Januari Makamba na Bumbuli taabani

Januari Makamba na Bumbuli taabani

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Bumbuli ni Jimbo linaloongowa na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia,Januari Makamba. CCM kindakindaki. Kada wa uhakika aliyepikwa akapikika. Akakabidhiwa Bumbuli ili aiongoze kama Mbunge. Lilikuwa Jimbo jipya lililohitaji Mbunge mpya. Bumbuli ikampata Januari Yusuph Makamba.

Bumbuli ina maumivu makali ya kimaendeleo. Haina miundombinu ya uhakika kama barabara. Barabara hazipitiki kwa tabasamu hasa wakati wa mvua. Zikiwa kwenye miinuko na kona,hazina hata changarawe. Zinateleza na kuogofya.

Masoko ya uhakika ya mazao. Mazao huzagaa hadi kuoza. Mbunge yuko Dar anaitumikia nchi. Maji safi na salama yapo kwa uchache na kwa wenye nazo. Wengi wanakunywa maji hatarishi na ya kujitoa mhanga.

Kuonana na Mbunge ni kwa njia ya facebook,twitter na instagram. Wanabumbuli wengi humuona Mbunge wao luningani tu. Maendeleo ya wananchi yamesimama. Yamebaki vilevile yakiwa yamepakwa chokaa badala ya rangi.

Taasisi ya Januari Makamba ya Maendeleo ya Bumbuli ipo mitandaoni ikinoga kwelikweli. Ina mipango na mikakati ya uhakika. Kwenye jamii halisi,hakuna kitu. Migogoro ya ardhi inazizima Bumbuli.

Wananchi lakini wanajivuna kuwa na Mbunge Naibu Waziri. Kuwa na Mbunge kijana anayetamani kuongoza nchi. Kwa hayo tu. Pia,kupata misaada ya hapa na pale toka mfuko wa Mbunge/Jimbo. Lakini,hawawezeshwi kujitegemea.

Januari na Bumbuli yake. Januari na Jimbo lake. Januari na wananchi wake. Januari na mikakati yake. Tafadhali wajali wananchi wako kimaendeleo yao ili wawe kielelezo cha kufaa kwako.

Jimboni kwanza!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
mzee tupa kuna watu wanamtetea eti hilo jimbo ni jipya,je amekuwa mbunge kwa miaka mingapi?
__edit post yako yabla hajaja mwalimu. FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
Huyu Dogo na Pala lake kazi Yake kula bata mjini akuna kitu anafanya kwenye jimbo lake nashauri UKAWA wamshukie wachukue lile jimbo
 
Ameshindwa kumaliza mgogoro wa kiwanda cha chai Mponde na kusababisha ukata wa hali ya juu. Ni yeye ndiye alihamasisha wananchi kuvamia kiwanda na kumfukuza muwekezaji bila kuwa na mipango mbadala. Kwa sasa wakulima wanalazimika kupeleka chai yao kiwanda cha Amani, chai inaharibika njiani kwa sababu ya umbali.
 
Unachosema ni kweli nilikwenda uko mwanzo mwa mwaka huu nikiwa kwenye reseach yangu nilipaswa kukaa kule kwa week moja ila ilishindikana kwasababu netwark ya sim hamna baadhi ya maeneo mf.kuna shule ya kata inaitwa Kihitu yaan pale walimu wanatembea km karibia 5 kufata mtandao.
 
Kazi kuwaandalia bongo movie chakula cha jion Serena Hotel. Vijana 350 @90,000=.

Ulimbukeni hiyo pesa kwa sehem kama Bumbuli ni kubwa sana ingesaidia hata kisima ama vitanda vya wagonjwa.

Atakuwa na laana jimbo alichukua kwa zengwe kumuangusha Mzee Sherukindo.

Ndio maana na system haimkubali kazi "kutoa siri" za ndani. Hana maadili na kipara chake.
 
Bumbuli ni Jimbo linaloongowa na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia,Januari Makamba. CCM kindakindaki. Kada wa uhakika aliyepikwa akapikika. Akakabidhiwa Bumbuli ili aiongoze kama Mbunge. Lilikuwa Jimbo jipya lililohitaji Mbunge mpya. Bumbuli ikampata Januari Yusuph Makamba.

Bumbuli ina maumivu makali ya kimaendeleo. Haina miundombinu ya uhakika kama barabara. Barabara hazipitiki kwa tabasamu hasa wakati wa mvua. Zikiwa kwenye miinuko na kona,hazina hata changarawe. Zinateleza na kuogofya.

Masoko ya uhakika ya mazao. Mazao huzagaa hadi kuoza. Mbunge yuko Dar anaitumikia nchi. Maji safi na salama yapo kwa uchache na kwa wenye nazo. Wengi wanakunywa maji hatarishi na ya kujitoa mhanga.

Kuonana na Mbunge ni kwa njia ya facebook,twitter na instagram. Wanabumbuli wengi humuona Mbunge wao luningani tu. Maendeleo ya wananchi yamesimama. Yamebaki vilevile yakiwa yamepakwa chokaa badala ya rangi.

Taasisi ya Januari Makamba ya Maendeleo ya Bumbuli ipo mitandaoni ikinoga kwelikweli. Ina mipango na mikakati ya uhakika. Kwenye jamii halisi,hakuna kitu. Migogoro ya ardhi inazizima Bumbuli.

Wananchi lakini wanajivuna kuwa na Mbunge Naibu Waziri. Kuwa na Mbunge kijana anayetamani kuongoza nchi. Kwa hayo tu. Pia,kupata misaada ya hapa na pale toka mfuko wa Mbunge/Jimbo. Lakini,hawawezeshwi kujitegemea.

Januari na Bumbuli yake. Januari na Jimbo lake. Januari na wananchi wake. Januari na mikakati yake. Tafadhali wajali wananchi wako kimaendeleo yao ili wawe kielelezo cha kufaa kwako.

Jimboni kwanza!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Tatizo ni wapinzani. Jimbo jeupe
 
huyu tapeli eti ofisi ya maendeleo ya bumbuli kaifungua dar.
twitter ndio mahali anapotumia kuhutubia wananchi wa bumbuli.
 
aisee hilo jimbo sio jipya lilikuwa la mzee shulukindo.....khe mbona mwanzoni mwa ubunge wa huyo kijana niliooona matangazo kibao akiionesha ofisi yake ipo gorofani mie nikafikiri bumbuli kuna magorofa, maji ,umeme. mmmmmmhhh nisalimieni mashewa
 
Ila ukweli Upo na lazma usemwe kwa upande wa halmashauri Idara ya afya imezozora kabisa wakati mwingine wabungee wa mikoani ni vzr wakawa Hands on na Sio Lazma wawe na pesa mf bumbuli inapata ruzuku ya maendeleoo kutoka serikalini lakini miradi hii imekosa usimamizi wa kutosha na ndio maana Hamna maendeleoo chanya na muhimu wabungee wawe wanakaa jimbonii ili kutatua matatizo ya wananchi wake kwa ukaribuu na kujua matatizo Yao mf kuna wakati Tulikuwa kwenye Research kule jimbonii tukashindwa kwenda zahanati ya mghwashwe jinsi ilivyo mbali ila pia unafikiri barabara za bumbuli zinatia huruma sana na Watoto wengi wa kike hawasomi kabisa!!
 
mhhhh makubwa sana haya

attachment.php
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom