Jamani mwenzenu Napendwa, ila

Jamani mwenzenu Napendwa, ila

ladyfurahia

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
14,758
Reaction score
9,589
Hay! waungwana marafiki zangu Namshukuru Mungu kuniweka hata siku hii ya leo niko mzima buheri wa afya njema, wengine hatunao leo hii kwanini mm ni nani mpaka nikawepo, jamani? hiviyo sina budi kumshukuru Mungu hata wewe rafiki yangu mpenzi wangu huna budi kumshukuru Mungu kila uionapo leo.

Wapendwa wangu wa moyoni leo tena nimekuja na jambo hili ambalo nimeonelea niliseme hapa kwenu ili tujadili na kupata ufumbuzi wa kina. labda nianze kwa kuuliza swali hili hapa: samahani kama mtaboreka wanaume wa humu mjengoni? ni hivi: hivi ni kwanini ninyi wanaume mnakuwa vicheche na mnakuwa watu wa ajabu sana kuwatenda wake zenu?

Hamuoni kuwa mnasambaratisha ndoa zenu na kuleta mitafaruku ndani ya ndoa na mgawanyikano kati ya kizazi na kizazi? Mkipenda kujibu haya kazi kwenu. Jambo ambalo nimeona niliseme ni hili kwa upande wa wanaume ambao wamekuwa vicheche hata kwangu imenitokea kwani nimejaziwa wanawake lukuki hata wengine sijui majina hao hasa nimebaki naumia ndani kwa ndani nimemuomba kaka Erickb52 asaidie jahazi hili linaingia majini kajitahidi kaka wa watu kunisaidia laikini wapi? nimeona sasa ninyi marafiki zangu mnisaidie kwa huyu mtu kwani bado nampenda na sitaki kumuacha kwani tuliahidiana mbele ya mashahidi kuwa sisi tu mwili mmoja na Alichokiunganisha Mungu mwanadamu hawezi kukitenganisha, hivyo naendelea kuvumilia tu japokuwa ni karaha na mateso ndani ya ndoa lakini bado naendelea kuwepo tu msije sema kuwa mm ni king'ang'anizi lahasha wala ni ndoa lazima niijenge japokuwa inayumba sana sasa, ugomvi, manyanyaso yamekuwa mengi, ingawaje ananipenda naye hawezi nitamkia chochote kuhusu kutalikiana kwani bado ananipenda japokuwa ananiletea wanawake humu home.

Juzi kati kwenye majira ya jioni tumekaa tunasubiri msosi akaniangalia na kunikodolea macho kisha akasema mwenyewe kupitia kinywa chake "My love barafu wa moyo wangu unataka nikufanyie nini ili uone nakupenda japokuwa nimekuwa mtu nisiyemwaminifu? maneno haya aliyatamka yeye mwenyewe kwani aliona anavyonifanyia na kunipa stress kila wakati ingawaje nilishamwambia kuhusu tabia yake ya kicheche na kutamanni wanawake wa nje. Nikamwangalia kwa macho maangavu na yenye mvuto wa mapenzi kisha nikamwambia niletee au nipe chochote upendacho, mume wangu laaziz wangu Mentor wa maisha.

Akaniangalia na kusema kuwa nitakununulia gari aina ya VITZ (sijui kama nimedanganywa hapa) ila moyoni nilijawa na furaha na nilifurahia nikamrukia na kumpa kiss la agape, kwa furaha niliyonayo japokuwa bado ANANIPENDA jamani mpaka nikasahau machungu, manyanyaso yote hapa nilipo nasubiri huo muujiza utendeke nipate kufurahi na kuwa mwenye kicheko ndani ya ndoa yangu waungwana je mmelionaje hili?

Nawatakia siku njema na kazi njema
 
sijui amenilisha nini huyu kiumbe jamani yani nimekuwa teja wa mapenzi kiasi hichi kaka? kupenda kubaya sana lakini acha niendelee kumvumilia tu ipo siku atabadilika
Dada hivi ni kwanini Mentor anakusumbua hivyo?
 
@ladyfuraha we mchoyoooo... wiki kadhaa tu zilizopita ulisema ubachela umekushinda, ukawa unatafuta mtu. Kumbe ushampata kimya kimya, hata kukaribishana jamani!...
 
[Ujue sio wanamme wote wananyanyasa wake zao? Ni baadhi tu

Ila sababu unampenda, basi kaa ukijua 'hiari yashinda utumwa'


Ila, umemsamehe sababu umeona haja ya kumsamehe au sababu ya vits?
 
haa haa haaaaa samahani sana mm sio mchoyo best nilijisahau tu kukukaribisha basi usikonde utakaribia nitakapopata mtoto mwingine
@ladyfuraha we mchoyoooo... wiki kadhaa tu zilizopita ulisema ubachela umekushinda, ukawa unatafuta mtu. Kumbe ushampata kimya kimya, hata kukaribishana jamani!...
 
yani nimemsamehe 7x70=70 na roho yangu haina dosari naye yeyote na bado nampenda tena sana, na waala sio vitz ndo imenipelekea kumsamehe basi tu moyo wangu wa huruma na upendo, na mwenye mvuto wa kuwa na amani kwani kwake nimejitosheleza kabisa best una jingine jipya?
[Ujue sio wanamme wote wananyanyasa wake zao? Ni baadhi tu

Ila sababu unampenda, basi kaa ukijua 'hiari yashinda utumwa'


Ila, umemsamehe sababu umeona haja ya kumsamehe au sababu ya vits?
 
haa haa haaaaa samahani sana mm sio mchoyo best nilijisahau tu kukukaribisha basi usikonde utakaribia nitakapopata mtoto mwingine

Dah... unajua mi nilikuwa najipanga lakini. Kila siku naingia PM nishushe mistari, but mdomo ulikuwa mzito...
 
teh teh siku utakayogundua kuna mwenzio kapewa BMW X5 usisite kuja kutuambia humu tutakuwa pamoja tu
na uskimfumania pia usisite kuja kutuambia sawa??
 
[Ujue sio wanamme wote wananyanyasa wake zao? Ni baadhi tu

Ila sababu unampenda, basi kaa ukijua 'hiari yashinda utumwa'


Ila, umemsamehe sababu umeona haja ya kumsamehe au sababu ya vits?


we Kongosho unafikiri kuparamia daladala ni starehe eeeh heri apate stress kwenye vitz kulizo kwenye dcm la mbagala....


Serious...

Hapo bi dada aamue moja kuvumilia na package yake (maradhi ya ngono)

au atafte ustaarabu wake(hapa napo vitz bye bye)
 
Last edited by a moderator:
Nakutakia heri na furaha katika ndoa yako

Uvumilivu unalipa, hasa kwa unayempenda

yani nimemsamehe 7x70=70 na roho yangu haina dosari naye yeyote na bado nampenda tena sana, na waala sio vitz ndo imenipelekea kumsamehe basi tu moyo wangu wa huruma na upendo, na mwenye mvuto wa kuwa na amani kwani kwake nimejitosheleza kabisa best una jingine jipya?
 
Hapa ntajua wasiolipenda pendo letu...

Hata nimebadili nimepata dili leo nitanunua Subaru i think ntakuachia ile Verossa yangu...haya waache sasa waseme!
 
Pole sana dear,
lkn kwanini mentor unamsumbua huyu mrembo hivi hujui kuwa yeye ni wa thamani sana kwako hebu badilika kidogo jamani.
 
Mkuu haikuaza leo wala jana,tangu enzi za manabii ibrahim,solomon,yakobo,daudi etc na hao mitume wataenda peponi.sema tuu siku hizi wanaume wanaficha hawawi wawazi kama enzi zile
 
dawa kubwa ya kumtuliza mwanamke na kumfanya alete chakula haraka na kiwe kitamu wala asiunguze ni kumdanganya. Samahani ladyfurahia napita.
 
Back
Top Bottom