Kutokana na tafsiri yako au makamba mwenyewe?Ile hotuba kali ya Nape bungeni dhidi ya gesi huko kusini inawafanya kuweweseka,hapo anatafuta cheo kwa kuonyesha Nape ni mfitini kwa serikali na watu kama baba yake mzee Nnauye.
Sad!
Kila mtu anatoa tafsiri ya kwake. Tafsiri ya nani itakuwa sahihi?Jamani muwe mnasoma kwanza huku mmetulia hapo kamuabishaje Mzee Nnauye? soma taratibu anamaanisha ushahidi wa Mzee huyo marehemu ndio ulimfanya baba yake arudishwe kazini. Maana nyingine ni kuwa mzee huyo hakuogopa lile genge lilitaka kumfutilia mbali Mzee Makamba anachojaribu kutuambia January ni kuwa Nape ni jasiri, msema kweli na haogopi kuudhi makundi mengine ya kinafiki na hii tabia karithi kwa baba yake.Sina ushabiki na mwanakijani yyt.
Mzee alishtakiwa kuiba nyama (ng'ombe) kwenye sherehe, kesi ikafanyika waliohudhuria kwenye sherehe mmojawapo akaulizwa ubwabwa ulikuwa mkavu au ulikuwa na nyama? akajibu ulikuwa na nyama, kesi ikaisha walioshtaki wakashushuka .Nilikuwa nashangaa sana mwanafunzi anarisiti masoma yote na la kiswahili ss nimeamini.Kila mtu anatoa tafsiri ya kwake. Tafsiri ya nani itakuwa sahihi?
Mmh!! Kwaiyo nilifeli kiswahili?Mzee alishtakiwa kuiba nyama (ng'ombe) kwenye sherehe, kesi ikafanyika waliohudhuria kwenye sherehe mmojawapo akaulizwa ubwabwa ulikuwa mkavu au ulikuwa na nyama? akajibu ulikuwa na nyama, kesi ikaisha walioshtaki wakashushuka .Nilikuwa nashangaa sana mwanafunzi anarisiti masoma yote na la kiswahili ss nimeamini.
Jamani muwe mnasoma kwanza mzee huyo hakuogopa lile genge lilitaka kumfutilia mbali Mzee Makamba anachojaribu kutuambia January ni kuwa Nape ni jasiri, msema kweli na haogopi kuudhi makundi mengine ya kinafiki na hii tabia karithi kwa baba yake.Sina ushabiki na mwanakijani yyt.
January , hekima ya wazee kama Makamba ndiyo inayopooza munkari ya vijana.Pitia ujumbe wa Makamba anaosema kaupata alivyoenda kijijini kumuona mzee Makamba
Mkuu January kuna vitu vingine kweli nia inaweza kua nzuri lakini unisons between the lines unagundua ujumbe unamapungufu makubwa sana. Kwa culture au desturi za kiafrika usitegemee meza kuu ikaletewa ubwabwa hauna nyama, sembuse mgeni rasmi? Ingekua kaulizwa mshiriki nje ya meza kuu au mgeni rasmi hapo justification ingekuwepo. Sisemi mzee makamba aliswaga ng’ombe Lushoto ila nisemacho evidence aliyoitumia ku proove kuwa hapakua na udokozi it doesn’t held water. Maana kunauwezekano pia ukatakiwa kununua ng’ ombe kumi wa sherehe na wakanunuliwa watano au wakanunuliwa kumi kweli ila wakatumika watano tu na wengine watano wakapekekwa kusiko julikana. Na huenda mzee Makamba alikasmu majukumu ya ununuzi wa ng’ombe kwa wachini yake na wao wakapiga dili. kwa maana hiyo majibu ya Mzee Nnauye yalikua sahihi ya kuwa kweli alikula nyama lakini hainaanishi ng’ombe wote waliotakiwa kununuliwa walinunuliwa. Mzee Makamba anaweza kuwa sahihi pia kuwa aliwapa pesa kamili wale aliowatuma kununua ng’ombe na wakamuaminisha kuwa walinunua. This evidence based on one person or two can not justify the majority who attend in that ceremony. Sometimes maongeozi ya baba na mwana bora yakabaki nyumbani tu. Huenda mzee angejua you will share in the social media huenda angeiweka vizuei stori yake isiache mashaka katika ushahidi.
Mkuu pengine hujawahi kuwa na ndugu au wewe mwenyewe kutumikia Taifa katika ngazi za juu.Mmmh.. Swali hilo kuwa kama ndio utetezi siukubali, labda Mwalimu alimuonea huruma kwa jinsi alikuwa amechoka na kumrudisha CCM kazini
Kweli kabisa hata vipande vyanyama vikiwa sita wanakula wageni tuu. Ufisadi ccm ni jadi aiseeSasa si inawezekana alinunua nyama kilo 10 buchani kwa ajili ya wageni rasmi na wale ng'ombe na mbuzi akawaswaga kuwapeleka kijijini kwake. Ufisadi ulianza zamani nchi hii!
Huyo aliyesema hivyo hana maadili kabisa, ana roho mbaya kabisa.Mkuu siku ukisikia mtu akisema ni bora baba yako au mama yako au mmoja wa familia yako afe tu, utajisikiaje??
Ni bora angekufa tu, sina la kujivunia kutoka kwake.
Wale wale ,wanajijenga kupitia wazazi wao,ndio ttz la CcmHuyu jamaa nae ifike mahali ajijenge yeye kama yeye, umaarufu kupitia mzee wake sioni ukimfikisha popote.