Wana JF, kuna dada anaomba msaada ili aweze kupata haki yake anayoona inataka kudhulumiwa.
Mdada huyu alikuwa anafanya kazi katika shirika moja linaitwa SEDA tawi la Kagera ila makao makuu yake ni ARUSHA, kafanya kazi miaka miwili lakini leo kaachishwa kazi kwa kosa la KUBEBA UJAUZITO kabla hajaolewa, kwa hiyo kavunja masharti na adhabu yake ni kufukuzwa kazi, shirika lenyewe linashughulika na mambo ya mikopo midogomidogo kwa wananchi, Je, kwa sheria ya kazi hii ni sahihi? kwahiyo kama alipata ujauzito wao walitaka autoe? anadai mkataba aliojaza haukuwa na kipengele hicho. Je bado kuna mashirika yanaweza kuwa na sera au sheria za namna hii kweli au ni unyanyasaji kwa wanawake wenyewe wanafanyiwa kwani inasemekana mabosi wakuu ni wanawake na hawajaolewa, sasa wamemtumia Email ya kukabidhi kila mali ya shirika lakini hawataki kumpa barua ya kuachishwa kazi wala pesa za kusafirisha mizigo hadi kwao kama sheria ya kazi inavyosema pale mwajiri anapoamua kusitisha mkataba wa mwajiriwa wake. Tumsaidieje kiushauri wadau na pia hii inaweza kuwa somo kwa waajiri wenye sheria kandamizi zinazokiuka haki za binadamu. Ahsante naomba kuwasilisha ila msaada wa kisheria ni muhimu sana, mhanga kwao ni Shinyanga.😛arty:
Mdada huyu alikuwa anafanya kazi katika shirika moja linaitwa SEDA tawi la Kagera ila makao makuu yake ni ARUSHA, kafanya kazi miaka miwili lakini leo kaachishwa kazi kwa kosa la KUBEBA UJAUZITO kabla hajaolewa, kwa hiyo kavunja masharti na adhabu yake ni kufukuzwa kazi, shirika lenyewe linashughulika na mambo ya mikopo midogomidogo kwa wananchi, Je, kwa sheria ya kazi hii ni sahihi? kwahiyo kama alipata ujauzito wao walitaka autoe? anadai mkataba aliojaza haukuwa na kipengele hicho. Je bado kuna mashirika yanaweza kuwa na sera au sheria za namna hii kweli au ni unyanyasaji kwa wanawake wenyewe wanafanyiwa kwani inasemekana mabosi wakuu ni wanawake na hawajaolewa, sasa wamemtumia Email ya kukabidhi kila mali ya shirika lakini hawataki kumpa barua ya kuachishwa kazi wala pesa za kusafirisha mizigo hadi kwao kama sheria ya kazi inavyosema pale mwajiri anapoamua kusitisha mkataba wa mwajiriwa wake. Tumsaidieje kiushauri wadau na pia hii inaweza kuwa somo kwa waajiri wenye sheria kandamizi zinazokiuka haki za binadamu. Ahsante naomba kuwasilisha ila msaada wa kisheria ni muhimu sana, mhanga kwao ni Shinyanga.😛arty: