Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 3,621
- 6,510
Mara kwa mara nimekuwa nasikia baadhi ya miradi inayofanywa na serikali huko Dodoma, nabaki kujiuliza kwamba mbona yanaenda kinyume na malengo yaliyokusudiwa ya kujenga mji wa kiserikali?
Jana nilisoma mahali kwamba wanajenga viwanja vikubwa vya mchezo wa golf na lengo ni kupafanya Dodoma kuwa kitovu cha utalii wa michezo. Hivi viwanja vya Kawe, Lugalo na Gymkhana vimeleta utalii kiasi gani mpaka sasa? Hivi kupeleka mradi huo Dodoma ni wazo sahihi kweli na ni kipaumbele cha mji huo kwa sasa na hata kwa siku zijazo?
Miradi mingine unaona ina nia ya kukuza population ya Dodoma kwa kasi na kuwa na mji wenye hekaheka nyingi mfano wa Dar es Salaam jambo ambalo nadhani ni kinyume na malengo ya kuhamishia ofisi za serikali huko.
NB. Nilianza kuona kuna shida kwenye maono ya viongozi kwa kitendo cha kujenga Ikulu Dodoma ambayo ni copy and paste ya Ikulu ya Dar es Salaam. Nadhani fikra hizo ndiyo wanaendelea nazo katika miradi mingine.
Jana nilisoma mahali kwamba wanajenga viwanja vikubwa vya mchezo wa golf na lengo ni kupafanya Dodoma kuwa kitovu cha utalii wa michezo. Hivi viwanja vya Kawe, Lugalo na Gymkhana vimeleta utalii kiasi gani mpaka sasa? Hivi kupeleka mradi huo Dodoma ni wazo sahihi kweli na ni kipaumbele cha mji huo kwa sasa na hata kwa siku zijazo?
Miradi mingine unaona ina nia ya kukuza population ya Dodoma kwa kasi na kuwa na mji wenye hekaheka nyingi mfano wa Dar es Salaam jambo ambalo nadhani ni kinyume na malengo ya kuhamishia ofisi za serikali huko.
NB. Nilianza kuona kuna shida kwenye maono ya viongozi kwa kitendo cha kujenga Ikulu Dodoma ambayo ni copy and paste ya Ikulu ya Dar es Salaam. Nadhani fikra hizo ndiyo wanaendelea nazo katika miradi mingine.