Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,015
- 9,883
NDANI YA MISTARI
BAD MAN - D KNOB FT CANNIBAL
Mtumishi wa Bwana, Innocent Sahani aka kinundu kichafu "Dirty Knob" kwa kifupi D KNOB akiwa na Mla nyama kutoka Mombasani waliangusha dude hili lililoishika Afrika Mashariki lakini kuna mstari mmoja umenifanya niwashirikishe;
D anaifungua stanza ya pili kwa kusema;
"KAMA NINGEKUWA MIMI, NISINGEKUWA MSHKAJI NA MIMI" Dakika ya kwanza, sekunde sifuri.
Nimekuwa na tafsiri mbili hapa;
Mosi, kama yeye angekuwa mtu mwingine basi asingekuwa na urafiki na D Knob. Kwa maana hii, anaona D Knob ana tabia ambazo haziwafai watu mpaka wakafanya urafiki au ushirika naye.
Maana ya pili ni kwamba, anamwambia mtu ambaye ana USHKAJI na NGWEA kwamba kama angekuwa yeye, basi asingekuwa na USHKAJI na NGWEA kwa sababu NGWEA alikuwa anajiita AKA MIMI.
Lakini kumbukumbu zangu zinaonesha kwamba D aliwahi kulumbana na Fid Q tu kimistari na siyo msanii mwingine, sembuse Ngwea!!!
Je D alimaanisha nini?
LUAH ( LENGO, UWEZO, AKILI, HISIA)
BAD MAN - D KNOB FT CANNIBAL
Mtumishi wa Bwana, Innocent Sahani aka kinundu kichafu "Dirty Knob" kwa kifupi D KNOB akiwa na Mla nyama kutoka Mombasani waliangusha dude hili lililoishika Afrika Mashariki lakini kuna mstari mmoja umenifanya niwashirikishe;
D anaifungua stanza ya pili kwa kusema;
"KAMA NINGEKUWA MIMI, NISINGEKUWA MSHKAJI NA MIMI" Dakika ya kwanza, sekunde sifuri.
Nimekuwa na tafsiri mbili hapa;
Mosi, kama yeye angekuwa mtu mwingine basi asingekuwa na urafiki na D Knob. Kwa maana hii, anaona D Knob ana tabia ambazo haziwafai watu mpaka wakafanya urafiki au ushirika naye.
Maana ya pili ni kwamba, anamwambia mtu ambaye ana USHKAJI na NGWEA kwamba kama angekuwa yeye, basi asingekuwa na USHKAJI na NGWEA kwa sababu NGWEA alikuwa anajiita AKA MIMI.
Lakini kumbukumbu zangu zinaonesha kwamba D aliwahi kulumbana na Fid Q tu kimistari na siyo msanii mwingine, sembuse Ngwea!!!
Je D alimaanisha nini?
LUAH ( LENGO, UWEZO, AKILI, HISIA)