Janeth Rithe: Serikali iwasikilize Wamiliki wa mabasi

Janeth Rithe: Serikali iwasikilize Wamiliki wa mabasi

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2014
Posts
643
Reaction score
1,603
TAARIFA KWA UMMA

Serikali Iwasikilize Wamiliki wa Mabasi.

Kwa wiki sasa, sekta ya usafirishaji imeingia mushkeli baada ya Chama cha wamiliki wa mabasi Tanzania (TABOA) kutishia na hata kusitisha huduma zao kwa baadhi ya mikoa hapa nchini.

Chanzo cha mgomo huo, kinatajwa kuwa ni kutokana na mabadiliko ya mfumo wa ukatishaji tiketi kwa njia ya kielektroniki ambao Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Ardhini (Latra) inataka wamiliki wa mabasi kutumia mfumo mpya ujulikanao kama POS.

Baadhi ya wadau wa biashara ya usafirishaji abiria nchini wanadai mfumo huo mpya unawalazimisha kuwa na kiasi cha fedha katika laini ya simu au wakala wa huduma za fedha kwa makadirio yanayolingana na nauli tarajiwa kwa idadi ya viti vya basi ili kuweza kufanyakazi.

Mfumo huo unatajwa kusababisha matatizo kadhaa yakiwamo baadhi ya wamiliki wa mabasi kupigwa faini za mara kwa mara na hata wengine kufungiwa magari yao kutokana na kutokujua vema matumizi ya mfumo huo.

Kutokana na mkanganyiko huo, sisi ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kupitia Latra kuitisha kukao na wamiliki wa mabasi ili kujadiliana kwa pamoja mfumo gani rafiki utumike kukata tiketi za abiria ili kuondoa malalamiko na misigano isiyokuwa ya lazima.

Pili ACT Wazalendo tunaitaka Latra kufanyakazi kwa kuzingatia weledi wa kitaaluma na kukumbuka kwamba mifumo inayotumia teknolojia ya kisasa inayoingia nchini ni mipya kwetu, hivyo inahitaji muda wa kutosha kwa wadau kuielewa na kuitumia kwa ufasaha.

ACT Wazalendo tunaona badala ya Serikali kulumbana na wamiliki wa mabasi na hata kutishia kuwafungia au kuwapiga faini zisizo na tija, ni wakati sasa wa kufanyia kazi malalamiko yao kwa kina sambamba na kutoa elimu kwa wadau faida ya mfumo huo mpya.

Aidha sisi ACT Wazalendo tunaona kwamba wakati Latra inaendelea kutatua changamoto za mfumo huo mpya, iwaruhusu wamiliki wa mabasi kuendelea kutumia mashine zinazotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) maarufu EFD's licha ya kuwa nazo zinakabiliwa na changamoto za mtandao kulingana na jiografia ya nchi yetu.

Sisi ACT Wazalendo, tunaamini njia pekee ya kutatua changamoto ni kukubali kusikilizana kwa njia ya mashauriano na kusikilizana.

Imetolewa na:
Janeth Joel Rithe
N/Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma.

Leo Machi 12, 2021

Screenshot_20210312-155900_1615554035811.jpg
Screenshot_20210312-155912_1615554062385.jpg
 
Huo mfumo ni wa kishetani na umetengenezwa na mtu kilaza wa teknolojia, mbona POS za halmashauri hazilazimiki kuwa na real money ili zifanye kazi.
 
Huo mfumo ni wa kishetani na umetengenezwa na mtu kilaza wa teknolojia, mbona POS za halmashauri hazilazimiki kuwa na real money ili zifanye kazi.
Hebu fafanua tafadhali..

Kwani hizi mashine zina utofauti gani na uwakala wa TIGo pesa na Mpesa!?
 
Tofauti ni kubwa sn, hii machine inatakiwa iwe kama POS zingine kazi kubwa ni kutoa risiti maana huu siyo uwakala wa mpesa
Hizi mashine wanapewa wenye mabasi au mawakala binafsi wa ukatishaji tiketi!?

Kama ni mawakala binafsi security ya wenye mabasi na wateja wasafiri ni ipi!?

Huyu wakala anayekatisha tiketi.. mtaji wake yeye ni nini!?
 
Huo mfumo ni wa kishetani na umetengenezwa na mtu kilaza wa teknolojia, mbona POS za halmashauri hazilazimiki kuwa na real money ili zifanye kazi.
Mkuu kama kuna kitu hukijui usiwe unacomment
 
Kama unaweza kununua gari la 250 mil iweje ukose 3mil ya kudeposit kwenye POS yako
 
La wamiliki mnaweza kuliingilia na kulipazia sauti,ILA likija suala la maslahi ya madereva/wafanyakazi ambao haohao Taboa na Tatoa ndio waajiri wao hua hamuongei!!
 
Hizi mashine wanapewa wenye mabasi au mawakala binafsi wa ukatishaji tiketi!?

Kama ni mawakala binafsi security ya wenye mabasi na wateja wasafiri ni ipi!?

Huyu wakala anayekatisha tiketi.. mtaji wake yeye ni nini!?
Bora wangepewa EFD machine kama ilivyo kwa wafanya biashara wengine
 
Bora wangepewa EFD machine kama ilivyo kwa wafanya biashara wengine
Shida wao kama mawakala hawana Gari. Ukiwapa EFD unawapa kwa kigezo gani!?
Wakikatishwa tiketi kisha wakaondoka na fedha!? Mwenye basi anazipataje!? Naye akigoma kuwasafirisha watu.. abiria analindwaje!?

Kwao hii ni biashara.. waweke deposit sawa na fedha watakayo ipata.. sioni ugumu uko wapi.. mimi nina basi wewe ni abiria yeye ni wakala.

Kwenye mashine anaelfu ishirini, huduma yake ni elfu moja, fedha ya mwenye basi ni elfu 19... Nikikagiwa tiketi.. akiamua kukimbia mfumo unayo pesa ya mwenye gari.. mbona ugumu hakuna!?

Shida stand zina wezi wengi na matapeli wanaopenda kitonga
 
Shida wao kama mawakala hawana Gari. Ukiwapa EFD unawapa kwa kigezo gani!?
Wakikatishwa tiketi kisha wakaondoka na fedha!? Mwenye basi anazipataje!? Naye akigoma kuwasafirisha watu.. abiria analindwaje!?

Kwao hii ni biashara.. waweke deposit sawa na fedha watakayo ipata.. sioni ugumu uko wapi.. mimi nina basi wewe ni abiria yeye ni wakala.

Kwenye mashine anaelfu ishirini, huduma yake ni elfu moja, fedha ya mwenye basi ni elfu 19... Nikikagiwa tiketi.. akiamua kukimbia mfumo unayo pesa ya mwenye gari.. mbona ugumu hakuna!?

Shida stand zina wezi wengi na matapeli wanaopenda kitonga
No yaani mwenye mabasi wapewe EFD mashine kama wengine mkuu
 
Wenye mabasi wakipewa EFD ni sawa.. na mawakala watapewa nini mkuu!?
Si kuna ofisi za mabasi mkuu? wakala atakuwa anawasiliana na mwenye basi anamwabia nina shilingi 5 ya abiria fulani kata huko uliko pesa yako ipo ofisi, kuna kuwa na tiketi za mkono pamoja na online.
Wenye mabasi wakipewa EFD ni sawa.. na mawakala watapewa nini mkuu!?
 
Si kuna ofisi za mabasi mkuu? wakala atakuwa anawasiliana na mwenye basi anamwabia nina shilingi 5 ya abiria fulani kata huko uliko pesa yako ipo ofisi, kuna kuwa na tiketi za mkono pamoja na online.
Mie nadhani Mawakala iwe biashara au entity inayojitegemea.. na Wenye mabasi wanaweza kuanzisha mawakala wao wa kuajiriwa ofisini.. ili kuondoa double standards..

Wakala ukiwa na ubia naye alikata tiketi ipewe uzito uleule sio amekatia ofisini ndio anaonekana wa maana.

Na lazima tuamue kama tunataka kutumia mfumo ..basi tutumie mfumo.. sio huku mfumo huku makaratasi.. hatuwezi kwenda.

Kwa mfumo huu sio kama wenye mabasi wanalalamika.. nina shaka.huenda wanaolalamika bioy wale wale madalali wanaonyonya abiria na wenye mabasi.

Mfumo uko safi... Ila inahitaji elimu kutolewa ya kutosha..
 
Back
Top Bottom