Rais wa Matajiri
JF-Expert Member
- Sep 14, 2018
- 1,475
- 607
Hello Tanzania!
___________________
Unajua ukifanya ulinganifu wa Utawala wa Mkapa, Mwinyi, Kikwete na huyu John Utagundua kuwa Ndugu John ndiye Kiongozi anaedaiwa kuungwa mkono na Genge là Wahuni wengi zaidi Kuliko wakina mkapa sababu watu kama Mtei walishindwa Kuunga mkono juhudi za Mwalimu Yaani walikuwa tayari kupoteza kazi Kupinga kama kuna Uhuni ulifanywa na Wenye Nguvu, Léo wakina Mtatiro wakina waitara, wakina Ryoba wanaunga mkono eti mtu si Falsafa au itikadi Unaweza kusema huu ni uhalifu zaidi wa Kifikra kwa Vizazi vyetu
Anyway naomba kuzama kwenye Hoja Nimekuwa nikifuatilia kwa kina hii hamahama tena nimefanya hivyo mtu kwa mtu , Mwanzoni sikupata shaka sana na hii ni baada ya kuhama Dk Mollel na rafiki yangu Mh Maulid Mtulia ikiwa ni pamoja na madiwani wengine wenye vinasaba vya U-CCM kwani binafsi niliamini wameamua kweli Kwa ridhaa yao kurejea walikotoka na nikaipongeza sana CHADEMA kwa kusimamia demokrasia kwa vitendo kwa kuwaache Viongozi hao waende kwa amani na nadhani Watanzania ni mashahidi Wa hili,Lakini leo
najaribu kuifikiria CCM Kwa Upande mmoja na CHADEMA Kwa Upande Wa pili, Najaribu kuitazama CCM kama chama dola na CHADEMA kama chama kinachoitaka dola wakati wowote kuanzia mwaka 2020. Najaribu kuifikiria hatma ya CCM yenye dola dhidi ya CHADEMA hii yenye nguvu midhili ya tembo dume aliyejeruhiwa Kwa mbaali naanza kuuelewa huu mchezo.
Watanzania wenzangu nisaidieni kujibu haya maswali muhimu Kwa ili kuleta uelewa Wa pamoja juu ya mada yetu hii.
1 ) Je kunauwezekano Wa CHADEMA kutuma vijana wake CCM kwaajili ya mipango yao ya mbeleni kupitia hamahama hizi zinazoendelea?
2 ) Je ni kweli umaarufu wa CCM umeongezeka sasa baada ya wabunge/madiwani Wa Upinzani kuiunga mkono CCM na Rais Magufuli JP?
3 ) Je ni kweli kwamba CHADEMA wameshindwa na hawana uwezo wa kuzuia hii hamahama hata Kwa kumtoa kafara mmoja Wa wasaliti hao ili kuwa fundisho kwa wengine?
4 ) Kwanini Uongozi Wa CHADEMA umekuwa kimya hata Kwa kukemea tu na mara nyingi wamekuwa wakifanya vikao na wahanga hawa siku chache kabla ya kujitosa kwao CCM?
5 ) Kwanini CHADEMA wameamua kuachana na marudio ya Uchaguzi ili kuipa nafuu ya gharama za uchaguzi CCM na Serikali yake na kulifanya zoezi hili la hamahama kuwa rahisi zaidi je ni kwa faida ya nani?
Hebu tuulizane Sisi Kwa Sisi hawa vijana wanaotimkia CCM toka Upinzani ni kweli kwamba fikra na nadhiri zao wanakwenda nazo huko CCM au wanaziacha CHADEMA yaani phenotipically wataonekana ni CCM wakati huohuo genotypically wakisalia kuwa CHADEMA ? Je ni kweli kwamba huyu mbunge/diwani X anaweza kusahau kirahisi harakati alizozifanya Kwa zaidi ya mwongo mmoja na nusu au zaidi eti kwaajili ya kurudia Ubunge/Udiwani wake uleule?
Hebu tujiulize kama huyu mbunge/diwani anapofika tu CCM kwa ubunge/Udiwani wake moja kwa moja anakuwa kiongozi Wa Chama na hii ni Kwa mujibu Wa katiba ya CCM, Inamtaja Mbunge/diwani kuwa ni mjumbe katika vikao mbalimbali vya Chama, Nisaidieni wanaCCM kuna-siri yeyote itakayoihusu CCM itasitirika machoni pa huyu diwani/mbunge ili asiipate na kuipeleka alikotoka niambieni nani anajua hili?
Narudia swali langu " Je kwenye hii
hamahama nani beneficiary mkubwa kati ya CCM na CHADEMA hapo baadae ?" tukiiaagalia hii hamahama kwa jicho la tatu la moyoni kunakitu kita-klik tu akilini na hicho ninachokizungumzia..
Kuna haja ya wanaccm na CCM yenyewe kutafakari kwa kina Ugeni huu mkubwa kama wanavyouita wao ,Kuna mwanamziki mmoja Wa Bongo fleva amewahi kuimba naomba kuunukuu mstari mmoja anasema " Mbwa ni mbwa hata umpe Mchina " anamaanisha Mbwa yule ambae wewe unaogopa kumla kisa ni Mbwa ila Mbwa huyohuyo ni kitoweo muhimu tena kitamu kweli kweli kwa Mchina japo anabaki kuwa ni Mbwa yule yule. Ni shetani peke yake ndio anaweza akaamini kuwa Patrobas Katambi ni mwanaCCM leo na anaipenda Kwa dhati tena ni tahira tu anayeweza kudhania Marwa Ryoba anakwenda CCM hivihivi au Waitara yule intelijensia mkuu CHADEMA eti leo nae ni MwanaCCM hii hamahama inamaswali mengi kuliko majibu, Ni wiki mbili tu zimepita tangu nimwone Ryoba Marwa kwa macho yangu akiwa na kikao kizito na Viongozi wakuu Wa CHADEMA pale Jijini Dodoma hata yeye anajua kwani niliwaona wote, Je kilikuwa kikao cha kumpa maelekezo mujarabu?? Narudia tena ni kichaa peke yake tu ndio anayeweza kuamini kuwa huu mkakati wa hamahama si mkakati Wa CHADEMA/Upinzani unaoratibiwa na CCM pasipo kujua , Narudia ni laani pekee ndio zinaweza kukufanya uamini kuwa Julius Mtatiro ni mwanaccm kama anavyojitangaza, Eti mtoto Wa Marehemu Chacha Zakayo Wangwe yule shujaa Wa CHADEMA Tarime/Mara mdogo wangu Zakayo Wangwe amabe familia yao inafadhiliwa na CHADEMA hata sasa eti nae ni mwana-CCM nasema ni kichaa tu ndio anayeweza kuamini mambo haya tena ni kwa ukichaa wake tu na si vinginevyo.
CCM najua kunawatu wachache miongoni mwenu wanafaidika na mkakati huu moja kwa moja hasa kwaku-overestimate dau la kinachosemwa na CHADEMA kuwa ni "Dau la Ununuzi" lakini hili game CHADEMA wametoboa kirahisi zaidi tena kwa uratibu wenu ninyi wenyewe kumbukeni hizi ni Siasa sio Team za mpira na usajili Wa wachezaji, Hebu fikiria hili kama Upinzani unajumla ya madiwani 1,074 na Wabunge zaidi ya 116 yaani tunazungumzia Viongozi wapya Wa CCM toka Upinzani 1,190 soon watakuwa ndani ya CCM kama viongozi tena Wa wananchi/Chama, CCM simameni mnionesheni ulipo " Usalama Wa chama chenu " kuelekea 2020, Kumbukeni hawa ni watu watakaokuwa na ushawishi na maamuzi ndani na inje ya chama kwenye majimbo/Kata watakazokuwa wakiziongoza,Sikieni hii CCM itawafaa sana " Mtu kuwa mpinzani ni Fikra zake sio Sare za chama anazovaa wala kadi aliyonayo " CCM na WanaCCM lazima muongeze Umakini kwenye hili, Eti unamsikia mtu kama Bernard Mwakyembe anasema nae ni CCM lakini ukimtazama usoni haelekei kabisa kuwa ni MwanaCCM Kuna kitu tunaita " Facial expression " kamwe huwezi kuamini na ili kuamini hili lazima uwe na faili tena lililojaa pale Dodoma kwenye ile hospitali yetu maarufu iliyoko mlimani, nasema awamu hii CCM mmejishikisha pabaya huku, na hakika CHADEMA 2020 watafanya makubwa tuupe muda nafasi hakika utanena.
Wanawalaghai eti wanakuja kumuunga mkono Rais Magufuli JP, Jiulizeni kweli Magufuli anaweza kumvutia Mbunge/diwani kabla ya kuwavutia Wanachi ? Naomba kuwapongeza "think tankers " wote Wa CHADEMA kwa hili 2020 CCM vipande vipande.
Moderators, Uzi huu siku ya kuvunjika vipande vipande Kwa CCM nitaomba muurudie plzzz
___________________
Unajua ukifanya ulinganifu wa Utawala wa Mkapa, Mwinyi, Kikwete na huyu John Utagundua kuwa Ndugu John ndiye Kiongozi anaedaiwa kuungwa mkono na Genge là Wahuni wengi zaidi Kuliko wakina mkapa sababu watu kama Mtei walishindwa Kuunga mkono juhudi za Mwalimu Yaani walikuwa tayari kupoteza kazi Kupinga kama kuna Uhuni ulifanywa na Wenye Nguvu, Léo wakina Mtatiro wakina waitara, wakina Ryoba wanaunga mkono eti mtu si Falsafa au itikadi Unaweza kusema huu ni uhalifu zaidi wa Kifikra kwa Vizazi vyetu
Anyway naomba kuzama kwenye Hoja Nimekuwa nikifuatilia kwa kina hii hamahama tena nimefanya hivyo mtu kwa mtu , Mwanzoni sikupata shaka sana na hii ni baada ya kuhama Dk Mollel na rafiki yangu Mh Maulid Mtulia ikiwa ni pamoja na madiwani wengine wenye vinasaba vya U-CCM kwani binafsi niliamini wameamua kweli Kwa ridhaa yao kurejea walikotoka na nikaipongeza sana CHADEMA kwa kusimamia demokrasia kwa vitendo kwa kuwaache Viongozi hao waende kwa amani na nadhani Watanzania ni mashahidi Wa hili,Lakini leo
najaribu kuifikiria CCM Kwa Upande mmoja na CHADEMA Kwa Upande Wa pili, Najaribu kuitazama CCM kama chama dola na CHADEMA kama chama kinachoitaka dola wakati wowote kuanzia mwaka 2020. Najaribu kuifikiria hatma ya CCM yenye dola dhidi ya CHADEMA hii yenye nguvu midhili ya tembo dume aliyejeruhiwa Kwa mbaali naanza kuuelewa huu mchezo.
Watanzania wenzangu nisaidieni kujibu haya maswali muhimu Kwa ili kuleta uelewa Wa pamoja juu ya mada yetu hii.
1 ) Je kunauwezekano Wa CHADEMA kutuma vijana wake CCM kwaajili ya mipango yao ya mbeleni kupitia hamahama hizi zinazoendelea?
2 ) Je ni kweli umaarufu wa CCM umeongezeka sasa baada ya wabunge/madiwani Wa Upinzani kuiunga mkono CCM na Rais Magufuli JP?
3 ) Je ni kweli kwamba CHADEMA wameshindwa na hawana uwezo wa kuzuia hii hamahama hata Kwa kumtoa kafara mmoja Wa wasaliti hao ili kuwa fundisho kwa wengine?
4 ) Kwanini Uongozi Wa CHADEMA umekuwa kimya hata Kwa kukemea tu na mara nyingi wamekuwa wakifanya vikao na wahanga hawa siku chache kabla ya kujitosa kwao CCM?
5 ) Kwanini CHADEMA wameamua kuachana na marudio ya Uchaguzi ili kuipa nafuu ya gharama za uchaguzi CCM na Serikali yake na kulifanya zoezi hili la hamahama kuwa rahisi zaidi je ni kwa faida ya nani?
Hebu tuulizane Sisi Kwa Sisi hawa vijana wanaotimkia CCM toka Upinzani ni kweli kwamba fikra na nadhiri zao wanakwenda nazo huko CCM au wanaziacha CHADEMA yaani phenotipically wataonekana ni CCM wakati huohuo genotypically wakisalia kuwa CHADEMA ? Je ni kweli kwamba huyu mbunge/diwani X anaweza kusahau kirahisi harakati alizozifanya Kwa zaidi ya mwongo mmoja na nusu au zaidi eti kwaajili ya kurudia Ubunge/Udiwani wake uleule?
Hebu tujiulize kama huyu mbunge/diwani anapofika tu CCM kwa ubunge/Udiwani wake moja kwa moja anakuwa kiongozi Wa Chama na hii ni Kwa mujibu Wa katiba ya CCM, Inamtaja Mbunge/diwani kuwa ni mjumbe katika vikao mbalimbali vya Chama, Nisaidieni wanaCCM kuna-siri yeyote itakayoihusu CCM itasitirika machoni pa huyu diwani/mbunge ili asiipate na kuipeleka alikotoka niambieni nani anajua hili?
Narudia swali langu " Je kwenye hii
hamahama nani beneficiary mkubwa kati ya CCM na CHADEMA hapo baadae ?" tukiiaagalia hii hamahama kwa jicho la tatu la moyoni kunakitu kita-klik tu akilini na hicho ninachokizungumzia..
Kuna haja ya wanaccm na CCM yenyewe kutafakari kwa kina Ugeni huu mkubwa kama wanavyouita wao ,Kuna mwanamziki mmoja Wa Bongo fleva amewahi kuimba naomba kuunukuu mstari mmoja anasema " Mbwa ni mbwa hata umpe Mchina " anamaanisha Mbwa yule ambae wewe unaogopa kumla kisa ni Mbwa ila Mbwa huyohuyo ni kitoweo muhimu tena kitamu kweli kweli kwa Mchina japo anabaki kuwa ni Mbwa yule yule. Ni shetani peke yake ndio anaweza akaamini kuwa Patrobas Katambi ni mwanaCCM leo na anaipenda Kwa dhati tena ni tahira tu anayeweza kudhania Marwa Ryoba anakwenda CCM hivihivi au Waitara yule intelijensia mkuu CHADEMA eti leo nae ni MwanaCCM hii hamahama inamaswali mengi kuliko majibu, Ni wiki mbili tu zimepita tangu nimwone Ryoba Marwa kwa macho yangu akiwa na kikao kizito na Viongozi wakuu Wa CHADEMA pale Jijini Dodoma hata yeye anajua kwani niliwaona wote, Je kilikuwa kikao cha kumpa maelekezo mujarabu?? Narudia tena ni kichaa peke yake tu ndio anayeweza kuamini kuwa huu mkakati wa hamahama si mkakati Wa CHADEMA/Upinzani unaoratibiwa na CCM pasipo kujua , Narudia ni laani pekee ndio zinaweza kukufanya uamini kuwa Julius Mtatiro ni mwanaccm kama anavyojitangaza, Eti mtoto Wa Marehemu Chacha Zakayo Wangwe yule shujaa Wa CHADEMA Tarime/Mara mdogo wangu Zakayo Wangwe amabe familia yao inafadhiliwa na CHADEMA hata sasa eti nae ni mwana-CCM nasema ni kichaa tu ndio anayeweza kuamini mambo haya tena ni kwa ukichaa wake tu na si vinginevyo.
CCM najua kunawatu wachache miongoni mwenu wanafaidika na mkakati huu moja kwa moja hasa kwaku-overestimate dau la kinachosemwa na CHADEMA kuwa ni "Dau la Ununuzi" lakini hili game CHADEMA wametoboa kirahisi zaidi tena kwa uratibu wenu ninyi wenyewe kumbukeni hizi ni Siasa sio Team za mpira na usajili Wa wachezaji, Hebu fikiria hili kama Upinzani unajumla ya madiwani 1,074 na Wabunge zaidi ya 116 yaani tunazungumzia Viongozi wapya Wa CCM toka Upinzani 1,190 soon watakuwa ndani ya CCM kama viongozi tena Wa wananchi/Chama, CCM simameni mnionesheni ulipo " Usalama Wa chama chenu " kuelekea 2020, Kumbukeni hawa ni watu watakaokuwa na ushawishi na maamuzi ndani na inje ya chama kwenye majimbo/Kata watakazokuwa wakiziongoza,Sikieni hii CCM itawafaa sana " Mtu kuwa mpinzani ni Fikra zake sio Sare za chama anazovaa wala kadi aliyonayo " CCM na WanaCCM lazima muongeze Umakini kwenye hili, Eti unamsikia mtu kama Bernard Mwakyembe anasema nae ni CCM lakini ukimtazama usoni haelekei kabisa kuwa ni MwanaCCM Kuna kitu tunaita " Facial expression " kamwe huwezi kuamini na ili kuamini hili lazima uwe na faili tena lililojaa pale Dodoma kwenye ile hospitali yetu maarufu iliyoko mlimani, nasema awamu hii CCM mmejishikisha pabaya huku, na hakika CHADEMA 2020 watafanya makubwa tuupe muda nafasi hakika utanena.
Wanawalaghai eti wanakuja kumuunga mkono Rais Magufuli JP, Jiulizeni kweli Magufuli anaweza kumvutia Mbunge/diwani kabla ya kuwavutia Wanachi ? Naomba kuwapongeza "think tankers " wote Wa CHADEMA kwa hili 2020 CCM vipande vipande.
Moderators, Uzi huu siku ya kuvunjika vipande vipande Kwa CCM nitaomba muurudie plzzz