Je huu ndiyo udukuzi unavyokuwa?

Je huu ndiyo udukuzi unavyokuwa?

Eustow Jw

Member
Joined
Jan 1, 2019
Posts
36
Reaction score
62
Habari wanajukwaa.

Naombeni msaada wenu Kwa anayejua hili tatizo ambalo lipo kwenye laini yangu ya Vodacom

Mara kadhaa kwenye simu yangu nasikia inasema

Samahani namba unayopiga haipatikani Kwa sasa tafadhari jaribu tena baadaye,

Baada ya muda tena inajirudia hivyohivyo,

Wakati mwingine inasema huna salio la kutosha kupiga simu hatimaye napokea sms ya kupata Mkopo wa nipige tafu, ingawa ninakuwa na dk nyingi tu,

Yote hayo yanavyofanyika kwenye simu nikiangalia ili nijue kuwa nimempigia nani
Sikuti namba yoyote ile.

Juzi nilipiga Vodacom huduma Kwa wateja nikaishia kujibiwa kuwa niweke password kwenye simu kwamba inajipiga,
Wakati huo namwambia kuwa sioni namba yoyote Ile kama nimeipigia, mtoa huduma anakazia Tena Kwa kusema weka password tu, na hata hakusema ngoja nikutazamie nione shida ipo wapi.


Na muda si mrefu nimesikia simu hii imepiga halafu mtu akapokea akakohoa kama mara tatu hivii,

Akasema Hallooow nikamjibu kuwa wewe ni nani akajibu Kwa lugha nisiyoifahamu hata kwenye kiingereza haipo,
Bora ingekuwa kiingereza ili nihojiane naye nijue kinachoendelea, ikabidi niweke alama ya Aeroplane mode ndipo ikakata,
Hiyo alama huwa naiweka endapo tatizo hili nikilisikia na sauti hukata,

Simu ninayoitumia ni AZUMI,
Kwhy mpaka sasa sijajua shida Ni nini.

Je huu ndo udukuzi wenyewe ?

Naombeni msaada kwenu waungwana.
 
Simu yenyewe tu jina lake ni jina la.... Ndo hao wanapokea na kujipigia sometime. Na hiyo ndo lugha yao. Azumi ni Azumini kirefu chake. Hatari sana. Kanunue simu zinazofahamika hizo nyingine si za matumizi ya binadamu.
 
Simu yenyewe tu jina lake ni jina la.... Ndo hao wanapokea na kujipigia sometime. Na hiyo ndo lugha yao. Azumi ni Azumini kirefu chake. Hatari sana. Kanunue simu zinazofahamika hizo nyingine si za matumizi ya binadamu.
Unamaanisha wanachukua taarifa zangu ?
 
Nunua sim card ya mtandao mwingine, weka kwenye simu yako uone kama hayo mambo yanaendelea kutokea.

Yakiendelea basi tatizo ni simu, nunua simu nyingine.

Yasipoendelea tatizo ni hiyo sim card, nenda ufanye kurenew hiyo line uone itakuaje au achana nayo tu kama sio namba muhimu.
 
Simu yenyewe tu jina lake ni jina la.... Ndo hao wanapokea na kujipigia sometime. Na hiyo ndo lugha yao. Azumi ni Azumini kirefu chake. Hatari sana. Kanunue simu zinazofahamika hizo nyingine si za matumizi ya binadamu.
Dah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom