mapipando
JF-Expert Member
- Jun 8, 2015
- 2,922
- 3,563
Heshima kwenu wakuu,
Kuna jamaa hapa kazini alikuwa anazungumzia mambo kadha wa kadha kuhusu mahusiano.Jambo moja kati ya hayo limenifanya kulipa uzito wake na kuona ni vyema nikalifikisha hapa angalau lijadiliwe kwa mapana yake.
Amesema hivi,mtu yeyote ambaye tarehe yake ya kuzaliwa ni tasa, mtu huyo kamwe hatadumu kwenye ndoa yake kama ataoa ama kuolewa na mtu ambaye tarehe yake ya kuzaliwa pia ni tasa. Ikiwa sababu moja kubwa ni kwamba watu wa namna hiyo huwa siku zote wanapenda kuwa juu na wababe hata kama wamekosa.
Kaenda mbali zaidi na kusema kuwa amefanya utafiti hasa katika ndoa zilizovunjika na zile zenye migogoro mikubwa na kugundua kuwa watu hao tarehe zao za kuzaliwa ni tasa.
Nini mtazamo na uelewa wako juu ya hili?
Karibuni tujadiliane pengine tutapata ufumbuzi wa matatizo ya kuvunjika kwa mahusiano/ndoa.
Kuna jamaa hapa kazini alikuwa anazungumzia mambo kadha wa kadha kuhusu mahusiano.Jambo moja kati ya hayo limenifanya kulipa uzito wake na kuona ni vyema nikalifikisha hapa angalau lijadiliwe kwa mapana yake.
Amesema hivi,mtu yeyote ambaye tarehe yake ya kuzaliwa ni tasa, mtu huyo kamwe hatadumu kwenye ndoa yake kama ataoa ama kuolewa na mtu ambaye tarehe yake ya kuzaliwa pia ni tasa. Ikiwa sababu moja kubwa ni kwamba watu wa namna hiyo huwa siku zote wanapenda kuwa juu na wababe hata kama wamekosa.
Kaenda mbali zaidi na kusema kuwa amefanya utafiti hasa katika ndoa zilizovunjika na zile zenye migogoro mikubwa na kugundua kuwa watu hao tarehe zao za kuzaliwa ni tasa.
Nini mtazamo na uelewa wako juu ya hili?
Karibuni tujadiliane pengine tutapata ufumbuzi wa matatizo ya kuvunjika kwa mahusiano/ndoa.