Je, ATCL inahujumiwa kibiashara? Tutumie a political will kuinusuru au tuiache iangamizwe na ushindani?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,499
113,610
Wanabodi,

Declaration of Interest Kuhusu Uzalendo.
Naomba ku declare interest yangu kuhusu uzalendo wangu kwa nchi yangu, kwa sababu, ukiibua hoja yoyote humu, kuhusu utendaji usioridhisha wa mashirika yetu ya umma ya kizalendo, utanyooshewa vidole kwa kutuhumiwa wewe sio mzalendo. Ile siku nilipoibua mjadala huu kuhusu ATCL,
ATCL, tuache siasa kwenye usafirishaji abiria. It's not fair kuchelewesha abiria kwa dakika 45 wakiwa ndani ya ndege, kumsubiria abiria mmoja kigogo ambaye ni waziri
nilishutumiwa hadi na maziri husika kwa kukosa uzalendo, hivyo kuomba headline ibadilishwe!. Ndege ya ATCL yachelewa kuondoka ndani ya muda; watoa ufafanuzi!

Uzi huu ni uthibitisho wa uzalendo wangu, unapoona kuna uwezekano wa shirika lenu kuhujumiwa kwa ushindani usio sawia na mashirika ya nje, wazalendo wa kweli hatuwezi kunyamaza. Hivyo huu ni uzi wa kizalendo, kwanza kwa kuuliza swali tuu, jee kuna uwezekano, Shirika la Ndege la Fast Jet, linalihujumu shirika letu la Ndege la ATCL, kwa kuvamia routes za ATC na wao kupunguza bei kwa more than 50%!. Baada ya swali, pia ninatoa mapendekezo ya hatua za kuchukua, kufanya protection ya kilicho chetu.

ATCL inakwenda Kigoma mara mbili kwa wiki, kwa kutumia ndege yetu ya Bombadier -400, inayotumia Pangaboi, hivyo safari kuchukua muda wa saa 2.45, kwa nauli ya TZS 365,000 (japo tulielezwa nauli ni 165,000), lakini leo nimeona tangazo kuanza kuuzwa kwa tiketi za Fast Jet, kwenda Kigoma, ambapo safari zitaanza tarehe 1 Mwezi Machi, Fast Jet watazindua safari kati ya Dar es salaam na Kigoma kwa safari 3 kwa wiki, siku za Jumanne, Alhamis na Jumamosi kwa nauli ya Tsh 123,000. kwa kutumia ndege za kisasa aina ya Embraer E 190 ambayo ni Jet engine, safari itachukua muda saa moja tuu!.

Jee uamuzi huu wa Fast Jet, ni uamuzi tuu wa kawaida wa kibiashara, ili kuleta ushindani kwa kutoa more choices na ku provide some better a cheaper options kwa wateja wa usafiri wa anga, au una lengo la kuihujumu ATCL?, kwa kuifuata kule inakoruka, na wewe unapeleka ndege yako route ile ile, unaongeza frequency, unapunguza nauli, unatumia ndege bora Zaidi ya jet engine, wakati mwenzako ana bangaboi, unafanya direct route, kuruka kwa muda mfupi Zaidi wakati mwenzako anapitia Dodoma!, kuna mtu kweli ambaye ni time conscious na cost conscious ataendelea kupanda ATCL kwenda Kigoma, tangu siku Fast Jet, itaanza kuruka route hiyo?.

Kwa Nini Ndege Hazipangiwi Routes na TCAA Kama Mabasi Yanavyopangiwa na Sumatra, au Masafa na TCRA?.
Ukinunua dala dala, unaomba kibali Sumatra, wanakuonyesha routes zenye nafasi unachagua, kama unataka routes Fulani zenye mabasi mengi, unaambiwa hiyo route imejaa!. Vivyo hivyo kwa TCRA kwenye kugawa masafa, wengi wangetaka kutangazia DSM kwa sababu ndio kwenye wateja wengi, lakini TCRA inakulazimisha kwenda sehemu ambako redio hazijajaa!. Vivyo hivyo kwa Kampuni za simu, kulazimishwa kwenda hata sehemu kusiko na soko!. Kama ilivyo kwa regulators wengine kuwapangia players, kwa nini TCAA pia isiyapangie routes haya mashirika ya ndege ili wasigombee routes na kuuwana?, pia iwapangie nauli kama Sumatra?.

Kama ATCL inakwenda Kigoma, kwa nini Fast Jet nayo iende Kigoma tena kwa bei nusu ya ATCL?.
Kwa nini TCAA wasiilazimishe Fast Jet iende Singida, Iringa, Tanga, au route ambayo haina kabisa ndege?, kwa nini ndege zisongamane Dar, Mwanza, Kia, ect wakati Tanzania tuna routes kibao, na destinations tele hazina ndege?!.

Hostile Kick Out na Hostile Take Over ni Mbinu Chafu za Ku Create Monopoly Kwa Kuwafungasha Virago Wapinzani Wako, Kama ilivyo Inside Trading!.
Mimi licha ya kuwa ni mwanahabari wa kujitegemea, pia ni mfanyabiashara wa huduma za Radio na TV Programs production. Zikitangazwa tenda za utayarishaji wa Vipindi, washindani wako wenye akili Zaidi hufanya "inside trading", kwa ku collude na watu a ndani, kujua bajeti iliyotengwa, kisha kwenye tenda yao, wana quote bei ya chini ajabu kuliko hata bei ya soko, tenda inafunguliwa wewe bei yako inakuwa juu, unakuwa kicked out, mwenzako mwenye bei ya chini, anashinda tenda, kisha wale wanamfanyia appreciation kurekebisha viwango, na kumlipia pesa stahiki hadi ziada ili agawe cha juu as kick backs!.

Jee hiki kinachofanywa na Fast Jet sio hostile kick out of ATCL out of business kwa wao kushusha sana nauli ili ATCL akose wateja kwenye routes hizo, ajitoe kwenye hizo routes, ndipo Fast Jet waweke gharama halisi?. Mbinu hii hutumika kumuondoa mshindani wako kwenye soko kwa kuweka nauli za chini sana na kujiendesha kwa hasara kwa muda fulani, kisha akiisha fungasha na kuondoka, ndipo wewe utawale soko na kutoza nauli halisi?!.

Hostile take over ni kama kile kitu kilichofanyika kwa kwenye ile vita ya bia, (the beer war), kati ya KBL na TBL, Kenya walishusha bei ya bia zao zinazokuja Tanzania, na kuuzwa kwa bei ya chini kuliko bia za TBL, ilifikia mahali watu wa mikoa ya Arusha na Moshi kunywa zaidi Tusker kuliko Ndovu, vita hii ikamalizwa kwa makubaliano ya wakubwa, kuuziana viwanda juu kwa juu, matokeo yake kiwanda cha Kibo, kikafungwa!.

Jee bei hii ya tiketi ya Fast Jet ya Dar-Kigoma, TZS 123,000/= is it realistic, au wameshusha ili kuiua ATCL?.

Nini Kifanyike Kuinusuru ATCL na Ushindani Usio Sawia.
  1. A Political Will, Kulazimisha Twiga Aendelee Kuchanja Mbuga!. Kwa vile ATCL ni ndege yetu, lazima tufike mahali. nchi yetu ichukue maamuzi ya kisiasa ya kuinusu ATCL dhidi ya ushindani usio sawia kutoka ndege za mashirika ya kipepari na kibeberu, hata kama uamuzi huo utakuwa unakwenga against free trade, ikiwemo kuandika waraka kwa taasisi zote za umma, wizara, idara na Wakala za serikali, kwa safari zote za kikazi, lazima kwanza waitumie ATCL, hata kama ni ghali zaidi na inakwenda pole pole kuliko jet engines, lakini fedha za umma kwenye usafiri wa ndani, lazima kwanza ziende ATCL, kama hawana route hiyo ndipo wapande ndege nyingine!. Hili linawezekana, mimi nimefanya kazi na Waingereza chini ya FCO, watu wote wanaolipiwa usafiri na serikali ya UK. lazima kwanza wapande BA, hata kama nauli ya BA ni juu na ghali kuliko ndege nyingine, ikiwa BA hawana route hiyo ndipo wapande ndege za mashirika nyingine.
  2. Tutumie Protectionism Kuchukua Protective Measures Kulinda ATCL. Hapa ni kuhakikisha ATCL inalindwa kibiashara kwa namna nyonyote ikiwemo some exclusive routes, na kuitumia TCAA kufanya restrictive measures kuzuia routes za ATCL kuingiliwa, na kuitumia Fair Competition kuzuia mashirika mengine yasishushe bei below average to make a business sense ili tuu kuwaua washindani wako wa kibiashara. Ikibidi ATCL ipewe some monopoly fulani hadi I stabilize kibiashara na kutawala soko. Hili liliwahi kufanyika kulinda viwanda vya ndani dhidi ya cheap imported products.
  3. Kuandaa Kampeni za Uzalendo Watanzania Wazalendo Tupande ATCL!, hii ni kampeni maalum ya kujenga upya moyo wa uzalendo kwa wasafiri wa ndege wa Tanzania, kujitolea kupenda kupanda ndege za ATCL kwa kuhimiza penda chako, jenga chako, kama Watanzania wote, tutapanda ATCL hivyo hivyo ilivyo despite all the odds, baada ya miaka michache, ATCL nayo itakuwa na uwezo wa kununua jet, na kufanya safari za haraka, na hizi pangaboi za Bombadia zitakuwa ni za group routes kusafirisha makundi ya wanafunzi na wanavyuo kwenye group trips.
  4. ATCL Isibweteke!. I know ATCL is making losses na serikali inaibeba ndio maana inazuia taarifa ya ukaguzi isiwekwe public. Hata kama serikali itachukua hatua za kuibeba ATCL kwa kila aina ya mbeleko, Uongozi na Menejment ya ATCL inawajibu wa kutobweteka na mbeleko ya serikali, bali nayo ijibebe kuhakikisha inatoa huduma bora na za ushindani, isije kufika mahali anayekubeba akachoka. sisi tunaoamua kupanda ndege za ATCL, pia tusafiri huku tunapata raha kwa huduma nzuri, na sio tusafiri na ATCL kwa sababu tuu ya uzalendo lakini watu tunasafiri huku tunakereka, tunanuna na tumekunja nyuso!.
  5. Tuisalie ATCL Ifanikiwe. Kwa kadri ndege zetu zinavyozidi kuchelewa kuachiliwa, ndivyo washindani wa ATCL wanavyozidi kuipiga bao, kwa kujiimarisha!, hivyo natoa wito kwa Watanzania wote wazalendo wenzangu, pia tutumie nguvu ya sala, kuombea ndege zatu ziachiliwe, ATCL ipeleke ndege kila kona.
  6. Hili ni la kwangu binafsi, kwa routes za Mwanza, kama ATCL kila siku kwenye route hiyo, itampangia rubani mmoja mdada mweupe kama shombe shombe , najua hajaolewa!, na kumtangaza huyu rubani Binti ndie rubani wa kudumu wa ndege za ATCL kwa route ya Mwanza!. Ndege ikiwa njiani kwenye mazingira tulivu, aweke auto pilot na kutoka cockpit kuja kusalimia abiria!, nawahakikishia ndege ya ATCL route ya Mwanza, kila siku itajaza abiria mijibaba ya Kisukuma, hata wale Wasukuma wanaosafiri kwa mabasi, wakijua wanaendeshwa na rubani mwanadada Cheupe!, watadunduliza na kuhakikisha wanapanda ndege za ATCL tuu, na hata ikitokea Fast Jet na Precision hata wakaweka nauli ya bure, bado ATCL ndio itajaza kwanza abiria wa Mwanza, halafu wengine ndio watafuatia!.
Hitimisho.
ATCL ni ndege yetu, inahitaji upendo wetu na protection yetu, kama tunavyozipenda familia zetu, ukiisha oa au kuolewa lazima umpende mkeo, hata kama utakutana na mwanamke mrembo vipi, au mke umpende mumeo, hata kama utakutana na mwanaume mwingine tajiri vipi!.
Huu ndio uzalendo wa kweli!, hivyo namalizia kwa lile lile swali la msingi, tukiona kama ATCL inakabiliwa na ushindani usio sawia, jee tutumie utashi wa kisiasa kuinusuru ATCL yetu, au tuachie tuu huu ushindani uendelee, na kuilazimisha ATCL lazima ihimili ushindani huu na kusaidiwa ili isishindwe. Najua ATCL inaendeshwa kwa hasara kwa kubebwa na serikali, bila kuisaidia ATCL kwa a political will, serikali itaendelea kuibeba hadi lini?. Watanzania sasa ndio tunabidi tuibebe ATCL kwa uzalendo, au mnataka tuiache tuu ijifie after spending all that much?.

Jumatatu Njema.
Paskali
 
Hata watoto darasani wanafanya mtihani mmoja na mwenye akili anapasua,waache washindane,huko Kigoma kulikuwa na Precision na Fast Jet ilisimama kwa muda.Ila sina uhakika kama Precision bado inakwenda huko
 
Tangazo LA nauli LA fastjet linasema nauli kuanzia 123,000 halisemi ni 123,000.ukiingia kukata ticket nauli kubwa kuliko hiyo hupati ya 123,000.Hiyo ni lugha ya kibiashara ya kuita wateja inaitwa invitation to treat.Ni sawa na unaenda dukani unakuta kwenye kioo wameweka suti ya maana bei wamebandika 15,000 unaingia mkuku dukani kuwa nataka Hiyo ya 15,000 wanakujibu zimeisha za bei hiyo zipo za laki mbili tukupe?ndio mambo ya hizo offer za fastjet
 
Naona sio sawa kuwa condition mfano civil servants/government officials kupanda ATCL..

Hili Shirika halijafikia hadhi ya BA ivyo kuwafanyia promo ya namna hiyo kwamba watumishi wote wa serikali wapande ATCL..

Juzi hapa nasikia iligoma kufyatua matairi wakati inataka ku land KIA leo uanze kulazimisha watu wapande ndege ambayo haina ubora na pia kiusalama haipo vizuri, hilo naona Mkuu sio sawa..

ATCL bado sana Mkuu. Ndege zenyewe mbili hazina ubora, mara ndege mbovu, mara safari imesogezwa mbele, mara safari imekuwa cancelled.. Halafu uwafanyie promo..?? Fanyia promo kitu kizuri bwana.
 
Tuna tume ya ushindani FCC ambayo ni sleeping lion ...hii tume kama ingefanya kazi yake kwa mujibu wa sheria ingesaidia sana uchumi wetu. Kinyume chake wamekuwa wakisubiri zaidi kesi badala ya kuingilia mambo kabla hayajafika hatua ya athari. Ukisoma sheria iliyounda ile tume ni mzuri kweli lakini ni kama pambo kwa yanayoendelea. Sijui wanasubiri JPM nao awatembelee ghafla ndio wajue wajibu wao?
 
Naona sio sawa kuwa condition mfano civil servants/government officials kupanda ATCL..

Hili Shirika halijafikia hadhi ya BA ivyo kuwafanyia promo ya namna hiyo kwamba watumishi wote wa serikali wapande ATCL..

Juzi hapa nasikia iligoma kufyatua matairi wakati inataka ku land KIA leo uanze kulazimisha watu wapande ndege ambayo haina ubora na pia kiusalama haipo vizuri, hilo naona Mkuu sio sawa..

ATCL bado sana Mkuu. Ndege zenyewe mbili hazina ubora, mara ndege mbovu, mara safari imesogezwa mbele mara safari imekuwa cancelled.. Halafu uwafanyie promo..?? Fanyia promo kitu kizuri bwana.
Mfanyakazi wa serikali hupanda gari za serikali kwa nini akatae kupanda ndege ya serikali. Si ni chombo cha usafiri cha mwajiri wake wapande ndege za ATCL
 
Mi napendelea ushindani hu uendelee zaidi, tena ningependa hata Precision na yenyewe iweke route ya huko kwa kina Zitto ili mwishoni mwa siku wateja wafaidike. Huoni shida tunayo ipata kwa Tanesco!? Ilikua hivyo Enzi za TTCL pia. Fastjet na ATCL wangeweka pia route ya Mwanza KIA as well ili Precision nae ashike adabu; njia hiyo huyu jamaa ana bei za ajabu sana. Ushindani ni muhimu kwa huduma bora; angalia sasa hvi, nani anaangaliaga TBC kwa habari makini? Nani anasikilizaga TBC taifa kwa habari makini!? Jibu hakuna au kama wapo basi ni less than 20 % ya customers wa hizo huduma, why, jibu ni rahisi tu, "Huduma bora" ndio watu wanacho tafuta.
 
Wanabodi,

Declaration of Interest Kuhusu Uzalendo.
Naomba ku declare interest yangu kuhusu uzalendo wangu kwa nchi yangu, kwa sababu, ukiibua hoja yoyote humu, kuhusu utendaji usiridhisha wa mashirika yetu ya umma ya kizalendo, utanyooshewa vidole kwa kutuhumiwa wewe sio mzalendo. Ile siku nilipoibua mjadala huu kuhusu ATCL,
ATCL, tuache siasa kwenye usafirishaji abiria. It's not fair kuchelewesha abiria kwa dakika 45 wakiwa ndani ya ndege, kumsubiria abiria mmoja kigogo ambaye ni waziri
nilishutumiwa hadi na maziri husika kwa kukosa uzalendo, hivyo kuomba headline ibadilishwe!.

Uzi huu ni uthibitisho wa uzalendo wangu, unapoona kuna uwezekano wa shirika lenu kuhujumiwa kwa ushindani usio sawia na mashirika ya nje, wazalendo wa kweli hatuwezi kunyamaza. Hivyo huu ni uzi wa kizalendo, kwanza kwa kuuliza swali tuu, jee kuna uwezekano, Shirika la Ndege la Fast Jet, linalihujumu shirika letu la Ndege la ATCL, kwa kuvamia routes za ATC na wao kupunguza bei kwa more than 50%!. Baada ya swali, pia ninatoa mapendekezo ya hatua za kuchukua, kufanya protection ya kilicho chetu.

ATCL inakwenda Kigoma mara mbili kwa wiki, kwa kutumia ndege yetu ya Bombadier -400, inayotumia Pangaboi, hivyo safari kuchukua muda wa saa 2.45, kwa nauli ya TZS 365,000 (japo tulielezwa nauli ni 165,000), lakini leo nimeona tangazo kuanza kuuzwa kwa tiketi za Fast Jet, kwenda Kigoma, ambapo safari zitaanza tarehe 1 Mwezi Machi, Fast Jet watazindua safari kati ya Dar es salaam na Kigoma kwa safari 3 kwa wiki, siku za Jumanne, Alhamis na Jumamosi kwa nauli ya Tsh 123,000. kwa kutumia ndege za kisasa aina ya Embraer E 190 ambayo ni Jet engine, safari itachukua muda saa moja tuu!.

Jee uamuzi huu wa Fast Jet, ni uamuzi tuu wa kawaida wa kibiashara, ili kuleta ushindani kwa kutoa more choices na ku provide some better a cheaper options kwa wateja wa usafiri wa anga, au una lengo la kuihujumu ATCL?, kwa kuifuata kule inakoruka, na wewe unapeleka ndege yako route ile ile, unaongeza frequency, unapunguza nauli, unatumia ndege bora Zaidi ya jet engine, wakati mwenzako ana bangaboi, unafanya direct route, kuruka kwa muda mfupi Zaidi wakati mwenzako anapitia Dodoma!, kuna mtu kweli ambaye ni time conscious na cost conscious ataendelea kupanda ATCL kwenda Kigoma, tangu siku Fast Jet, itaanza kuruka route hiyo?.

Kwa Nini Ndege Hazipangiwi Routes na TCAA Kama Mabasi Yanavyopangiwa na Sumatra, au Masafa na TCRA?.
Ukinunua dala dala, unaomba kibali Sumatra, wanakuonyesha routes zenye nafasi unachagua, kama unataka routes Fulani zenye mabasi mengi, unaambiwa hiyo route imejaa!. Vivyo hivyo kwa TCRA kwenye kugawa masafa, wengi wangetaka kutangazia DSM kwa sababu ndio kwenye wateja wengi, lakini TCRA inakulazimisha kwenda sehemu ambako redio hazijajaa!. Vivyo hivyo kwa Kampuni za simu, kulazimishwa kwenda hata sehemu kusiko na soko!.

Kama ATCL inakwenda Kigoma, kwa nini Fast Jet nayo iende Kigoma tena kwa bei nusu ya ATCL?.
Kwa nini TCAA wasiilamishe Fast Jet iende Singida, Iringa, Tanga, au route ambayo haina kabisa ndege?, kwa nini ndege zisongamane Dar, Mwanza, Kia, ect wakati Tanzania tuna routes kibao, na destinations tele hazina ndege?.

Hostile Kick Out na Hostile Take Over ni Mbinu Chafu za Ku Create Monopoly Kwa Kuwafungasha Virago Wapinzani Wako, Kama ilivyo Inside Trading!.
Mimi licha ya kuwa ni mwanahabari wa kujitegemea, pia ni mfanya biashara wa huduma za Radio na TV Programs production. Zikitangazwa tenda za utayarishaji wa Vipindi, washindani wako wenye akili Zaidi hufanya "inside trading", kwa ku collude na watu a ndani, kujua bajeti iliyotengwa, kisha kwenye tenda yao, wanaweka bei ya chini ajabu kuliko hata bei ya soko, tenda inafunguliwa wewe bei yako inakuwa juu, unakuwa kicked out, mwenzako mwenye bai ya chini, anashinda tenda, kisha wale wanamfanyia appreciation kulipia pesa stahiki na kugawa cha juu as kick backs!.

Jee hiki kinachofanywa na Fast Jet sio hostile kick out of ATCL out of business kwa wao kushusha sana gharama ili ATCL akose wateja kwenye routes hizo, ajitoe kwenye hizo routes, ndipo Fast Jet waweke gharama halisi?. Mbinu hii hutumika kumuondoa mshindani wako kwenye soko kwa kuweka ghara za chini sana na kujiendesha kwa hasara kwa muda Fulani, kisha akiisha ondoka, ndipo wewe utawale soko!.

Hostile take over ni kama kile kitu kilichofanyika kwa kwenye ile vita ya bia, (the beer war), kati ya KBL na TBL, Kenya walishusha bei ya bia zao zinazokuja Tanzania, na kuuzwa kwa bei ya chini kuliko bia za TBL, ilifikia mahali watu wa mikoa ya Arusha na Moshi kunywa Zaidi Tusker kuliko Ndovu, vita hii ikamalizwa kwa makubaliano ya wakubwa, kuuziana viwanda juu kwa juu, matokeo yake kiwanda cha Kibo, kikafungwa!.

Jee bei ya tiketi ya Fast Jet ya Dar-Kigoma is it realistic, au wameshusha ili kuiua ATCL?.

Nini Kifanyike Kuinusuru ATCL na Ushindani Usio Sawia.
  1. A Political Will, Lazima Twiga Aendelee Kuchanja Mbuga!. Kwa vile ATCL ni ndege yetu, lazima tufike mahali. nchi yetu ichukue maamuzi ya kisiasa ya kuinusu ATCL dhidi ya ushindani usio sawia kutoka ndege za mashirika ya kipepari na kibeberu, hata kama uamuzi huo utakuwa unakwenga against free trade, ikiwemo kuandika waraka kwa taasisi zote za umma, wizara, idara na Wakala za serikali, kwa safari zote za kikazi, lazima kwanza waitumie ATCL, hata kama ni ghali Zaidi na inakwenda pole pole Zaidi lakini Fedha za umma kwenye usafiri wa ndani, laaima kwanza ziende ATCL, kama hawana route hiyo ndipo wapande ndege nyingine!. Hili linawezekana, mimi nimefanya kazi na Waingereza chini ya FCO, watu wote wanaolipiwa usafiri na serikali ya UK. lazima wapande BA, hata kama ni ghali, ikiwa BA hawa route hiyo ndipo wa[ande routes nyingine.
  2. Tuchukue Protective Measures Kulinda ATCL. Hapa ni kuhakikisha ATCL inalindwa kibiashara kwa namna nyonyote ikiwemo some exclusive routes, na kuitumia TCAA kufanya restrictive measures kuzuia routes za ATCL kuingiliwa, na kuitumia Fair Competition kuzuia mashirika mengine yasishushe bei bolow bussness sense ili tuu kuwaua washindani wako wa kibiashara. ili ATCL ipewe some monopoliy Fulani hadi I stabize kibiashara na kutawala soko. Hili liliwahi kufanyika kulinda viwanda vya ndani dhidi ya cheap imported products.
  3. Kuandaa Kampeni za Uzalendo Watanzania Wazalendo Tupande ATCL!, hii ni kampeni maalum ya kujenga upya moyo wa uzalendo kwa wasafiri wa ndege wa Tanzania, kujitolea kupenda kupanda ndege za ATCL kwa kuhimiza penda chako, jenga chako, kama Watanzania wote, tutapanda ATCL hivyo hivyo ilivyo despite all the odds, baada ya miaka michache, ATCL nayo itakuwa na uwezo wa kununua jet, na kufanya safari za hasaka, na hizi pangaboi za Bombadia zitakuwa ni za group routes kusafirisha makundi ya wanafunzi na wanavyuo kwenye group trips.
  4. Hata kama serikali itachukua hatua za kuibeba ATCL kwa kila aina ya mbeleko, Uongozi na Mehejment ya ATCL inawajibu wa kutobweteka na mbeleko ya serikali, bali kuhakikisha inatoa huduma bora na za ushindani, ili sisi tunaoamua kupanda ndege za ATCL, pia tusafiri huku tunapata raha kwa huduma nzuri, na sio tusafiri na ATCL kwa sababu tuu ya uzalendo lakini watu tunafiri huku tumekunja nyuso!.
  5. Kwa kadri ndege zetu zinavyozidi kuchelewa kuachiliwa, ndivyo washindani wa ATCL wanavyozidi kuipiga bao, hivyo nayoa wito kwa Watanzania wazalendo wenzangu, pia tutumie nguvu ya sala, kuombea ndege zatu ziachiliwe, ATCL ipeleke ndege kila kona.
  6. Hili ni la kwangu binafsi, kwa ndege za Mwanza, kama ATCL kila siku itampangia rubani mmoja mdada mweupe kama shombe shombe Fulani, na najua hajaolewa!, na kumtangaza ndie rubani wa ndege za Mwanza!, nawahakikishia ndege ya Mwanza, kila siku itajaza abiria mijibaba ya Kisukuma, hata wale Wasukuma wanaosafiri kwa mabasi, watadunduliza na kuhakikisha wanapanda ATCL, na hata ikitokea Fast Jet na Precision hata wakaweka nauli ya bure, bado ATCL ndio itajaza kwanza halafu wengine ndio watafuatia!.
Hitimisho.
ATCL ni ndege yetu, inahitaji upendo wetu na protection yetu, kama tunavyozipenda familia zetu, ukiisha oa au kuolewa lazima umpende mkeo, hata kama utakutana na mwanamke mrembo vipi, au mkeo umpende mumeo, hata kama utakutana na mwanaume mwingine tajiri vipi!.
Huu ndio uzalendo wa kweli!, hivyo namalizia kwa lile lile swali la msingi, tukiona kama ATCL inakabiliwa na ushindani usio sawia, jee tutumie utashi wa kisiasa kuinusuru ATCL yetu, au tuachie tuu huu ushindani uendelee, na kuilazimisha ATCL lazima ihimili ushindani huu na ikishindwa, then tuiache tuu ijifie?.

Jumatatu Njema.
Paskali


Tuitungue fastjet, huo ndo uzalendo, mimi naweza kutengeneza grenade tutegee na kuilipua, tukiangusha moja tu nina uhakika watu wataigopa kwa sababu ya kuhofia usalama wao, ATC yetu lazima isimame hata kama ikibidi hujuma dhidi ya ndege nyingine ili zishindwe, na iwe hivyo!

image406.jpg
 
Mimi nimeacha kabisa kuzungumzia mambo ya ndege za ATCL na makinikia maana ndiyo yalipelekea Lissu kupigwa risasi, bila Mungu kuingilia kati tusingekuwa naye Lissu, kuzungumzia mambo ya ndege za ATCL na makinikia unahitaji kuwa na moyo wa chuma, hivi zile ndege zilizoagizwa zimefika au bado hatujalipa deni, makinikia tutalipwa lini
 
Ukweli mchungu toka Ujamaa kufa kibudu hakuna Shirika LA Serikali lililofanya Vizuri.

Angalia TBC, TTCL, n.k yalivyo na angalia mashirika ambayo yaliuza baadhi ya share yanavyofanya vizuri.

Tukitaka ATCL ifanye vizuri wauze share kwa makampuni mengine. Kama ilivyo KenyaAirways.
 
Tuitungue fastjet, huo ndo uzalendo, mimi naweza kutengeneza grenade tutegee na kuilipua, tukiangusha moja tu nina uhakika watu wataigopa kwa sababu ya kuhofia usalama wao, ATC yetu lazima isimame hata kama ikibidi hujuma dhidi ya ndege nyingine ili zishindwe, na iwe hivyo!

image406.jpg
Jamani hebu angalieni mawazo ya uvccm yeye anafikiria kuua watu tu ili waogope kama walivyomfanyia tundu Lissu, mawazo ya hovyo sana haya
 
Tangazo LA nauli LA fastjet linasema nauli kuanzia 123,000 halisemi ni 123,000.ukiingia kukata ticket nauli.kubwa kuliko hiyo hupati ya 123,000.Hiyo ni lugha ya kibiashara ya kuita wateja inaitwa invitation to treat.Ni sawa na unaenda dukani unakuta kwenye kioo wameweka suti ya maana bei wamebandika 15,000 unaingia mkuku dukani kuwa nataka Hiyo ya 15,000 wanakujibu zimeisha za bei hiyo zipo za laki mbili tukupe?
Nimecheka kinyama, unaingia mkuku, msemo wa longtime, unaambiwa zimeisha, tukupe za laki mbili, unanywea, unatoka kichwa chini
 
Pasco umevurugwa...unaelewa maana ya soko huria?...uzalendo MYFOOT...uzalendo ni pamoja na kupata vitu kwa bei rahisi..kaman wewe unatikisa pesa kwenye miti sie tunazitafuta kwa jasho na pia tuna budi kuzitumia kwa busara sana...penye ushindani wa bei tutafuata huduma za bei rahisi...WACHA ATCL WAFIE MBALI maana hawawezi ushindani...it is the survival for the fitest...you lose you die.

KWA HOJA ZAKO NA NISIWE MZALENDO MILELE NA NIPIGWE RISASI NIFE IJULIKANE MOJA.
 
Makampuni ya Serikali hayapaswi kupewa exclusive rights katika route yoyote maana dhumuni kuu ni watu wapate usafiri,kodi ipatikane pia kampuni zishindane na kampuni nyigine, pesa izunguke watu wapate Mkate wao katika kiwango halali na biashara iwe bora, ATCL ikiwa kama Fastjet, TTCL kama Vodacom mbona hakuna shida kabisa, biashara ushindani katika mizani yenye uwiano,Serikali inalijua hilo, 'issue' ni ATCL imejipanga vipi kutoa Huduma bora..
 
Back
Top Bottom