Je, Bunge lina ubaguzi kwa walemavu?

Je, Bunge lina ubaguzi kwa walemavu?

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2021
Posts
3,211
Reaction score
3,614
Baadhi ya watu wanaoishi na ulemavu wamebahatika kuwa Wabunge kwy Bunge la JMT.

Tumeona walemavu wa viungo vya mwili wakiwa Wabunge vivyo hivyo kwa walemavu wa macho na masikio isipokuwa tu walemavu wa ubongo.

Maswali yangu ya kuomba maarifa ni haya:-

1. Je, Katiba ya JMT, Sheria, Sera ya Walemavu na Haki za Binadamu zinasemaje kuhusu haki ya Vigugumizi kuwa Wabunge?

2. Je, Vigugumizi ni walemavu kwa tafsiri?

3. Je, ni Kigugumizi wa ngazi ipi anawezakuwa Mbunge (Kigugumizi kikali au Kigugumizi cha Wastan)?

4. Je, kwa muda ule mfinyu sana wa Mbunge kuchangia hoja Kigugumizi ataweza? Au atanyanyapaliwa kwa kugongewa kengele wakati hajaweza kufikisha ujumbe wa hoja anayochangia!

5. Nini kifanyike (hususan kwenye muda wa kuchangia hoja) ili Vigugumizi wawezekuwa Wabunge?



Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom