JamiiForums: Tumerejea baada ya kutoweka hewani kwa wiki 3

Maxence Melo

JF Founder
Feb 10, 2006
4,230
13,415
Wakuu,

Tumerejea hewani baada ya siku 21 tukiwa hatutoi huduma hii.

Kilichotokea:

Mnamo Jumapili, tarehe 10 Juni 2018 tulipata kuiona notisi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) ikitutaka kusitisha huduma mara moja nasi tulitii na kusitisha siku hiyo.

Tuliwasiliana na Mamlaka na ilitusikiliza na tukafuata taratibu za kujisajili ambapo wikiendi hii imetupa leseni ya miaka 3 na kuturuhusu kuendelea na huduma kwa wateja wetu.

Pamoja na mengine, tuliwasilisha maoni yetu kwa maandishi kwa mamlaka(TCRA) juu ya vipengele vya kanuni tunavyoona hazitekelezeki na kutoa mapendekezo ya maboresho. Tulisisitiza mambo manne kwa haraka:

1) Kanuni ya 5 kipengele (e) kinavunja haki ya faragha ya watanzania iliyowekwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi na utekelezaji wake utakuwa changamoto kwa wengi.

2) Kanuni ya 10 kipengele (b) inayolifanya kosa la jinai kutoweka nywila(password) kwenye kifaa cha kidijitali, tulishauri iangaliwe upya.

3) Kanuni ya 6 kipengele (3) inayotoa muda wa saa 12 kuondolewa kwa maudhui yanayolalamikiwa tulishauri iangaliwe upya kwani kwa uzoefu wetu inazuia haki ya kusikilizwa na kupelekea kuzimwa sauti za wananchi.

4) Gharama za usajili zilizowekwa zinazuia baadhi ya wanaotoa huduma kuendelea kufanya hivyo kwani si wote wenye uwezo huo na si kila blog inafanya kazi kibiashara. Tulipendekeza ikibidi yawekwe madaraja ili hata wale wadogo wasiachwe nyuma.

Mwisho:

Tunasikitika kwa kilichotokea hivyo tunaomba radhi kwa watumiaji kwa usumbufu wowote uliotokana na kusitishwa kwa huduma hii. Pia tunawashukuru kwa uvumilivu wenu na kuendelea kuwa nasi katika kipindi chote huduma ikiwa haipatikani.

Wateja wetu walio nje ya mipaka ya Tanzania walioathirika na yaliyotokea, tunawaomba radhi sana.

KUHUSU USALAMA WA DATA:
Kwa wale ambao wanahitaji kuongeza kuimarisha faragha zao, kwenye profiles zenu mnaweza kuweka email mpya ya kuwa inatumika hapa JamiiForums na kwingineko mitandaoni. Tengeneza email mpya kupitia Hushmail - Enhanced email security to keep your data safe au Secure email: ProtonMail is free encrypted email ili uwe unaitumia kwa mawasiliano yaliyo salama zaidi. Ukiamua kutumia jina halisi (verified), wasiliana nasi ili tulithibitishe na uwekewe VERIFIED badge.

Tunatambua kuwa Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania imetoa ulinzi wa Uhuru wa Kujieleza na Uhuru wa kutoingiliwa mawasiliano kwa mujibu wa Ibara ya 18:

Screen Shot 2018-07-01 at 19.04.57.png


Kwa kiswahili:

Screen Shot 2018-07-01 at 19.17.10.png


Mambo ya kuzingatia:
Wateja wetu tunawashauri kusoma sera yetu juu ya faragha na pia mwongozo wa ushiriki katika utoaji maoni katika JamiiForums.


Asante
 
Mkuu max, tupo pamoja katika jitihada zako na manguli wengine wa mitandao ya kijamii, za kutaka JF ifuate serikali inavyotaka.

Sasa kila sharti ambalo serikali imeweka (kupitia TCRA), JF wamelipiga chini na kila zuio limetafutiwa kiungo mchezaji na limeshughulikiwa kama yule kiungo mkabaji wa Uruguay Lucas Torreira alivyomuweka kapuni Christiano Ronaldo jana mjini Kazan.

Hivyo basi, JF imerudi hewani na tujiimarishe kwa kuwa na mikakati ya kupambana na shida kama hizi huko mbele.

Serikali itambue kwamba JF ina nguvu kubwa nyuma yake, nguvu ya uvumilivu na umakini.

Napenda sana kuwaasa wanachama wenzangu kwamba, tuitunze na kuilinda JF na JF nayo itatutunza.
 
Hongereni sana. Kwa kipindi cha wiki tatu bila kuwa na JF kimethibitisha umuhimu wa jukwaa hili kuwepo.

Niwapongeze pia kwa kufuata masharti muliyopewa na serikali na hasa kutoa maoni pale mulipogundua kuwa, huenda maslahi yetu sisi wateja wenu kwa baadhi ya mambo yanaweza kuwa mashakani na hivyo kutoa ushauri kwa nia ya kuboresha.

JF ni mashine kubwa ambayo haitakujafutika kirahisi kwa sababu ya hazina kubwa ya mawazo ya wadau ambayo yanaifanya JF kuwa maarufu kiasi cha kutaka kutekwa nyara na au kuigizwa na majirani zetu.

Nawashauri wadau tujiepushe kutoa matusi tunapochangia kwa sababu unapotukana watu wengine utarajie kupata matusi pia na hivyo kupoteza lengo la jukwaa.
 
Shukrani nyingi sana Maxence Melo kwa mapito yote uliopita ninaamini sasa watu tutumia jukwaa hili kwa manufaa ya wengi ma si kwa makwazo ya wengi.

Rai yangu kwa watumiaji wenzangu wa mtandao huu nafasi yoyote inayotokea leo itumie vizuri ili kesho utabasamu kwa mema na mazuri uliofanya jana.

Mungu atujalie kuwaza na kutenda yalio mema kwa manufaa ya wengine .
 
Ahsanteni sana na hongereni pia uongozi mzima wa JF kwa kulishughulikia suala lile hadi tumerudi hewani tena, maana tuliimiss sana hii platform.

Mbarikiwe sana kwa kulipigania hili pasi kukubali baadhi ya vipengele vya sheria vinavyonyima uhuru wa kujieleza kufuatwa.
 
Poleni sana! Hata hivyo, hili ni fundisho kwetu sote kwamba mtu unapokuwa na neema, fursa, platform yoyote, ni vyema kuitumia vizuri kabla haijaondoka kwani fursa tunazokutana nazo kwenye dunia hii si za kudumu.

Aidha, kwa kuwa JF imerudi, huu ndio muda wa kila mtu kuitumia vizuri kwa namna ambayo italeta positive impact kwa jamii na nchi yetu kwa ujumla ili hata siku ikitokea tena vinginevyo, tuwe tulishaitumia vizuri kutimiza wajibu wetu.
 
Wakuu kabla ya yote nachukua nafasi hii kuwasalimia na kuwapa pole wote mlioguswa na kadhia iliyotokea. Kwa kifupi huwezi KULA MUWA BILA KUKUTA FUNDO.

Baada ya Muhtasari huo nijikite kwenye mada yangu... Kiukweli kwa leo nimekuja kuiombea dua tu hii forum yetu ya JF kwa Mungu muweza wa yote aendelee kuilinda.

Naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom