James Mbatia: Wagombea wa NCCR katika Jimbo la Vunjo kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wote wameenguliwa

cutelove

JF-Expert Member
Oct 3, 2017
3,317
7,509
Wagombea wote waliochukua fomu na kuzirejesha wameunguliwa katika vijiji 60 kati ya 78

Wagombea hao ni wa vyama vya upinzani, kwa mujibu wa James Mbatia,hata yule ambaye amepewa fomu ya kumpitisha kugombea,ameanza kulazimishwa airejeshe kwa msimamizi wa uchaguzi

===

MBATIA: WAGOMBEA WA NCCR KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA JIMBO LA VUNJO WAMEENGULIWA WOTE

Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia amedai Wanachama wa chama hicho waliochukua fomu kugombea uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika jimbo la Vunjo, wameenguliwa wote

Amesema “Waliamua kufanya uteuzi na kubandika fomu za majina ya Wagombea Novemba 4 badala ya Novemba 5, 2019 kama Kanuni na ratiba ya Uchaguzi inavyoelekeza.”

Ameongeza “Huwezi kuamini Wagombea wetu wote Jimbo la Vunjo wameenguliwa. Mchezo uliofanyika ni hatari kwa usalama wa nchi na tayari nimeiandikia Serikali barua ya malalamiko,"

Aidha, amesema "Katika Kijiji cha Komakundi eneo la Njiapanda ya Himo, Msimamizi Msaidizi alimpatia Mgombea wetu fomu ya kuteuliwa na hivi sasa wanashinikiza airejeshe, agizo ambalo tumeligomea."
 
Muosha huoshwa.

Naona wanahamu kubwa kuvuruga amani kwa kiburi chao.
 
Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia amesema wanachama wa chama hicho waliochukua fomu kugombea uchaguzi wa Serikali za mitaa katika jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro wameenguliwa wote.

“Waliamua kufanya uteuzi na kubandika fomu za majina ya wagombea Novemba 4 badala ya Novemba 5, 2019 kama kanuni na ratiba ya uchaguzi inavyoelekeza.”

"Huwezi kuamini wagombea wetu wote jimbo la Vunjo wameenguliwa. Mchezo uliofanyika ni hatari kwa usalama wa nchi na tayari nimeaidnikia Serikali barua ya malalamiko,” amesema Mbatia ambaye ni mbunge wa Vunjo.

Amesema walioenguliwa ni katika vijiji 60 kati ya vijiji 78 vya jimbo hilo. Vitongoji 372 na mitaa 18 ya mamlaka ya mji mdogo wa Himo.

"Katika kijiji cha Komakundi eneo la Njiapanda ya Himo msimamizi msaidizi alijichanganya na kumpatia mgombea wetu fomu ya kuteuliwa na hivi sasa wanashinikiza airejeshe, agizo ambalo tumeligomea,” amesema Mbatia.
 
Wapinzani wote na viongozi wao wapumbavu ,tatizo lenu mnaogopa bunduki,leteni tukio LA che gwavala(nimeandika siosijui),aliondoka afrika akaenda kuchinjwa Bolivia ,naomba futeni upumbavu wenu harafu mtuletee kitu tukifanyanye ili dunia ijue ,ccm haitarudia ukundu huo
 
Back
Top Bottom