Je, mwanao anadhurika na diapers za Moflix?

Je, mwanao anadhurika na diapers za Moflix?

Prof Griff

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2008
Posts
6,762
Reaction score
5,276
Hizi pampers aka diapers ni za bei poa sana lkn naona mtoto anapata matatizo ya kubabuka ngozi ya chini ya miguu na viganja vya mikono.

Je, kuna wengine wamepatwa na maswahiba kama haya kwa wanao?
 
Sipendi mwanangu avae diapers hata ziwe za Bei ghali, mi baba ila ni mwendo wa clean nepi hata Kama mama hatokuwapo namfunga mwenyewe, nafua mwenyewe, uvivu wa kushika uchafu wa mtoto ndo sababu ya hayo ma pempas
 
Sipendi mwanangu avae diapers hata ziwe za Bei ghali, mi baba ila ni mwendo wa clean nepi hata Kama mama hatokuwapo namfunga mwenyewe, nafua mwenyewe, uvivu wa kushika uchafu wa mtoto ndo sababu ya hayo ma pempas
Hizi old school nappies ni changamoto sababu watoto hawapendi haswa usiku sababu hazifyonzi majimaji
 
Hizi old school nappies ni changamoto sababu watoto hawapendi haswa usiku sababu hazifyonzi majimaji
Anaweza vaa pempers usiku ila mchana si vyema.

Ni kweli usiku ni usumbufu kwake na kwako pia sababu mtaamka hata mara 5.ila mchana jitahidi avae za kawaida sababu anaweza hata asivae pia.
 
Kwa ulichokiandika ni kama uandike, hivi mwanao anadhurika na NIDO ya COWBELL.

Au mwanao anadhurika na COLGATE YA WHITEDENT?!

Kimsingi Pampers ni jina la kampuni inayotengeneza Diapers za watoto..... So hapa product ni Pampers na Pampers ni product brand name....
 
Kama uko Dar nakushauri beba mbili tatu wapelekee TBS pale ubungo kama malalamiko, kama sio wao basi ni TMDA pale external.

Kwa wanavyo mgwaya magu watalifanyia kazi. Ukiona kimya nenda tena kufuatilie, kama wakikuzingua nenda wizarani. Wataisoma namba.
 
Back
Top Bottom