Makau Js
Member
- May 25, 2017
- 93
- 233
NIMEMUONA raisi wa TFF NDUGU Jamali Malinzi akikosea Mlango wa Karandinga. Imenigusa sana. sizungumzii tuhuma zinazomkabili. Nawaza katika muktadha wa kiutu na kujifunza.
Hakukosea mlango wa kuingia katika karandinga kwa sababu haujui. La hasha. Ni mawazo na namna alivyo sasa. Wiki kadhaa nyuma alikuwa miongoni mwa binadamu wenye mafanikio na hadhi katika jamii. Kazini alienda kwa gari la thamani lenye kiyoyozi na alirudishwa nyumbani kuungana na familia yake kwa unyenyekevu. Leo ana amrishwa, anashurutishwa. Hana cha kufanya ila kutii.
Katika maisha kuna ajali nyingi sana. Unaweza kunusurika katika magari, ndege, meli na pikiki ila ukanasa katika tuhuma fulani. Nayo hiyo ni ajali.
Malinzi hana amri tena, hana uhuru tena. Kichwa chake hakiwezi kuwa sawa. Bila shaka alipotea mlango kwa sababu mwili ulikuwa pale ila akili ilikuwa sehemu nyingi ikijiuliza bila kupata majibu. Leo mimi niko hapa? Nachanganyika na hawa? Siwezi kuamua lolote ila kutii amri? Mbona dunia inanisaliti kwa kiwango hiki?
Hakukosea mlango wa kuingia katika karandinga kwa sababu haujui. La hasha. Ni mawazo na namna alivyo sasa. Wiki kadhaa nyuma alikuwa miongoni mwa binadamu wenye mafanikio na hadhi katika jamii. Kazini alienda kwa gari la thamani lenye kiyoyozi na alirudishwa nyumbani kuungana na familia yake kwa unyenyekevu. Leo ana amrishwa, anashurutishwa. Hana cha kufanya ila kutii.
Katika maisha kuna ajali nyingi sana. Unaweza kunusurika katika magari, ndege, meli na pikiki ila ukanasa katika tuhuma fulani. Nayo hiyo ni ajali.
Malinzi hana amri tena, hana uhuru tena. Kichwa chake hakiwezi kuwa sawa. Bila shaka alipotea mlango kwa sababu mwili ulikuwa pale ila akili ilikuwa sehemu nyingi ikijiuliza bila kupata majibu. Leo mimi niko hapa? Nachanganyika na hawa? Siwezi kuamua lolote ila kutii amri? Mbona dunia inanisaliti kwa kiwango hiki?