Mributz
Senior Member
- Aug 29, 2022
- 112
- 388
Timu ya Manispaa ya Kinondoni imetangaza kuvunja Benchi lake la Ufundi kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wake na kumtangaza Kocha Jamhuri Kihwelo 'Julio' kuchukua mikoba ya Thiery Hitimana.
''Bodi ya timu ya Manispaa ya Kinondoni (KMC FC) baada ya kukaa kikao mapema leo asubuhi imeamua kuvunja benchi lote la Ufundi lililokuwa likiongozwa na Kocha Thiery Hitimana baada ya kufikia makubaliano kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa timu msimu huu.''- KMC
Wana Kino Boys hao @kmcfc_official wameongeza kuwa ''Hivyo basi Uongozi umefikia makubaliano na Kocha Jamhuri Kihwelo Julio ambaye atachukua timu akiwa na benchi lake la ufundi.''