Tanganyika1
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 422
- 86
Jamani huku kwetu mbagala tangu juzi umeme upo tena kwa muda mrefu sana. Hata ukikatika muda mfupi tu unarudi. Sasa sijaelewa mgao umepungua au? Kama umepungua how? Mana juzi tu songas walibainisha kuwa mitambo yao imefikia uwezo wake wa juu katika kuzalisha gesi ya kusukuma mitambo ya kuzalisha umeme. Nahvyo hawawezi kutoa gesi kwa mitambo mipya iliyo agizwa na tanesco ambayo itazalisha mw 100. Aidha songas wanafanya project ya kupanua mitambo ya kuzalisha gesi ambayo itakamilika mwaka 2013. Sasa jamani kama tanesco wamepunguza mgao wamefanyaje? Natanguliza shukran zangu.