Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 10,588
- 7,956
Marahaba kwa wale walio wadogo kwangu na shikamoni wakubwa wangu wana JF members. Jamani kuna kitu kina nitatiza kidogo katika suala la heshima, uungwana, na privacy hapa Tanzania. Nauliza hivi kwa sababu simple common sense inaniambia kuwa nyumba ya kulala wageni pale unapochukua chumba, you are given all the respect as mpangaji and that you are protected by law na wenye hiyo nyumba. Sasa najiuliza, hii kasi ya kukamata watu bila ridhaa yao wanapokuwa wanajifariji kwenye ma guest nani ameidhinisha? Kama ni serikali, sasa kwanini wabunge hawakamatwi kule Dodoma na hapa mjini? Hivi ni uungwana kweli kwenda kuvunja guest na kumkamata mtu anakula raha kwa pesa zake yeye mwenyewe? Kugegedana ni kitu cha kawaida, hakuna mtu anayekubali kwenda guest bila kuwa na mapungufu nyumbani kwake. Yes, kuna wanaokwenda guest kujiuza lakini pia ni shida yao si ya umma, na pia kuna wale wanaokwenda kwa ajili ya kukidhi mahitaji yao. Sasa kwa nini waingiliwe na kudhalilishwa wakati wanakula raha zao? Jamani, tujirekebishe kwani tunaonekana wapumbavu kwa wageni waliopo hapa nchini.