asante kwa jibu lako mkuu Superb2014 japo siombi msaada wa kutaka kujua kama inawezekana au lah kwa sababu kwangu mi binafsi huwa naamini ni kitu ambacho hakiwezekani,hivyo lengo kuu la uzi huu ni wana MMU kushare mambo yoyote yaliyowahi kuwapata maishani mwao kutokana na kuamimi katika kumbadilisha mtu au jitihada za kutaka kubadilika kwa ajili ya mtu au kuona kutoka kwa jirani au Rafiki au ndugu ambao waliamini Katika kumbadilisha mtu au kubadilika kwa sababu ya mtu Fulani.Kumbadilisha mtu mzima mwenye meno 32 ni shida sana, ngoja wengine waje watakusaidia zaidi.
labda nikupe mfano mdogo tu mkuu zamani niliamini katika nguvu ya kumbadilisha mtu,lakini kuna mtu alinifanya niamini kuwa hakunaga kitu kinaitwa kumbadilisha mtu mzima,licha ya kumpenda sana na yeye kunipenda sana na kujitahidi sana kutumia mbinu kadhaa za kutaka abadilishe tabia yake Fulani konki hakiuwezekana,and very bad enough tayari kashatangulia mbele za haki mpaka sasa hivi tunavyoongea,hivyo from then na kutoka kwenye experience hiyo nilijifunza kuwa mtu mzima habadilishwi na naendelea kuamini hivyo kutokana na mifano mbali mbali nayoona kutoka kwa ndugu jamaa marafiki na majirani,hivyo ningependa kupata uzoefu mwingine mbalimbali kutoka kwa members humu.asante kwa jibu lako mkuu Superb2014 japo siombi msaada wa kutaka kujua kama inawezekana au lah kwa sababu kwangu mi binafsi huwa naamini ni kitu ambacho hakiwezekani,hivyo lengo kuu la uzi huu ni wana MMU kushare mambo yoyote yaliyowahi kuwapata maishani mwao kutokana na kuamimi katika kumbadilisha mtu au jitihada za kutaka kubadilika kwa ajili ya mtu au kuona kutoka kwa jirani au Rafiki au ndugu ambao waliamini Katika kumbadilisha mtu au kubadilika kwa sababu ya mtu Fulani.
mkuu kila mwa MMU hii mada inamhusuKwahiyo sisi ambao sio wahenga huu uzi hautuhusu??
ah okay sawa sawa mamie princess ariana asante kwa experience uliyoshare na sisi,kwa hiyo tuseme kwa uzoefu huo uliotupa unamaanisha as kwa wewe unaamini mwanamke anaweza kubadilishwa ila mwanaume hapana si ndio mamie,kama nimeelewa vizuri?nmewahi kubadilishwa, Nikawa navaa nikabu mpaka tulipoachana , imenifanya watu wengi wadhani mimi ni muslim,maana sometimes navaa sana majuba
Ila wanaume hawabadilikagi kirahisi na sijawahi kutaka kumbadilisha mtoto wa mtu.. Let asshole be asshole you will sleep better.
ah okay sawa sawa mamie princess ariana asante kwa experience uliyoshare na sisi,kwa hiyo tuseme kwa uzoefu huo uliotupa unamaanisha as kwa wewe unaamini mwanamke anaweza kubadilishwa ila mwanaume hapana si ndio mamie,kama nimeelewa vizuri?
na je alitumia nini kukubadilisha huyo mwandani wako?ulikuwa unahisije kwa yale mabadiliko ndani yako?ulikuwa ukifurahia au ulifanya tu kwa sababu yake?
okay good mamie asante kwa kushare experience yako pamoja nasiKama kitu kipo ndani ya uwezo wangu sioni sababu ya kumkwaza mwandani wangu, hasa vitu kama mavazi baby hataki nivae jeans sivai kama najua tunaonana navaa anachopenda kwanini nimfanye asiwe comfortable na mimi! Uzuri nikionana na baby mara2 tatu wakati tunaanza mahusiano lazima nimuulize wewe unahisi nikivaaje napendeza? Jumpsuit/suruali/dress? atakachochagua nafollow trend...Na hio sio kwa wanawake wote ni baadhi mmoja wapo mimi wengine kama hunogewi na anavyovaa chapa lapaHapangiwi
Nilishambadilishaga x.man angu, kipindi nasoma alikua mgum sana yaan akikutana namm salam anataka anipe tano tukitembea hatak nimshike mkono..nikiwa na rafiki zangu eti hatak mazoea anatoa salam uku anapita anaenda kunisubiria mbele yaan mkavumkavuu
Siku nilimtolea uvivi nkamchana ukweli akabadilika mwez tuu, siku nlimtembelea kwake alikua na washkaji nilivopush tu mlango akaja kunivua viatu niingie yaan wenzie walishangaa wakaanza kumcheka eti uhuni wote mapenzi yamembadilisha.
Mambo madogo yoote nlimbadilisha ila bangi mbaka leo anavuta.
alinambia tangu akiwa mtoto alikua muhun.hahahahahahahahahahaha hapo mwisho nilipobold pamenichekesha sana my dear
hongera kwa kuweza kumbadilisha mwandani wako,lakini nina maswali machache,je mwandani wako alikuwa msela tokea utotoni mwake?au nisema usela wa mwandani wako ilikuwa ni utu wake wa ndani au ni tabia aliyojifunza tu ukubwani labda kutokana na peer pressure? unahisi ni kwa nini imeshindikana kwake kuacha bangi?
aisee sasa Mr swahiba92 kulingana na ufafanuzi wako hapo juu kuhusiana na hulka na tabia huyu mwenzetu anaweza akawa amefall wapi mkuu,haiba yake au tabia yake huo uhini mpaka akaweza kubadilika? na tukisema ni tabia tuseme wazazi walikuwa wasela pia hivyo na yeye akawa msela,au imekaaje hii mkuu?alinambia tangu akiwa mtoto alikua muhun.
asante kwa mchango wako mujarabu kabisa mkuu Mzimu wa Kolelo,kwa hiyo wewe mwenzetu unakubali kuwa inawezekana kumbadilisha mtu ila ni baada ya muda mrefu na kwa hatua ndogo ndogo,hivyo unaweza kukubali kuingia katika ndoa na mtu unayeona kabisa ana shida Fulani ambazo wewe binafsi huoendezwi naye ukiamini hatua kwa hatua na baada ya muda unaweza kumbadilisha mwenzi huyo?Inawezeka lkn kumbuka kwanza kinachombadilisha mtu ni uhalisia
si wewe na maneno yako yenye vina na mizani au matendo kutaka aige unavyofanya au namna unavyoishi
inahitaji muda na kujitolea na wakati mwingine hadi ghalama za kifedha kwa huyo mtu ndugu mpenz unayetaka kumbadilisha 7bu ni mambo yenye kuhitaji moyo
binadamu ameumbwa kwa utashi wa kuamua lipi afanye lipi asifanye na amepewa akili kutambua lipi zuri lipi baya ndo mana hata ukimaliiza kufanya zinaa huwa unajutia na pengne hata kuahidi nafsi yako kutorudia 7bu unajua fika ni chukizo kwa MUNGU lkn wkt unaikimbilia zinaa unaina jambo zuri tu 7bu akili yako inakutuma hvyo
huwezi kumtaabisha mtu kwa ulazima eidha Manpower ulokuwa nayo au pesa ama mapenzi kutaka awe unavyotaka wewe au watu fulani
huwezi kuitaabisha akili yake kumladhimisha kutaka kumuaminisha jambo ambalo anaona kwake ni sawa kuwa si sawa sana sana utaishia kupata maigizo tu
njia nzuri na sahihi kumbadilisha mtu kwanza
ni kukubaliana na hali halokuwa nayo eidha mlevi mwizi malaya anayevuta sigala madaw nk n.k
kisha kuanza kwenda naye taratibu bila kuingilia mipaka ya mtindo wake wa maisha au kumpa mahubili mengi yaan kuwa naye katika life style yake onesha unakubaliana naye 7bu ni maisha yake
ila unatakakiwa pia uoneshe kuwa wewe hayo mambo huwezi yafanya
*hapa ndipo pana msingi katika kumfikishia ujumbe ili asikuone mnafiki au km wengne na mahubili yao
inahitajika yeye ndo aone kuwa jambo hilo kwa wewe huna manufaa nalo
lkn haliathiri urafiki au mahusuano yenu na hata ktk maongezi kwa mfano akihitaji kujua kwann hupendi kunywa pombe au hupendi mademu au kwann hutaki tupige deal hii ya wizi nk inahitajika busara katika kumueleza ili kumuwin
mfn :- unaweza kumjibu mm sinywi pombe 7bu inaniathili sana kiafya hapo sasa unaweza kupangilia vina jinsi gani pombe inavyokuathiri kiafya kumbuka usianze kumtolea mifano ya wengne au kumuelezea itavyomuathiri yeye mana unaweza kupata jibu moja kwa walevi wanzinzi au wavutaji walokubuhu atakwambia nina miaka 20 navuta sigara au nina miaka 10 mm napiga kavu bila condom na sijapata hata gono achilia mbali ukimwi
unachopaswa ni kutumia uhalisia kufikisha ujumbe kwa wakati huo kuendana na mazingira na maongezi mnayozungumza kwa wakati huo
ambapo km mnakuwa mpo pamoja sana kwa kipindi kirefu na una nia hasa ya kumbadilisha basi taratibu ataanza kwa kujaribu kuishi km wewe au kufanya km wewe mwisho wa siku anabadilika kabisa
mfano mm niliwahi mbadirisha rafiki tu tulikutana katika nyumba moja tuliopanga kuweza kiswali swala 5 km ninvyoswari bila mm kujua kuwa kuna mambo nilokuwa nayafanya yalikuwa yanamvutia aliniambia tu mwenyewe "unajua kila saa tupo wote lkn ikifika muda wa swala wewe unainuka unatuacha ss lkn unarudi unakuwa na sisi tunaendelea na maisha na mara chache sana unaongea kuhusu dini ulazimishi mtu awe km wewe unagusia tu mambo machache muhimu hvyo nikajiuliza kwan mm nashindwa nn
mana wewe ukienda ukiswali ukirudi na mambo yako yanaenda vilevile hvyo basi na mm nikaona nianze kuswali km wewe ndio" mana mpk sasa nami naswali
hvyo ni machache katika mengi ambayo yanaweza kumbadilisha mtu mzima kuwa katika tabia bora au maisha yenye afya nk
Sent using Jamii Forums mobile app
asante kwa ufafanuzi yakinifu mkuu swahiba92 umeeleza vizuri sana mkuuNinachofahamu mimi huwa kuna kitu kinaitwa HULKA NA TABIA.. Sasa hulka ni vile vitu ambavyo mtu amezaliwa navyo kabisa. Mfano kiburi au Ukimya.. hivi vitu mtu hawezi kubadilika labda kwa wale wanaoamini Vitabu vitakatifu tunasema Hadi Mungu aingilie kati na kutenda muujiza ndipo mtu anaweza kubadilika. Lakini TABIA ni vitu ambavyo mtu huwa navyo kulingana na mazingira tu, na mazingira yakibadilika au kampan ya watu wake wa karibu ikibadilika na yeye hubadilika.
Mfano ukarimu. Binti akizaliwa ktk familia ya watu wakarimu na yeye atakuwa tu mkarimu coz mfano kila siku wazazi wanaarika wageni na yeye atajikuta tu aanavutiwa na kuanza kuarika watu wa rika lake na asipofanya hivyo wazazi watakuwa wanamuuliza wewe huna marafiki? Lakini binti huyu akiondoka ktk mazingira ya ukarimu ya nyumbani na kwenda chuo na kukutana na kampan tofauti au Akaolewa na mwanamme Asiye mkarimu na asiyependa wageni Anaweza kubadilika na yeye ukarimu ukaisha au yule Mme Akaambukizwa na yeye Akawa mkarimu.
Hivyo Tabia hubadilika kulingana na mazingira uliyopo na kampan ya watu ulio nao. Lakini Hulka ya mtu Haibadiliki wala Haibadilishwi na mtu mwingine.. Isipokuwa Mungu mwenyewe Aliyemuumba..
Sent using Jamii Forums mobile app