Poleni na majukumu waungwana, kuna jambo linamtatiza mwenzetu nimeona ni busara nililete kwenu kwakuwa hapa ni uwanja mpana pasipo shaka atapata ufumbuzi na mwenzi wake. Hii ni familia ya wanandoa, jamaa anasema kwa mapenzi aliyonayo kwamke wake anaamini kama binadam naye anachoka kwa majukumu ya nyumbani, mwenzetu huyu anasema amejijengea utamaduni wa kufanya shuguli za ndani, ikiwemo kufua,kupika kufagia ndani na nje. Anasema anaona fahari kama mwanume kushiriki na mwenzi wake katika utekelezaji wa majukumu ya familia hususani kazi za ndani.
Anasemma babake mzazi ambaye ni marehemu sasa ndo aliye wajenga hasa kwa utekelezaji shuguli za ndani, anasema babake alikuwa hodari sana wa kupika hasa vitafunwa,na ansema katika familia yao hakukuwa na kazi maalum kwa watoto wa kike wala wa kiume. Ansema ameanza kupika na kufua nguo zake mwenyewe akiwa darasa la pili. Hivyo hata ndugu zake wanapomtembelea hawashangai wakikuta anapika, au kufanya shuguli za ndani. Anasema mfumo wa maisha anaoishi na mke wake umependwa sana na kaka wa mke wake ambaye ilifika mahali alimwambia natamani kuishi kama wewe shemeji uishivyo na dadangu.
Sasa mambo yako hivi, majuzi mke wa huyu bwana mpenda majukumu ya nadani, alifanya safari mkoani kumtembelea kakake alipohamishiwa kikazi, baada ya kurudi akasimulia jinsi kakake mambo yanavyomwendea vizuri, bwana huyu akisimulia anasema baada ya siku moja alirudi nyumbani akakuta mke wake anaongea na simu, bwana huyu anasema baada ya kubaini kilicho kuwa kikizungumzwa ilibidi atulie mahali ili kupata uhondo wa kinachozungumzwa.
Anasema simu ile mke wake alikuwa akimsimlia mamake aliyoyakuta kwa kaka yake, anasema mama mwenzagu kaka ameshikwa hajiwezi yuko mateka, anasema huwezi amini siku naingia kwa kaka chakula cha usiku kaka ndo aliandaa chakula cha usiku mimi nikiwa na wifi ukumbini, anasema nilipochoka ni pale kaka alipo fua nepi za mtoto huku anachekacheka, anasema mama fanya haraka tumwokoe kaka anaangamia, anasema kwajinsi nilivyo chukia niliondoka bila kuaga wakiwa kazini, nikamwabia kaka mimi naondoka nimepigiwa simu mtoto nyumbani anaumwa, na wifi sijamwambia chochote.
Sasa hapa huyu bwana anasema baada ya kubaini hayo amestisha utendaji wa majukumu ya ndani aliokuwa akifanya kwahiari yake, jambo ambalo limezusha mtafaruku mkubwa ndani ya nyumba kwakuwa mke wake aliisha jenga mazoea. Anasema yeye hajashikwa anafanya hayo kwa utashi na si kushikwa, lakini kama mke wake anasema kakake ameshikwa basi ameamua kusitisha kila kitu na hataki tena kusikia kitu kinaitwa shuguli za ndani, kwani mke wake amemwona kama mtu asiye na shukrani
Je ndugu mdau tunawashauri nini hawa wanandoa? Huyu mama mme wake amemfanyi akaona ni sahihi lakini kakake kumfanyia wifi yake anaona kashikwa.
Anasemma babake mzazi ambaye ni marehemu sasa ndo aliye wajenga hasa kwa utekelezaji shuguli za ndani, anasema babake alikuwa hodari sana wa kupika hasa vitafunwa,na ansema katika familia yao hakukuwa na kazi maalum kwa watoto wa kike wala wa kiume. Ansema ameanza kupika na kufua nguo zake mwenyewe akiwa darasa la pili. Hivyo hata ndugu zake wanapomtembelea hawashangai wakikuta anapika, au kufanya shuguli za ndani. Anasema mfumo wa maisha anaoishi na mke wake umependwa sana na kaka wa mke wake ambaye ilifika mahali alimwambia natamani kuishi kama wewe shemeji uishivyo na dadangu.
Sasa mambo yako hivi, majuzi mke wa huyu bwana mpenda majukumu ya nadani, alifanya safari mkoani kumtembelea kakake alipohamishiwa kikazi, baada ya kurudi akasimulia jinsi kakake mambo yanavyomwendea vizuri, bwana huyu akisimulia anasema baada ya siku moja alirudi nyumbani akakuta mke wake anaongea na simu, bwana huyu anasema baada ya kubaini kilicho kuwa kikizungumzwa ilibidi atulie mahali ili kupata uhondo wa kinachozungumzwa.
Anasema simu ile mke wake alikuwa akimsimlia mamake aliyoyakuta kwa kaka yake, anasema mama mwenzagu kaka ameshikwa hajiwezi yuko mateka, anasema huwezi amini siku naingia kwa kaka chakula cha usiku kaka ndo aliandaa chakula cha usiku mimi nikiwa na wifi ukumbini, anasema nilipochoka ni pale kaka alipo fua nepi za mtoto huku anachekacheka, anasema mama fanya haraka tumwokoe kaka anaangamia, anasema kwajinsi nilivyo chukia niliondoka bila kuaga wakiwa kazini, nikamwabia kaka mimi naondoka nimepigiwa simu mtoto nyumbani anaumwa, na wifi sijamwambia chochote.
Sasa hapa huyu bwana anasema baada ya kubaini hayo amestisha utendaji wa majukumu ya ndani aliokuwa akifanya kwahiari yake, jambo ambalo limezusha mtafaruku mkubwa ndani ya nyumba kwakuwa mke wake aliisha jenga mazoea. Anasema yeye hajashikwa anafanya hayo kwa utashi na si kushikwa, lakini kama mke wake anasema kakake ameshikwa basi ameamua kusitisha kila kitu na hataki tena kusikia kitu kinaitwa shuguli za ndani, kwani mke wake amemwona kama mtu asiye na shukrani
Je ndugu mdau tunawashauri nini hawa wanandoa? Huyu mama mme wake amemfanyi akaona ni sahihi lakini kakake kumfanyia wifi yake anaona kashikwa.