Je, inaruhusiwa kukataa cheo ndani ya Idara?

Je, inaruhusiwa kukataa cheo ndani ya Idara?

Kivule

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2012
Posts
639
Reaction score
662
Habari ndugu zangu,

Kwa mfano mtu kaajiriwa Serikalini yuko Idara fulani na akateuliwa kua Mkuu wa Kitengo fulani kwenye hiyo Idara na mkuu wake wa idara lakini yeye hapendi kua kiongozi anapenda kua mtumishi wa kawaida.

Je, kwa Sheria za Utumishi inaruhusiwa kukataa uteuzi ulioteuliwa na Mkuu wako wa Idara?
 
Sasa umekuwa mtumishi ili uwe kuruta daima au? Ni uzezeta na hofu za kijinga kukataa cheo.
Nikuombe usipende kutumia maneno makali kwa mtu usiyemfahamu. Ata Mimi siwezi kukujibu Ivo sababu sikufahamu na ata kama nakufahamu nisingeweza kutumia neno "zezeta". Naweza kukujibu kama ulivonijibu pengine una umri mkubwa kama mzazi wangu au naweza pia kua na umri mkubwa kama mzazi wako.
 
Kuna jamaa yangu alikuwa polisi miaka hiyooo mkoa fulani. Alikuwa trafiki, alipandishwa cheo akatolewa kwenye utrafiki, akaona ujinga akaacha kazi.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
Ahsante sana mkuu, kwanini hakuandika barua ya kukataa uteuzi au ukiteuliwa hakuna kukataa? Kama una shughuli zako pembeni za kukuingizia hela na zinahitaji uangalizi ni vyema kubaki mfanyakazi wa kawaida tu
 
ukiongezewa cheo maana yake ni kukuongezea majukumu.

Unaweza ukafurahi kumbe wanataka kukupoteza.

Binafsi sipendi cheo, mwaka 2009 walitaka kunipandisha cheo kuwa mganga mkuu wa hospital flan hapa nchini nilikataa katakata.

watu walinishangaa wakiwemo madaktari wenzangu lkn mm mipango yangu zaid ya hicho cheo.

Ukiwa una akili timamu utajua kuwa cheo ni kibaya sana japo kila mtu ana priority yake.
 
ukiongezewa cheo maana yake ni kukuongezea majukumu.

Unaweza ukafurahi kumbe wanataka kukupoteza...
Nashukuru sana mkuu Kwa maneno yako ya busara kabisa. Ulichokiongea apo ni kikubwa sana na kwa upande wangu nakuelewa sana. Ulifanya utaratibu gani kukataa cheo walichokupa? Uliandika barua ya kukataa cheo? Na je hakukua na shinikizo na kubanwa kisheria?
 
Hi hoja kwa Nini hutaki kupanda cheo au uhamisho pana Nini Happ ulipo Sasa hivi? Takukuru na vyombo vya dola lazima vikufuatilie

Pia kwenye barua ulikubali kuwa utakuwa tayari kufanya kazi yeyote utakayopangiwa iweje Leo ugome?

Huyo traffic SEMA ilikuwa enzi hizo za ujinga ingekuwa Leo angekoma
Naomba usiingize siasa mkuu ayo mambo ya awamu. Mi naamini awamu zote wamefanya kazi nzuri na kila awamu kiu kubwa ni kutuletea maendeleo. Hakuna kiongozi ambae anataka aondoke bila kuleta maendeleo. Tuishie apo.
 
Hi hoja kwa Nini hutaki kupanda cheo au uhamisho pana Nini Hapo ulipo Sasa hivi? Takukuru na vyombo vya dola lazima vikufuatilie

Pia kwenye barua ulikubali kuwa utakuwa tayari kufanya kazi yeyote utakayopangiwa iweje Leo ugome?

Huyo traffic SEMA ilikuwa enzi hizo za ujinga ingekuwa Leo angekoma
Mkuu una mawazo mgando Sana....au upo kule wanakoishi na rushwa Kama ndugu!
 
Kuna jamaa yangu alikuwa polisi miaka hiyooo mkoa fulani. Alikuwa trafiki, alipandishwa cheo akatolewa kwenye utrafiki, akaona ujinga akaacha kazi.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
Ukiwa traffic uko kwenye ulaji. Asubuhi unatoka nyumbani na miatano ya nauli jioni unarudi na laki moja
 
1. Kwenye barua yako ya kuajiriwa uliyosaini kwenye job descriptions si umekubali kuwa utafanya pamoja na any other duties assigned by supervisor? Sasa supervisor anakupa majukumu mengine unakataa maana yake nini si anarejea kwenye mkataba uliosaini na kukulima tu ?

2.hizi sababu eti sitaki majukumu kisa mambo yangu ya kuingiza kipato pembeni yatakwama ni ya ujjinga!..kwa hiyo nchi yako unataka ije kujengwa na Otieno.wa Kenya au okonkwo wa Nigeria?..

3. Wewe kwani hukwenda induction training na kuapa kuwa sasa umekubali kuhenga nchi na kutekeleza majukumu yako ?....Unaweza kuwa na haki ya kukataa majukumu lakini si kwa sababu hizo za kimtaani taani ..
 
Ndio inaruhusiwa Bora kuwa mfagizi lumumba kuliko kuwa Polepole maana hata mbinguni hutaenda.
 
Naona swali halipati majibu makini ya kisheria. Mimi si mwajiriwa wa serikali lakini swali nimelipenda.

Kwa mnaojenga hoja kwamba ulazima wa kukubali cheo kipya ni kwamba kwenye mkataba wa ajira mtu anakuwa amekubali "na majukumu mengine yoyote atakayopangiwa na mwajiri"...Je mwajiri akiamua kukubadilishia majukumu na kukupa machache zaidi ambayo yanastahili cheo kidogo zaidi (ambapo itaendana na malipo kupungua), na hapo pia utakubali tu kwa vile muajiri ameamua kukupangia majukumu mengine?

Chukulia umeajiriwa kama mwalimu. Halafu mkuu wako anakuagiza ufue nguo za wanafunzi. Hilo ni "jukumu lingine".. utakubali? Na ukijataa, je sheria itakulinda pamoja na mkataba "kuruhusu" kupangiwa majukumu mengine?

Naomba tutafakari hayo kabla ya kukimbilia majibu mepesi ya "utapewa na majukumu mengine". Ukipandishwa cheo ambacho huwezi kukimudu, na nafasi yako ya sasa unaitendea haki, sioni kwanini ulazimike kukubali.. na swali la mdau ndo linakuja: utaratibu wa kukataa cheo (politely) ukoje?
 
... Changamoto unatolewa kwenye kitengo ambacho daily unapiga mishindo,unaonana na wateja moja kwa moja,daily mipango. ..sasa unapandishwa cheo huko unaenda kusubili vipoaho uchwara.....na jamaa kabana hakuna safari....
 
Ndiyo, kama zipo sababu za msingi.
Lakini kaa ukijua utakuwa unapishana na mema siku daima hata pale utakapokuwa upo tayari kuyafaidi
 
Mkuu Kivule, hiyo uliyopewa ni "offer" ambayo unaweza kuikubali ama kuikataa. Ingawaje si jambo la kawaida kwa muajiriwa kuaminiwa ili apewe madaraka ya juu akakataa, kwa kuwa muajiri atapata mashaka juu uadilifu na uaminifu wako.

Katika hali ya kawaida ukipata madaraka ya juu, huambatana na ongezeko la mshahara na marupurupu mengine. Sasa kwa kukataa kwako ni lazima muajiri wako ataona kuna mgogoro kati ya "personal objectives" dhidi ya "organisational objectives" hali inayopelekea wewe kusimama ktk maslahi yako binafsi, badala ya muajiri kuwa yanapaswa kupewa kipaumbele.

Lakini ktk dhana za menejimenti ya rasilimali watu, ipo ile inayotambulika kama kanuni ya Petro, ambayo ili kutopoteza maana yake kwa lugha ya Kiingereza tunaweza kuinukuu kama ifuatavyo:

The Peter Principle is a concept in management developed by Laurence J. Peter, which observes that people in a hierarchy tend to rise to their "level of incompetence": The underlying fact being employees are promoted based on their success in previous jobs until they reach a level at which they are no longer competent, as skills in one job do not necessarily translate to another.

Pengine hili ndilo linakupa wasiwasi na kutokujiamini. Ondoa mashaka ukijukumishwa zaidi na muajiri wako kuwa tayari kujukumika, kwani kuna faida nyingi za kupandishwa cheo zaidi ya kubaki na cheo kimoja tu kwa muda mrefu.
 
Nikuombe usipende kutumia maneno makali kwa mtu usiyemfahamu. Ata Mimi siwezi kukujibu Ivo sababu sikufahamu na ata kama nakufahamu nisingeweza kutumia neno "zezeta". Naweza kukujibu kama ulivonijibu pengine una umri mkubwa kama mzazi wangu au naweza pia kua na umri mkubwa kama mzazi wako.
Soma tena coment yangu utaelewa
 
Kila siku naona wafanyakazi wakuandika humu na kulalamikia kutokupandishwa madaraja au waliopandishwa wakidai stahiki zinazoambatana na madaraja hayo.

Leo naona kinyume chake.

Kama hutaki cheo usidai mshahara wa ngazi hiyo, ukikataa cheo kimoja hutopandishwa tena hata siku ukiomba.

Nakushauri chukua ulichopewa, ukisusa wenzio watakula.

Unamuogopa nani humo ofisini au vyeti feki unaogopa uta ji expose.

Dunia hii inamaajabu sana na hayatoisha.
 
Back
Top Bottom