Je, manabii hawa wanaombea na watu wanapata kweli?

Je, manabii hawa wanaombea na watu wanapata kweli?

Joined
May 29, 2022
Posts
51
Reaction score
100
Kwema viongozi!

Natumaini mko poa kabisa mnaendelea na maisha kama kawaida.

Swali langu leo nataka kufahamu, je hawa watumishi wa Mungu huwa wanaombea watu na wanapata kweli wanachokiomba?

Kama kuna mtu ambaye alishahudhuria katika moja ya makanisa hayo na yumo humu ndani atupe ushuhuda na wengine twende tukauone mkono wake bwana.
 
Nenda kwa imani, nenda kichwa kichwa…. kama kondoo.
 
Kwema viongozi! Natumaini mko poa kabisa mnaendelea na maisha kama kawaida. Swali langu leo nataka kufahamu, je hawa watumishi wa Mungu huwa wanaombea watu na wanapata kweli wanachokiomba? Kama kuna mtu ambaye alishahudhuria katika moja ya makanisa hayo na yumo humu ndani atupe ushuhuda na wengine twende tukauone mkono wake bwana.

Kuna tatizo nilipata nikiwa mjamzito nikawa nahudhuria sana hospital ila still bado hali ilibaki pale pale, nilienda kwa Mwamposa nikiwa na Imani naenda kupona , Mungu ni mwema nilipona na nilijifungua salama. Kwa upande wangu Mwamposa na Mwakasege ni watumishi ninaowaamini.
 
Mithali 26:4
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, Usije ukafanana naye.


Ukawe na jioni njema mtu wa Mungu [emoji120]


Dah kumbe na mistari ya biblia unaijua, basi wewe ni kilaza.

Uliwahi kuona wapi mtu anaulizia nguvu ya watumishi wa Mungu tena mitandaoni kama anaulizia dawa za kienyeji?

Una akili sawa sawa kweli wewe? Yani unaenda kwenye social network kuulizia kama mchungaji fulani ana nguvu za Mungu au hana nguvu za Mungu?

Hata mimi ambae ni muislamu siwezi kuulizia habari za Bulldozer au Baba lao kwa staili yako.

Narudia tena wewe ni kichaa.
 
Hata kwenye Biblia imeandikwa usimtafute alie hai miongoni mwa wafu.

Inafundishwa unapaswa kutumiwa hekima na busara unapo tafuta jambo fulani.

Unatafuta samaki basi nenda baharini au ziwani
 
Pole kwa shida uliyonayo ndgu yangu.

Ishu ya kutafuta justification ni ngumu sana mitandaoni we tafuta njia ya kutatua hilo tatizo lako, kama umeona huko kwa mwamposa/mussa ndo kunafaa we nenda tu hapa hutapata kitu zaidi ya kuchanganywa zaidi.
 
Dah kumbe na mistari ya biblia unaijua, basi wewe ni kilaza.

Uliwahi kuona wapi mtu anaulizia nguvu ya watumishi wa Mungu tena mitandaoni kama anaulizia dawa za kienyeji?

Una akili sawa sawa kweli wewe? Yani unaenda kwenye social network kuulizia kama mchungaji fulani ana nguvu za Mungu au hana nguvu za Mungu?

Hata mimi ambae ni muislamu siwezi kuulizia habari za Bulldozer au Baba lao kwa staili yako.

Narudia tena wewe ni kichaa.
We mchawi kumbe una akili zako[emoji1][emoji1][emoji1]
 
Kuna tatizo nilipata nikiwa mjamzito nikawa nahudhuria sana hospital ila still bado hali ilibaki pale pale, nilienda kwa Mwamposa nikiwa na Imani naenda kupona , Mungu ni mwema nilipona na nilijifungua salama. Kwa upande wangu Mwamposa na Mwakasege ni watumishi ninaowaamini.
Haya, asante... Kuna mwingine mwenye ushuhuda? 👂
 
Ni kweli ingawa mimi siamini kati ya hawa manabii. Nakumbuka mwaka 2011/12 kuna mama aliugua baada ya kupona akawa kiwete. Siku kuna nabii katembea mtaa wetu muujiza ukamshukia huyo mmama akapona kabisa ila alimuonya asirudi tena dhambini.

Mmama baada ya kupona akaanza kuruka na viben10 na tungi kwa sana matokeo yake 2016 alitangulia mbele za haki. Kwenye ibada ya kumzika nabii akakumbushia lile onyo.

Miujiza ipo mkuu kikubwa imani yako ndio itakuponya.
 
Back
Top Bottom