Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,264
- 105,428
Zaidi, kama mtu anakubali logic na anaelewa "proof by contradiction" na anajua kusoma, na kashafuatilia thread hii, ataona kwamba uthibitisho huo unaodaiwa ushatolewa mara lukuki hapa.Sasa atathibitishaje kitu ambacho anaamini hakipo!?.Nyinyi mnaoamini kipo ndiyo mnapaswa kuthibitisha uwepo wa Mungu.Mi namwelewa sana Kiranga.
Acheni kuzunguka mbuyu wenyewe.
Sasa kama kipofu anabishana tofauti ya rangi nyekundu na bluu wakati haioni, mimi siwezi kuwajibika kwa hilo.
Na kwa kweli huo utakuwa ushahidi zaidi kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo.
Maana angekuwepo, dunia isingekuwa na vipofu.