Jamii humpongeza sana kijana aliyefanikiwa kujenga nyumbani na anakuwa mfano wa kuigwa

Wang Shu

JF-Expert Member
Feb 1, 2014
2,563
3,708
Katika mafanikio kila mtu hutamani hayafikie basi ni kumiliki nyumba ni moja ya ndoto ya kila mmoja na rika tofauti, kila mtu anataka kuwa na kwake na familia yake.

Kwa Hali ya maisha ya sasa ni ngumu kiasi kujenga angali kijana,wapo wanaofanikiwa kujenga nyumba ya kuishi kipato cha kawaida hawa watu naweza sema ni "Silence Motivation Speaker".

Jamii inayomzunguka hasa vijana wa rika lake na wale wa karibu yake wanapata msukumo wa ujasiri wa kuthubutu wakiamini kumbe inawezekana!

Miaka 2 iliyopita nilipatwa na roho ya wivu wa maendeleo na kujitafakari Sana ni pale rafiki yangu niliyesoma nae aliponambia anapaua nyumba yake ya chumba 2 nilimuuliza swali moja tu "Umewezaje?"

Ni rafiki yangu ambaye nilimtangulia darasa 1 tulikuwa kama ndugu tulipanga chumba kimoja shule za kutwa changamoto nyingi tulitatua pamoja hatimae nilimaliza nikamuacha anaendelea na masomo.

Baada ya miaka kadhaa ananipa taarifa anajenga yeye alafu mimi bado nimepanga sikukubali kirahisi namna hiyo niliona kumbe naweza kujenga zaidi yake,hatimae sasa mwaka huu 2020 unaisha na mimi nampatia taarifa kuwa boma langu lipo kwenye linta.

Asante Sana rafiki yangu hujanipatia pesa lakini matendo yako na maneno yako ni vitu muhimu kwangu.
 
Usishindane kuwekeza liabilities, wekeza assets.Assets huzalisha liabilities but liabilities haziwezi zalisha assets.Nyumba,gari ya kutembelea,vifaa vya thamani vya ndani ni liabilites.Shamba, duka, utaalamu/ujuzi, company ni assets.
Tujifunze kwa wahindi, wanapanga kariokoo wanna miliki viwanda,mashamba makubwa,maduka makubwa.
Kwa nini wasomi wanazidi kupungukiwa akili Ktk competitive economy? What if wazazi wetu wangetuachia mashba makubwa yaliopandwa mazao ya kudumu badala ya xili nyumba walizokuwa wanashindana kuzijenga, tungekuwa wapi? Hongera umepata pa kulala ila hujasolve tatizo la kipato kisicho tetereka wala kutosheleza.
 
Usishindane kuwekeza liabilities, wekeza assets.Assets huzalisha liabilities but liabilities haziwezi zalisha assets.Nyumba,gari ya kutembelea,vifaa vya thamani vya ndani ni liabilites.Shamba, duka, utaalamu/ujuzi, company ni assets.
Tujifunze kwa wahindi, wanapanga kariokoo wanna miliki viwanda,mashamba makubwa,maduka makubwa.
Kwa nini wasomi wanazidi kupungukiwa akili Ktk competitive economy? What if wazazi wetu wangetuachia mashba makubwa yaliopandwa mazao ya kudumu badala ya xili nyumba walizokuwa wanashindana kuzijenga, tungekuwa wapi? Hongera umepata pa kulala ila hujasolve tatizo la kipato kisicho tetereka wala kutosheleza.

Labda hujamwelewa...! Anauza viwanja na kununua. Ana duka za nguo...! Hakuna mtu mwenyew maisha mazuri asiyependa kuishi pazuri..wahindi ni utamaduni wao..lakini unahakika ya flow ya hela mkuu ni halali kabisa kujenga nyumba nzuri na ukawa na samani nzuri ....

Mie napata shida moja sehemu moja zaidi...watanzania wengi hawana mzuka wa kuwa na viwanda Wala makampuni ..yaani wote tunaishia kuchuuza tu.( Hii inaniboa balaa) mfano tuseme huyu ticha angefungua kampuni akawa anadeal na ishu za ardhi(real estate) .yaani tunaishia kupata hela za kututosha tu sisi na familia zetu. Hakuna za kuwekeza had vitukuu wazikute. Huu utamaduni unapaswa uigwe ..kwamba mjukuu wangu aje akutane na Mali zangu na kampuni ya Bibi alokuwa anaitwa Wangari!

°Yaani wkulima wapande miti(mfano) wajukuu waje wakute miti ya Babu zao...
°Kwenye madini wjukuu wakute kampuni kubwa inayodeal na madini.
yaani kote
Yaan natamani kila sector kuwe na uchumi imara usiotetereka
 
Labda hujamwelewa...! Anauza viwanja na kununua. Ana duka za nguo...! Hakuna mtu mwenyew maisha mazuri asiyependa kuishi pazuri..wahindi ni utamaduni wao..lakini unahakika ya flow ya hela mkuu ni halali kabisa kujenga nyumba nzuri na ukawa na samani nzuri ....

Mie napata shida moja sehemu moja zaidi...watanzania wengi hawana mzuka wa kuwa na viwanda Wala makampuni ..yaani wote tunaishia kuchuuza tu.( Hii inaniboa balaa) mfano tuseme huyu ticha angefungua kampuni akawa anadeal na ishu za ardhi(real estate) .yaani tunaishia kupata hela za kututosha tu sisi na familia zetu. Hakuna za kuwekeza had vitukuu wazikute. Huu utamaduni unapaswa uigwe ..kwamba mjukuu wangu aje akutane na Mali zangu na kampuni ya Bibi alokuwa anaitwa Wangari!

°Yaani wkulima wapande miti(mfano) wajukuu waje wakute miti ya Babu zao...
°Kwenye madini wjukuu wakute kampuni kubwa inayodeal na madini.
yaani kote
Yaan natamani kila sector kuwe na uchumi imara usiotetereka
Umeongea jambo lamsingi sana tungekuwa tunarithishana assets tungekuwa mbali sana niliwai kuwa na rafiki muitaliano biashara wanayofanya now ni 6th generation yaaan vizazi 6 vimepita na bado wanaendelea sema kiafrica africa tunakosea vingi kwanzia mwanzoni napia siri nyingi sana zinaendelea kwanzia uzalishaji hadi mambo yakifedha hapo bado ujaweka chuki,wivu havijawai tuacha salama
 
Umeongea jambo lamsingi sana tungekuwa tunarithishana assets tungekuwa mbali sana niliwai kuwyaanua na rafiki muitaliano biashara wanayofanya now ni 6th generation yaaan vizazi 6 vimepita na bado wanaendelea sema kiafrica africa tunakosea vingi kwanzia mwanzoni napia siri nyingi sana zinaendelea kwanzia uzalishaji hadi mambo yakifedha hapo bado ujaweka chuki,wivu havijawai tuacha salama
Yaani mm ndo napigania hicho tu...sema akili zetu ni shida ..huko huko kwa familia anatokea mwizi mdokozi.. Mara aibe hela aipeleke kwa mganga yaan tafurani dah...sijui shida ni nn
 
Usishindane kuwekeza liabilities, wekeza assets.Assets huzalisha liabilities but liabilities haziwezi zalisha assets.Nyumba,gari ya kutembelea,vifaa vya thamani vya ndani ni liabilites.Shamba, duka, utaalamu/ujuzi, company ni assets.
Tujifunze kwa wahindi, wanapanga kariokoo wanna miliki viwanda,mashamba makubwa,maduka makubwa.
Kwa nini wasomi wanazidi kupungukiwa akili Ktk competitive economy? What if wazazi wetu wangetuachia mashba makubwa yaliopandwa mazao ya kudumu badala ya xili nyumba walizokuwa wanashindana kuzijenga, tungekuwa wapi? Hongera umepata pa kulala ila hujasolve tatizo la kipato kisicho tetereka wala kutosheleza.
Ahsante kuna kitu nimejifunza kwa ujumbe wako
 
Back
Top Bottom