Je, Bunge litamfukuza Zitto kwa "kutokuhudhuria" vikao; hasaini kupokea posho!?

Ungekuwa na kibahasha wangeandika chochote utakacho wewe, kama unabisha muulize Pasco wa JF. Tatizo ni bahasha za lunch au usafiri, sio za rushwa hapana, mnhhhh!

Kweli FF nao wana namna yao ya kujikimu,kama wafanyakazi serikalini hasa maboss wanavojipa safari na warsha kujazia kusustain life kuelekea mwisho wa mwezi
 
Wao tu na roho zao, lakini JamiiForums bado iko juu na itaendelea kuwa juu.
Naweza kununua magazeti alafu ukashangaa siku ikapita bila ya kuyasoma, Niko busy na JF yangu.
Na mara nyingi nasoma magazeti umeme ukiwa umekatika ndio napotezea time kusubiri Ngeleja arudi niendelee kuperuzi JF.
 
Mkapa huwa yuko sahihi sana kuwaita hawa waandishi wetu wa habari ni matango pori! viva Mr Clean.
 


pamoja na hayo tukiruhusu bila kupiga kelele watu waje ku copy na kwenda ku paste kwenye hizo mwanahalisi zao huko kwa kibali cha kutaja source tu tutakua hatuwasaidii sana waandishi wetu,inatakiwa waumize vichwa huko kwenye ma newz room zao sio kuketi tu wakisubiri wakichungulia chungulia humu kuna kipi wakibebe kama kilivyo kisa eti watatutaja,hapana wafanye kazi si wanalipwa?au wana volunteer
 
nafikili si HABARI LEO ni hawa JAMBO LEO....Mi pia nimeona nkashangaa sana..kumbe uandsh wa habari hata mimi naweza
 
Wewe ulitakaje ? Ulipwe? Wana habari wapo kazini na wanatafuta news popote pale hata Chooni so wewe unatakiwa ufurahi tu kwani wengi hawana access ya kutizama jf au hawaijui kabisa na hata ukuwaambia hawataelewa kitu kama wataka ijulikane itafika tu na itajulikana hii jf. hata kama mwandishi alipoosha kuwa ni forum nyingine basi wadadisi watafuatilia na kukuta mwandishi alichemsha na ukweli utajulikana JF itakuwa juu tu.

Taarifa za dini zimeanzwa kuhubiriwa miaka mingi sana na bado hazijaenea maeneo yote ya dunia sembuse jf..
habari au taarifa hazna mwenyewe ukipata lete humu na wao kakiziona wazisambaze tu kwani watu wote wanahitaji upata habari sio sababu kimeandikwa humu ndio kisipelekwe kule kwani 99% ya news za humu jf zinatoka kwenye vyombo vingine vya habari...

Wataka nao walalamike kama wewe? tulia uishi kwa amani wacha kujikera kama mashabiki wa Arsenal, liverpool na Taifa Stars na Yanga....

Shabikia Man U ufurahie Maisha.
 

Mkuu unakuwa online wakati wote unafanya kazi saa ngapi?
au wewe ni mwajiriwa wa JAMIIFORUM Moderator tete...tete..te poa bana
wewe kaa hapo muda wote utuangalie kama Invisible
 
Mkuu,

Nadhani hujaelewa hoja ya mwanzisha thread.

Hata hivyo, tumewasiliana na uongozi wa New Habari Corp na wameahidi kulifanyia kazi hili na kusema haitatokea siku nyingine.

 
Mkuu, Nadhani hujaelewa hoja ya mwanzisha thread. Hata hivyo, tumewasiliana na uongozi wa New Habari Corp na wameahidi kulifanyia kazi hili na kusema haitatokea siku nyingine.

Mkuu Tech,

Umenisaidia. Nimelog makusudi ili nimjibu huyu jamaa kuwa ni wapi ktk thread yangu nimezuia watu au waandishi wasije kutafuta humu habari.

Duduwasha inabidi tumfunde kwamba JF kumejaa wataalamu ambao hawakuzuii kuleta habri yako. Tuna hamu ya kuisoma lakini neno linaloongoza kwa wingi humu ni "source". Yaani kama tuna utata na habari yako basi maliza utata huo kwa kutletea source.

Wakati sisi tunaleta source, hawa waandishi wanachota hivyohivyo. Kwa wale wenye ugumu wa kuelewa kwa mara ya kwanza narudia hapa ili waelewe kuwa mimi nadhani hata JF nzima haina tatizo na kuichota habari ilivyo hapa na kuiepeleka ikauze magazeti yao.

Ninachogomba ni ile principle ya copying inayomtaka copyist atamke source alikoitoa habari yake.

Nimefuri jibu lako ambalo limemuonyesha jamaa na wenzake kuwa JF kuna watalaamu hawishii kupiga porojo, maana umeenda hadi kuwasiliana na Habari Corporation na wao wamekiri kutorudia makosa kwa maelezo yako.

Sasa kama wao waandishi wamekiri binafsi sina ugomvi nao tunawakaribisha maadam watoe quotation ni wapi walikoitoa na si WANABIDII ambako nako walichota huku.

Binafsi sikupenda kuituma habari hii kwa WANABIDII kwa sababu nina ugomvi binafsi na hiyo forum. Ugomvi ni kwamba mara kadha natuma post kama hii lakini hawaitoi. Sasa ya nini kujihangaisha wakati kuna JAMII FORUM inayokaribisha watu kama sisi na post kama hizi.

Hizi ni zama za utandawazi, kama WANABIDII wanataka prosperity hata kuzidi JF waruhusu critical arguments kama huku.

Go go JF
 
miaka miwili iliyopita wachunguzi wa mambo walikuwa wakisema "it is a matter of time for jf to lead this industry" lakini sasa kila mtu anajua ukuisema Jamiiforums unamaanisha nini katika kubadilishana habari.

Challenge iliyopo hivi sasa kwa jf ni jinsi gani ya kuwafikia watu wengi zaidi na hasa wa vijijini ambapo hata magazeti hayafiki, nina imani jf itafika huko ambako hata magazeti hayakuwahi kuota kufika
 
Wakuu kuna tetesi nimezipata kisha nikaunganisha dot zangu nami nikaona kuna kaukweli.
Kuna kigogo mmoja wa ccm kaniambia kuwa Zitto anaweza kufukuzwa ubunge kwa mpango maalum uliosukwa na watu kadhaa akiwepo Kikwete, Makinda,Kabwe Zitto na wengineo.
Lengo lao ni kumjenga tena Zitto awe mjadala wa kitaifa na kumpa umaarufu. Baada ya hapo Zitto atatumika kutumia umaarufu huo kuibomoa Chadema ili ccm ipate ahueni uchaguzi ujao. Lengo ni Zitto kuondoka na nusu ya wanachadema hasa vijana ili kujiunga na chama kipya ambacho na chenyewe kitasajiliwa na kupata usajili bila mizengwe kwa ushirikiano wa niliowataja.
Chama kipya ni azimio lao baada ya mpango wao wa kuteka nccr kukwama. Zitto atagombea urais kupitia chama hicho na anatarajiwa kuwa mshindi wa pili na chadema mshindi wa 3. Lengo chaguo la JK kupitia CCM liweze kupeta.​
Uchunguzi wa wakubwa - wanausalama baada ya kuzunguka nchi nzima, wameona kuwa bila kusambaratisha Chadema mwaka 2015 ccm haiwezi kupita hata kwa kupita kura. Wamefanya utafiti mdogo mikoa 18 ya Tanzania bara. Kilichowashangaza zaidi ni kukubalika kwa Chadema hata katika mikoa ambayo Chadema haina nguvu kabisa kama Tabora, Ruvuma, Lindi na Mtwara.
Kwahiyo, mpango uliopo ni kumjenga zitto ili aibomoe chadema. Akaniambia zitto anaweza kuondoka na wabunge wasiopungua 3 kama mambo yataenda vizuri na madiwani karibu kumi.
Mpango huo unategewa kuwa karibu na mwaka 2015. Hata hivyo, kuna mambo mengine yakikaa vizuri wanaweza kuamua hata kabla ya hapo.
Akamalizia hata shutuma za Zitto dhidi ya baraza la mawaziri bungeni hatafanywa kitu mwisho wa siku.
Nawasilisha.
 
Hivi mbunge anafukuzwa kwa kutohudhuria vikao au kutosaini mahudhurio ya vikao? Sasa kama ushahidi mwingineo k.v hansard, mikanda ya video nk kuonesha kwamba mbunge alikuwepo kwenye kikao cha Mkutano wa Bunge atafukuzwaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…