati kabla ya 2015, basi CCM isisimamishe mgombea ili kuwasahaulisha watanzania (angalau kwa kipindi) yaliyotokea Arumeru, ama kama itashiriki basi viongozi wa kitaifa waende tu wale wa sekretariet na si wengine kama hawa kina Lusinde, Pia kwa wakti huu kwa vile wapiga kura wengi ni vijana basi tuwaamini vijana kama (mimi Falesy Mohamed kibassa), January Makamba, mwigulu Nchemba; Hussein Bashe maana ndo wenye mvuto (usiniulize mimi mvuto nimeutoa wapi, wewe nipe kazi)
v. CCM tumekuwa na kampeni saidizi kwa CHADEMA na kwa muda mrefu hakuna aliyelisemea isipokuwa kwenye miongoni mwa vikao Mh. Lowassa aliligusia kwa kusema "Kampeni dhidi ya UFISADI ilikuwa ni ya CHADEMA hivyo kuibeba kama ya ccm ni hatari (maneno nimehaulisha); na NEC haijatoa msimamo juu ya hii kampeni; hivi hatujui kuwa kutaja hilo neno tu UFISADI lina link na CHADEMA? Au tumeisahau Operesheni SANGARA ambayo mzee wangu Makamba aliwahi kuibeza na kuiita Operesheni Dagaa? Au tumesahau kuwa CDM walishafanya hii kampeni hadi ikaingia vichwani mwa watanzania na wakaelewa? Au tumesahau kuwa hii ina hatimilki ya CDM? Au hatujui kuwa wao wakiisema kwa maneno mepesi wanaeleweka kuliko sisi? Ninakuomba mwongozo mwenyekiti!
Mwisho; natoa mwito kuwa CCM ijiimarishe kwa kuchukua wataalamu wa kweli na kuwaweka hadharani badala ya kufanya nao kazi kwa siri ili wasaidie chama katika mipango mikakati na watakaofanya tafiti yakinifu kuelekea maeneo ya mapambano (Angalia CDM wana maprofessor makini kama Prof Safari, Prof Baregu na vijana wasomi makini). Kwa nini CCM tumefanya siri wakati siri za chama zinavuja kila siku? Ninalipenda wazo lako la kutumia vijana wasomi lakini kujitegemeza sana na walioko vyuoni si wakati wake maana hawana "mentors" wa uhakika!!! napenda tuwe na maprofessor ambao tutawatumia kwa ajili ya Coaching na Mentoring ya vijana kutoka vyuoni si kiitikadi tu bali kitafiti kitaifa na Chama ili wanapokuwa na ukada wa Chama wanjua Taifa ndo namba moja!

I remain Royal to my party CCM and my Nation TANZANIA
wewe CCM au Mamluki?naona kama unapiga majungu vile , ya Arumeru yamepita acha wananchi wa Arumeru wenyewe waendeshe jimbo lao siyo muda wa propaganda tena.N lini Rais alisema atashrikiana na Wana-Arumeru endapo SIOI angeshinda kama si majungu hayo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom