Sakasaka Mao
JF-Expert Member
- Sep 29, 2016
- 9,911
- 11,779
Swali lake siyo gumu bali mafundisho ya dini ndiyo yanayokanganya. Pia ukianza kutathimini mafundisho hayo ndiyo unaanza kujiuliza kama unavyosema wewe kwamba; hivi kweli shetani aliumbwa na Mungu?Swali lako gumu sana inawezekana shetani hakuumbwa na mungu!
Kama aliumbwa na Mungu, baada ya maasi ilishindikanaje kuangamizwa moja kwa moja?
Je kweli alitupwa jehanamu? Je siku ya kiama atahukumiwa tena kwa kosa lake hilo alilotiwa nalo hatiani? Je kama wakosefu wanatupwa jehanamu la moto baada ya kufariki, siku ya kiama wataopolewa kwanza motoni ili waje kuhukumiwa? kama sivyo, kiama ni siku ya hukumu kweli? Je kuna kiama cha jumla ama kiama ni siku mtu anafariki na kupata hukumu yake kutokana na matendo yake?
Mafundisho ya dini yana contradiction sana. Na ukitaka kuuliza maswali ya kuchanganua namna hii, wanakugeuka ili usiendekee kuchimbua.