Nafaka
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 12,157
- 31,334
Kuna ndugu yangu flani huu ni mwaka wa tatu anadai ameokoka, anasali sana, anafunga sana. Lakini tatizo langu kwake ni kwamba anajitenga na watu kasoro familia na marafiki wa karibu wa huyo anayedai ni mama wake wa kiroho. Ila waliobaki anasema ni wachawi. Story zake kila siku anasema wamempiga flani katika maombi, yani story zake ni za kuwapiga watu katika maombi tu.
Mara fulani kafa ile ajali ilikuwa imetegeshewa sisi ili Mungu katuokoa ikampata fulani. Kuna kipindi alipkuwa anaiona anasema oooh mara sijui ndugu yetu gani alikuwa kanifuata ananiroga basi anaanza kuniombea nanivuta nywele na masikio.
Nikaona isiwe tabu nikawa simtembelei sana. Yani kila failure ya maisha yake anasema karogwa japo mambo mengi kafail kwa kutofuata ushauri na kufanya kama inavyotakiwa.
Sasa jana tumekorofishana baada ya kuniambia kuwa sijui mwanangu karogwa, anahitaji kuombewa nitoe sadaka awekewe wakifu eti anadai wakati wanasali na mama yake wa kiroho wameambiwa hivyo na Mungu.
Ikabidi nijaribu kumwelewesha kwamba, mimi mambo yake mengi siyaamini. Nikamwambia kajitenga na kila rafiki yake kwasababu ya kuamini kila mtu mchawi, hadi mijusi anaiua anasema inatumwa na wachawi wanaitumia kupeleleza.
nikajaribu kureason naye nikamwambia mimi naona failure ya maisha yake nyingi zimetokana na yeye mwenyewe ajifunze kutokana na makosa kuliko kutafuta scapegoat.
Kuna kipindi kila mara alikuwa anaanguka akiwa anaomba eti roho mtakatifu amempanda anasema kuongea na kutoa utabiri ambao kwa maono yangu haukuwahi kutokea. Nikamwambia kipindi hicho nilianza kuwa na mashaka kuwa huenda kapata tatizo la kisaikolojia.
Nilivyo mwambia hivyo akasema Mungu anisamehe akanikatia simu. Nimebaki ninasikitika muda mwingine ninawaza au mimi ndiye nimepotoka nina imani haba. Maana mimi naona anapotea anatumia muda mwingi akiomba saana pasipo kujishughulisha wala kuwaza atatokaje.
Mara fulani kafa ile ajali ilikuwa imetegeshewa sisi ili Mungu katuokoa ikampata fulani. Kuna kipindi alipkuwa anaiona anasema oooh mara sijui ndugu yetu gani alikuwa kanifuata ananiroga basi anaanza kuniombea nanivuta nywele na masikio.
Nikaona isiwe tabu nikawa simtembelei sana. Yani kila failure ya maisha yake anasema karogwa japo mambo mengi kafail kwa kutofuata ushauri na kufanya kama inavyotakiwa.
Sasa jana tumekorofishana baada ya kuniambia kuwa sijui mwanangu karogwa, anahitaji kuombewa nitoe sadaka awekewe wakifu eti anadai wakati wanasali na mama yake wa kiroho wameambiwa hivyo na Mungu.
Ikabidi nijaribu kumwelewesha kwamba, mimi mambo yake mengi siyaamini. Nikamwambia kajitenga na kila rafiki yake kwasababu ya kuamini kila mtu mchawi, hadi mijusi anaiua anasema inatumwa na wachawi wanaitumia kupeleleza.
nikajaribu kureason naye nikamwambia mimi naona failure ya maisha yake nyingi zimetokana na yeye mwenyewe ajifunze kutokana na makosa kuliko kutafuta scapegoat.
Kuna kipindi kila mara alikuwa anaanguka akiwa anaomba eti roho mtakatifu amempanda anasema kuongea na kutoa utabiri ambao kwa maono yangu haukuwahi kutokea. Nikamwambia kipindi hicho nilianza kuwa na mashaka kuwa huenda kapata tatizo la kisaikolojia.
Nilivyo mwambia hivyo akasema Mungu anisamehe akanikatia simu. Nimebaki ninasikitika muda mwingine ninawaza au mimi ndiye nimepotoka nina imani haba. Maana mimi naona anapotea anatumia muda mwingi akiomba saana pasipo kujishughulisha wala kuwaza atatokaje.
