Janga la Corona: Umoja wa Afrika mnatuangusha

Janga la Corona: Umoja wa Afrika mnatuangusha

mmteule

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
6,035
Reaction score
15,072
Najiuliza kwa Sauti, ingekuwaje mamia ya vifo vya COVID - 19 vinavyotokea Italy, Ufaransa, China nk nk vingeikumba Afrika.

?? Umoja wa Ulaya wangekuwa kimya hadi sasa?? Si kweli hata kidogo wenzetu wana moyo wa Upendo na Ubinadamu na Akili ya Kidiplomasia hakika tungepata misaada ya kila namna ikiwemo misaada ya Vifaa tiba na Wataalam kama ilivyotokea wakati wa Vifo vya EBOLA.

Nadiriki kusema kuwa AU mmetufedhehesha Waafrika kwani mmeshindwa kupeleka MADAKTARI 1500 (yaani angalau madaktari 30 kutoka kila nchi Mwananchama) happo ITALY kusaidia huduma za Afya kutokana na Kuzidiwa na Kesi za COVID -19.

Hivi mnadhani ni lini sisi Waafrika tutawasaida hao tunaowatukana Mabeberu kila siku? Hatujachelewa wakati ni sasa tuchukue hatua. Vijana tuko tayari....
 
Mwenyekiti wa huo muungano ni nan? Huo umoja upo kiupigaji Sana , ni jipu
 
Ndugu yangu achana na hayo mawazo...Kama we ni muislamu ingia msikitini omba Mwenyezi Mungu atuepushe, Kama we mkristo ingia kanisani omba Mwenyezi Mungu atukinge...Madaktari 30 kila nchi afrika watoke wapi...? Madaktari wenyewe huko afrika wakisikia we una Corona wanatimua...! Acha kbs masihara
 
Nakubaliana na wewe 100%.

Ila ninavyowajua wa-Italy ni bora afe kuliko atibiwe na ngozi nyeusi/manyani.

Madaktari wapelekwe wakasaidie kusogeza madrip na kusomba maiti hapo sawa ila sio kutibu.
 
Labda kukusaidia kuwaza....e'm tutafakari sisi Afrika eneo gani tupo strong ktk vita hii tunaweza kusaidia wenzetu wa Italy..! Je msaada wetu uwe ni ule wa kupeleka madaktari (technology) ?..asilani hatuwezi..! Hawa madokta wetu bado hawajaimaliza vita ya TB na Kifaduro..!

Mi napendekeza kwa kuwa Afrika inalo eneo kubwa, Ki inchi kama italy ni kidogo kwa eneo basi wale watakaopimwa na kuonekana hawana Corona waje afrika tuwape 'pande fulani la ardhi' wajistiri mambo yakiwa powa huko kwao watarudi kuendelea na maisha...!
 
Huwezi saidia mtu wa nje wakat wewe mwenyewe khar yako ni tete...

Kufanya hivyo ni sawa na kujizika shimoni
 
mmteule, Mkuu Mmteule, hapa utakuwa unaionea bure AU. Africa hatuna uwezo huo.
The only thing AU can do to Italy ni kutoa tuu pole!.
Nchi za Africa hazina madaktari hata wa kuzuia tuu malaria, ndio iwe Corona?.

Ni kufuatia hali halisi ya uwezo wa bara la Africa kukabili majanga, Mungu ndio ametukingia mkono Africa kufanya athari ziwe kidogo ukilinganisha na China na Ulaya.
P
 
Mkuu Mmteule, hapa utakuwa unaionea bure AU. Africa hatuna uwezo huo.
The only thing AU can do to Italy ni kutoa tuu pole!.
Nchi za Africa hazina madaktari hata wa kuzuia tuu malaria, ndio iwe Corona?.

Ni kufuatia hali halisi ya uwezo wa bara la Africa kukabili majanga, Mungu ndio ametukingia mkono Africa kufanya athari ziwe kidogo ukilinganisha na China na Ulaya.
P
Paschal uwezo wa kupeleka Madaktari ambao hata wangekuwa wabeba Machela huko Italy tunao sema tu Viongozi wetu wamekosa weledi katika Diplomasia ya hili janga la COVID-19
 
Ndugu yangu achana na hayo mawazo...Kama we ni muislamu ingia msikitini omba Mwenyezi Mungu atuepushe, Kama we mkristo ingia kanisani omba Mwenyezi Mungu atukinge...Madaktari 30 kila nchi afrika watoke wapi...? Madaktari wenyewe huko afrika wakisikia we una Corona wanatimua...! Acha kbs masihara
Ha haaaa nouma Sana , sasa kama watu wanaenda udaktari ili wapate ajira unategemea nn sasa
 
Ndugu yangu achana na hayo mawazo...Kama we ni muislamu ingia msikitini omba Mwenyezi Mungu atuepushe, Kama we mkristo ingia kanisani omba Mwenyezi Mungu atukinge...Madaktari 30 kila nchi afrika watoke wapi...? Madaktari wenyewe huko afrika wakisikia we una Corona wanatimua...! Acha kbs masihara
Madaktari wana miiko yao mkuu hawawezi kukimbia kazi kamwe kutokana na janga.
 
Kwani hao umoja wa ulaya wamepeleka madaktari wangapi? Pia kwa taarifa yako huko itali mtu mweusi na mzungu akipata kolona anatibiwa mzungu mtu mweusi anaachwa kwanza, sasa we pelekwa wanyakyusa wako huo wakawe makuli wa kubeba maiti hakuna mzungu atakubali kutibiwa na mtu mweusi. Kwa ubaguzi wao waache wapambane na hali zao.
 
Mimi daktari siwezi kwenda huko kubeba laana za wazungu,madaktari wa kiafrika wakienda huko watakuwa wamejitakia kufa kwa kunyanyapaliwa na kubebeshwa maboksi ya dawa.
Paschal uwezo wa kupeleka Madaktari ambao hata wangekuwa wabeba Machela huko Italy tunao sema tu Viongozi wetu wamekosa weledi katika Diplomasia ya hili janga la COVID-19

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wamezidiwa na CAF. Angalau CAF wamejadili changamoto ya corona na kuamua njia bora ya kuendesha mchezo wao.
 
Najiuliza kwa Sauti, ingekuwaje mamia ya vifo vya COVID - 19 vinavyotokea Italy, Ufaransa, China nk nk vingeikumba Afrika.

?? Umoja wa Ulaya wangekuwa kimya hadi sasa?? Si kweli hata kidogo wenzetu wana moyo wa Upendo na Ubinadamu na Akili ya Kidiplomasia hakika tungepata misaada ya kila namna ikiwemo misaada ya Vifaa tiba na Wataalam kama ilivyotokea wakati wa Vifo vya EBOLA.

Nadiriki kusema kuwa AU mmetufedhehesha Waafrika kwani mmeshindwa kupeleka MADAKTARI 1500 (yaani angalau madaktari 30 kutoka kila nchi Mwananchama) happo ITALY kusaidia huduma za Afya kutokana na Kuzidiwa na Kesi za COVID -19.

Hivi mnadhani ni lini sisi Waafrika tutawasaida hao tunaowatukana Mabeberu kila siku? Hatujachelewa wakati ni sasa tuchukue hatua. Vijana tuko tayari....
Sisi tunasuburi kwa hamu wapone, then tuombe misaada.
Mungu warehemu Waafrika!!
 
Acha kujidharau
mmteule, Mkuu Mmteule, hapa utakuwa unaionea bure AU. Africa hatuna uwezo huo.
The only thing AU can do to Italy ni kutoa tuu pole!.
Nchi za Africa hazina madaktari hata wa kuzuia tuu malaria, ndio iwe Corona?.

Ni kufuatia hali halisi ya uwezo wa bara la Africa kukabili majanga, Mungu ndio ametukingia mkono Africa kufanya athari ziwe kidogo ukilinganisha na China na Ulaya.
P

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom