Ukiunganisha dots utagundua hata yule Mbunge mzazibari aliyemuita Yuda alikuwa ni mjumbe tu. Binafsi nitashangaa sana kama Yuda atafuata nyayo za Job kujiuzulu kutokana na mashinikizo. Ninaamini alijifunza kwa yaliyomkuta mwenzake.
It's getting even murkier!
Ni hivi: Nchimbi ataitwa kwenye Kamati ya Maadili (Mwekekiti, Wassira).
Halafu atajadiliwa kwenye Kamati Kuu (CC) ya Chama (Mwenyekiti, Samia)
Pengine hadi hapo maamuzi yatakuwa tayari yametolewa juu yake ya kuonywa; kukaripiwa, au kufukuzwa ndani ya chama.
Kama hadi hapo hali itakuwa bado ni ngumu (yaani kakomalia kutojiuzulu).
Swala lake litajadiliwa ndani ya NEC (Mwenyekiti Samia).
Halmashauri Kuu itaamua kumfukuza/ kumbakisha? kwa wajumbe kupiga kura ya siri? Sina hakika kama Samia na Genge lake anaweza kuwa na subira ya namna hiyo, kwa sababu wanajuwa NEC inaweza kuwaangusha wao na kumsafisha Nchimbi.
Hapa jaribu pia kurejea kwenye uteuzi wa Mgombea wa CCM wa u_Rais, Samia alivyojipitisha kwa msaada wa Kikwete.
Je, kuna uwezekano kukaitishwa kikao cha Mkutano Mkuu wa Chama juu ya swala hilo?
Sidhani kuwa Nchimbi bado atakuwa yupo ndani ya CCM hadi wakati huo; iwapo kama hakujidhatiti vizuri na kuwa na timu nyuma yake itakayomfikisha huko.
Binafsi naamini, kwa hali ilivyo ndani ya chama hicho, inawezekana kabisa Nchimbi akashinikiza maamuzi yafikie kwenye ngazi hiyo ya chama; yaani ya Mkutano Mkuu.
Hiyo ndiyo pekee inayoweza kumsalimisha.