Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,551
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali la tathmini kuhusu upinzani kuweza kuchukua nchi uchaguzi wa 2020. Kwa upande wa huku Tanzania Bara, ulizungumzia upinzani ni unazungumzia Chadema, hivyo hili bandiko kuihusu Chadema, as a representative wa upinzani kwa huku Tanzania Bara, vipi kuhusu Chadema, seriousness yake, its abilities and the capabilities kuelekea uchaguzi wa 2020. Hivi CHADEMA, hii, hivi ilivyo, inawezo wa kushinda uchaguzi wa 2020?, na hata ikatokea ikashinda kwa muujiza tuu kama wa Kenya, Zambia na Malawi, jee inaweza kuendesha nchi?. Is it a serious party?, is it capable, is it credible?. Is it organized?, does it have succession plan?. Is it mature enough opposition, kuweza kukabidhiwa ikulu ya Nchi yetu 2020?.
Au kutokana na mashaka mashaka, hata ukitokea muujiza wa Chadema kushinda uchaguzi, jee itatangazwa na kukabidhiwa nchi?. I doubt, kwasababu I have a feeling kuwa nchi inakabidhiwa by vetting and not voting, ushindi kwenye kura za urais depends not only on the votes casted, but he who counts the votes!.

Maswali haya ni kufuatia tathmini yangu jinsi Chadema inavyo deal na baadhi ya issues mbalimbali na ndogo ndogo tuu ikiwemo the current one ya uteuzi wa wawakilishi wake kwenye Bunge la EALA. Chadema kuna wakati ina behave childish na ikikwama kwa kutofuata sheria, taratibu na kanuni, ina pandisha na kupaza loud noises za baby cry kuwa inaonewa!.

Kutawala nchi sio jambo dogo au jambo la mchezo mchezo. Ikulu yetu haipaswi kugaiwa kwa majaribio bali kwa uhakika, tutakaye mkabidhi ikulu yetu ni lazima kwanza atuthibitishie amekomaa, na anawezo, mature enough with the abilities and capabilities, na sio tuu kumpa mtu ikulu yetu kwa kumjaribishia simply kwa sababu tuu CCM imeshindwa hili na lile na baadhi ya watu wameichoka sana CCM mpaka basi!.

CCM inaendelea kushinda na kuchaguliwa mwaka hadi mwaka, na itaendelea kuchaguliwa sio kwa sababu CCM is the best party, au CCM imeweza au inauwezo kivile!, no!. CCM has failed this nation many times since then, CCM imeshindwa na ilishindwa siku nyingi na inaendelea kushindwa, kwa kufanya madudu mengi tuu ya ajabu ajabu, lakini bado imekuwa ikiendelea kushinda kwa kuchaguliwa mwaka hadi mwaka kwa mazoea tuu kwa sababu, Tanzania bado hatuna mbadala muafaka wa kuiondoa CCM!, lakini baada ya kuingia Magufuli na mambo makubwa anayoyafanya, uchaguzi mkuu wa 2020, CCM itashinda kwa kishindo, sio kwa mazoea bali for a reason.

Yaani Tanzania bado hatuna any serious, capable and a credible opposition party ya kuwapa wapiga kura wa Tanzania a choice to choose from, hivyo CCM kujikuta ikiendelea kuchaguliwa na kushinda kwa ku sail through na upepo wa mazoea, kwa sababu ndio the only one iliyopo!, we have no any serious, capable na credible choice to choose from, hivyo we have no choice. Matokeo yake ni CCM inashinda kwa an easy ride ya mazoea na itaendelea kushinda na kushinda tena na tena mpaka tutakapo pata a credible opposition such that we'll have a choice to choose from!.

Kwa Zanzibar hakuna ubishi kuhusu uwezo wa CUF as a credible opposition kuweza kutawala Zanzibar, lakini kwa upande wa huku Tanzania Bara, bado kabisa hatuna any serious, capable and a credible opposition ya kuiondoa CCM na kuikabidhi Ikulu yetu.

CHADEMA ndio angalau angalau wameonyesha nia na dalili za kuweza kuaminiwa, na kiukweli wakiamua, wanaweza kabisa, ila natatizwa na haya madudu yao madogo madogo yanayo onyesha all signs za immaturity kwa upande wa Chadema, such that bado ni chama ambacho hakijaonyesha ukomavu wa kutosha enough to convince Tanzanians kuikabidhi ikulu yetu comes 2020, waipige chini CCM na kuikabidhi Chadema Ikulu yetu ya Magogoni.

Jee kwa maoni yako, unaiona Chadema as a credible,capable na serious opposition, iliyokomaa na kuwa mature enough with the ability, capability and credibility ya kukabidhiwa ikulu yetu 2020?.

Kwa upande wangu, honestly, I don't think, ila kabla sijasema why I don't think and what should we do, naomba kupata mawazo yako, assuming uchaguzi wa Tanzania utaendeshwa kwa uhuru na haki, na chama kitakacho shinda kimeshinda kwa haki, Jee Chadema hata kikishinda, kinauwezo?. Kimeonyesha uwezo wa utayari wa kutawala nchi endapo kitashinda uchaguzi 2020?. Ila kabla hata hakijashinda huo uchaguzi wa 2020, kwa Chadema hii tunayoiona sasa, jee inao huo uwezo wa kushinda?.

Na hata tukiachana na udhaifu wa upinzani imara, everything has it's limits, suppose CCM imewafikisha Watanzania at their limits wakaamua sasa imetosha, they've had enough of CCM and now they are fed up hivyo kuamua liwalo na liwe, wakaipiga chini CCM kwenye sanduku la kura na kuichagua Chadema, jee CCM itakubali kuachia?. Can you just imagine mtu aliyepo Ikulu kukabidhi madaraka sijui kwa nani hiyo 2020, is it possible?.
Kuna mtu yoyote ameishawahi kusikia maandalizi yoyote ya succession plan ya changing arms kwa vyombo vya serikali, na vyombo vyetu vya dola na vyombo vya ulinzi na usalama, kujiandaa kukitumikia chama kingine chochote nje ya CCM?.

Kwanza tuu hata ikatokea Watanzania wengi zaidi wakaichoka CCM na kuipiga chini kwenye sanduku la kura, jee huyo mshindi halali atatangazwa?!, na Tume hii hii?!, Au inawezekana zoezi zima la uchaguzi wa vyama vingi ni kwenye ubunge tuu na udiwani, lakini kwenye urais, licha ya the playing field kutokuwa level, inawezekana uchaguzi wa rais ni igizo tuu la uchaguzi?!.

Nawatakia Furahi Dai Njema.
Paskali.
Rejea.
CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga! - jamiiforums.com

CHADEMA: Tujadili Utayari wa Kutawala Nchi 2015 | Page 7 ...

Kuelekea 2020: CHADEMA Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If ...


Kuelekea 2020: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM ...

CHADEMA Ikipewa Nchi, October 2020, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala ...

Mtazamo: Kanda ya Kaskazini, CCM imechokwa mpaka basi ...

Kuichagua tena CCM, Je ni kielelezo cha kufanya informed decision ...

Ikitokea CCM ishinde, Je ushindi huo ni kutokana kuwekeza kwenye ...

Watanzania ni ignorants au tumelogwa?


CHADEMA Hamkujipanga, hamjajipanga, hamjipangi na hamtajipanga ...

Wenye Matumaini na Upinzani Kushika Dola!, Sahauni! CCM Inajiandaa Kuua Kabisa na Kuuzika Jumla

Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?


Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze...
 
Ingekuwa Hivi Alivyondika Pascal Mayala Basi Mama Zetu Nina Hakika Wasingetuzaa Yaani Mama Akizaa Mtoto Mwenye Matatizo Huwa Siyo Mwisho Wa Uzazi


Sasa Mature Unaypitaka Wewe Ni Ipi?
Duniani Kote Vyama Mbalimbali Vinaongaza Nchi Zao Bila Hilo Neno Mature
Watanzia Wengi Wanataka Kuona Ccm Siku Moja Inapisha Tena Kwa Amani Sana

Tuendelee Na Ccm Hata Kama Itashindwa Uchaguzi Ndicho Ulichoandika Wewe
 
Kama Chadema ilimuita yule jamaa yako fisadi lakini alipohamia kwao akageuzwa kuwa jembe tena bila ridhaa ya wanachama sitegemei chama hiki kiwe serious kupewa nchi.

Kama kiongozi wake mkuu anatuhumiwa katika ngada ,ukwepaji kodi na uhujumu wa NHC na anakaa kimya sitegemei kama wanaweza kuaminiwa.

Kama chadema inadiriki kuilaumu serikali eti itakosa misaada kwa kuwa inaminya demokrasia ...bado chadema inaamini nchi itakombolewa na wahisani hivyo sio chama chenye fikra mbadala.

Kama chadema kinajiita chama cha demokrasia ilihali mwenyekiti wao ni wa kudumu na upatikanaji wa wabunge wa kuteuliwa au viongozi mbalimbali wa kanda unategemea majina ya mfukoni sioni kama chama hiki kinafaa kuwa mbadala wa CCM.

Kama chadema kina viongozi wanaotegemea ufuasi wa wahalifu ili kuingia madarakani ...hili ni jambo hatari kwa usalama wa nchi.nilimsikia lema kama waziri kivuli wa mambo ya ndani akiwakumbuka marafiki zake wafungwa na mahabusu tena kwenye hotuba yake rasmi.nini kitazuia chama hiki kuendeshwa kwa fedha na matakwa ya wahalifu?Tulishuhudia chadema ikiwatetea wafanyabiashara wanaokwepa kodi,wafanyakazi wazembe na wabadhirifu na watu wa aina hiyo.yaani chadema na wahalifu ni washikaji.

Kama chadema hii inategemea kupata kiki za msibani badala ya kujitoa na kushiriki na wafiwa sitarajii watanzania wenye akili zao timamu waipe kura kuongoza taifa hili takatifu.

Ni chadema hiihii kila kukicha inatukana vyombo vya ulinzi na usalama yaani kuanzia polisi,jwtz na Tiss...sitegemei hawa kupewa nchi hii ya wazalendo.

Kwa ufupi CCM ni Alpha na Omega upinzani uliopo ni chachu tu ya kuisaidia /kui-Check CCM ilete maendeleo kwa nchi.
 
CHADEMA ndio angalau angalau wameonyesha nia, na kiukweli wakiamua, wanaweza kabisa, ila natatizwa na haya madudu madogo madogo yanayo onyesha all signs za immaturity kwa upande wa Chadema, such that bado ni chama ambacho hakijaonyesha ukomavu wa kutosha enough to convince Tatanzanians kuikabidhi ikulu yetu comes 2020, waipige chini CCM na kuikabidhi Chadema Ikulu yetu ya Magogoni.

Tatizo la CHADEMA ni Mbowe

Kile chama kimekuwa kikubwa sana kuliko uwezo wake

Yes..Amefanya mengi..lakini uwezo wake umefika mwisho...Hawezi kufanya kingine kipya ambacho hajawahi kufanya...Tatizo kubwa zaidi ni yeye anaamua kila kitu

Huwezi kufanya jambo lile lile kila siku...kwa namna ile ile na kutegemea majibu tofauti...

CHADEMA ikitaka kutokufa ikubali kufanya mabadiliko ya ndani ya msingi kabisa na kukihuisha chama .

Chama kikijenge katika msingi imara na thabiti ya kitaasisi.....waweke mifumo inayowawezesha kuweka sera imara...tested policies...na mwisho watengeneze demokrasia ya kweli ndani ya chama.
 
Ni chadema hiihii kila kukicha inatukana vyombo vya ulinzi na usalama yaani kuanzia polisi,jwtz na Tiss...sitegemei hawa kupewa nchi hii ya wazalendo.

Mkuu unaweza kuwa umeandika kinazi sana...lakini una hoja katika sentensi yako

Nchi yoyote ile duniadi..yoyote ile...Rais anapitishwa na system.....Kama state ikikukataa huwezi kuwa rais

Hivyo CHADEMA wana kazi kubwa sana ya kuwashawishi "system" kwamba wanaweza kukabidhiwa dola....

Vituko walivyofanya mwaka 2015...vilikuwa vituko vya karne...Huwezi kumchukua mtu aliyekuwa Vetted out na "System" na kutaka kumuingiza ikulu.

Wafanye siasa makini na wajitahidi kuondo confrontation na vyombo vya "state"
 
Sidhani kabisa wala sitaki kuona chadema ikipewa ikulu!!marafiki zako siyo wazuri kwa mstakabali Wa nchi yetu!!eg 2015 liko kundi katika mataifa ya jirani walikuwa wakishangilia nchini mwao kuwa mtu wao (labda ni kabila lao) wanaingia ikulu ya Tanzania!! Sasa unaweza kujiuliza what was the agenda behind!!
Hawa hawaaminiki kabisa na hawasimamii wanayosema!!eg ni the list of shame!!waliwataja watu kwenye list kuwa ni mafisadi papa but still again waliwachukuw ni kuwafanya wagombea wao!!

Wanaopendekezwa kugombea urais 2020 kupitia chama hiki wanajulikana so wasafi kiasi hicho!!eg Mr zero(Ranchi) na richmonduli!!

Hawana watu wakushika nyadhifa serikalini kwa jinsi hiyo lazima wazime watu kutoka CCM!eg yule jamaa Wa Kenya ilikuw awe governor Wa BoT!

Sasa MTU ambaye anataka ikulu ataanzaje kuwatukana majeshi ya nchi Yake?
Hawana mshikamano Wa kizalendo!!eg .wafanyakazi hewa ,watuhumiw wa madawa ya kulevya wanatetewa na wanasheria Wa chama hiki !!sasa hapo kina uzalendo kweli?na utampaje ikulu MTU ambaye anadalili za kutokuwa mzalendo?
 
Demokrasia ndio inayoamua, ccm na chadema ni vyama tu, majibu ya maswali yako yanajibiwa kwa kura kupitia chaguzi. Kama demokrasia ndo inayoamua kwamba mwenye kura nyingi ndiye mshindi hayo ya kuhoji uwezo wa chadema yanahojiwa kwa taratibu zipi? Kama wananchi watasimama pamoja na chadema bila kujali mapungufu yao nani huyo atakathubutu kupingana na maamuzi ya wananchi?

Uchaguzi mkuu 2015 ingawa tume ya uchaguzi iliwapa ccm ushindi ila wengi hata miongoni mwa wana ccm waliamini ccm haikushinda na kama kungekuwa na kura za wazi ukweli ungejulikana. Kwahiyo kuendelea kwa ccm kuwepo madarakani sio kipimo cha wao kukubalika kwa sababu hata tume ya uchaguzi inaendeshwa na wao kwa mwamvuli wa serikali, kwa namna hiyo nani ataamini kama uwepo wao unategemea kura za kweli au kura hewa?
 
Mkuu unaweza kuwa umeandika kinazi sana...lakini una hoja katika sentensi yako

Nchi yoyote ile duniadi..yoyote ile...Rais anapitishwa na system.....Kama state ikikukataa huwezi kuwa rais

Hivyo CHADEMA wana kazi kubwa sana ya kuwashawishi "system" kwamba wanaweza kukabidhiwa dola....

Vituko walivyofanya mwaka 2015...vilikuwa vituko vya karne...Huwezi kumchukua mtu aliyekuwa Vetted out na "System" na kutaka kumuingiza ikulu.

Wafanye siasa makini na wajitahidi kuondo confrontation na vyombo vya "state"
Unaweza kutuambia systeam hiyo inatengenezwa na watu gani?
 
Back
Top Bottom