Jamani wadada muwe na huruma

Jamani wadada muwe na huruma

Mada nyingine bwana.......

Mleta mada angekuwa na huruma angemsaidia huyo jirani yake....... Hata hivyo, tunatakiwa kujifunza kushangaa mambo ya wengine lakini tuwe na kifua cha kuwaachia waendelee wapendavvyo!
 
Namba zake sina wala sizitaki na za kwangu hana, maana ni shida alijaribu kumuomba wife namba zangu alikataliwa. Alijua mara naweza kula kiboga kwenye uvungu.

Teeeeh....! Usinifanyie hivyo tafwadhali😉😉
 
Wanawake wanajifanya kutetea ila ukweli utabaki kuwa pale pale.
 
MMU raha sana, utamjua mtu na tabia yake dhahiri kwa kuangalia tu comment zake, cheki wanawake humu wanacho comment utajua ndivyo walivyo.
Na hata wanaume pia ukiona anayefurahia aina ya life hilo ujue yeye naye ni wa type hiyohiyo.
Huwezi kufagilia kwa vyovyote vile aina hiyo ya maisha ya wawili hayo hata kama wanapendana.
 
Hayo ni mapenz yao cyo kila kitu kurogwa km kampa likizo kutokana na penz lake je
 
Niko na mpangaji mwenzangu tangia tujuane yapata mwezi tena kwenye nyumba hiyo, ila cha kusikitisha anaishi na mwenzi wake kama vile hana mke ona hii mwanamke huyo mume wake anafagia nyumba yeye hata kujitikisa kuzoa taka alizokusanyiwa hawezi. Leo mida ya saa 1:30 usiku mume ametoka kazini hakupikiwa chakula ikabidi aingie jikoni na kujihudumia mwenyewe cha kushangaza mwanamke huyo ni mvivu hata kuosha vyombo alivyolia chakula vinakaa kama siku 2 havijaoshwa. Jamani haya maisha anayoishi mume mwenzangu yanasikitisha cha kusikitisha zaidi mchana mzima mke wake anaongea na mabwana kupitia sim hii nimeileta kwa wale wadada wenye tabia kama za huyo.

Hebu tuwekee na yakwako hadharani(kuna usemi unasema,kama kutangaza aibu za wenzio ni rahaa,tangaza yako.
 
Hayo ni mapenz yao cyo kila kitu kurogwa km kampa likizo kutokana na penz lake je

Hakuna cha likizo hapo ni utumwa mimi mke wangu hajawahi na hatowahi, tatizo lenu mnapima akili za mwanaume limbukeni akiwa hola unaangushia hapo hapo. Kuna siku mke wangu atamani kunijaribu lakini namtolea mimacho huyo anatoka nduki kwenda kufanya kazi zake za ndani. Kwamfano wife akinambia kesho naomba unifanyie kitu fulani na mimi namwambia ikifika alfajiri nakuamsha ujiandae kwenda kazini mimi nibaki nafanya hiyo kazi. Basi anakua na adabu sio misichana ya sasa iliyokua haikufunzwa majumbani kwao yanakaa na mishoga kazi zao kufundishwa kumchuna mwanaume anapokua nae.
 
Kwani huyo me hana ndugu wa kumwambia?

Kabla hawajapanga walikua na nyumba yao, walikua wanaishi na familia ya mume, kwabahati nzuri mama mtu alikua hapendi tabia anazofanyiwa mwanae, ikabidi amwambie hata kama mke alikua hapendi. Na ndo maana mke huyo huyo akamburuza mume wake wakapange nyumba nyingine ambayo ndo hiyo niliyo mimi.
Kwakweli mwanamke hajatulia, na kipindi anakuja kuhamia, nikamuona style zake nikajaribu kumwambia wife kwamba huyu mdada anaonekana hajatulia, ila ngoja tuendelee kuishi nae tutapata majibu zaidi.
 
mkuu tatizo wanaume wengi tunakurupuka kwenye suala la ndoa.
 
Back
Top Bottom