dudus
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 22,116
- 49,360
Nimeshangazwa sana na Mh. Rais na waliomwandalia hotuba yake, ukiacha upupu mwingine mwingi, jinsi walivyoikweza sukari hata kuifanya kama topic inayojitegemea kwenye hotuba yake. Hivi sukari na masuala kama ya elimu (rejea matokeo machafu ya form four mwaka uliopita, kupanda kwa kasi kwa ada za shule na vyuo mbalimbali, n.k), kuporomoka kwa kasi kwa uzalishaji katika maeneo mbalimbali, suala tete la ajira na mishahara duni, hali duni za wananchi (maisha kwenye nyumba za tembe, n.k. na mikakati ya kukabiliana nayo), migogoro inayoendelea huko uarabuni na kwingineko na hatma ya watanzania wenzetu waishio huko (wajibu na nafasi ya serikali ni nini?), kufilisika kabisa kwa mashirika muhimu kwa uchumi na hadhi ya taifa (reli, ATC, n.k.), suala muhimu kwa amani na utulivu wa nchi yetu - ARDHI (mashamba ya Mbarali, Mbulu, Bagamoyo, hata Zanzibar, n.k.); n.k. n.k.
Haya ndio masuala ambayo nilitegemea kama kiongozi mkuu wa Jamhuri na Amiri Jeshi Mkuu yanaangukia chini ya mamlaka yake tena ayazungumzie katika ngazi ya kitaifa (top-level). Badala yake anatuletea habari za tamtam - SUKARI ama kweli Tz yafaa pia kuitwa Jamhuri ya Sukari. Wenzetu leo wanaongelea si tu kwenda bali kuishi anga za mbali rais unazungumzia bei ya sukari gulioni. Na Meneja Masoko ya Kariakoo au Tandale azungumzie nini?
Lakini sukari nchi hii ina siri gani? Nakumbuka ilishawahi kumtimua waziri fulani na naibu wake tena wasomi wazuri tu; mmoja profesa na mwenzie dakta. Nadhni kuna kamchezo fulani kanawavutia hata wakuu kuingia kichwa kichwa; ni suala la muda tu.
Haya ndio masuala ambayo nilitegemea kama kiongozi mkuu wa Jamhuri na Amiri Jeshi Mkuu yanaangukia chini ya mamlaka yake tena ayazungumzie katika ngazi ya kitaifa (top-level). Badala yake anatuletea habari za tamtam - SUKARI ama kweli Tz yafaa pia kuitwa Jamhuri ya Sukari. Wenzetu leo wanaongelea si tu kwenda bali kuishi anga za mbali rais unazungumzia bei ya sukari gulioni. Na Meneja Masoko ya Kariakoo au Tandale azungumzie nini?
Lakini sukari nchi hii ina siri gani? Nakumbuka ilishawahi kumtimua waziri fulani na naibu wake tena wasomi wazuri tu; mmoja profesa na mwenzie dakta. Nadhni kuna kamchezo fulani kanawavutia hata wakuu kuingia kichwa kichwa; ni suala la muda tu.