gasper kolila
Member
- Oct 26, 2009
- 16
- 0
Kuhusu swala la umeme kuwa janga la kitaifa, ni kitu kilichosababishwa na serikali yenyewe kwani watendaji wake wameshindwa kufikiri mapema
na kutafuta suluhisho la kero hii. Tumepata tabu kiasi cha kutosha kwa sababu ya watu wachache wenye madaraka wanayoyatumia vibaya.
Kama ni kukosa mafuta ya kuendeshea mitambo ya IPTL tu kwanini sasa wasisimamishe posho za wabunge ili kunusuru taifa na giza pamoja na
kunusu uchumi utakaoporomoka ghafla bila viongozi wenyewa kugundua?
Wabunge bila aibu wanajua kabisa wakiwa wanajadili swala nyeti kama vile bajeti, na mambo mengine ya kitaifa kwa maslahi ya taifa na wananchi akiwa na mbunge ni mmojawapo, wanadhubutu kijadili kisiasa kwa maslahi ya chama..Hii ni aibu na italichukua taifa muda mrefu kujuta.
Viongozi wanatakiwa watazame maisha ya watoto wao na wajukuu na hata vitukuu lakini hawalijui hilo.
Viongozi waache ubinafsi, chuki za kisiasa ili waliongoze taifa kwenye njia ifaayo waache vioja na minyukano isiyo na maana sana kwa taifa na kizazi kijacho. Chadema nawafagilia kwani wako kwenye good track, ni wamoja so hawatupi wasiwasi.
na kutafuta suluhisho la kero hii. Tumepata tabu kiasi cha kutosha kwa sababu ya watu wachache wenye madaraka wanayoyatumia vibaya.
Kama ni kukosa mafuta ya kuendeshea mitambo ya IPTL tu kwanini sasa wasisimamishe posho za wabunge ili kunusuru taifa na giza pamoja na
kunusu uchumi utakaoporomoka ghafla bila viongozi wenyewa kugundua?
Wabunge bila aibu wanajua kabisa wakiwa wanajadili swala nyeti kama vile bajeti, na mambo mengine ya kitaifa kwa maslahi ya taifa na wananchi akiwa na mbunge ni mmojawapo, wanadhubutu kijadili kisiasa kwa maslahi ya chama..Hii ni aibu na italichukua taifa muda mrefu kujuta.
Viongozi wanatakiwa watazame maisha ya watoto wao na wajukuu na hata vitukuu lakini hawalijui hilo.
Viongozi waache ubinafsi, chuki za kisiasa ili waliongoze taifa kwenye njia ifaayo waache vioja na minyukano isiyo na maana sana kwa taifa na kizazi kijacho. Chadema nawafagilia kwani wako kwenye good track, ni wamoja so hawatupi wasiwasi.