Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,502
- 9,282
Vyombo vya ulinzi na usalama wilayani Kyerwa Mkoani Kagera vinamshikilia mkazi mmoja wa kijiji cha Kishanda anayejulikana kwa jina la Kamugisha Alfred kwa tuhuma za kumchoma mkuki na kumsababishia kifo askari wa mamlaka ya hifadhi za taifa Matonda Masungu aliyekuwa akimtafuta ili kumtia mbaroni kutokana na kutuhumiwa kufanya ujangili ndani ya hifadhi mpya ya Rumanyika.